Ruge Mutahaba live Jumatatu tarehe 22.05.2017 CLOUDS 360

Ruge Mutahaba live Jumatatu tarehe 22.05.2017 CLOUDS 360

Status
Not open for further replies.
kweli, ndomana tunajiuliza kwann,! daah tuyaache haya mkuu
Baada ya yeye kuonyesha dharau kwa watumishi wa serikali. Nakuheshimu unavyomheshimu mwenzako,kama unamdharau usiyemjua hata mimi sintakuheshimu.
 
Katika haya yanayoendelea na kwa kumsikiliza Bwana Makonda ni vema Ruge na Clouds media waseme ukweli..kuna mambo yana ukakasi kidogo, inaweza ikawa kweli Makonda alivamia na inaweza ikawa ni katika kile ambacho Clouds wanakifanya kila siku katika kutaka maslahi...Ruge sema ukweli tupe CCTV yote tuone ukweli...

Nimalizie tu kuwa CLOUDS TUNAOMBA CCTV YOTE NA MAELEZO YALIYOKAMILIKA..Bila hivyo mtakuwa mnatugombanisha hadhira...waiting for next episode

My conc; Tuweke unafiki pembeni kila kitu kiwekwe peupe mimi sina side katika hili natamani kujua ukweli sio rahisi kuamini hivi vitu anavyoongea Makonda na sio rahisi kumuelewa Ruge na Clouds Media...Twendeni sawa tuache matusi.

RC MAKONDA anasema anayajua mabaya mengi ya Ruge je...hakuna cha kuongea hapo as a clouds?
Mbona ukweli unajulikana Wakuu! Hata confidence ya Ruge imeshuka sana. Ila ajue siku za mwizi ni arobaini tu!
 
Tuwe tuna sikiliza kwamakini tuache kusikiliza kwa mihemko. Makobda alisema alikuwa kwenye mkutano na waziri wa tamisemi. Je ulitaka amsikilize afisa wake aliekwenda bila taarifa au Waziri wake??

Baada ya kumaliza huo mkutano ndio alitoroka.

Mjipange kwelikweli kumsafisha hiyo jamaa.
 
ni sahihi mkuu maana naona kuna vitu vinaongelewa hapa vina ukakasi sana,,najua matusi na kebehi zitakuja ila sasa tunatakiwa kubalance story ...makonda kasema ni vema clouds watupe ushahidi
ushahidi upi na ile CCTV footage imetembea sna na MAria Sarungi kaipin ktk.account ya twitter nenda utaiona.
 
Nachoamini mimi makonda ni mkosefu sio tu kwa inshu ya clouds kuna mengi sana kafanya kinyume, na hayo maneno aliyoongea hakuna ukweli wowote ule anatafuta coverage tu...ingekuwa clouds kuna uozo mbona alikuwa nao bega kwa bega mwanzo? Je huo uozo alikuwa hautambui? Iweje sasa ivi baada ya kumpotezea ndio aseme anajua mabaya mengi ya ruge? Huyu jamaa hakuna kiongozi hapo
 
Marafiki wakigombana chukua jembe ukalime.
Wakipatana chukua kapu ukavune,
 
mkuu hatetewi makonda wala hatetewi Ruge tunataka ukweli as long as na yy kasema clip ya cctv yote itoke y tusipewe yote tuache kushikiwa akili watanzania it might be kweli alivamia o not but wahusika waprove basi tuache utata
Sisi hatujasikiliza hicho kipindi, hembu wewe uliesikiliza tuambie, je amesema hakwenda Clouds usiku ulea au la? kama alikwenda, je alikwenda kufanya nini? na kwanini alikwenda na askari wenye silaha za moto?
 
Mwaga mboga ni butue ugali......................"something fishy here",toeni CCTV footage yote km hakuna tatizo, kuna kitu nimekipata kwa kusikiliza makonda narudia tena "something fishy here"
 
M
Naona katumia miezi kutengeneza uongo. Si angetoka immediate na kuongea kilichotokea.

Utata maelezo ya Makonda:
Nilikuwa nyumbani naangalia shilawadu,ikafika saa 4:30,nikaona hakuna dalili ya kipindi cha yule mwanamke kuruka hewani,nikawapigia simu wakawa hawapokei,ikabidi niende maana nilikumbuka nilikuwa sijamaliza kufanya editing ya documentary yangu!Nilipofika nikaingia,nikamuona kijana mmoja wa kipindi,nikamuita nikimtania mmekula hela!Hiyo ilikuwa saa 4:45!Nikampigia simu Ruge kutaka kujua kwanini kipindi hakijaenda hewani,nikaenda kufanya kilichinipeleka pale ambapo ilikuwa editing!Nikamaliza na kuondoka!

Maswali:
1.Iweje baada ya kuona shilawadu hawarushi habari ya gwajima ndio ukumbuke una kazi ya kuedit hujaimaliza huko clouds?

2.Muda wa kuingia na kutoka clouds inaonekana kwenye cctv footage inaonesha hukufikisha hata nusu saa ndani ya clouds,je
-Muda ulitoshaje kumuhoji kijana mmoja juu ya kutokuruka kwa kipindi,kupiga simu kwa Ruge na kufanya naye mazungumzo na kuedit kazi yako?
 
Akupe CCTV yote wewe ni nani?! Moja ya maazimio ya Jukwaa la Wahariri ilikuwa ni kuwaambia polisi wachunguze kiundani tukio lile!! Sasa kwanini usiwaulize hao polisi ikiwa walichunguza au hapana?!
Hakuna kesi iliyofunguliwa na wahariri wala ruge mwenyewe.Watachunguza nini walalamikaji ni hewa:
 
Wewe upo nchi gani? Kwa walioko TANZANIA wanaelewa kuwa kuna kamati iliundwa na aliyekuwa waziri wa habari Ndg. Nape Nnauye kuchunguza tukio la uvamizi wa Makonda kwenye ofisi za Clouds Media. Upande wa CLOUDS walihojiwa na ile kamati, chakushangaza siku wanakwenda kuhoji upande wa pili haikuwezekana kwani Ndg. Makonda alitoroka kwa kupitia mlango wa nyuma..

NYONGEZA: Baada ya ripoti ile ilivyotoka tu, ilisababisha aliyekuwa waziri wa habari kufukuzwa kazi na nafasi yake kuchukuliwa na mtu mwingine..

MAKONDA ALIVAMIA CLOUDS MEDIA.
 
Katika haya yanayoendelea na kwa kumsikiliza Bwana Makonda ni vema Ruge na Clouds media waseme ukweli..kuna mambo yana ukakasi kidogo, inaweza ikawa kweli Makonda alivamia na inaweza ikawa ni katika kile ambacho Clouds wanakifanya kila siku katika kutaka maslahi...Ruge sema ukweli tupe CCTV yote tuone ukweli...

Nimalizie tu kuwa CLOUDS TUNAOMBA CCTV YOTE NA MAELEZO YALIYOKAMILIKA..Bila hivyo mtakuwa mnatugombanisha hadhira...waiting for next episode

My conc; Tuweke unafiki pembeni kila kitu kiwekwe peupe mimi sina side katika hili natamani kujua ukweli sio rahisi kuamini hivi vitu anavyoongea Makonda na sio rahisi kumuelewa Ruge na Clouds Media...Twendeni sawa tuache matusi.

RC MAKONDA anasema anayajua mabaya mengi ya Ruge je...hakuna cha kuongea hapo as a clouds?

Mkuu wa mkoa anasema anayajua mabaya mengi ya Ruge mbona hajachukua hatua?
By the way sijaona sehemu ambayo Ruge ameongea uongo kila kitu amekubali kuhusu issue ya Gwajima na pia kuvamia studios.
Nlichokia hapo jamaa alikuwa anafanya divide and rule Kati ya clouds na EFM
Wasipo angalia wamekwenda.
 
Mbona ukweli unajulikana Wakuu! Hata confidence ya Ruge imeshuka sana. Ila ajue siku za mwizi ni arobaini tu!
Imeshukaje, au kwa uelewa wako na uwezo wako wa kufikiria nan confidence imeshuka hapo! yeye alikataa kutoka saiv anasema clouds watoke! mbna mnafkiria kwa kutumia kichwa cha nyuma, anyway what we need ni ukwel
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom