Mtikila kukopa pesa kwa Rostam sioni kama ni tatizo kwavile walikuwa ni marafiki, na ni jambo la kawaida sana hapa kwetu Tanzania kwa mtu asiye fisadi kukopa pesa ilikukamilisha mambo kadhaa kwa maisha yake, as mishahara haiendani na ugumu wa maisha. Tatizo linakuja kwa Rostam ambaye alitegemea kuwa kwavile amemkopa pesa rafikiye basi huyo rafikiye awe kibaraka wake, kamwe asifungue mdomo juu yake which was wrong on Mtikila's side, yeye anatimiza wajibu kama watanzania wengine wenye mapenzi mema na Tanzania kukemea ufisadi, hajali ni nani na amemfanyia nini,,,kitu ambacho naona ni sahihi kabisa, sisi sote (ambao si mafisadi) kuna namna moja au nyingine tumeweza omba msaada kwa wenye navyo na tumesaidiwa, je nao wangetugeuka na kutangaza hadharani tungeendelea kujilaumu au tungemuona huyo alietugeuka kuwa ni mnafiki tu.
Rostam amedhihirishia umma kwamba yeye ni fisadi No1. kwanini hakujibu tuhuma za ufisadi akaingia katika kutapatapa ooh, naishi na mke wangu, nafanya biashara tangu 1700's hilo sio alilotakiwa kueleza!!! Kama ni biashahara halali then Tanzania ingekuwa kati ya nchi tajiri ati, tangu enzi hizo mtu anapata mipesa tu.
and last, lawama zote ziende kwa vyombo vya sheria hapa Tz, mtu kama ni fisadi ashitakiwe, afungwe! mambo ya kuwaacha mitaani wajitutumue na kuita waandishi kushuka nao verse za taarabu sio sahihi, na kuanzia sasa tutegemee press conference nyingi tu, ndio kumekucha sasa.