Son of Gamba
JF-Expert Member
- Oct 26, 2012
- 4,358
- 6,077
usitupotezee muda ndugu kwa vifungu vyako vya agano la kale wakatoliki hawaongozwi kwa sheria bali kwa imani kama Yesu mwenyewe alishasema kama agano la kale lisingelikuwa na mapungufu hakungelikuwa na haja ya agano jipya. amri mpya ya mapendo inakamilisha yote yaliyoko kwenye amri kumi za Mungu pendelea kusoma agano jipya itakusaidia kuiamsha imani yako haba.Y
YESU KRISTO alisema hivi :usitupotezee muda ndugu kwa vifungu vyako vya agano la kale wakatoliki hawaongozwi kwa sheria bali kwa imani kama Yesu mwenyewe alishasema kama agano la kale lisingelikuwa na mapungufu hakungelikuwa na haja ya agano jipya. amri mpya ya mapendo inakamilisha yote yaliyoko kwenye amri kumi za Mungu pendelea kusoma agano jipya itakusaidia kuiamsha imani yako haba.
"Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua Torati au manabii, la sikuja kutangua bali kutimiliza. Kwa maana amini nawaambia mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka yodi moja, wala nukta moja ya Torati haitaondoka hata yote yatimie. Basi mtu yeyote atakayevunja Amri moja katika hizi zilizo ndogo na kuwafundisha watu hivyo ataitwa mdogo kabisa katika ufalme wa mbinguni. Ball mtu atakayezitenda na kuzifundisha huyo ataitwa mkubwa katika ufalme wa mbinguni". Mathayo 5:17-19
"Mkizishika Amri zangu mtakaa katika pendo langu kama vile mimi nilivyozishika Amri za BABA yangu na kukaa katika pendo lake". Yohana 15:10
Ukisoma Maandiko utaona kuna mahali BWANA YESU anasema tujifunze kutoka kwake (Mathayo 11:29). Sasa jiulize ujifunze nini kutoka kwake kama siyo kujifunza kuzishika Amri za BABA yake kama yeye alivyozishika?
Na Je, hujasoma wewe kuwa Yakobo 2:14-17 anasema "imani bila matendo ni bure"? Yakobo anafundisha kuwa imani ili iwe hai ni lazima iambatane na matendo na sehemu moja wapo ya matendo ya imani ni kuzishika Amri. Watakatifu wote wa MUNGU wanazishika Amri.
Malizia kwa kusoma Ufunuo 14:12
"hapa ndipo penye subira ya Watakatifu hao wazishikao Amri za MUNGU na imani ya YESU KRISTO".
Alaaa kumbe! Watakatifu ni hao wazishikao Amri za MUNGU na imani ya YESU KRISTO. Kumbe "imani ya YESU" pamoja na "kuzishika Amri za MUNGU" ndiyo humkamilisha mtu kuwa Mtakatifu!!!
Kama ndiyo hivyo ni Ibilisi gani huyo anayetudanganya kuwa Amri za MUNGU zimepitwa na wakati na hatuna haja ya kuzishika?
Ibilisi huyo ndiye kanisa katoliki, anafundisha uongo na udanganyifu ili kuwapoteza hata wateule wa MUNGU.
Nami nawakumbusha tena, "tokeni kwake enyi watu wangu msishiriki dhambi zake wala msipokee mapigo yake". Ufunuo 18:4