RPC Arusha na ulinganishi wa vyeo JWTZ na PT

RPC Arusha na ulinganishi wa vyeo JWTZ na PT

Tafsiri ya Jeshi na majukumu yake Dunia nzima havitofautiani. Na neno linalotumika kuwatambua ni moja tu! Nalo ni Jeshi.

Kwa Tanzania Polisi kuitwa Jeshi ni neno lililozoeleka na linalotumika mara kwa mara kwenye mazungumzo na kusikika masikioni mwa watu kwa njia ambayo linaonekana limetumika pahala sahihi lakini maana yake ni tofauti kabisa na lilivyozoeleka kutumika.

Wanaolinda mipaka au ardhi ya nchi/Dola kwa kutumia nguvu ya silaha dhidi ya wavamizi wa nje hiki kikundi cha jumla ya watu kinaitwa Jeshi. Dunia nzima ndivyo kinatambulika hivyo.

Kikundi cha jumla ya watu waliyopewa mamlaka ya ndani ya Dola/nchi kulinda usalama wa raia na mali zake hiki kikundi kinajulikana ni Polisi.

Polisi ni Polisi na Jeshi ni Jeshi.
Kasome katiba ibara ya 147 ndo utajijua kuwa hujui unachokisema, unaongea maneno ya vijiweni.
 
Wewe mlinzi mguu sawa, nyuma geuka. Kanywe Pepsi nakuja kulipa
 
A wishful thinking!! Polisi ni idara ya kiraia. Kijeshi kuna commissioned na non commissioned. Sasa huwezi kumlinganisha gazetted officer wa polisi na commissioned officer a jeshi. Vyeo vya makamishina hutolewa na rais, ambapo kuanzia luteni usu jwtz. Mwenye nyota moja jw ni kamishna, hiyo ni fact, huwezi kumlinganisha na gazetted officer.
Soma maana ya commissioned officer hii hapa nimekuambatanishia, wala haina maana hiyo mnayoizusha sijui mmeitolea wapi. Ndio maana hata Polisi au Magereza wanapopata nyota moja wanabadilishiwa mikataba yao ya ajira wanatoka katika ajira ya mkataba wanaingia katika ajira ya kudumu. Kwa zamani hata katika mifuko ya hifadhi ya jamii walikuwa wanatoka GEPF wanaingia PSPF. Kuja Rais kufanya hiyo commission ni utaratibu tu. Ndo maana kuna vyeo vikubwa zaidi ya hapo lakini wanavalishwa na ma CO tu au CDF
20190915_105744.jpeg
 
Mr Pianoman huelewi ulichoandika.
Commisioned officer anapewa na Rais wa nchi si vinginevyo.
JWTZ kuanzia 2Lt ni commisionend officer.
Wengine ni other ranks.
Vyeo vya Police ni non commisioned offrs labda makamishena waliopewa na Rais kiutaratibu kiutawala.
Jibu liko wazi, mmeelewa??
Shida yenu sijui ni elimu?? Kwanini hamtaki kujifunza zaidi?? Yaani ulimsikia instructor wako JKT basi ndo hivyo hivyo hamtaki kujifunza tena, yaani mnakera kweli. Soma maana ya commissioned officer hii hapa.
20190915_105744.jpeg
 
Mzee baba usijilishe Upepo na kujitoa ufahamu... Lugha ya kiswahili inaupungufu mkubwa wa Misamiati... Hivyo neo JESHI kwa Convinience likabidi litumike pia kwa hivyo vyombo vingine vya Kiraia...

Nyie ni POLICE FORCE and NOT ARMY/ MILITARY.....
Kama tatizo lilikuwa ni upungufu wa misamiati kwanini wote wamepewa masharti yanayofanana katika katiba, kama wengine raia wengine wanajeshi kwanini masharti ya kikatiba yafanane au ndo upungufu wa misamiati???

Kisheria hakuna linaloshindikana inapotakiwa kutofautisha vitu viwili aidha kwa kiswahili au kwa lugha yoyote ile. Acha maneno ya vijiweni soma vizuri Katiba yako ibara ya 147 na 150 utaelewa.
 
Hivi na wale jamaa wa Suti nyeusi na wao wakoje vyeo vyao wakikutana na polisi na jeshi.?
 
Mtu asie na mafunzo ya kimedani anakuwaje mwanajeshi? [emoji38][emoji38][emoji38][emoji23][emoji23][emoji23][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji377][emoji377][emoji377][emoji2445][emoji2445][emoji2445]
Nikuulize mgambo ni jeshi au sio jeshi?
 
Napenda kuuliza kama kwenye gwaride Mkuu wa majeshi anakuja na Rais kwenye gari moja na gwaride lina polisi zimamoto magereza jkt n.k na hapo IGP anakuwa jukwani anatoa saruti kama vyeo ni sawa kwanini na yeye asiwepo kwenye gari?
 
Hivi na wale jamaa wa Suti nyeusi na wao wakoje vyeo vyao wakikutana na polisi na jeshi.?
wale hawaingiliani na hao askari,lengo ni kuwawekea uhuru katika kushauri jambo.

fikiria afisa mdogo kabisa ameona kiashiria kibaya cha usalama halafu iwepo barrier kuonana na rpc matokeo yake ni hasi.
 
Napenda kuuliza kama kwenye gwaride Mkuu wa majeshi anakuja na Rais kwenye gari moja na gwaride lina polisi zimamoto magereza jkt n.k na hapo IGP anakuwa jukwani anatoa saruti kama vyeo ni sawa kwanini na yeye asiwepo kwenye gari?
mwenye gwalide lote ni la cdf pale,ukitaka kuona hiyo nenda kwenye sherehe za polisi cdf nayeye atakaa jukwaani kimyaa.
 
Mimi Naona, ACP ni sawa na luteni usu kwa kigezo kuwa Commissioned officers wa police ni kuanzia ACP Wakati commissioned officers wa tpdf ni kuanzia luteni usu, SACP ni sawa na luteni, ! ! Kwa wanaolewa zaidi wanisaidie
Maana ya commissioned officer hii hapa
20190915_105744.jpeg
 
Soma maana ya commissioned officer hii hapa nimekuambatanishia, wala haina maana hiyo mnayoizusha sijui mmeitolea wapi. Ndio maana hata Polisi au Magereza wanapopata nyota moja wanabadilishiwa mikataba yao ya ajira wanatoka katika ajira ya mkataba wanaingia katika ajira ya kudumu. Kwa zamani hata katika mifuko ya hifadhi ya jamii walikuwa wanatoka GEPF wanaingia PSPF. Kuja Rais kufanya hiyo commission ni utaratibu tu. Ndo maana kuna vyeo vikubwa zaidi ya hapo lakini wanavalishwa na ma CO tu au CDF View attachment 1208054
Weka na gazetted ndio nikujibu
 
mwenye gwalide lote ni la cdf pale,ukitaka kuona hiyo nenda kwenye sherehe za polisi cdf nayeye atakaa jukwaani kimyaa.
Kwa hiyo kwenye gwaride wale polisi na magereza wanakuwa chini ya CDF? na kama polisi ni jeshi kutokana CDF kuwa mkuu wa majeshi IGP yupo chini ya CDF?
 
Kwa hiyo kwenye gwaride wale polisi na magereza wanakuwa chini ya CDF? na kama polisi ni jeshi kutokana CDF kuwa mkuu wa majeshi IGP yupo chini ya CDF?
Gwaride ni la JESHI na maanisha TPDF.... Ndio maana wakuu wa Guard zote lazima wawe wanajeshi... Hakuna mkuu wa Guard Polisi ama magereza..
 
Kwa hiyo kwenye gwaride wale polisi na magereza wanakuwa chini ya CDF? na kama polisi ni jeshi kutokana CDF kuwa mkuu wa majeshi IGP yupo chini ya CDF?
mkuu wa majeshi~ni mkuu wa majeshi ya ulinzi(anga,maji,ardhi),si na usalama.

mengine yana wakuu wao.

sherehe za kitaifa zenye gwalide zinaandaliwa chini ya jwtz,ndio sababu cdf anasimama kwa wote.

IGP anakuwa chini ya CDF kiprotokali ila si kimajukumu,haripoti kwake.
 
Leo nimecheka Sana mpaka .na ujinga usiokuwa na uelekeo sasa inaenda wiki ya pili .Polisi siyo Mwanajeshi ni RAIA mkakamavu sawa kabisa sasa unataka upigiwe salute ya nini wakati huyo ni Raia tu? haaaaaa.Salute salute salute Hivi hapa Tanzania kilianza nini kati ya TPDF na Tanzania Polisi? .Mimi huwa naona huku mitaani tu kuwa mtu anayeitwa mabregedia jenerali ndiyo wanapewa huduma saws na ACP wa Polisi yaani kuanzia makazi ulinzi mpaka Heshima katika jamii Ila hao Vinyota kimoja na viwili sehemu zote mbili maisha yao yanalingana tu na magumilu aahaa kwa ufupi wanataabika tu .Sasa inabidi Serikali itambue kuwa ACP wa Polisi anatakiwa aishi kama Luteni Usu wa Jwtz maana kinachofanywa sasa ni upendeleo mbaya sana.Haaaaaaaaaaaaaaa
Upendeleo katika nini...?
 
Ukweli ndo huo humu ndani wajinga wengi wanaongea wasichokijua, majeshi yetu yote yanaundwa na katiba moja. Kwahiyo yote yapo sawa yanatofautiana majukumu tu, na tange(seniority).
Huyo meja alifanya kosa kubwa sana kuwai kutokea katika historia ya ulimwengu
 
Aisee vyeo vya Kijeshi pamoja na kufundishwa Jeshini nilishindwa kabisa kuvikariri...[emoji23][emoji23]
Dogo umesahau uwanja wa damu tulikaa chini ya mti koplo Daniel jlokta alitufundisha hivyo vyeo
 
Dogo umesahau uwanja wa damu tulikaa chini ya mti koplo Daniel jlokta alitufundisha hivyo vyeo
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Wee jamaa Mgambo mojaa... asieee sema wame alikuwa akija na yale mabanzi yakee...
 
Back
Top Bottom