...Mtikila tumemshtukia anatumiwa na CCM na siasa zake za kibaguzi na jazba hazina nafasi kwa wananchi walio wengi,ila tunashukuru mchango wake wa kuishtaki serikali katika mambo mengi ambayo naona wengi tulikuwa hatujui
Koba,
Unaweza kutufafanulia, je anatumiwa na CCM vipi? Kuchangiwa na Rostam hizo pesa tayari
ni kutumiwa na CCM?
Kweli Mtikila atakubali kwenda kote huko jela akitetea haki ya Mtanganyika ili atumiwe na CCM?
Nafikiri hili neno la kumwambia kila mwanasiasa ambaye hatukubali naye kwamba anatumiwa na CCM, limechuja na limepitwa na wakati.
Kuna wanasiasa kibao tunaowashabikia hapa, wanapigana vikumbo kila siku na viongozi wa CCM lakini hatusemi badala yake tunamshambulia mtu kama Mtikila ambaye kwa kweli kachangia sana kwenye mapambano ya kudai haki ya Mtanganyika.