Kuna habari kwamba, baadhi ya Maaskofu wanakutana Dar es Salaam katika ukumbi wa Travatine Hotel Magomeni, kujadili na kutoa tamko kuhusu Rostam kwenda kujisafisha katika Kanisa la KKKT, Kinondoni. Kwa mwenye taarifa kamili atupatie tafadhali. Nimetumiwa sms na mtu mmoja aliyeko Dar, walioko Dar jujulisheni
Nimejulishwa kwamba wanakutana pale pale Kanisani KKKT Kinondoni, inawezekana pia wakakutana katika ukumbi mwingine wowote, lakini la msingi ni kwamba wanasema ni kweli kuna kitu kama hicho
Lakini hawa watu wa kanisa si walimwalika wenyewe au alijipeleka? Kuuma na kupuliza kutawaponza, inawabidi waamue haya mambo ya vuguvugu yatawasuta!
ni Dhahiri Rostam Kuhusishwa Na Kashfa Ya Richmond Ambayo Imekuwa Gumzo La Kila Siku Nchini Ndicho Chanzo Na Sababu Ya Yeye Kualikwa Kanisani Hapo. Miaka Yote Rostam Yupo Nchini Humu Kwa Nini Asialikwe Anaalikwa Sasa? Ni Dhahiri Miongoni Mwa Waumini Hao Kuna Mtu Ambaye Anafahamiana Na Rostam Na Kwa Pamoja Wakala Njama Kuhakikisha Anaalikwa Kanisani Hapo Ili Aweze Kwenda Kutoa Vijisenti Vyake Na Kupata Ukumbi Wa Kuzungumza Na Kuwapiga Wananchi Wanaohoji Juu Ya Ufisadi. kitendo Cha Rostam Kwenda Kanisani Na Kutoa Kauli Alizotoa Ni Kulidhalilisha Kanisa Lililomualika Na Kkkt Kwa Ujumla.
Kwa Wale Waliangalia Televisheni Na Kumuona Rostam Akizungumza Watakubaliana Kwamba Uso Wake Ulionyesha Kutahayari Wakati Akitamka Maneno Ya Kuwapiga Vijembe Wanaoshutumu Ufisadi Na Kuzusha Mambo Ya Uchawi! Cha Kusikitisha Sana Ni Kwamba Baadhi Ya Waumini Walimshangilia Kwa Makofi Na Vigelegele! Ama Kweli Umaskini Na Hali Ngumu Za Maisha Vinatupeleka Pabaya. hivi Wananchi Wangelikuwa Na Maisha Bora Na Makanisa Hayo Kuweza Kusimama Imara Kwa Kujitegemea Kwa Kila Jambo Kutokana Na Sadaka Za Waumini Wao, Rostam Angelipata Wapi Ukumbi Wa Kwenda Kulikejeli Kanisa?
Wanamjadili Rostam ili wamrudishie sadaka yake?
Mama napendekeza ile pesa ya RA tuiite hongo au rushwa maana haikuambatana na maneno matakatifu bali maneno ya kidunia au ya mtu wa mataifa.
Kwa kuwa alizunguka mbuyu basi zile pesa ni najisi kwa hiyo hazifai hata kazi ya ufalme wa Mungu,wamrudishie zote