Pesa ya lodge wewe, pesa ya chakula na vinywaji wewe, mkimaliza kuzini pesa ya nauli wewe, pesa ya matumizi wewe. Kijana, tafakari una akili timamu?

Kiboko ya Jiwe

JF-Expert Member
Apr 7, 2020
12,705
36,157
Ngono ni kitu kinachotukuzwa sana bila ya sababu za msingi. Mwanadamu ana matamanio makuu 3.
1. Kufanya ngono
2. Kula na
3. Kutawala (kuwa kiongozi, kumiliki mali na vitu vizuri).

Kijana amepata kibarua siku analipwa posho yake anahaha kutafuta kabinti wakale kahela kake ambako ni kadogo.

Ila kwakuwa kichwani mwa kijana mpumbavu kumejaa uchafu hakuna shida atalipia lodge, atampa nauli ya kuja na kurudi huyo binti. Binti atanunuliwa chips na kuku na kama mlevi basi atamlewesha na mwisho wa safari itambidi ampe pesa ya kumuhonga na binti malaya asiye na aibu, aliyekosa mafundisho sahihi atapokea pesa mimacho imemtoka na ataanza kutaja shida zake zingine.

Kijana amka.

Kijana huyu mpumbavu ataponda kapesa kidogo anachopata akijisemea maendeleo atafanya akipata kazi nzuri. Uzee unamjia, anakwenda kuzeeka na ufukara.

Kijana mzinzi hata akipata pesa kiasi gani ni bure kabisa. Kama kichwa chako hakiwezi kutulia bila kuwaza ngono ni vyema uoe. Si lazima ufanye sherehe. Hata kusogezana sio mbaya ilimradi tu mumeelewana na wazazi wenu wanatambua. Ndoa sio ile sherehe na makamera. Ile ni sherehe tu. Nendeni kwa mchungaji awafungishe ndoa ofisini kwake au mwiteni ustadhi awafungishe ndoa nyumbani kwenu.

Zinaa inaondoa baraka. Zinaa inakusogeza karibu na kifo.
 
Na ukioa utawaza hapo home pesa ya kula wewe, kadi wewe, luku wewe, uniform za madogo wewe, dstv wewe, nguo za wife wewe.

Hivi huwa unajua kuzaliwa mwanaume ni tofauti na kuzaliwa mwanamke? Sasa wewe ulitakaje boss, mkienda Lodge alipe bidada na pombe akununulie?

Huna hela tu
 
Back
Top Bottom