Rostam aibukia kanisani!

Kupeshana, kuombana na ufisadi ni vitu tofauti kabisaa. Goood Mtikila. Assume mke au mume wako mnafanya ofisi moja na mmoja wao ni bosi. Je mkihitilafiana mpaka ndo ikavunjika huko ofisini kutakalika kweli? kumbe leo ukipewa msaada au mkopo inabidi ushabikie hata maovu? sitaki kuamini kuwa hata shetani akisema ameonewa tutapiga makofi.

Be careful
 
Sasa Jamani kizunguzungu kimenikuta! Lakini all in all mimi mtikila namwaminia sana no matter what. He dare to speak his mind!
 
mtikila Mchungaji Na Hao Kondoo Wa Wanaochungwa Nae Huyu Mchunga Ndio Kazi Yake Kuchota Huku Nakule . Wakati Wa Sakata La Manji Na Mengi Usiku Tukimwona Haideri Plaza Akishuka Kila Jioni Sasa Hapo Ipo Ofice Ya Nani Kazi Kwenu Lakini Nilikutana Nae Akitoka Huko Kama Paka Mwizi . Asubuhi Tayari Yupo Maelezo Ku Ropoka .... Domo Kaya Kweli . Likaja Sakata La Kadhi Kaitwa Atumike Tena Usiku Usiku Huyo Avinjari Ndani Kwa Wachungaji Wenziwe Pale Kivukoni Na Baadae Kama Ada Lazima Apite Haideri Plaza Kwa Mangi Meza Akajaze Chaji Za Kuropoka . Kwa Hio Kuchukua Tena Kwa Rostam Si Ugeni Ndio Mjini Bongo Utaishi Vipi? Mabo Ya Bongo Hayo , Kazi Kwenu Wachunwaji Wa Mtikila

Namwaza mtikila na suluari lake lililoshikizwa mabegani mbavu zangu zinavunjika, Kweli mjini shule
 
Report ya Mwakyembe ilieleza ubaya wowote wa Rostam Aziz? mbona sioni hapo mahali? Katika watanzania milioni 40 ameona pa kwenda kukopa ni kwa Rostam tu?????????????????????Haiingii akilini.

Katika watanzania Milioni 40 aliangalia na kugundua kwamba mtu pekee ambaye akimwendea atampatia fedha kwa urahisi huku huyo mtu akitegemea kupata fadhila kadhaa toka kwa Mchungaji alikuwa ni Rostam... hili ni kutokana na madhambi yake...

The real issue hapa nadhani ni RA na si Mchungaji Mtikila, maana tukaamua tuanze fukua na kuanika majina yote ya waliofaidi kupitia kwa mafisadi sidhani kama patatosha. Listi ni kubwa. Mtikila amefichuliwa na hajabisha juu ya hilo... Nina hakika kwamba alikuwa na sababu ya Msingi mpaka kuchukua hizo pesa.

Mona nimepata fununu kwamba hata Chacha Wangwe yupo katika payrol ya RA na ni kwamba their main task ni kuvuruga upinzani kuhakikisha kwamba hautakuja kuwa na nguvu ya kushika hatamu.

Hapa Watanzania kinachotakiwa kufanyika ni kuweka nguvu pamoja na kupambana na mafisadi na mara tutakapofanikiwa kupambana na Mafisacdi wa Kuu ambao ni kama mizizi then hizi product za ufisadi itawa ni jambo rahisi sana kuzichomoa.

Siamini kama Spin Master RA anafanikiwa katika kugeuza mawazo ya watanzania Milioni 40 uliowataja hapo juu kutoka kuwapigia kelele MAFISADI mpaka kuanza wapigia kelele wale ambao wamefaidi matunda ya Mafisadi. Na kwa hakika tupo wengi!!!

Mtikila aliona Rostam ndio the easy way out, katoka kwa kutumia hilo lakini mpaka sasa natumaini hajawa corrupted na kuanza kumuabudu huyo RA. Na hata kama moyoni mwake anamuabudu lakini kile ambacho Watanzania tunaona ni Mwanaharakati Mtikila akipambana na Wadhalimu. Hilo nadhani kwa sasa linatosha. Ila tu tutahitaji fahamu ukweli wa Christopher Mtikila!!! Ni wa Kushoto ama Kulia?
 
Rostam amgeuzia kibao Mch. Mtikila





Mchungaji Christopher Mtikila... habari kamili soma pembeni.
*Asema alimpa Sh 3 milioni kujenga Kanisa
*Aanika stakabadhi alizosaini hadharani

*Mtikila akiri kupokea hela, asema alimkopa

*Pia adai fedha hizo ni za serikali si zake


Na Ramadhan Semtawa


MBUNGE wa Igunga, Rostam Aziz, ameibua madai mapya na mazito, akisema kuna watu wazito na maarufu nchini wanapiga kampeni chafu dhidi yake huku akianika hadharani stakabadhi ya malipo ya Sh 3 milioni alizompa Mwenyekiti wa Chama cha Democratic (DP), Mchungaji Christopher Mtikila.


Akizungumza kwa mara ya kwanza na vyombo vya habari tangu awe mbunge kwa miaka 16 sasa, ikiwa pia ni baada ya kuibuka mjadala wa kudaiwa kutumia Kanisa kujisafisha, Rostam aliyaita matamshi ya Mtikila kuwa ni yenye uhusiano na kampeni chafu zinazoendeshwa na mtandao wa watu wazito na maarufu nchini dhidi yake. Hata hivyo hakuwataja.


Katika hotuba yake ya maandishi, Rostam alisema haoni kosa kuchangia Sh 7 milioni kwa Kwaya ya Amkeni katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKTT), Usharika wa Kinondoni, kwani hata Mtikila aliwahi kumwomba kiasi cha Sh 3 milioni kwa ajili ya ujenzi wa kanisa, ambazo alimpa Aprili 14, 2008 kisha akatia saini.


"Fedha zangu ni pato halali linalotokana na jasho langu, kutokea mwaka 1852 huko Tabora kwa mababu zangu. Kwa kutambua fedha zangu ni halali, hata Mtikila mwenyewe Aprili 14, 2008, alikuja kuniomba nikampa na akaupokea mchango wangu wa Sh 3 milioni kuendeleza shughuli za kanisa lake," alisema Rostam na kuongeza:


"Hivi kuwaambia wengine kwamba, ni dhambi kuchukua mchango wangu wakati yeye mwenyewe amepokea fedha kutoka kwangu, tuiteje kama si unafiki, tena unaofanywa na mtu anayejiita Mchungaji. Maneno ya Mtikila ni yenye harufu ya chuki, wivu, ubaguzi na ufisadi."


Hata hivyo, Mchungaji Mtikila alipoulizwa na gazeti hili jana kuhusiana na kupokea fedha hizo kutoka kwa Rostam, alikiri lakini akasema ni mkopo wake binafsi na wala hazikuwa za kuendeleza shughuli za Kanisa wala ujenzi wowote kwani wapo wafadhili wakiwemo kutoka nje wanafadhili Kanisa lake, ambalo linaitwa Full Salvation (Wokovu Kamili).


"Ni kweli, Rostam ni rafiki yangu sana, tena siku nyingi, lakini alinipa Sh 3 milioni kama mkopo, si fedha za kuendeleza Kanisa kama anavyosema. Muulizeni Kanisa gani, mimi sijengi Kanisa wala siendelezi, wapo wafadhili wa kanisa. Ni fedha za mradi wangu na ni mkopo," alisisitiza Mtikila.


Mtikila alipoulizwa tena katika mahojiano mafupi kwa njia ya simu, kwamba mkopo huo alipaswa kuurejesha kwa muda gani na ni mradi gani hasa aliufanya, alijibu tena: "Ni mradi wangu fulani hivi, muda wa kurejesha mkopo ulipaswa kuwa within two months (ndani ya miezi miwili)."


Katika mahojiano hayo, Mtikila alipoulizwa zaidi, kwamba hadi jana miezi miwili ilipita vipi hakuweza kurejesha fedha hizo, alijibu: "Ahaa ni kana kwamba mkopo ni mkopo tu, hata serikali bado inadaiwa na wafadhili na haijalipa hadi sasa, ila mimi nitamlipa ndani ya wiki moja hadi mbili kuanzia sasa."


Mtikila alipoulizwa zaidi, kwamba hata kama ni mkopo, vipi alikopa fedha kwa mtu ambaye amekuwa akimuita fisadi na mwenye kumiliki fedha chafu kwa kuwa pia alipinga Rostam kutoa fedha kwa KKKT, alijibu: "Ni kana kwamba zile fedha si chafu ni za nchi yetu, ni za serikali yetu, sema tu matumizi yake na amezipataje."


Wakati Mtikila akijitetea kwa hayo, Rostam aliweka bayana mambo mbalimbali, akimhusisha Mwenyekiti huyo wa DP na mtandao unaoendesha kampeni chafu dhidi yake.


Rostam alisema, amekuwa akihusishwa na tuhuma mbalimbali na kutoa ruksa kwa wenye ushahidi kuupeleka katika vyombo vya dola ili ashughulikiwe na kuongeza kwamba, tuhuma za kumiliki Kampuni ya Kagoda inayohusishwa na ufisadi wa wizi wa Sh 40 bilioni katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), hawezi kuzungumzia kwani kuna timu ya Rais inafanya kazi ya uchunguzi wa tuhuma hizo.


Alipoulizwa kwamba, kama azma yake ya kwenda kanisani haikuwa kujisafisha, kwa nini aliamua kwenda kuzungumzia mambo hayo kuhusu tuhuma dhidi yake na baadhi ya watu wengine kwamba ni chuki badala ya kuzungumza siku zote tangu kuibuka kwa sakata la Richmond mwaka 2006, alijibu: "Kwanza sikwenda kujisafisha, nilialikwa, nilitaka viongozi wa dini wajenge maadili mema katika nchi."


"Nimeamua kuwaita ili kuweka rekodi sahihi, kutokana na matukio ya wiki hii inayomalizika leo (wiki iliyopita iliyoisha jana), nimeamua kufanya hivi baada ya Mchungaji Mtikila kuitisha mkutano na kuamua kunitukana na hata kuhoji uhalali wa KKKT kunialika kuwa mgeni rasmi katika sherehe za uzinduzi wa albamu ya Kwaya ya Amkeni," alisema Rostam, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).


Rostam alisema baada ya mkutano huo, KKKT Dayosisi ya Mashariki na Pwani, walipata shinikizo wakatoa taarifa ya kuukana mwaliko wa kanisa hilo, Usharika wa Kinondoni.


"Huu ni mwendelezo tu wa kampeni chafu inayoendeshwa na watu wachache, ambao ni maarufu na wazito katika jamii yetu, waliojiunga pamoja katika ushirika usio mtakatifu, ambao kwa kutumia malengo yao wanayojua wao, wameamua kuchafua majina, hadhi na heshima ya baadhi yetu," alisema.


Mbali na Mtikila, Rostam alisema ndani ya kikundi hicho, wamo ambao hawaridhiki na nafasi za uongozi walizonazo na ambao wamejenga chuki kwa kudhani na kujiaminisha kuwa, labda alihusika (Rostam) kuwazuilia, kujichukulia fursa za ufahari na hadhi wasizostahiki kwa vyeo vyao.


"Siweki visasi na kutaka kumkomoa mtu eti kwa sababu tu kampuni yangu ilikosa zabuni fulani katika mchakato wa ushindani wa kibiashara au katika kubinafsisha mashirika ya serikali," alisema bila kufafanua zaidi.


Alifafanua kwamba, mjadala uliozushwa kuhusu kuchangia fedha katika KKKT umekusudiwa kutimiza ajenda za kisiasa na wivu wa kibiashara. Hata hivyo, hakutaja ni nani mwenye wivu wa kibiashara na ajenda binafsi dhidi yake zaidi ya kuongeza kuwa: "wahusika watajijua."


Rostam aliongeza kwamba, hakuanza leo kulisaidia Kanisa hilo kwani hata katika ujenzi pia alishiriki na pia amekuwa akishirikiana na madhehebu mengine, ikiwemo ya dini ya Kiislamu.


"Leo hii kushiriki katika shughuli za Kanisa lile lile nililochangia kunapofanywa kama vile ni kitu cha ajabu na kunidhalilisha kwamba, kuna ajenda nyingine wanayoielewa hao waliozusha mjadala huu. Ufanisi wa haraka wa Mtikila kukusanya watu na kutoa tamko lazima uwe unaratibiwa na watu wanaoelewa wanachofanya," alisema.


Alisema hana matatizo yoyote na KKKT na kwamba mikakati hiyo michafu na kifisadi haiwezi kumfanya arudi nyuma, bali atazidi kuipenda nchi yake na kusema ukimya wake haukuwa woga wala haogopi kitu.


Wiki iliyopita, Rostam alihudhuria hafla ya uzinduzi wa albamu ya Kwaya Amkeni katika Usharika wa Kinondoni. Pamoja na mambo mengine, alilishukuru Kanisa kwa kumwalika na kutambua usafi wake na kuachana na maneno aliyoita ya kijiweni, uzushi, chuki na kuchafuana.


Kauli hiyo iliibua mjadala mzito hadi KKKT, Dayosisi ya Mashariki na Pwani kukana mwaliko wa Rostam. Hata hivyo, mwenyewe jana alisisitiza ni msafi na kwamba mwenye ushahidi wa uchafu wake aende mahakamani, zikiwemo tuhuma za kumiliki kampuni za Richmond na Dowans.
 
Mtikila hajatuangusha....kama kuna dume mpaka sasa kwenye hili game ni Mtikila. Yeye amemuendea Rostam Aziz kabla ya ripoti ya Dr Mwakyembe kutoka, amekopa/amepewa Mil 3. Lakini mara baada ya ripoti ya Rostam Aziz kutoka Mtikila hakumuonea aibu kwa sababu eti alishawahi kumkopa/kumuomba Mil 3 huko nyuma. Mtikila alipogundua kuwa Rostam Aziz ni Nyani, hakumuangalia usoni; aibu wala woga Mtikila akaanza kupambana naye moja kwa moja...

Rostam mpaka sasa ametuthibitishia kuwa yeye ni FISADI kwa kugawa/kutoa/kukopesha pesa kwa wanasiasa/mashirika ya dini na wanajamii wengine huku akiwa na nia ya kuonewa aibu akiwa anatuibia Watanzania.

Bravo Mtikila, pambana nao hao kama walivyo.

Hapendwi mtu, Taifa mbele.

Mimi nakubalina nawe Yebo Yebo, bado Mtikila ni kiboko, kweli unaweza kupewa pesa na fisadi na bado ukamtukana. Unajua hizi fedha za mafisadi zinatakiwa zichukuliwe kwa namna yoyote kwani ni za watanzania kugawana. Nawashauri hata KKKT wasifikirie kurudisha pesa ambazo RA alichanga, kimsingi ni za watanzania isipokuwa wenzetu wamejichukulia tu isivyohalali. Ni lazima Mtikila atatuambia ilkuwaje akaomba hou "mkopo" na kwa nini bado anamshambulia mfadhili wake.
 
Ni Watanzania wachache mno waliokuwa wakijua wanayoyajua sasa kutokana na maovu yaliyokuwa yakitendwa na watu kwa kutumia nafasi zao za uongozi ama kwa kutumia majina yao. Vyombo vya Habari na vyama vya Upinzani ndio vimeweza kuwaelimisha wananchi kuhusu yanayoendelea nchini mwetu ambayo wala isingelikuwa hivyo tusingeliweza kuyajua. Mtikila ni Mtikila yawezekana kabisa alikuwa akijua kwamba fedha anazopewa hana uhakika kama ni safi lakini alizipokea kama anavyosema mwenyewe ni fedha zilizoporwa kutoka kwa walalahoi.

Hivi mbona hatujiulizi, hawa matajiri waliomea kama uyoga kwa kipindi kifupi sana nchini humu utajiri huo wameupataje jamani? Mpaka tunafika mwaka 2000 tajiri mwarabu aliyekuwa akisikia alikuwa Bakhresa. Huko Igunga kuna biashara gani ya kutoa bilionea mgawa fedha za bure?
 
...jina lenyewe mizozo, sijui nikujibu nini?

Hata hivyo Koba...Ni koba la mapesa ama koba mkoba namba tano?
Anyways...Wewe huamini kuwa sasa nchi yetu IKO KWENYE MZOZO WA MAMA WA MIZOZO YOTE TANGU TUPATE UHURU!?

Mzozo wa Mizozo don't mind..Wengine tunalizimia jina lako hilo la mizozo kwani ndiyo MIZOZO YENYEWE HII YA KUWATETEA MAFISADI!
 
Hata hivyo Koba...Ni koba la mapesa ama koba mkoba namba tano?
Anyways...Wewe huamini kuwa sasa nchi yetu IKO KWENYE MZOZO WA MAMA WA MIZOZO YOTE TANGU TUPATE UHURU!?

Mzozo wa Mizozo don't mind..Wengine tunalizimia jina lako hilo la mizozo kwani ndiyo MIZOZO YENYEWE HII YA KUWATETEA MAFISADI!

Hapa Kamanda umenena sana... tuko pamoja katika hili na ni kwamba mpaka kitakapoeleweka na mafisadi wakakosa kwa kukimbilia...

Tuko pamoja hatua kwa hatua katika hili!!!
 
Mtikila hana habari kuwa kuna Saccos anakoweza kukopa akiweka akiba????Anadhalilishwa sasa...Duh!!!
 
Mr. Mtikila mistake: When denouncing RA cash donation to KKT Church; at the same time he was supposed to reveal that RA borrowed him Tshs 3million. By not mentioning that cash he borrowed from RA was some sort of hiding something. I see Mtikila here did something fishy.
 
Mr. Mtikila mistake: When denouncing RA cash donation to KKT Church; at the same time he was supposed to reveal that RA borrowed him Tshs 3million. By not mentioning that cash he borrowed from RA was some sort of hiding something. I see Mtikila here did something fishy.

NOT AT ALL!

ROSAMA alipotowa pesa za KKKT alijisafisha MADHABAUNI.

Hakufanya hivyo kwenye milioni tatu na hivyo kachukizwa kwani kageukwa!

Sasa kama Mtikila kamgeuka anachukia..Sijuwi kama JK akifanya hivyo kutatokea nini.

Ama anaogopa kuvamiwa na IRAN?

Mi nasema nimemwelewa Mtikila na nitapigania POINTI YAKE HADI PALE SOMEONE ATAKAPO PROOVE WRONG!

LONG LIVE MTIKILA!

LONG LIVE WAZALENDO!
 
kama mnakumbuka mwaka 1995 ni huyu Mtikila alituambia wadosi hawafaikuwa marafi zetu, kumbe yeye nyuma ya pazia anapokea mkopo, siwezi kuiita hongo kwa sababu fisadi RA alimwambia aweke sign yake naye hakujua kama ni mtego haya na aende mahakamani kushitakiwa kuwa RA ameghushi saini yake. jamaa ni muigizaji tu anatumia upumbbavu wa watu kama faidi wote hao ni ccm.
 
Street wiser...

ccm NI WASIOTAKA ISSUE IJADILIWE BUNGENI NA PIA WASIOTAKA KESI IFUNGULIWE MAHAKAMANI.

1995 UHURU NA HAKI YETU TULINYIMWA NA MWALIMU,MARANDO,LAMWAI NA KINA KABURU!

Mtikila ni the OPPOSITE OF THE ABOVE...!

Make sense?
 
Kwenda kukopa hela kwa fisadi ni wrong period! Hakuna excuse hapa kwa Mitkila, inamfanya apoteze ile moral authority aliyokuwa nayo kabla ya rostam kusema ni public, angekuwa na akili ya siasa Mtikila angesema mapema kuwa aliwahi kukopa hela kwa Rostam,

Message ya Mtikla kwa mabadiliko ya taifa, bado iko pale pale na kuna ambao tuko macho kuiendeleza mpaka tuone mwisho, na Mtikila bado anasimama tall kuliko viongozi wengi sana ambao tulitakiwa kuwategemea kuanzia Upinzani mpaka CCM, ninarudia kuwa Mtikila bado anasimama tall kuliko viongozi wenmgi sana sio wachache wa taifa letu ambao tulitakliwa kuwategemea, Saulo alikuwa akiua watu wa Mungu lakini baadaye alibadilika na kuwa mtu wa Mungu inakubalika hiii,

Mtikila anaweza bado kujiosha na kuwa msafi tena lakini kwa sasa ni mchafu na ananuka, kwani benki za kukopa zipo wazi, sasa huwezi kwenda kukopa hela za ufisadi halafu ukabaki unasimama kama mwanzoni, ni watu kama huyu Mrtikila ndio wanamfanya Rosatm kuwa n kichwa kikubwa na jeuri, it is about time tukaanza kuichukua message nzito za Mtikila to the next level kwa sababu ni ;cear kuwa Mtikila hawezi haya mapambano na yeye ananuka pia,

Lakini bado tunaweza kumpa nafasi ya kujisafisha, lakini rostam hasafishiki mpaka kwenye mkono wa sheria tu! Ingekuwa nchi za wenzetu sasa hicvi angeteuliwa Special Prosecutor na bunge kuchunguza sababu za Rosatm kumpa hizo hela Mtikila kwa sababu lazima kuna something fishy na sherisa ya jamhuri kuhusu kuepana kwao hela, lakini bongo ndio hivi yataishia hivi hivi!
 
Mtikila lazima aje na majibu clean na yenye mashiko na sio kama haya aliyokuja nayo kuwa eti ooh nilikopa mara nini?

Atajikuta akionyesha rangi zake za asili na wale wote ambao mara kwa mara wamekuwa wakimtumia huyu ze Mtikila kuna haja ya kujiangalia na kujitafakari kwani mambo yatawaweka hadharani na ndio yameanza hivyo,
 
Mnajua jamani siasa ni game moja chafu sana....tusije kushangaa kuwa huyu Mtikila ni mole wa CCM.....mnakumbuka Shikuku wa Kenya?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom