RPC Arusha na ulinganishi wa vyeo JWTZ na PT

RPC Arusha na ulinganishi wa vyeo JWTZ na PT

Mwanajeshi kuua ni suala la mtu binafsi halihusiani na kulichafua jeshi zima kama unavyotaka kuaminisha watu.

Utovu wa utu na unyama hauegemei kada ya mtu ni sawa na kuongelea mchawi.

Unapokaa nyuma ya keyboard usijisahau sana na kuanza kupakaza chuki zako binafsi kwa taasisi zenye kuheshimika na taifa.

Raia yeyote wa Tz akiwemo mwanajeshi, akitenda jinai atawajibika kwa makosa yake mwenyewe binafsi na si taasisi nzima.

Hapa mada imeanzishwa kupima ulinganifu wa vyeo, badala yake wewe unaigeuza na kuipeleka kwenye mauaji na chuki zako, what for?
Uko sawa aharishe kuku asingiziwe bata kisa kawaida bata huwa anaharishaga siku zote hata kama haumwi
 
Nimekuunga mkono Mkuu....Watu wanafikiri Brigdea Jeneral ni cheo kikubwa sana jeshini kumbe cha kawaida tu ..
Nani kakuambia ni cheo cha kawaida.Umeshawahi pitia angalau JKT.
Ukijua tu maana ya neno brigade utajua sio cheo cha ki sport.
Ngoja nikupe flow chart ya mchoro
Askari mmoja-Section-Platoon-kombania-Kikosi-Battalion-Brigade
askari wakiwa labda tisa inakuwa ni section
section zikiwa angalau 9 zinakuwa platoon
platoon zikiwa mbili au tatu inakuwa ni kombania
Kombania zikiwa sita hadi kumi inakuwa ni kikosi
vikosi vikiwa vingi inakuwa na battalioni
Battalion juu yake ni brigade
Unaposikia ni mkuu wa brigade ya mfano mashariki unaweza kuta anaongoza Dar,Tanga hadi Mtwara
Ukisikia brigade ya kati unaweza kuta ni Tabora,dodoma,
Brigadier ni mtu mkubwa sio wa ki sport hata wakati wa vita vya Kagera kina Musuguri,Mayunga,Marwa,Kombe,Kiwelu,Kimario,Mwita Ernest Kiaro.John Butler Walden walikuwa ni ma brigadier.
Sasa katika medani za kivita ni hivyo ila Jeshini kuna taaluma zingine.
Ukiwa daktari wa jeshi lakini brigadier maana yake kwa taaluma yako hiyo unakuwa unaongoza brigade kwa huo udaktari wako
 
Nani kakuambia ni cheo cha kawaida.Umeshawahi pitia angalau JKT.
Ukijua tu maana ya neno brigade utajua sio cheo cha ki sport.
Ngoja nikupe flow chart ya mchoro
Askari mmoja-Section-Platoon-kombania-Kikosi-Battalion-Brigade
askari wakiwa labda tisa inakuwa ni section
section zikiwa angalau 9 zinakuwa platoon
platoon zikiwa mbili au tatu inakuwa ni kombania
Kombania zikiwa sita hadi kumi inakuwa ni kikosi
vikosi vikiwa vingi inakuwa na battalioni
Battalion juu yake ni brigade
Unaposikia ni mkuu wa brigade ya mfano mashariki unaweza kuta anaongoza Dar,Tanga hadi Mtwara
Ukisikia brigade ya kati unaweza kuta ni Tabora,dodoma,
Brigadier ni mtu mkubwa sio wa ki sport hata wakati wa vita vya Kagera kina Musuguri,Mayunga,Marwa,Kombe,Kiwelu walikuwa ni ma brigadier.
Sasa katika medani za kivita ni hivyo ila Jeshini kuna taaluma zingine.
Ukiwa daktari wa jeshi lakini brigadier maana yake kwa taaluma yako hiyo unakuwa unaongoza brigade kwa huo udaktari wako
Umeeleza vyema chief
 
Umeeleza vyema chief
Tuko pamoja Hip hop Uchwara.
Mimi sio mwanajeshi ila kama kwa mtu aliyepitia JKT kwa miaka yetu ile ya 1986 haya mambo lazima uwe unayajua.Unakuta mtu anakurupuka tu hata mgambo hajawahi kwenda anaelezea asichokijua na ana underrate nafasi za watu.
Brigadiers hata raisi anawajua na nadhani hawezi hata toka nje ya nchi bila kutoa taarifa.
Nakumbuka mwaka 1986 nilikuwa Ruvu JKT mkuu wa kikosi alikuwa ni Luteni Kanali Meena.Nilipohamia Maramba Tanga mkuu wa kikosi akawa Major Urio.
Unaona sasa cheo cha brigadier kilivyo? namanisha kiko juu mno
 
Back
Top Bottom