Mnunuzi Mkubwa wa Makaa ya Mawe Kenya ni Bambuli Cement Mombasa na Athi river Nairobi.
Monthly consumption yao ya Makaa ya Mawe ni ndogo sana kiasi cha kutoa meli Mtwara uipeleke Mombasa.
Kumbuka Bandari iko Mtwara Makaa yapo Songea -500-600km, loading and offloading, ukifika Mombasa port uanze kuoffload na kupakia kwenye malori tena, nk.
Bado Mombasa port waandae facility ya kushushia coal nk.
Hizi hesabu zilishafanyika, ikaoekana sio economical, ndio maana unaona hayo malori yanatembea kwenda MSA na NRB.
aim ya kila operation ni kurun at low cost, sidhani kama kungekuwa na opportunity ya kupunguza cost basi Bamburi na Athi river wasingeitumia.
Kumbuka pia Mombasa port hakuna terminal ya makaa maana yake lazima ijengwe, sasa ni economic kuijenga kwa kupokea meli ya 5000tone monthly?
SA large volume ya Coal inasafirishwa kutoka Mpulanga to Richard bay kwenye wagons kwa ajili ya exportation, pale Richard bay port kuna coal terminal maarufu inaitwa RBCT. Lengo ilikuwa kuondoa cost za malori maana volume ni kubwa na production ni kubwa na zipo dedicated berth pale Richard bay kwa ajili ya Coal tu maana mzigo ni mkubwa.
Kiasi kikubwa cha Coal ya Tanzania ni export nje ya EA na largest producer wa coal ni Ruvuma coal, akifuatiwa kwa mbali na Jitegemee, RA- Taifa mining bado wanasuasua kwenye production.
Moja ya changamoto ya coal ya Tanzania ni market kwasababu ya high moisture contents.
Kwasasa Ulaya wanastock kiasi kikubwa cha Coal Kwa ajili ya power generation incase Russia akizingua, supplier wao mkubwa kutoka Tanzania ni Ruvuma Coal.
ndani ya mitaa ya Khartoum Sudan