Rais Samia: Mifumo wa kudai haki jinai nchini imeharibika kutokana na kupuuza mifumo ya maadili

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,814
11,991
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akizindua Tume ya Kuangalia Jinsi ya Kuboresha Taasisi za Haki Jinai chini Ikulu, Chamwino Mkoani Dodoma leo tarehe 31 Januari, 2023



Katibu Mkuu kiongozi Moses Kusiluka

Jukumu kubwa la tume ni kufanya tathmini ya kina ya mfumo wa haki jinai kwa lengo la kufanya maboresho makubwa ili kukidhi matakwa ya serikali na jamii ya Tanzania kwa ujumla.

Taasisi za haki jinai zitakazofanyiwa kazi na tume ni;

~ Jeshi la Polisi
~ Ofisi ya Taifa ya Mashtaka
~ TAKUKURU
~ Jeshi la Magereza
~ Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya

Tume ina jumla ya Wajumbe 11 ambao ni;
  1. Mwenyekiti wa Tume Jaji Mkuu Mstaafu - Mohamed Othman Chande
  2. Makamu Mwenyekiti - Balozi Ombeni Sefue
  3. Laurean Vilomena Ndumbaro
  4. Jaji Eliezer Feleshi
  5. Dkt. Edward Kamanywa Hoseah
  6. Balozi Ernest Jumbe Mangu
  7. Saada Ibrahimu Makungu
  8. Omary Issa
  9. Yahya Khamis Hamad
  10. Baraka Leonard
  11. IGP Mstaafu Said Mwema

Sekretariat ya kuisaidia tume yenye Wajumbe watano ambao ni;

  1. Ramadhani Kailima
  2. Evata Mushi
  3. James Kilabuko
  4. Benjamin Mwakisongole
  5. Ally Mirza

Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango
Kumekuwa na manung'uniko mengi kutoka kwa wanachi ambayo yanaonesha kuwa mfumo wa haki jinai una changamoto nyingi kama vile kwenye ukamataji, wananchi kujua haki zao, ucheleweshwaji wa upepelezi nk.

Rais Samia Suluhu Hassan
Katika kipindi cha miongoo kadhaa mfumo wa kudai haki jinai nchini imeharibika kwa kupuuza mifumo ya maadili.

Mifumo ipitiwe upya kuangalia wapi pana makosa na kufanya marekebisho ili mambo yaende vizuri.

Tume imeundwa na watu ambao wametoka kwenye taasisi ambazo zinakwenda kuchunguzwa, mfano kutoka TAKUKURU, Rais wa Tanganyika Law Society, IGP wawili kutoka Jeshi la Polisi, Mwanasheria Mkuu, sababu wanajua wapi kuna matatizo na walipotetereka na itakuwa rahisi kuonesha penye matatizo na wapi pa kuboresha.

Kutokana na ukubwa wa kazi tume itakuwa na muda wa miezi minne kuwanzia tar 1/2/2023 hadi 30/5/2023 kupeleka ripoti (kamili au ya kwanza kutokana na muda utakavyokuwa) kwa Rais Samia.

Taasisi hizo zinazoenda kufanyiwa kazi na tume zina malalamiko mengi na zinatakiwa kwenda kuangaliwa, ili kubainisha matatizo hayo na yaweze kufanyiwa kazi.



Hakuna kitu kibaya kukichepusha Duniani kama kuchepusha kama haki ya mtu, kama wewe hutaki kunyang'anya haki yako basi unatakiwa kutengeneza mfumo ambao kwa kiasi kikubwa angalau inalinda haki za watu.

Baadhi ya mambo kadhaa yanayohitaji kuangaliwa kwenye taasisi hizo ni;
~ Utendaji wa taasisi hizo.
~ Masuala ya mafunzo ya ajira.
~ Mifumo ya ajira.
~ Upandishwaji wa vyeo katika taasisi hizo.
~ Matumizi ya TEHAMA na Ubunifu.
~ Fikra za kiutendaji na mahusiano kati ya taasisi hizo na raia.

Kwenye tatizo lolote zitaundwa timu, kwakuwa wataalamu wapo; kuchunguza kuna matatizo gani katika sekta mbalimbali.

Tume zimekuwa zikiundwa lakini mapendekezo yao yamekuwa hayafanyiwi kazi, hivyo tume hii inatakiwa kwenda na mapendekezo wa ya jinsi ya kuboresha kutokana na changamoto zitakazoibuliwa ambapo itarahisisha matatizo kushughulikiwa haraka.
 
Ni kuchezea hela za walipakodi hakuna jipya tutakalosikia. Aliunda tume kuchunguza wizi bot baada ya kifo cha yule mwehu mpaka leo hakuna mrejesho
 
Siku ambayo dunia itaanzisha medali ya wishy -washy, Tanzania ya sasa itakuwa mshindani wa kutumainiwa kwa medali hiyo!
 
Mheshimiwa Rais Samia Suluhu amezindua tume ya kuangalia jinsi ya kuboresha taasisi za haki jinai ambayo itapitia Jeshi la Polisi, Magereza, TAKUKURU, DCEA, Ofisi ya Taifa ya Mashitaka na kutoa mapendekezo ya maboresho yatakayoimarisha utoaji haki kwa wananchi.

Lakini pia amesisitiza kuwa "Hakuna kitu kibaya duniani kukichepusha kama haki ya mtu, kama wewe hutaki kunyanganywa haki yako kwa hiyo inabidi utengenze mfumo kwa kiasi kikubwa angalau tunalinda haki za watu"- Rais Samia Suluhu

Vilevile Rais Samia Suluhu ameonyesha nia yake ya dhati kusimamia haki za wananchi hasa wasio na uwezo amesema kuwa "Watu wasio na uwezo wa mamlaka wala fedha wamekuwa wakipoteza sana haki zao. Wamekuwa wakikumbwa na mambo ambayo hayakupaswa yawakumbe na wale ambao walikuwa wanafanya makosa, wanaepushwa na makosa sababu uwezo wao kihadhi na kifedha"

Watanzania tuna kila sababu ya kumshuru Mungu kutupa Rais anaesimamia haki maana hapo awali watu walikua wanafungwa kwa kesi za kusingiziwa lakini leo tunaona Tanzania ni ya haki upendo na amani.
 
kama kuna Polisi humu anisamehe mimi nikikuta Polisi anapigana na nyoka nitamsaidia nyoka kwa kweli …

wana laana sana hawa viumbe mpaka hua najiuliza ni binadamu wenzetu au wenyewe wameumbwa na Mungu mwingine ?
 
Na YULE WAZIRI WA KILIMO BASHE...NAYE AMEUNDA TUME YA KUSHUGHULIKIA UTAPELI KWENYE KILIMO...

NI TUME TUME TUME...PESA SI ZIPO...TUMEKOPA ZA KUTOSHA...
 
Watu walioishi na kukulia kwenye mfumo huo huo watakujaje na idea mpya,leteni mashirika ya nchi zenye mifumo bora ya haki wawafanyie consultation vinginevyo hizi ni danadana tu,hao wazee wengi wameshajichokea hawana jambo jipya.
 
kama kuna Polisi humu anisamehe mimi nikikuta Polisi anapigana na nyoka nitamsaidia nyoka kwa kweli …

wana laana sana hawa viumbe mpaka hua najiuliza ni binadamu wenzetu au wenyewe wameumbwa na Mungu mwingine ?
Ukikuta Anapigana Na Nyoka, Utamsaidia Nyoka Chap Kuamua Huo Ugomvi
 
Ni kuchezea hela za walipakodi hakuna jipya tutakalosikia. Aliunda tume kuchunguza wizi bot baada ya kifo cha yule mwehu mpaka leo hakuna mrejesho
😂😂😂🤣🤣🤣😂😂😂
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akizindua Tume ya Kuangalia Jinsi ya Kuboresha Taasisi za Haki Jinai chini Ikulu, Chamwino Mkoani Dodoma leo tarehe 31 Januari, 2023



Katibu Mkuu kiongozi Moses Kusiluka
Jukumu kubwa la tume ni kufanya tathmini ya kina ya mfumo wa haki jinai kwa lengo la kufanya maboresho makubwa ili kukidhi matakwa ya serikali na jamii ya Tanzania kwa ujumla.

Taasisi za haki jinai zitakazofanyiwa kazi na tume ni;
~ Jeshi la Polisi
~ Ofisi ya Taifa ya Mashtaka
~ TAKUKURU
~ Jeshi la Magereza
~ Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya

Tume ina jumla ya Wajumbe 11 ambao ni;
  1. Mwenyekiti wa Tume Jaji Mkuu Mstaafu - Mohamed Othman Chande
  2. Makamu Mwenyekiti - Balozi Ombeni Sefue
  3. Laurean Vilomena Ndumbaro
  4. Jaji Eliezer Feleshi
  5. Dkt. Edward Kamanywa Hoseah
  6. Balozi Ernest Jumbe Mangu
  7. Saada Ibrahimu Makungu
  8. Omary Issa
  9. Yahya Khamis Hamad
  10. Baraka Leonard
  11. IGP Mstaafu Said Mwema

Sekretariat ya kuisaidia tume yenye Wajumbe watano ambao ni;
  1. Ramadhani Kailima
  2. Evata Mushi
  3. James Kilabuko
  4. Benjamin Mwakisongole
  5. Ally Mirza

Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango
Kumekuwa na manung'uniko mengi kutoka kwa wanachi ambayo yanaonesha kuwa mfumo wa haki jinai una changamoto nyingi kama vile kwenye ukamataji, wananchi kujua haki zao, ucheleweshwaji wa upepelezi nk.

Rais Samia Suluhu Hassan
Katika kipindi cha miongoo kadhaa mfumo wa kudai haki jinai nchini imeharibika kwa kupuuza mifumo ya maadili.

Mifumo ipitiwe upya kuangalia wapi pana makosa na kufanya marekebisho ili mambo yaende vizuri.

Tume imeundwa na watu ambao wametoka kwenye taasisi ambazo zinakwenda kuchunguzwa, mfano kutoka TAKUKURU, Rais wa Tanganyika Law Society, IGP wawili kutoka Jeshi la Polisi, Mwanasheria Mkuu, sababu wanajua wapi kuna matatizo na walipotetereka na itakuwa rahisi kuonesha penye matatizo na wapi pa kuboresha.

Kutokana na ukubwa wa kazi tume itakuwa na muda wa miezi minne kuwanzia tar 1/2/2023 hadi 30/5/2023 kupeleka ripoti (kamili au ya kwanza kutokana na muda utakavyokuwa) kwa Rais Samia.

Taasisi hizo zinazoenda kufanyiwa kazi na tume zina malalamiko mengi na zinatakiwa kwenda kuangaliwa, ili kubainisha matatizo hayo na yaweze kufanyiwa kazi.



Hakuna kitu kibaya kukichepusha Duniani kama kuchepusha kama haki ya mtu, kama wewe hutaki kunyang'anya haki yako basi unatakiwa kutengeneza mfumo ambao kwa kiasi kikubwa angalau inalinda haki za watu.

Baadhi ya mambo kadhaa yanayohitaji kuangaliwa kwenye taasisi hizo ni;
~ Utendaji wa taasisi hizo.
~ Masuala ya mafunzo ya ajira.
~ Mifumo ya ajira.
~ Upandishwaji wa vyeo katika taasisi hizo.
~ Matumizi ya TEHAMA na Ubunifu.
~ Fikra za kiutendaji na mahusiano kati ya taasisi hizo na raia.

Kwenye tatizo lolote zitaundwa timu, kwakuwa wataalamu wapo; kuchunguza kuna matatizo gani katika sekta mbalimbali.

Tume zimekuwa zikiundwa lakini mapendekezo yao yamekuwa hayafanyiwi kazi, hivyo tume hii inatakiwa kwenda na mapendekezo wa ya jinsi ya kuboresha kutokana na changamoto zitakazoibuliwa ambapo itarahisisha matatizo kushughulikiwa haraka.

Naomba hiyo tume iwasiliane nami ili niwajulishe rushwa inavyofanyika Tanzania la sivyo watakuwa wanaandika hadithi za kusadikika . Wasipoteze hela za walipakodi maskini kwani wote walioteuliwa wanajua jinsi rushwa inavyo fanyika Tanzania.
 
Back
Top Bottom