Rostam aibukia kanisani!

Rostam aibukia kanisani!

Wakuu wangu, mabibi na mabwana,

RA kama nyinyi ana source zake za kupata hela kihalali. Ana/alikuwa na share Voda, kuna Caspian etc. Sasa sielewi kama kila anachotaka kutoa nyinyi mnasema ni ufisadi.

Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Mmezidi kulaumu na kuzomea utafikiri wamachinga.

Fikirieni kidogo mtaelewa kuwa anazo hela halali pia.

Fair Player ni wewe Pain Killer! Kweli Rostam ana mkono mrefu. Kutoka kufilisi viwanda vya ngozi, kuwekeza caspian-kubeba tenda za kiserikali kwenye ukandarasi wa migodi yote mikubwa mpaka ujenzi wa yale majengo pacha ya BOT yaliyokuzwa bei kupindukia. Kutoka Fedha za EPA kupitia Kagoda na mashirika mengine mpaka kuwaleta kwa Ubia Dowans. Kutoka Mweka hazina wa CCM mpaka kuweza kupenyeza mkono wake hapa Jamii Forums. Ama kweli. Fedha sabuni ya roho. Mwenye fedha sio mwenzako. Nimefanya kazi karibu sana na cycles za Rostam, hili la kanisani nililisema kabla hata ya yeye kwenda kanisani. Suala ilikuwa ni kanisa gani tu, sasa KKKT imeingia mkenge. Alijaribu katoliki parokia moja akagonga mwanga. Tuendelee tu kuwa na utumishi uliotukuka kwa fisadi, he is our hero for now. Mfadhili wetu CCM, mhisani wetu mtandao. Mdau wa kweli katika maendeleo ya Taifa

PM
 
Wananchi mkipewa feza msiikatae ni haki kabisa ,yaani mnaichukuwa kwa ndelemo na shelehe ,kisha mishatulia mnamueleza mheshimiwa kwamba msimamo bado upo palepale ,mafisadi lazima wakasemee mahakamani nani aliwasaidia kutorosha feza.Hakuna kulainika ,feza anayoitoa inatafunwa na kizimbani anapandishwa mtu.
 
Fair Player ni wewe Pain Killer! Kweli Rostam ana mkono mrefu. Kutoka kufilisi viwanda vya ngozi, kuwekeza caspian-kubeba tenda za kiserikali kwenye ukandarasi wa migodi yote mikubwa mpaka ujenzi wa yale majengo pacha ya BOT yaliyokuzwa bei kupindukia. Kutoka Fedha za EPA kupitia Kagoda na mashirika mengine mpaka kuwaleta kwa Ubia Dowans. Kutoka Mweka hazina wa CCM mpaka kuweza kupenyeza mkono wake hapa Jamii Forums. Ama kweli. Fedha sabuni ya roho. Mwenye fedha sio mwenzako. Nimefanya kazi karibu sana na cycles za Rostam, hili la kanisani nililisema kabla hata ya yeye kwenda kanisani. Suala ilikuwa ni kanisa gani tu, sasa KKKT imeingia mkenge. Alijaribu katoliki parokia moja akagonga mwanga. Tuendelee tu kuwa na utumishi uliotukuka kwa fisadi, he is our hero for now. Mfadhili wetu CCM, mhisani wetu mtandao. Mdau wa kweli katika maendeleo ya Taifa

PM

PM, strong accusations, very strong mzee. Kumbuka nimeuliza swali kuwa kati ya EPA na Caspian ipi ilianza. Sijajibiwa napewa ngonjera zisizo na kichwa wala miguu.

Na kama kawaida yenu mkishaishiwa na hoja mnaingia personal. Unataka ID yangu sijui ya nini???!!!. Hapa tunajidiliana bila names calling, issue ipo wapi?, jibu maswali na kuwa specific na sio kama MAMA anavyo jumuisha mambo.

Kwa wananielewa toka enzi za BCS mimi sio wa kununuliwa na nina aamini Rostum ana uwezo wa kuja mwenyewe humu kuandika, why amnunue mtu.

Na kwa faida yako mimi sio Painkiller na wala sina umoderator wala u admin hapa JF. Ni mTZ mwenye uchungu na nchi hii kama wewe ila tatizo mimi nina analyse mambo na kufikiri kabla sijaandika. Hiyo ndo tofauti yangu na wewe!
 
Na kwa taarifa yako. RA ana mkono mrefu kwa wenye NJAA au wanaoendekeza njaa na sio mimi.
 
Rostam aliangukia kanisa

na Martin Malera
Tanzania Daima~Sauti ya Watu

MBUNGE wa Igunga, Rostam Aziz (CCM), amesema taifa liko kwenye wakati mgumu kisiasa na kijamii, hivyo amewaomba wananchi watumie makanisa kulirejesha katika mstari ulio sahihi.

Rostam alitoa kauli hiyo jana katika sherehe ya uzinduzi wa albamu ya kwaya ya Amkeni ya Kanisa la Kilutheri Tanzania, iliyofanyika katika viwanja vya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Usharika wa Kinondoni, Dar es Salaam, ambapo alikuwa mgeni rasmi.

Huku akishangiliwa na umati wa waumini waliohudhuria uzinduzi huo, mbunge huyo anayeandamwa na jinamizi la ufisadi, alisema waumini wa dini hawamtuhumu mtu, hawamshutumu, hawapendi wenye wivu na wenye chuki bali wanapenda haki.

Akionekana kuwashangaza waumini kutokana na maneno yake ya ucha Mungu, Rostam alisema ana watoto watatu ambao aliahidi kanisani hapo kwamba anataka awalee katika misingi ya dini ili wawe wananchi bora na waadilifu hapo baadaye.

"Nawashukuru kwa kuamua kunialika kuwa mgeni rasmi leo, hii ni ishara kwamba mmeamua kupuuza viji-maneno na upuuzi wa vijiweni. Nafurahi kuwa miongoni mwenu…hamtuhumu, hamshutumu, hampendi wenye wivu na wenye chuki, mnapenda haki. Ninao watoto watatu na nataka niwalee katika misingi hii,'' alisema Rostam huku akishangiliwa na umati wa watu walioshiriki hafla hiyo.
Alisema hivi sasa nchini, watu wameanzisha tabia ya kuchukiana mpaka kuzushiana uchawi na kuombeana vifo, na kusisitiza kuwa wananchi watumie makanisa kukemea vitu hivi.

Ingawa katika kauli hiyo hakutaja mtu, lakini mbunge huyo ambaye hajawahi kupata mpinzani katika jimbo lake, alikuwa akizungumzia tukio la hivi karibuni bungeni, ambako Mbunge wa Bariadi Mashariki, Andrew Chenge (CCM) na ofisa mmoja mwandamizi wa Bunge, walituhumiwa kuweka vitu aina fulani ya uchawi au sumu ya kisasa ndani ya ukumbi wa Bunge.

Hata hivyo, suala hilo hadi sasa bado linashughulikiwa na vyombo vya dola, ambako Spika wa Bunge, Samwel Sitta, alikabidhi mikanda inayodaiwa kuonyesha picha za wahusika walipokuwa ‘wakiwanga' bungeni.

Rostam aliendelea kuwaambia waumini hao kuwa mbali ya matatizo ya kisiasa, pia kuna matatizo ya kijamii kama vile ndoa kuvunjika kila kukicha, watoto wa mitaani kuongezeka, madanguro na dawa za kulevya kukithiri, ambayo alisema yanasababishwa na mmomonyoko wa maadili, hivyo kusisitiza wito wake wa kutaka makanisa kuiombea nchi ili kurejesha katika hali ya matumaini, upendo na amani.

Katika hafla hiyo, Rostam alitoa mchango wa sh milioni tano kuchangia seti za vyombo vya muziki kwa kwaya ya Amkeni pamoja na jenereta yenye thamani ya sh milioni 2.6.

Katika siku za hivi karibuni, Rostam amekuwa akiandamwa na jinamizi la ufisadi kiasi cha baadhi ya wabunge na wananchi kutaka achukuliwe hatua za kisheria.

Wakati wa mkutano wa 10 wa Bunge, baadhi ya wabunge walitaka Rostam awajibishwe kutokana na kutajwa kuwa ndiye mmiliki wa Kampuni ya Richmond inayodaiwa kuihadaa serikali katika makubaliano ya kuzalisha umeme wa dharura.

Wakichangia ripoti ya Kamati Teule ya Bunge juu ya mkataba wa kuzalisha umeme wa dharura wa Richmond bungeni, Februari mwaka huu, baadhi ya wabunge walisema kitendo cha mbunge huyo kugoma kutoa ushahidi katika kamati hiyo iliyoongozwa na Dk. Harrison Mwakyembe kuwa ilikuwa ni dharau kwa Bunge na kwa Spika aliyeiunda.

"Hatuwezi kuhoji kwa sasa kwamba Richmond ni ya akina nani. Ukweli uko wazi kuwa ni wale walioshinikiza kampuni hiyo ipewe mkataba," alisema Mbunge wa Sikonge, Juma Mkumba (CCM).

Alisema Rostam katajwa kuwa na uhusiano na Richmond na pia anatajwa kuwa na uhusiano na Kampuni ya Dowans iliyokuwa inaendesha shughuli za Richmond kabla ya serikali hivi karibuni kuamua kuvunja mkataba wake.

Mbunge mwingine ambaye aliwahi kuchangia kutaka kuwajibishwa kwa Rostam ni Godfrey Zambi (CCM), Mbozi Mashariki ambaye alisema ni vyema achukuliwe hatua, kwa vile ni kiongozi wa CCM na yuko kwenye Halmashauri na Kamati Kuu ya chama hicho.

Alisema kitendo cha Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salva Rweyemamu, kunukuliwa akimtaja Rostam kuwa na uhusiano na Richmond ni ushahidi wa kutosha.

Wakati wabunge wakitoa shutuma hizo, Rostam alijiandaa kujibu bungeni, lakini katika hali isiyo ya kawaida, Spika wa Bunge, Samwel Sitta aliikataa hoja yake kwa kile kilichoelezwa kuwa kama angetoa maelezo hayo ni wazi kwamba angelitikisa Bunge.

Inadaiwa kuwa Rostam baadaye aliamua kuyapeleka maelezo yake kwenye Kamati ya CCM ambako yalijadiliwa na kumzuia mbunge huyo wa Igunga kuyasema bungeni.

Hivi karibuni, Rostam ambaye kwa mara mbili mfululizo amekuwa akipita bila kupingwa kwenye jimbo lake la uchaguzi, alitangaza kutowania tena ubunge, hali ambayo inaweza kuwa na uhusiano na tuhuma zinazomwandama kuhusu ufisadi.
 
Wananchi hawataki kutumia makanisa wala misikiti au mahekalu wananchi wanataka kuona sheria inafuata mkondo wake haraka iwezekanavyo ,nchi hii inaongozwa na sheria japo zinakiukwa lakini kwa hili tunataka kuona sheria inakuwa juu ya kila mtu aliehusika na ufisadi ,mambo ya kuombeana Mungu hakuna labda wahusika na wanafamilia wao ndio watakaoombeana au kwenda kwa magagula.
Hapa haombewi mtu ,hala fu hili la kutishana bora muliweke pembeni mambo ya kusema Taifa linapita kwenye mkondo wa hatari sio neno jepesi kulitumia ila wahusika itakuwa mnajua namna mlivyojipanga ikiwa mtachukuliwa hatua za kisheria, sasa tunataka sheria ichukue mkondo wake na tuone hilo mlilolipanga kama litafua dafu mbele ya wananchi wenye uchungu na hasira kwa nchi yao.
 
PM, strong accusations, very strong mzee. Kumbuka nimeuliza swali kuwa kati ya EPA na Caspian ipi ilianza. Sijajibiwa napewa ngonjera zisizo na kichwa wala miguu.

Na kama kawaida yenu mkishaishiwa na hoja mnaingia personal. Unataka ID yangu sijui ya nini???!!!. Hapa tunajidiliana bila names calling, issue ipo wapi?, jibu maswali na kuwa specific na sio kama MAMA anavyo jumuisha mambo.

Kwa wananielewa toka enzi za BCS mimi sio wa kununuliwa na nina aamini Rostum ana uwezo wa kuja mwenyewe humu kuandika, why amnunue mtu.

Na kwa faida yako mimi sio Painkiller na wala sina umoderator wala u admin hapa JF. Ni mTZ mwenye uchungu na nchi hii kama wewe ila tatizo mimi nina analyse mambo na kufikiri kabla sijaandika. Hiyo ndo tofauti yangu na wewe!

Kwani nani kasema we ni moderator? Nimesema painkiller, mpungazi wa maumivu ya ufisadi.

Rostam alianza kabla ya EPA; kumbuka kadhia za nyuma ya kufilisiwa kwa viwanda vya ngozi na yale mambo ya Japanese support. Hayo ndiyo yaliyopanua mtaji wake kwenye Caspian akahamia kwenye dili kubwa zaidi za makampuni ya madini na hata ujenzi wa barabara toka miaka mingi na majengo makubwa ikiwemo lile la BOT la hivi karibuni. Tenda nyingi zikiwa zinapatikana chini ya carpet na zikipewa fedha nyingi zaidi. Matokeo ya kukua kwa mtaji kwa njia hizo ndizo zilizopelekea Caspian kuwa wamiliki wa Vodacom Tanzania kwa kuwa na hisa nyingi. Zake na zile alizonunua toka kwa Noni. Kwa hiyo hayo ya Kagoda na EPA na yale ya Richmond na EPA ni madili ya karibuni tu ya kuendelea kutunisha mfuko. Na kumfanya aweze kufanya vizuri kazi ya Mungu ya kutoa misaada makanisani. Njia yake ni karibu sawa na njia ya Yusuph Manji.

PM
 
Wakuu wangu, mabibi na mabwana,

RA kama nyinyi ana source zake za kupata hela kihalali. Ana/alikuwa na share Voda, kuna Caspian etc. Sasa sielewi kama kila anachotaka kutoa nyinyi mnasema ni ufisadi.

Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Mmezidi kulaumu na kuzomea utafikiri wamachinga.

Fikirieni kidogo mtaelewa kuwa anazo hela halali pia.

Huyu ndiye fairplayer, mwenye kujisifu anafanya analysis na kutafakari kwa makini kabla ya kuandika. Huyu ndiye fairplayer anayewaita watanzania wenzake kuwa wamezoea kuzomea kama wamachinga. Huyu ndiye fairplayer, anayetangaza kwa sources za fedha za rostam ni halali. Huyu ndiye fair player anayefanya analyis na tafakari kabla kuongea. Huyu ndiye fairplayer, anayelalamika kwa kuitwa pain killer ya ufisadi!

PM
 
huyo Rostam na yeye kilichomfanya kujisafisha kanisani ni nini?kaalikwa kwenye harambee halafu yeye akaingiza mambo yake!watu wengine wanaudhi kweli
 
Asante PM,

Nadhani niliteleza kama kweli ulimaanisha paikiller ya mafisadi. Mi nilidhani ulimaanisha kingine, kwasababu kuna painkiller ambaye ni moderator humu. Asante.

Tatizo lililopo humu na kwa wa Tanzania wote kwa ujumla ni kuwa ukiwa unafanya biashara na ikatokea ukaDHANIWA kuwa umehusika basi hata biashara zako halali zote nazo ni UFISADI.

PM, Tutoke nje ya box, nayajua yote hayo ya ngozi n.k. Tuambie kama anaiba MBONA HAFIKISHWI MAHAKAMANI?. MBONA BADO NI MJUMBE CC YA CCM?.

Ina maana watu woote hao hawana AKILI ya kumwajibisha huyu bwana?
 
Wakati mnabishana kuhusu Zaka na usafi wake na Rostam kuwa fisadi, jimbo la Kinondoni taratibu linarudi mikononi mwa CCM na Peter Kabisa atakuwa mbunge 2010!

Kampeni imeanza, vita dhidi ya Ufisadi havitaingoa CCM. Rostam kaalikwa kanisani, kashangiliwa, katukuzwa na waumini waishio mkoa wa Dar ambao kila siku wanasoma nyeti na upekuzi kuhusu nani fisadi.

Jiulizeni, what wet wrong, kama Kinondoni wanamshangilia, itakuwa Maswa, Mpanda, Manyoni, Hai na Kaskazini Unguja?

Wapinzani, tafuteni hoja mpya kuing'oa CCM. Karata ya ufisadi haifai tena!
 
Kishoka,

Napenda watu kama wewe wanavyoona mambo. JF kweli bab kubwa. Tatizo la wengi ni kutotumia sensi ya sita kung'amua vitu.

Wapinzani kuwaondoa CCM madarakani ni ndoto!
 
FairPlay mbona unawapeleka watu mchaka mchaka kiasi hicho!!! Tanzania mtu msafi ni mtu maskini!
 
EWabongo wanapenda wawe maskini.

Ukiwa tajiri umeharibu sana ndo tatizo. Hata biashara ukifanya ni za kifisadi sijui wanatakaje!.

Ndo maana hatuendelei mshkaji. Wanaishia kudiscuss watu badala ya kuleta solution.
 
EWabongo wanapenda wawe maskini.

Ukiwa tajiri umeharibu sana ndo tatizo. Hata biashara ukifanya ni za kifisadi sijui wanatakaje!.

Ndo maana hatuendelei mshkaji. Wanaishia kudiscuss watu badala ya kuleta solution.

Hakuna Mtanzania anayependa umaskini! lakini utajiri tunaoutaka ni ule uliopatikana kihalali bila kufanya ufisadi au wizi kama uliofanywa EPA, Richmond na Kiwira ambapo Mkapa aliamua kuiba mchana kweupe.
 
Wakati mnabishana kuhusu Zaka na usafi wake na Rostam kuwa fisadi, jimbo la Kinondoni taratibu linarudi mikononi mwa CCM na Peter Kabisa atakuwa mbunge 2010!

Kampeni imeanza, vita dhidi ya Ufisadi havitaingoa CCM. Rostam kaalikwa kanisani, kashangiliwa, katukuzwa na waumini waishio mkoa wa Dar ambao kila siku wanasoma nyeti na upekuzi kuhusu nani fisadi.

Jiulizeni, what wet wrong, kama Kinondoni wanamshangilia, itakuwa Maswa, Mpanda, Manyoni, Hai na Kaskazini Unguja?

Wapinzani, tafuteni hoja mpya kuing'oa CCM. Karata ya ufisadi haifai tena!

Rev, tatizo la Wapinzani hawataki kabisa kusikia na kuufanyia kazi ushauri wa bure wanaopewa na Watanzania kwamba waunde chama kimoja chenye nguvu ili kupambana na CCM. Wameshashiriki katima chaguzu tatu zilizopita 1995, 2000 na 2005 pamoja na kuwa matokeo yao si ya kuridhisha hawajiulizi kulikoni na hawatoi sababu zozote za msingi za kutofuata ushauri tunaowapa Watanzania.
 
FairPlay mbona unawapeleka watu mchaka mchaka kiasi hicho!!! Tanzania mtu msafi ni mtu maskini!

Ni bora kuwa maskini, kuliko tajiri aliyeupata utajiri huo kwa kufanya ufisadi, ujambazi na kuandika mikataba bomu kama ule wa kununua rada ambapo mhindi na mafisadi walijipatia shilingi bilioni 12
 
Rostam aliangukia kanisa

na Martin Malera
Tanzania Daima~Sauti ya Watu

MBUNGE wa Igunga, Rostam Aziz (CCM), amesema taifa liko kwenye wakati mgumu kisiasa na kijamii, hivyo amewaomba wananchi watumie makanisa kulirejesha katika mstari ulio sahihi.

Rostam alitoa kauli hiyo jana katika sherehe ya uzinduzi wa albamu ya kwaya ya Amkeni ya Kanisa la Kilutheri Tanzania, iliyofanyika katika viwanja vya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Usharika wa Kinondoni, Dar es Salaam, ambapo alikuwa mgeni rasmi.

Huku akishangiliwa na umati wa waumini waliohudhuria uzinduzi huo, mbunge huyo anayeandamwa na jinamizi la ufisadi, alisema waumini wa dini hawamtuhumu mtu, hawamshutumu, hawapendi wenye wivu na wenye chuki bali wanapenda haki.

Akionekana kuwashangaza waumini kutokana na maneno yake ya ucha Mungu, Rostam alisema ana watoto watatu ambao aliahidi kanisani hapo kwamba anataka awalee katika misingi ya dini ili wawe wananchi bora na waadilifu hapo baadaye.

“Nawashukuru kwa kuamua kunialika kuwa mgeni rasmi leo, hii ni ishara kwamba mmeamua kupuuza viji-maneno na upuuzi wa vijiweni. Nafurahi kuwa miongoni mwenu…hamtuhumu, hamshutumu, hampendi wenye wivu na wenye chuki, mnapenda haki. Ninao watoto watatu na nataka niwalee katika misingi hii,’’ alisema Rostam huku akishangiliwa na umati wa watu walioshiriki hafla hiyo.
Alisema hivi sasa nchini, watu wameanzisha tabia ya kuchukiana mpaka kuzushiana uchawi na kuombeana vifo, na kusisitiza kuwa wananchi watumie makanisa kukemea vitu hivi.

Ingawa katika kauli hiyo hakutaja mtu, lakini mbunge huyo ambaye hajawahi kupata mpinzani katika jimbo lake, alikuwa akizungumzia tukio la hivi karibuni bungeni, ambako Mbunge wa Bariadi Mashariki, Andrew Chenge (CCM) na ofisa mmoja mwandamizi wa Bunge, walituhumiwa kuweka vitu aina fulani ya uchawi au sumu ya kisasa ndani ya ukumbi wa Bunge.

Hata hivyo, suala hilo hadi sasa bado linashughulikiwa na vyombo vya dola, ambako Spika wa Bunge, Samwel Sitta, alikabidhi mikanda inayodaiwa kuonyesha picha za wahusika walipokuwa ‘wakiwanga’ bungeni.

Rostam aliendelea kuwaambia waumini hao kuwa mbali ya matatizo ya kisiasa, pia kuna matatizo ya kijamii kama vile ndoa kuvunjika kila kukicha, watoto wa mitaani kuongezeka, madanguro na dawa za kulevya kukithiri, ambayo alisema yanasababishwa na mmomonyoko wa maadili, hivyo kusisitiza wito wake wa kutaka makanisa kuiombea nchi ili kurejesha katika hali ya matumaini, upendo na amani.

Katika hafla hiyo, Rostam alitoa mchango wa sh milioni tano kuchangia seti za vyombo vya muziki kwa kwaya ya Amkeni pamoja na jenereta yenye thamani ya sh milioni 2.6.

Katika siku za hivi karibuni, Rostam amekuwa akiandamwa na jinamizi la ufisadi kiasi cha baadhi ya wabunge na wananchi kutaka achukuliwe hatua za kisheria.

Wakati wa mkutano wa 10 wa Bunge, baadhi ya wabunge walitaka Rostam awajibishwe kutokana na kutajwa kuwa ndiye mmiliki wa Kampuni ya Richmond inayodaiwa kuihadaa serikali katika makubaliano ya kuzalisha umeme wa dharura.

Wakichangia ripoti ya Kamati Teule ya Bunge juu ya mkataba wa kuzalisha umeme wa dharura wa Richmond bungeni, Februari mwaka huu, baadhi ya wabunge walisema kitendo cha mbunge huyo kugoma kutoa ushahidi katika kamati hiyo iliyoongozwa na Dk. Harrison Mwakyembe kuwa ilikuwa ni dharau kwa Bunge na kwa Spika aliyeiunda.

“Hatuwezi kuhoji kwa sasa kwamba Richmond ni ya akina nani. Ukweli uko wazi kuwa ni wale walioshinikiza kampuni hiyo ipewe mkataba,” alisema Mbunge wa Sikonge, Juma Mkumba (CCM).

Alisema Rostam katajwa kuwa na uhusiano na Richmond na pia anatajwa kuwa na uhusiano na Kampuni ya Dowans iliyokuwa inaendesha shughuli za Richmond kabla ya serikali hivi karibuni kuamua kuvunja mkataba wake.

Mbunge mwingine ambaye aliwahi kuchangia kutaka kuwajibishwa kwa Rostam ni Godfrey Zambi (CCM), Mbozi Mashariki ambaye alisema ni vyema achukuliwe hatua, kwa vile ni kiongozi wa CCM na yuko kwenye Halmashauri na Kamati Kuu ya chama hicho.

Alisema kitendo cha Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salva Rweyemamu, kunukuliwa akimtaja Rostam kuwa na uhusiano na Richmond ni ushahidi wa kutosha.

Wakati wabunge wakitoa shutuma hizo, Rostam alijiandaa kujibu bungeni, lakini katika hali isiyo ya kawaida, Spika wa Bunge, Samwel Sitta aliikataa hoja yake kwa kile kilichoelezwa kuwa kama angetoa maelezo hayo ni wazi kwamba angelitikisa Bunge.

Inadaiwa kuwa Rostam baadaye aliamua kuyapeleka maelezo yake kwenye Kamati ya CCM ambako yalijadiliwa na kumzuia mbunge huyo wa Igunga kuyasema bungeni.

Hivi karibuni, Rostam ambaye kwa mara mbili mfululizo amekuwa akipita bila kupingwa kwenye jimbo lake la uchaguzi, alitangaza kutowania tena ubunge, hali ambayo inaweza kuwa na uhusiano na tuhuma zinazomwandama kuhusu ufisadi.

Halafu huyu jamaa kweli ana mazarau..!

Yani anawapa hao masikini wenye njaa genereta na wakati kesha wa Richmond kinyama!

Halafu na hiyo kwaya nayo si amewapa pesa ili waendelee kuwaliwaza masikini kwa maneno ya kujifanya ni watakatifu na kumbe na wao ni mafisadi!

Wamejiingiza kwenye mtandao kwa kuwa voluntary slaves...!

AIBU TUPU!

Mambo yao ya ccm ambayo sitta alikataa yasizungumziwe bungeni pale RA alipodai ana utetezi wake mbele za bunge..yame geuzwa kuwa ya kisiasa na kupelekwa kanisani kwa wenye njaa licha ya kwamba spika anasali kanisani kwao!

Sitta kwani tatizo la RICHMOND lilipotokea kwa kusababishwa na huyo uliyemualika kanisani....Hukujuwa kuwa munahitaji genereta ya milioni 2?

Ama uliwambia waombe na MUNGU ATAWALETEA MTUMISHI WAKE AMA MALAIKA WAKE NA SASA NI RA?

Hivi kweli hao waumini bado walikuwa wanateseka hivyo na badala ya wewe unayeelewa issue yote kiundani kuwasaidia hiyo genereta na kuhakikisha kuwa yule aliyewasababishia mateso hayo anawajibishwa?

Halafu mazarau ingine alilleta ni pale anapowaambia waombe ili madawa ya kulevya yaliyowaharibu vijana kiasi kwamba hawajui hata kuwa Taifa limeuzwa...Tena nadhani hata hiyo bongo flava ni wao wanaifadhili ili vijana wabakie kwenye muziki na wao waendelee kuuza nchi!

Sasa hayo madawa ya kulevya ambayo listi yake anayo kikwete na Amina Chifupa alitaka kuiweka wazi akauwawa...Then huyu mtu anakuja kuwaambia waombe badala ya kuwashughulikia hao mazungu yenyewe ambayo ni wanamtandao!?

Kina Rostam waache siasa na wasubiri JK arudi na tunataka UKWELI!

So far naona JK ndiye engineer mwenyewe kwani wote walioko chini yake wakiminywa tu...wanaangalia juu..!Na juu yao..sijui kama ni Kikwete ama Mungu!

IT REMAINED TO BE SEEN!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom