Wanabodi,
Kumewahi kuwepo kwa dhana ya urais ni kupokezana kati ya Bara na Visiwani na kati ya Rais Mkristo na rais Muislamu.
Jee hizi ni dhana tuu, ama kiukweli, zina karata ya turufu. katika mustakabali wa taasisi ya urais wa JMT?!.
Kama ilivyotokea kwa mwanzo, watu kudhani marais kupokezana kati bara ya visiwani kwa Nyerere kutoka bara, then akaja Mwinyi kutoka Zanzibar, then Mkapa kutoka bara, aliyemfuatia Mkapa, hakupaswa kutoka Zanzibar?!. Kitendo cha rais kutoka bara, akafuatiwa na rais kutoka bara, kume break the circle ya coincidence ya kupokezana, na huu ni uthibitisho kuwa kwenye urais wa JMT, kupokezana ilikuwa ni dhana tuu!, hakuna kupokezana, rais ajaye, anaweza kabisa kutoka tena bara, na ajaye kutoka bara na anayefuatia na anaye fuatia hadi uwezekano wa rais wa JMT asitoke tena Zanzibar!.
Au rais ajaye, pia anaweza kutoka Zanzibar, akafuatiwa na Mzanzibari, akafuatiwa na Mzanzibari tena na tena tena na hata kuna uwezekano rais asitoke tena bara, kwa sababu hatuna utaratibu wa kupokezana!.
Vivyo hivyo kwenye hili la udini, Tanzania ni secular state, serikali haina dini, ila watu wake wana dini zao!. Rais nchi hachaguliwi na serikali isodini, bali huchaguliwa na watu wenye dini zao!. Jee kuna uwezekano, wa dini ya mgombea urais kuwa ni moja ya vigezo, vitakavyomfanya achaguliwe?!.
Japo haijaandikwa popote kuwa urais unapatikana kwa kupokezana kwa zamu, kati ya Wakristu na Waislamu, ila ni ukweli halisi kuwa by coincidence tuu Nyerere alikuwa Mkristo, akafuatiwa na Mwinyi, Muislamu, then Ben, Mkiristo, akaja JK Muislamu, hivyo 2015 coincidence inapaswa ku play in favour ya ni zamu ya Mkristo? If we don't break it!.
Vivyo hivyo hata kama imetokea rais wa kwanza akawa ni Mkristu, akafuatiwa na Muislamu, then akaja Mkristu, na sasa aliyepo ni Muislamu, kwa vile hakuna utaratibu rasmi wa kupokezana, ili kuundoa mfuatano huo wa coincidence tuu, mnaonaje kama rais ajaye awe Muislamu tena, na tena this time atoke Zanzibar, ili kupunguza marais wa kutoka bara tuu ndio wafuatane, yaani Mkapa alitoka bara, JK ametoka bara, na 2015 mnataka kutuletea tena rais wa kutoka bara?!, huu utangua kweli ni muungano wenye usawa?!.
Tukikubali to break the circle, ya urais hakuna kupokezana, wala hakuna zamu, pia tunaweza ku break kale ka secret code kuwa amkiwa Mkristo basi ni lazima awe wa dhehebu fulani!, yaani tujiaminishe kuwa kuwa rais alipokuwa Juliasi, it just happened kuwa pia alikuwa ni Mkatoliki, na alipokuja Bunyamini, pia it just happened alikuwa Mkatoliki, hivyo hata akija Membe ambaye ni Mkatoliki, it will be "just happened!", can't we break the "just happened!", kwa kuhakikisha wengine wenye uwezo nao pia wanakuwepo kwa kuthamiria to break the circles za just happened?!.
Yaani Tanzania tuendelee kuchagua rais kwamere coincidence kuwa it just "happened" au tudhamirie kumchagua kwa sababu?!.
Namalizia kuuliza, jee suala la zamu, kupokezana kati ya bara na visiwani, na kupokezana Wakristo na Waislamu, zina turufu yoyote katika siasa za urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?!.Do they just happened by a mere coincidence, na sisi tnaziacha hizo mere coincidences zi play part katika nafasi ya urais, or its about time to break the circle kwa kumchagua rais mpagani asiyetoka bara, wala visiwani?!.
Pasco