Mkuu umeandika maneno ya maana sana, lakini unfortunately, hali halisi haiko hivyo!
Labda kama unadhani tumepata marais wa dini za tofauti kila awamu kwa bahati mbaya?
Hilo hatuwezi kulikwepa mkuu!
It is an unwritten rule! Akija rais muislam awamu ijayo lazima kutakuwa na maneno!
Sioni kama kuna mtu aliyepata Urais wa ajili ya dini yake. Mwalimu alipotoka madarakani, alitaka nchi iongozwe na Mzanzibar... si kutokana na uhodari wao kwenye kuongoza bali alifahamu harakati za kisiasa za ZNZ... alihofu, akija m-Bara mwingine, ZNZ wanaweza kusumbua sana! INgekuwa lengo kuu la Mwalimu ni nchi kuongozwa na Mwislamu, basi angemwachia Rashidi Kawawa... lakini alitaka Mzanzibari.
It's very (un)fortunately kwamba, utakapoweka kigezo cha u-ZNZ, basi probability ya option husika kubeba na Uislamu ni 99%! Hata hivyo, probability hii kwa Mwalimu aliona ni kama kupiga ndege wawili kwa jiwe moja... jambo la msingi ni kwamba, hata kama ZNZ ingekuwa majority/all ni christians, bado urais 1985 ungeenda huko.
Tukija Mkapa, ingawaje by coincidence inaonekana ilikuwa ni kukamilisha ile trend, ukweli ni kwamba Mwinyi alikuwa ameivuruga sana hii nchi. Hapa Nyerere akataka apate mtu anayemuwamini... mtu anayemfahamu in and out!Kwa bahati mbaya, akadhani anamfahamu Mkapa kumbe alikuwa hamfahamu pamoja na kwamba alimfundisha mwenyewe na kufanya nae kazi!
2005 watu tunapenda sana kujitia upofu! Ulizeni NEC ya CCM 1995... KIkwete alikuwa na nguvu sana kwenye mchujo wa 1995... kama pangekuwa na fairness, JK ndie angesimama 1995 lakini kwa bahati mbaya, Mwalimu alitaka mtu anayemfahamu vizuri ili azibe mashimo yaliyoachwa na Mwinyi. Kwa wafuatiliaji wa siasa za nchi hii, wanakumbuka neno MIZENGWE liliibuka na kushika kasi Dodoma... ni kwamba Mwalimu alimfanyia mizengwe JK. Sasa basi, baada ya uchaguzi wa 1995, JK akajitahidi sana kujiepusha na kashifa zozote... na ile kupewa uwaziri wa foreign affairs kukamsaidia sana kujiepusha na domestic scandals. Hata watoto wake, akawa anasomesha shule hizi hizi za kiswahili, ili mradi tu pasije wakatokea wa kusema "watoto wake wanasoma Ulaya!" Kutokana na hilo, JK akaingia kwenye kinyang'anyiro cha 2005 akiwa na nguvu kubwa mno....Mtu pekee ambae angekuwa tishio kwa JK ni EL na SAS. Kwa bahati mbaya/mzuri, EL akaingia ubia na JK, kwahiyo tishio kuu akabaki SAS!
Hata hivyo, JK alikuwa na advantage moja ukiliganisha na SAS... kule ZNZ, bado zile siasa zao za Hizbu na ASP bado zilikuwa na nguvu... wanazi wa CCM kutoka ZNZ, wakamkwamisha SAS ingawaje watu wanasema JK alimchafua SAS.