Sakata la Lwakatare: Wanasheria CHADEMA walonga

Sakata la Lwakatare: Wanasheria CHADEMA walonga

[h=1]Lissu: Mwigulu na Ludovick ndio waliotengeneza video ya Lwakatare[/h]

[video=youtube_share;yR_sm3UYJcY]http://youtu.be/yR_sm3UYJcY[/video]
 
mimi nahisi Ludovic alikubali kuchezea CDM mchezo mchafu lakini akawataarifu CDM , na CDM wakaamua waendelee waone CCM wako tayari kufanya mangapi. kwenye press conference ya CDM wamesema mazungumzo ya Ludovic na Nchemba baada tu ya kikao chake na Lwakatare wameya rekodi....sasa walijuaje? labda kama wanarekodi maongezi yote ya Ludovic au Ludovic alikua amewapa CDM mchongo mzima wa CCM.

Swali la msingi ni kwamba, nani alitekeleza mipango ya kuwashugilikia wahandishi wa habari?
 
Mh. Tundu Lissu amebadilisha upepo kabisa wa swala la Lwakatare. Amesema wana mawasiliano baina ya Mwigulu na Ludovick wakiwasiliana muda mfupi tu baada ya Ludovick kutoka kwa Lwakatare. Lwakatare pia alipigiwa simu na Msaki siku moja kabla ya video ile kurekodiwa. Lisu anasema wakifika Mahakamani kesi ile haimalizi masaa 3 itakuwa imeisha.
Lissu: Mwigulu na Ludovick ndio waliotengeneza video ya Lwakatare - YouTube
 
Mie kwa mtazamo wangu nafikiri serikali ya CCM kupeleka hii kesi mahakamani kwa kutumia cheap video watakuwa wamejichoma kijiti cha muhogo masaburini. Kwa uelewa wangu: Unapotumia digital file(s) as evidence before the court(s), hapa una- involve computer forensic.

Kwa faida ya JF mambers and non-members: Wale mliosoma Cyber-crime or Cyber-security, Once you decide to present digital evidence before the court, you are mandated by law (sijui sheria ya kwetu) to show/prove that you're disciplined in associating elements of law and computer science to gather, secure, examine, and analyze data from computer systems, networks, wireless communications, and storage devices in a way that is admissible as evidence in a court of law. Kwa serikali yetu sina hakika if that happened.

1. The Magamba's gov needs to prove that whatever they gathered during their raid(s) wasn't contaminated.

2. The Magamba's gov needs to show how they examined the data collected (Ni computer lab gani waliweza ku-examine digital file from public domain in less than 17 hrs) iwapo mpaka dakika hii wameshindwa kukamata wale wezi wa TRA waliotumia mtandao 2 yrs ago (Kitillya knows what I'm talking about).

3. The Magamba's gov needs to prove they analyzed the collected data thoroughly and none of information byte(s) omitted/added.

4. The gov also needs to prove before the court that people who collected, secured, examined, and analyzed the data from Youtube domain are ethical and the whole process wasn't interfered by external pressure.

Inasemekana hiyo video ilikuwa edited, na sehemu nyingine ikiwa imeondolewa. Kwa mtazamo wangu, Information gathered wasn't secured before presented kwa mahakama ya Umma (video haijaonyeshwa mahakamani). Serikali inatakiwa ionyeshe hatua kwa hatua jinsi walivyoweza ku-secure hiyo process nzima hadi kumpeleka Lwakatare before the court.
Waeleze kama walikuwa na hiyo video kabla haijawekwa kwenye public domain (Youtube). Kama walikuwa hawana, waeleze hiyo process ya ku-gather and analyze digital file ilivyochukuwa muda mfupi bila ya kuwa na original storage media. Na kama walikuwa na original storage device(s), kwa nini sehemu ya video imekatwa?

Huu ni mtazamo wangu tu ingawa mimi si mwanasheria lakini nina background ya Digital Forensic Investigations.
 
Mkuu Pasco,naomba leo tutofautiane kidogo.hakuna mamlaka isiyohojiwa ktk dunia hii labda ya Mungu tu.sheria zipo ili zilinde haki za watu.kama DPP hawezi kuhojiwa mamlaka,then hiyo sheria inayompa mamlaka hayo hata kama ni katiba ya nchi is against human rights.lazima tuihoji hata hiyo sheria na sheria is subject to change(na ni muhimu sana kwa sheria kuwa subject to change).Pili,ni hatari kwa Chadema kumkana Lwakatare wakati uhusika wake is still a legal and technical debate !kumkana lwakatare itakuwa ni ku-justify uhusika wake,kitu ambacho hakijawa proven na chenye madhara kwao kisiasa.Tatu,suala la hii case kuwa legal ni la sasa,lakini baadae kwa kadri proceedings zinavyokwenda,ni lazima iwe political case,na kuna kila harufu ya kuwa political case.Lwakatare ni political figure kupitia Chadema na jamii inamtazama hivyo.naamini wanasheria wa Chadema wana uwezo wa kutosha kuhandle case hii kisheria na kisiasa bila kuathiri defence yao na wakifanya hivyo watakuwa wamemmaliza adui yao.tuwe wazi tu,hii case imelenga kumchafua lwakatare na Chadema kisiasa na kijamii,kwa vile kidhibiti kikuu cha mashtaka ambacho ni ile video,kuna maneno mle yanayojenga picha hiyo!let them hit the main target.hamna haja ya kuzunguuka.!you know always WHAT GOES AROUND.....!
 
Safi sana!mwigulu,nape,riz1,rage kuiua ccm kabla ya 2015.
 
Nani aliyemrekodi Lwakatare? Je, Lwakatare alijua kuwa anarekodiwa? Je, aliruhusu? Kama hakuruhusu, ilifanyika kihalali? Je, haivunji katiba ya nchi inayozungumzia privacy ya mtu? Je, baada ya kurekodiwa mkanda huo ulipelekwa wapi? Nani alikuwa nao? Je, umefanyiwa uhariri (editing) na nani? Je, aliyemrekodi alitumwa na nani?

Ina maana wamekubaliana kuwa video ni halisi hivyo wanakuja na hoja hizi au?
 
This is getting interesting. Jf tuwekeni hiyo video wengine tunaisikia tu. harafu mhe Lissu tunamwomba aende mbele zaidi
kutunyambulia sheria inayoruhusu kunyakua habari za email ama sms za mtu mwingine. Na kama tuhuma kuwa hio video ni ya kughushi, je ana uthibitisho gani kuwa sms na email tajwa si za kughushi?

Unafikiri vijana wa chadema wanajiuliza hayo???

Video hii hapa VID-20121228-00005 - YouTube
 
Mwigulu atawaumbua sana. Jamaa hayuko mnavyomfikiria. Aliposema ana cd mlisema mropokaji sasa mbona mnahangaika baada ya magaid kupelekwa lupango. The way I know the person is soo smart na ana taarifa nyingi sana za mauaji ya chadomo

Almost mipango yote haramu aliyohusika huyu kijana imekwenda mrama! Na hapa tulipofika, uwepo wake kwenye chama na hasa ngazi ya juu ya uongozi wa CCM - kunazua maswali. Kazi yake ni nini, au kitengo chake kinahusika na nini? Sitoshangaa kusiki vijana wanamkimbia huyu kijana mwenzao kwa 'hofu'.

Pili, ni muhimu wakubwa wakawa wanasoma alama za nyakati. Watanzania wa leo sio wa mwaka jana, na kwa hakika mazingira ya leo si ya mwaka 47. Siasa za Kisoviet hazina nafasi tena. Mtindo wa kubambikizia watu kesi umekuwepo kwa muda mrefu mno. Vijana wengi wa Tanzania wamezaliwa na kukulia kwenye mazingira ambayo imekuwa ni 'kawaida' polisi kumbambikia mtu kesi. Hivyo kwao, hii saga ya Lwakatare ni 'mchezo mwingine' wa polisi.

Hii kesi inaweza kuleta nuksi kuliko wanavyodhani wakubwa. Na ukiangalia matukio ya miaka hii ya karibuni utagundua kuwa CCM wanajua wanataka nini lakini hawajui madhara ya mipango yao, na wala hawana uwezo wa kukabiliana na madhara yatokanayo na hiyo mipango. Mwanza kuna mgogoro wa mabucha, Zanzibar FBI, na huku shule za Kata zimeanza kutoa matokeo. New thinking ndio njia pekee.
 
hapa slaa ataumbuka kumtuma ben kutega humu mtoni na kumtumia ludo maana mchemba cd anayo na kabla hajatinga kizimbani tutairusha fb na tweter muone slaa akimpa rwakatale maagizo kabla rwakatale haja mpa ludo

Subiri ukajibu kesi yako.

Hivi hujaenda kuwaambia watu wa mbozi kilichokusibu mkuu?
 
Mwigulu Mnchemba kanasa kwenye tundu anastahili kuwa ndani Huko Singida Polisi anathibitisha kuwa Mwigulu ni mmuaji kwa kupanga mipango ya uuaji kwa mwana CCM,Dar es salaam kasharekodiwa ,
haya tutamsikia bungeni mwenziwe Ridhiwani kaenda kumuangukua Manji amsafishe nyota kwa wananchi
 
Nilishasema na nasema tena pasipo kumung'unya neno mwigulu ndo mhusika mkuu wa hili jambo,jamaa ana roho mbaya sana
 
Mkuu Mpaka Kieleweke,
Kwanza poleni kwa yote!.
Pili mnayo team nzuri sana ya wanasheria, lakini nashauri, mara moja moja, muwe mnasikiliza maoni ya ma layman kama sisi kupitia humu jf.

Nasikitika kuwaambia kitendo cha kufungua kesi kuhoji mamlaka ya DPP, its a wastage of time!. Mamlaka ya DPP haihojiwi na mamlaka yoyote hata rais wa nchi, hawezi kuyahoji, hivyo you are fighting a loosing battle!.

Ni kweli timu yenu ya sheria is a good team, nashauri please seek legal opinion ya best criminal lawyers around, kwa sababu baadhi ya wanasheria wenu ni politiciancs, wajiangalie wasije wakaipoliticise hii kesi kuonekana its a political case, bali muendelee kuipigania iwe abduction na sio terrorisim!.

Mwisho mtake msitake, lazima Chadema kama chama, kitoe statement kuwa whatever mashitaka yanayomkabili Rwakatare, ni yake mwenyewe kama Rwakatare, vingenevyo hali ikiachwa ilivyo, kuna hatari ya jamii kuaminishwa kuwa hayo yaliiyotendeka, yamendwa kwa maelekezo ya chama, hivyo kuja kuwaingiza hata wasiokuwemo!.

Huu ni ushauri wa bure tuu toka kwa layman.

Pasco.

ungekaa kimya ungeonekana una busara umeongea kila mtu ame-endorse kuwa wewe ni semi-illiterate hata katika basics,
 
Back
Top Bottom