Rais Samia akutana na Baraza la Maaskofu (TEC), Kilaini aelezea Historia yake na utaifishaji wa mashule 1970

unaongea kwa kua sio mkatoliki au kwa kua hujanufaika moja kwa moja na ukatoliki lakini umekuzwa na kupata akili kwa uwepo wa kanisa katoliki.Kule kwenu kama sio kanisa katoliki maisha yangekuwaje? Heshimu aliyewakuza.Kanisa limelilea taifa lilipokua halijiwezi kutoa huduma sasa mmekua mnakua jeuri.Kama sio shule za kanisa akina mkapa,kikwete,makamba wangesoma wapi?Tazama maeneo ya wananchi wanaoshi karibu na parokia maisha yao yalivyo na unafuu.
Sijakuzwa na dini yoyote,mama akiwachekea hao atavuna mabua,hapo wanajaribu kumchokonoa Ili awaachie wasilipe kodi na leseni za biashara zao.

Shule na hospital zote za dini zinafanya biashara na sio kwamba zinatoa huduma kama wanavyosingizia, gharama huko ni kubwa karibu mara mbili ya taasisi za umma afu eti wanajisemesha.

Magu alikataa huo ujinga wa kutaka kutembelea visingizio ,lazima walipe kodi,wakate leseni na masltakwa mengine ya biashara za huduma.

Kiufupi hata sadaka zinatakiwa kulipwa kodi sasa hawa wanajificha kwenye maeneo kama vituo vya huduma za watoto yatima,wazee,walemavu nk nk..Huko ndiko kinaweza kupewa special treatment na sio kwingine
 
Yaani Hawa TEC wanashangaza,kwanza kwenye hospital zao wanaihujumu bima ya Afya kwa kuandika madawa lundo na kulazimisha vipimo.

Pili Hawa jamaa walikuwa wanaendesha taasisi za mafunzo ambazo hazikukidhi vigezo vya ubora sasa eti wanamwomba mama azifungue? Kwani mama ndio mdhibiti ubora wa Elimu na mafunzo?

Yaani wao wanaangalia tuu kupata pesa bila kujali matakwa ya ubora,naomba ieleweke kwamba si kweli kwamba kila kitu alochosimamia Magu kilikuwa kibaya,binafsi Sikuwahi mkubali kwa mengi ila kuna mengi mazuri lazima sheria isimamiwe.

Hii biashara ya ku lobby kwa Rais sio sawa na yote hii ni matokeo ya kuwa na Katiba mbovu kwamba kauli na utashi wa Rais ndio kinachosimamiwa,hili jambo halikubaliki
 
Nilishaandika kila kitu kuhusu mafundisho ya kanisa katoliki yanayopingana na "Maandiko".

Nenda kwenye jukwaa la Dini kule utakuta post zangu kuhusu "uongo" wa kanisa katoliki. Ni mambo mengi sana tena sana.

Kwa mfano, angalia Amri kumi za MUNGU zinazofundishwa na kanisa katoliki halafu linganisha na zile zilizoandikwa kwenye kitabu cha KUTOKA 20:1-17

Halafu soma ISAYA 8:19 Kumbukumbu la torati 18:11 uone ni jinsi gani MUNGU amekataza kuwaomba "wafu" lakini kanisa lako linafundisha na kuamini katika kuwaomba wafu.

Soma Mathayo 23:9 halafu uniambie ni kwanini Kiongozi wa kanisa lako unamwita "baba mtakatifu".

Hayo ni machache tu nimekudokeza.
Ellen G White katika ubora wake
 
Rais Samia Suluhu Hassan anatarajia kukutana na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) leo Juni 25, 2021

Rais atakutana nao katika Makao Makuu ya TEC, Kurasini



==========

5:30 Asubuhi: Rais Samia Suluhu ameshafika na kuimbwa wimbo wa Taifa, kinachoendelea kwa sasa ni utambulisho wa maaskofu

KILAINI AELEZEA HISTORIA YA BARAZA LA MAASKOFU TANZANIA
5:45 Asubuhi:
Anaeongea kwa sasa ni Askofu Method Kilaini na anaongelea historia ya baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania. Kilaini amesema Baraza la Maaskofu ndio uongozi wa Kanisa Katoliki na lilianza na ujio wa Kanisa Katoliki mwaka 1860.

Askofu Kilaini amesema Wamisionari walikuja na mambo matatu muhimu ambayo ni kueneza dini, kutibu wagonjwa na Elimu.

Kilaini amesema waingereza walikuwa wanaitawala Tanganyika kwa udhamini wa Umoja wa Mataifa hivyo hawakutaka kuwekeza. Ndipo Kanisa lilipoamua kujaza Ombwe lililobaki ambapo mwaka 1928 waliwekeana sera kwamba msisitizo uwe Shule. Kilaini anaendelea kwa kusema maaskofu waliweka sera endapo fedha ni kidogo na inabidi kuchagua kujenga shule au Kanisa, ni bora kuchagua shule na kuacha kanisa na ndio umekuwa msimamo wa kanisa hadi leo.

Kilaini: Mwaka 1956 wakaunda Rasmi umoja wa baraza la maaskofu linaloitwa TEC na kati ya waliounda, askofu mwafrika alikuwa mmoja, Laurian Rugambwa akiwa askofu wa Rutabwa na polepole waliingia mpaka sasa unaona nyuso za waafrika pekee.

Baraza hili liliendelea na sera hiyohiyo mpaka tulivyofika Uhuru mwaka 1961 na wakaunga mkono juhudi zote alizokuwa anazifanya Mwalimu Julius Nyerere.

Alivyofika mwaka 1969/70, Nyerere alisema naona mna shule nyingi lakini nataka ziwe za watu wote, akazitaifisha. Mwaka 1970 wakati anataifisha, Baraza la Maaskofu Tanzania lilikuwa na shule za msingi 1,420. Shule za sekondari 44, vyuo vya ualimu nane halafu shule za ufundi ambazo hazikutaifishwa za wavulana 15 na wasichana 48.

Na hizi zilizotaifishwa, mama utakumbana na hii historia katika utawala wako kwasababu mashule mengine yako katikati ya mission, mbele ni kanisa, nyuma ni nyumba ya mapadri na kushoto nyumba ya kanisa, sasa tukotuko lakini tunaenda vizuri, miaka mingi tumekwenda kwenda lakini kila mara inabidi kutia nguvu sana ili kuweza kukaakaa kwasababu hiki cha katikati hiki ni kiserikali serikali na kilichozunguka ni kimisheni misheni, imekuwa ni changamoto kila mara.

Tunakushukuru mama, unapoongea Lugha yako tunaipenda, usione tumevaa mabarakoa wote hapa, maaskofu wanatabasamu sana hapa, ni kwasababu ya matamko yako unayatoa, wote wanafurahi.




Askofu Mkuu(Gervas Nyaisonga)-Rais wa TEC: RISALA YA MAASKOFU

  • Hiki ni chombo cha juu kabisa cha uongozi wa kanisa katoliki Tanzania hivyo ujio wako kwetu na uwepo wako hapa, wewe ni kiongozi mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, ni heshma kubwa sana kwetu sisi wanabaraza pia ni ishara ya wazi kwamba unathamini baraza hili na mchango wake kwa maendeleo ya watanzania wote.
  • Tunamshukuru Mungu kukubali wewe kuwa kiongozi wa Taifa letu na tunakuombea hekima, afya na mshikamano, Mungu akuwezeshe kutimiza majukumu yako vyema. TECL linakuahidi ushirikiano katika kusimamia ustawi wa watanzania.
  • Tunakuomba uimarishe utawala wa sheria na ujenzi wa Taasisi imara za kidemokrasia ambazo ndio msingi wa utawala bora.
Mheshimiwa Rais tukiwa tunakupongeza na kukushukuru kuwa nasi hapa, hatuna budi tukushirikishe masuala kadhaa kwa ajili ya kutuwezesha sisi kama taasisi inayoshughulika na maendeleo ya kiroho na ustawi wa Watu.
  • Katika utekelezaji wa majukumu yetu, hatuna budi kushukuru ushikiano mzuri uliopo kati ya didi kama taasisi na serikali
  • Mheshimiwa Rais mwaka 2016 sera mbalimbali zilibadilika na kutukwamisha kutoa huduma za kijamii hasa elimu bila kujali uwekezaji mkubwa uliofanywa na kanisa kabla ya hapo hii imesababisha hasara kubwa kifedha na hata rasilimali nyingine pamoja na rasilimali watu
  • Lengo la Shule zetu sio kufanya biashara bali kutoa huduma bila kujali uwezo wa wazazi wanaotaka kueleimisha watoto wao kama ilivyo Sera ya Serikali yako ya Awamu ya Sita



RAIS SAMIA SULUHU
  • Niwashukuru kwa pongezi mlizonipa kwa kushika wadhifa huu mzito na kweli niwaambie ni mzito na mwanzo ni mgumu sana. Lakini mwa ushirikiano na maombi yenu nina imani tutavuka salama,"- Rais Samia Suluhu Hassan
  • Nawashukuru kwa kuwa pamoja na Serikali katika kipindi kizito tulichompoteza kiongozi wetu Hayati John Pombe Magufuli, kwa umoja wetu tuliomba na kushirikiana tukamaliza msiba kwa amani na utulivu na Taifa letu likabaki salama
  • Serikali inawapongeza Kanisa Katoliki kwa mchango wenu kwenye jamii, kwani mmewalea wanadamu kiroho, kiimani, kimaadili, kudumisha amani, kustawisha maisha ya wananchi, kupambana na umaskini, kupunguza tatizo la ajira na kuchochea maendeleo
  • Lengo langu ni kukutana na dhehebu moja moja la dini ili kujua mema na changamoto mlizonazo ili Serikali iweze kujua jinsi ya kuzifanyia kazi

Yesu yupi mkuu,yule wa chato?
 
Inaonekana hujui kama ni biashara au siyo biashara.
Kwa hiyo tafuta ukweli ulivyo kwanza ili ujiridhishe, halafu ulete mada tuijadili.
Haiitaji uwe na degree kujua hilo? Leo shule zao ambazo wanaomba au wanapewa msamaha wa Kodi, bado Ada zao ni za juu kwa waumini wao,alkadhalika hospital zao pia zipo juu sana
 
Jibu ni kuwa Wao ndio walikuwa 'vilainishi' vya wakoloni kupora!

Ulitegemea TAG au KKKT au Kanisa la Kakobe liwe na shule nyingi wakati halikuwa sehemu ya Agents of Colonialism?, Hizo shule ni sehemu ndogo sana ya resources zilizokuwa zinaporwa chini ya usimamizi wao
Sasa mmesikia wenyewe kwanini kanisani lina shule nyingi
 
Jibu ni kuwa Wao ndio walikuwa 'vilainishi' vya wakoloni kupora!

Ulitegemea TAG au KKKT au Kanisa la Kakobe liwe na shule nyingi wakati halikuwa sehemu ya Agents of Colonialism?, Hizo shule ni sehemu ndogo sana ya resources zilizokuwa zinaporwa chini ya usimamizi wao
Uko sahihi kiongozi wangu
 
Acha kulia lia......
kumbe una akili ndogo kiasi hiki

Kitendo cha Rais Samia kukutana na viongozi wa kanisa Katoliki pekee ni cha kibaguzi sana. Rais anahubiri haki huku akijua kuwa tabia aliyoianzisha ya kuwagawa Watanzania kwa imani ya Dini zao si cha kiungwana.

Tanzania ina madhehebu mengi sana kwa nn ukutane na dhehebu moja tu uyaache mengine huo sio ubaguzi?

Najitahidi sana kulazimisha kukupigiadebe lkn dah yataka moyo kwa hiyo utakutana na wasabato, Walutheri, waanglikani, PAG, Washia wasuni hapana umekosea sana
usiwe maskini wa akili ndugu baraza hilo ndilo lililomuomba aende kukutana nao ktk makao yao makuu pale kurasini ili wazungumzie changamoto zao. kwani kuna dini yeyote iliyomuomba akutane nayo akakataa? mbona kwenye baraza la Eid alikubali kwenda mbona pia alikutana na viongozi wote wa dini pale dodoma hata hivyo amesema huo si mwisho wa kukutana na viongozi wa dini so tegemea pia next time atakutana na wengineo shirikisha akili kabla ya kuchangia ndugu
 
usiwe maskini wa akili ndugu baraza hilo ndilo lililomuomba aende kukutana nao ktk makao yao makuu pale kurasini ili wazungumzie changamoto zao. kwani kuna dini yeyote iliyomuomba akutane nayo akakataa? mbona kwenye baraza la Eid alikubali kwenda mbona pia alikutana na viongozi wote wa dini pale dodoma hata hivyo amesema huo si mwisho wa kukutana na viongozi wa dini so tegemea pia next time atakutana na wengineo shirikisha akili kabla ya kuchangia ndugu
Hakukua na haja ya kuniquote. Hujaelewa kabisa hoja yangu!!?
 
Tunakuomba uimarishe utawala wa sheria na ujenzi wa Taasisi imara za kidemokrasia ambazo ndio msingi wa utawala bora.
Hii ni pointi muhimu mno na inaashiria kuwa serikali ya Magufuli haikuwa ikiongoza kidemokrasia wala kufuata misingi ya haki. Hata serikali yenyewe iliingia madarakani kwa kubaka uchaguzi mchana kweupe. Ni afadhali mwenda angefariki kabla ya uchaguzi na mama Samia aongoze nchi. Kama mwenda angefariki hata mwaka 2016 sasa hivi nchi ingekuwa imepiga maendeleo makubwa sana. Lakini Mungu mwenyewe anajua muda na wakati wa kuingilia kati ndio maana akatenda muujiza mwanzoni kabisa mwa awamu yake ya pili ya uongozi. Tunamshukuru Mungu kwa kila jambo. Amina🙏🙏
 
Samia tupe katiba mpya . Na Mungu atakupa pepo yake amrikiama. INSHAALLAH..!

Mimi nilivyoona anakutana na Catholic leaders akilini kwangu ikanijia kuna siku nyingine hapo mbele atakutana na Waislamu.
Swali je, wewe umewaza hivyo??? Kwani mama Samia siku za kukalia kiti zimeisha mpk ulalamike??? Why always negative guys.
mwambie huyo
 
UKWELI ni nini?

Kweli ni NENO la MUNGU na hilo NENO limeandikwa kwenye Biblia. Sasa kipimo cha "uongo" ni KWELI.

Kanisa katoliki linafundisha kinyume kabisa na KWELI ya NENO la MUNGU.
Soma Wagalatia 1:6-9
Son of Gamba asante sana kwa kuwa na ufahamu ambao wengi sana hawanao na kuwa macho kiroho.
 
usitupotezee muda ndugu kwa vifungu vyako vya agano la kale wakatoliki hawaongozwi kwa sheria bali kwa imani kama Yesu mwenyewe alishasema kama agano la kale lisingelikuwa na mapungufu hakungelikuwa na haja ya agano jipya. amri mpya ya mapendo inakamilisha yote yaliyoko kwenye amri kumi za Mungu pendelea kusoma agano jipya itakusaidia kuiamsha imani yako haba.
Nilishaandika kila kitu kuhusu mafundisho ya kanisa katoliki yanayopingana na "Maandiko".

Nenda kwenye jukwaa la Dini kule utakuta post zangu kuhusu "uongo" wa kanisa katoliki. Ni mambo mengi sana tena sana.

Kwa mfano, angalia Amri kumi za MUNGU zinazofundishwa na kanisa katoliki halafu linganisha na zile zilizoandikwa kwenye kitabu cha KUTOKA 20:1-17

Halafu soma ISAYA 8:19 Kumbukumbu la torati 18:11 uone ni jinsi gani MUNGU amekataza kuwaomba "wafu" lakini kanisa lako linafundisha na kuamini katika kuwaomba wafu.

Soma Mathayo 23:9 halafu uniambie ni kwanini Kiongozi wa kanisa lako unamwita "baba mtakatifu".

Hayo ni machache tu nimekudokeza.

Nilishaandika kila kitu kuhusu mafundisho ya kanisa katoliki yanayopingana na "Maandiko".

Nenda kwenye jukwaa la Dini kule utakuta post zangu kuhusu "uongo" wa kanisa katoliki. Ni mambo mengi sana tena sana.

Kwa mfano, angalia Amri kumi za MUNGU zinazofundishwa na kanisa katoliki halafu linganisha na zile zilizoandikwa kwenye kitabu cha KUTOKA 20:1-17

Halafu soma ISAYA 8:19 Kumbukumbu la torati 18:11 uone ni jinsi gani MUNGU amekataza kuwaomba "wafu" lakini kanisa lako linafundisha na kuamini katika kuwaomba wafu.

Soma Mathayo 23:9 halafu uniambie ni kwanini Kiongozi wa kanisa lako unamwita "baba mtakatifu".

Hayo ni machache tu nimekudokeza.
 
Back
Top Bottom