Lazime CCM, Msajili wa Vyama pia watawala wakasirike maana mdau mkubwa CHADEMA kutotokea leo huku kuna wadau wa maendeleo kutoka balozi za ulaya wamefika ukumbini na lazima mabalozi watajiuliza sababu za chama kikuu cha upinzani CHADEMA kutotokea kuna kitu hakipo sawa.
MABALOZI WA ULAYA UKUMBINI
Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam tarehe 11 Septemba, 2023.
View attachment 2745843
Mabalozi kutoka nchi mbalimbali wakiwa kwenye Mkutano Maalum wa Baraza la Vyama vya Siasa na Wadau wa Demokrasia Kutathmini Utekelezaji wa Mapendekezo ya Kikosi Kazi na Hali ya Siasa nchini katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam tarehe 11 Septemba, 2023