Lakini hebu twendeni nyuma na mbele, tusilikuze sana hili jambo. Kuna waumini kibao wanaotoa sadaka zao makanisani na misikini ambazo wamechota kutoka fungu walilolipata kwa njia ya kifasadi au nyingine. Hapa tusibadilishe mada ya ufisadi, kama Rostam ni fisadi hawezi kuwa Omega na Alfa, atakuwa sehemu ya huo mfumo wa ufisadi na zaidi ya yote atakuwa ni uzao wa huo mfumo wa ufisadi.
Watetezi wa mchungaji aliyemwalika Rostam kanisani wanaweza wakaja na hoja kama hizi:
Kanisa halipaswi kuwakataa wale wanaoamua kuingia nyumbani kwa Bwana. Kwa hiyo ukiangalia kwa jicho lingine ni kwamba kanisa lilipata nafasi nadra ya kufanikiwa kumleta mbele za bwana moja ya waliopotea. Sasa cha kujiuliza Rostam alipata nafasi ya kukiri, kutubu na kumrudia bwana? Hili ndio swali la msingi la kujadiliwa na hao maaskofu. Maaskofu wasiongozwe na siasa kwenye mjadala muhumu kama huu bali roho ya Bwana tu!
Sasa kama hao maaskofu watamsuta mchungaji au kiongozi wa kanisa aliyemwalika Rostam, watajuaje kama aliongozwa na roho ya Bwana katika kumwalika huko? Na je, wanajuaje kama Rostam aliongozwa na Bwana kusema maneno aliyoyasema na kutoa sadaka aliyotoa mbele za madhahabu ya Bwana wa Majeshi? Mtikila anaweza kutusaidi kujibu haya maswali?