Rais Samia: Kila mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake, lakini mbona mnakula sana mnavimbiwa? Jipimieni!

5525

JF-Expert Member
Apr 6, 2014
5,412
6,276
Nimemsikia Rais Mama Samia anasema kila mbuzi hula kutokana na urefu wa kamba yake akiwambia kikao na Mawaziri wake, sijuwi amemaanisha nini kwamba mawaziri sasa wataanza kugawana rasilimali na mapato?

Embu tujielekeze hapa kidogo wale watu wenye taaluma fasihi, Mama kila siku anatoa kamsemo mpya mpya.

Natanguliza shukurani.


"Mara moja nilisema kwenye baraza la mawaziri nikasema mimi najua kila mbuzi hula urefu wa kamba yake, jinsi kamba yako inavyokuruhusu ndivyo unavyokula lakini nikawaambia mbona mnakula sana? Mnavimbiwa! Si kweli kwamba hampati kwenye maeneo yenu, mnapata, lakini jipimie, jipimieni.

"Kuna mambo yanafanyika ni kufuru, kwa mfano lile nililosema kwa ujenzi wa meli. Meli moja kuna ki wakala huko pembeni kinalipwa dola milioni 2 kwa kila meli. Hiyo ni nini? Hiyo sio sawa, sijui kuna ujenzi wa barabara pesa itagaiwa kwanza weeee, barabara ikijengwa viwango vinakuwa compromised.

"Na sio barabara peke yake na mambo mengine, pesa inagawiwa kwanza kabla mradi haujafanywa, matokeo yake mradi unakuwa compromised. Na ndio maana sekta inakuwa ya mtu mmoja kuna mradi mkubwa basi serikali yote wanakuwa wasemaji wa ile sekta, ukiangalia kwa undani kila mmoja ameshakwenda kumuona aliyepata tenda hiyo kwa wakati wake kwahiyo maneno yanakuwa mengi kwa wakati mmoja, kwahiyo ndugu zangu lizingatieni hilo."
- Rais Samia akiongea na Mawaziri na Manaibu Waziri
 
Siyo kwa viongozi tuu, Mtu yeyote yule anayeongea kabla ya kupanga nini cha kusema, wapi pa kusemea, na namna ya kusema ni mtu mropokaji. Bahati mbaya kwa Tanzania ni kwamba hao ndio viongozi.

Na pia sio lazima Rais aandikiwe nini cha kuongea, hapana! Muhimu ni yeye mwenyewe kujiandalia nini cha kuzungumza. Vladmir Putin anajiandikia hotuba zake yeye mwenyewe, na hajawahi kutoa boko.
 
Rais akiwahutubia Mwaziri na makatibu wakuu, amasema anajua kila mtu anakula na atakula kwa urefu wa kamba yake lakini kwa sasa waanzidi hadi awanagombana. Je, hii si ndiyo maana ya Rais kuruhusu upigaji ila uwe wa kiistarabu?
 
Magufuli To Samia:

From Emperor Without Clothes To Empress Wtihout Shame!

16420724681430.jpg
 
Upotoshaji KAZI KWELIKWELI......

Mama ameongea mengi akitaja MUHALI.....

Ile hali ya kutoambiana ukweli kwa KUOGOPANA NA KUHOFIANA kutoudhiana.......

Amefuatilizia na kukanyana kuhusu ile tabia ya BAADHI YA MAWAZIRI/NAIBU MAWAZIRI kwenda "kuchomeana" kwake.....hapa ndipo KILA MTU ALE UREFU WA KAMBA YAKE na si vingi nevyo......

#Siempre JMT🙏
 
Nimemsikia mama anasema kila mbuzi hula kutokana na urefu wa kamba yake akiwambia kikao na Mawaziri wake, sijuwi amemaanisha nini kwamba mawaziri sasa wataanza kugawana rasilimali na mapato?

Emu tujielekeze hapa kidogo wale watu wenye taaluma fasihi, Mama kila siku anatoa kamsemo mpya mpya

Natanguliza shukurani
Mbuzi mwenye kakamba kadogo anakula majani mpaka hapa, mwezi kamba ndefu kidogo anakula mpaka paleee, mwenye likamba lireefuu anakula mpaka kuleeee!!!
 
Huyu mama bure kabisa, sijawahi ona kiongozi wa nchi hopeless like her. Yaani hapa bongo kama nchi imelamba garasa!! wakina Kagame na Museveni wanatucheka balaa toka kupoteza kiongozi mwenye vision hadi kuja kuokoteza hili garasa,.tumeliwa.
Kasema pia kama humpendi basi penda nchi yako
 
Huyu mama bure kabisa, sijawahi ona kiongozi wa nchi hopeless like her. Yaani hapa bongo kama nchi imelamba garasa!! wakina Kagame na Museveni wanatucheka balaa toka kupoteza kiongozi mwenye vision hadi kuja kuokoteza hili garasa,.tumeliwa.
Utauvimbisha moyo wako upate CARDIOMEGALY bureeee......🤣🤣

Mama yuko poa sana.....

Unapandishwa jazba KIRAHISI kwa KUDOKOLEWA maneno ya UPOTOSHAJI ?!!!😳
 
Huyu mama bure kabisa, sijawahi ona kiongozi wa nchi hopeless like her. Yaani hapa bongo kama nchi imelamba garasa!! wakina Kagame na Museveni wanatucheka balaa toka kupoteza kiongozi mwenye vision hadi kuja kuokoteza hili garasa,.tumeliwa.
Eeeh!jiangalie kijana tutakukula kichwa
 
Back
Top Bottom