Ruge Mutahaba live Jumatatu tarehe 22.05.2017 CLOUDS 360

Ruge Mutahaba live Jumatatu tarehe 22.05.2017 CLOUDS 360

Status
Not open for further replies.
Nafikiri Ruge chakufanya aweke tu clip ya kilichotokea ndani siku ile ili atutoe katika huu mkanganyiko.
RC kaomba hiyo clip wananchi tupewe nafikiri tupewe tuwe na hukumu sahihi
 
Dakika chache baada ya mkuu wa mkoa wa Dar, Paul Makonda kuongea Star TV, Mkurugenzi wa Clouds nae akawa na kipindi japo alisema hataongelea lakini amesema kesi ya uvamizi wamefungua labda kama polisi na mkuu wa mkoa hawana mawasiliano kinyume na tuhuma za Makonda aliedai kama Clouds walivamiwa, kwanini hawajafungua kesi ama kuripoti polisi.

Ruge amedai kwenye interview ya Makonda Star TV, upande wa redio walisahau kuzima Mic wakati wanaenda kwenye matangazo, sauti ilisikika ikidai 'Ruge leo tunamkomesha'.

Amesisitiza ajenda ya kipindi cha leo ilikuwa ni shukrani na sio kwa sababu kulikuwa na kipindi kingine. Amewataka watu wajifunze kusamehe akitolea mfano wa Dar mpya, amesema mtu anaweza kuogopa kufanya kazi tena na halmashauri kwa kuogopa kuimbiwa amekula hela, amedai gharama hazifanani.
 
Dakika chache baada ya mkuu wa mkoa wa Dar, Paul Makonda kuongea Star TV, Mkurugenzi wa Clouds nae akawa na kipindi japo alisema hataongelea lakini amesema kesi ya uvamizi wamefungua labda kama polisi na mkuu wa mkoa hawana mawasiliano kinyume na tuhuma za Makonda aliedai kama Clouds walivamiwa, kwanini hawajafungua kesi ama kuripoti polisi.

Ruge amedai kwenye interview ya Makonda Star TV, upande wa redio walisahau kuzima Mic wakati wanaenda kwenye matangazo, sauti ilisikika ikidai 'Ruge leo tunamkomesha'.
Kwa waliosikiliza ni kweli hayo maneno yametamkwa?
 
Walireport baada ya Sirro kuwauliza lakini bila kuulizwa wasinge fanya vile
 
Amakweli samaki anamengi ya kuongea ila mdomoni anamaji

Pongezi kwako ruge kwa kuonesha ukomavu wa kuwakiongozi na kiakili kwa kutotaka majibizano yasiwe mipasho maana unamengi ya kuongea lakini umekubali yaishe
Maana hata biblia katika mithali 26:4 usimjibu mpumbavu sawasawana.upumbavu wake usije ukafanana nae.
 
Nafikiri Ruge chakufanya aweke tu clip ya kilichotokea ndani siku ile ili atutoe katika huu mkanganyiko.
RC kaomba hiyo clip wananchi tupewe nafikiri tupewe tuwe na hukumu sahihi
Hakuna kitu hapo.Ni kazi ya shetani tu,
Hawa watu siku wakija kupatanishwa sijui sie wapambe tutaweka wapi sura zetu
 
Ruge kakosa cha kujibu naona anambwelambwela
 
sioni haja ya daudi bashite kujibiwa na yeyote yule huyu bwana kashapotea katika ramani anatumia uhuni kujirudisha kwenye vyombo vya habari si gwajima wala mutahaba wa kumjibu .................................... hapo ndo atakapolia zaidI
 
Ruge kakosa cha kujibu naona anambwelambwela
Utata maelezo ya Makonda:
Nilikuwa nyumbani naangalia shilawadu,ikafika saa 4:30,nikaona hakuna dalili ya kipindi cha yule mwanamke kuruka hewani,nikawapigia simu wakawa hawapokei,ikabidi niende maana nilikumbuka nilikuwa sijamaliza kufanya editing ya documentary yangu!Nilipofika nikaingia,nikamuona kijana mmoja wa kipindi,nikamuita nikimtania mmekula hela!Hiyo ilikuwa saa 4:45!Nikampigia simu Ruge kutaka kujua kwanini kipindi hakijaenda hewani,nikaenda kufanya kilichinipeleka pale ambapo ilikuwa editing!Nikamaliza na kuondoka!

Maswali:
1.Iweje baada ya kuona shilawadu hawarushi habari ya gwajima ndio ukumbuke una kazi ya kuedit hujaimaliza huko clouds?

2.Muda wa kuingia na kutoka clouds inaonekana kwenye cctv footage inaonesha hukufikisha hata nusu saa ndani ya clouds,je
-Muda ulitoshaje kumuhoji kijana mmoja juu ya kutokuruka kwa kipindi,kupiga simu kwa Ruge na kufanya naye mazungumzo na kuedit kazi yako?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom