Rais Samia akutana na Baraza la Maaskofu (TEC), Kilaini aelezea Historia yake na utaifishaji wa mashule 1970

usitupotezee muda ndugu kwa vifungu vyako vya agano la kale wakatoliki hawaongozwi kwa sheria bali kwa imani kama Yesu mwenyewe alishasema kama agano la kale lisingelikuwa na mapungufu hakungelikuwa na haja ya agano jipya. amri mpya ya mapendo inakamilisha yote yaliyoko kwenye amri kumi za Mungu pendelea kusoma agano jipya itakusaidia kuiamsha imani yako haba.Y

usitupotezee muda ndugu kwa vifungu vyako vya agano la kale wakatoliki hawaongozwi kwa sheria bali kwa imani kama Yesu mwenyewe alishasema kama agano la kale lisingelikuwa na mapungufu hakungelikuwa na haja ya agano jipya. amri mpya ya mapendo inakamilisha yote yaliyoko kwenye amri kumi za Mungu pendelea kusoma agano jipya itakusaidia kuiamsha imani yako haba.
YESU KRISTO alisema hivi :
"Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua Torati au manabii, la sikuja kutangua bali kutimiliza. Kwa maana amini nawaambia mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka yodi moja, wala nukta moja ya Torati haitaondoka hata yote yatimie. Basi mtu yeyote atakayevunja Amri moja katika hizi zilizo ndogo na kuwafundisha watu hivyo ataitwa mdogo kabisa katika ufalme wa mbinguni. Ball mtu atakayezitenda na kuzifundisha huyo ataitwa mkubwa katika ufalme wa mbinguni". Mathayo 5:17-19

"Mkizishika Amri zangu mtakaa katika pendo langu kama vile mimi nilivyozishika Amri za BABA yangu na kukaa katika pendo lake". Yohana 15:10

Ukisoma Maandiko utaona kuna mahali BWANA YESU anasema tujifunze kutoka kwake (Mathayo 11:29). Sasa jiulize ujifunze nini kutoka kwake kama siyo kujifunza kuzishika Amri za BABA yake kama yeye alivyozishika?

Na Je, hujasoma wewe kuwa Yakobo 2:14-17 anasema "imani bila matendo ni bure"? Yakobo anafundisha kuwa imani ili iwe hai ni lazima iambatane na matendo na sehemu moja wapo ya matendo ya imani ni kuzishika Amri. Watakatifu wote wa MUNGU wanazishika Amri.

Malizia kwa kusoma Ufunuo 14:12
"hapa ndipo penye subira ya Watakatifu hao wazishikao Amri za MUNGU na imani ya YESU KRISTO".

Alaaa kumbe! Watakatifu ni hao wazishikao Amri za MUNGU na imani ya YESU KRISTO. Kumbe "imani ya YESU" pamoja na "kuzishika Amri za MUNGU" ndiyo humkamilisha mtu kuwa Mtakatifu!!!

Kama ndiyo hivyo ni Ibilisi gani huyo anayetudanganya kuwa Amri za MUNGU zimepitwa na wakati na hatuna haja ya kuzishika?
Ibilisi huyo ndiye kanisa katoliki, anafundisha uongo na udanganyifu ili kuwapoteza hata wateule wa MUNGU.

Nami nawakumbusha tena, "tokeni kwake enyi watu wangu msishiriki dhambi zake wala msipokee mapigo yake". Ufunuo 18:4
 
Jambo la msingi tuwe wa kweli ktk kulipa kodi, maaana kuna miongoni mwetu kuna wakati fulani walitumia kivuli cha kanisa kupitisha bidhaa zao, magari na vifaa vingine bila kulipia kodi.
pia tusikubali watu wachache wasio waadilifu kuchafua taswira ya kanisa letu.
kuna walafi wa utajiri, waroho na wadanganyifu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni muda mchache sana tangu Baraza la Maaskofu Katoriki wamualike Mhe. Rais kwenye kikao chao na tukio Mhe. Rais kutoa kauli ambayo imepingwa sana na wapenda demokrasia na utawala wa haki na sheria.

Ushauri wangu kwa Baraza la Maaskofu Katoriki ni wakati mwafaka kutoa kauli ya kile walichoteta na Rais ili kulinda heshima ya chombo chao.

Hii itawaepusha kupotoka kwa Rais kuhusianishwa na mazungumzo naye ya faragha waliyofanya Kurasini baada ya kumuarika kwenye mkutani wao. Kwani walieleza kufanyika mazungumzo ya faragha kabla ya kupata chakula.
 
Ilikuwa mapema mno Baraza la Maaskofu Katoliki kumuamini Samia na kuketi naye na kumpamba kwa sifa kemukemu. Chombo kilichosheheni watu wenye weledi mkubwa watakuwa walipotosha na Katibu wao Dr. Kitima kwa mwaliko huo.

Lakini ninavyowaelewa viongozi hao wa kiroho Dr. Kitima watamshughulikua haraka na watamficha ambako hatasikika tena kama walivyofanya kwa Askofu msaidizi Kilaini baada ya kuonekana kuanza kumsifia Rais kwa sifa asizositahili kipindi hicho akiwa Dar..
 
Ni muda mchache sana tangu Baraza la Maaskofu Katoriki wamualike Mhe. Rais kwenye kikao chao na tukio Mhe. Rais kutoa kauli ambayo imepingwa sana na wapenda demokrasia na utawala wa haki na sheria...
Wewe unayejuwa mazungumzo hayo kati ya Rais na hao mapadre, na jinsi mazungumzo hayo ndiyo yanayosababisha unacholalamikia, kwa nini usiyaweke bayana hapa kuliko kupiga ramli na kuunganisha yasiyokuwepo, bali yamo ndani ya ndoto zako pekee!
 
Rais Samia Suluhu Hassan halisi sasa ndio anajitokeza, baada ya kulembalemba na kuweka hadaa nyingi.

Inawezekana asifikie ngazi aliyofikia mtangulizi wake kwa yale mambo machafu kabisa; lakini dalili tayari zinaonyesha kwamba huenda akatia hasara kubwa zaidi, hasa kwa yale ya mambo ya muda mrefu, ambayo madhara yake hayaonekani kwa muda mfupi.

Huu uchumi anaojenga wa kutegemea watu toka nje ndio watujengee uchumi, na kusahau juhudi za wananchi wetu ndizo ziwe kipaumbele zaidi, huenda tukaleweshwa kwa mategemeo ya neema hizo za nje huku tukijisahau kwamba jukumu la maendeleo ya nchi yetu ni la wananchi wenyewe hapahapa nchini mbele zaidi, wakichagizwa tu na hao wanaokuja kuchuma mali hapa na kuzipeleka kwao.

Mama anafungua nchi, huku akiwafungia ndani wananchi wake na kuwasahau.
 
Rais Samia Suluhu Hassan halisi sasa ndio anajitokeza, baada ya kulembalemba na kuweka hadaa nyingi.

Inawezekana asifikie ngazi aliyofikia mtangulizi wake kwa yale mambo machafu kabisa; lakini dalili tayari zinaonyesha kwamba huenda akatia hasara kubwa zaidi, hasa kwa yale ya mambo ya muda mrefu, ambayo madhara yake hayaonekani kwa muda mfupi...
Noted
 
Rais Samia Suluhu Hassan halisi sasa ndio anajitokeza, baada ya kulembalemba na kuweka hadaa nyingi.

Inawezekana asifikie ngazi aliyofikia mtangulizi wake kwa yale mambo machafu kabisa; lakini dalili tayari zinaonyesha kwamba huenda akatia hasara kubwa zaidi, hasa kwa yale ya mambo ya muda mrefu, ambayo madhara yake hayaonekani kwa muda mfupi...
Umenena ukweli kabisa

Sent from my TECNO LC6 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom