jmushi1
Platinum Member
- Nov 2, 2007
- 26,375
- 25,454
- Thread starter
- #401
Mkuu umeenda kwenye argument kwa kuniita mdini kwasababu tu nimesema utamaduni tulio nao ambao wengine mnauita bahati mbaya na mimi nasema ni mzuri?Ebu kaa na soma maandishi yako mwenyewe halafu nambie una discuss au una argue?..
Na rudi kunisoma miye halafu unambie kama na discuss ama nina argue maana mimi nakueleza hadi chimbuko mla kila hoja na nakupa mifano wewe umekazania kuwalaumu waislaam. Ni wapi mimi nimewalaumu wakristu kama sio wewe mdini?.
Mkuu hata hayo ya waislaam kujiandikisha kupigana ni fikra zako kwa sababu huwezi kunielezqa sababu gani Watanzania walikwenda kupigana vita ya South Afrika, Angola, Msumbiji na kadhalika kama ilikuwa Uafrika ama kuutaka Uhuru wao. Kwani hao hayo Mataifa mengine hawaendi kupigana vita nje? Juzi tu wamekufa Wamarekani wawili ktk vita ya Gaza na waliandikishwa wengi kupigana vita ya Bosnia.
Na ajabu ni kwamba huhesabu Waamerika na mataifa makubwa wanaokwenda nchi ya wengine iwe Iraq, Misri, Syria au Libya kwamba ni wadini kujiandikisha kupigana huko ila wale wanaojiandikisha kuwalinda wenyeji wa nchi hizo. wakenya na Ethipia wameingia vipi Somalia nchi isokuwa yao kupigana vita kama sio ushenzi halafu mashambulizi upande toka wa pili ni Ugaidi.
Mimi ni natinalist, napingana na Wazanzibar na napingana na utawala huu wa CCM bila kujali rais ni Kikwete au Mkapa. That's me!
Pia si nimesema huwezi kusema kuwa wewe si mdini kwasababu tu unaishi kwenye nchi ya magharibi?