Osama bin Laden killed!

Osama bin Laden killed!

Status
Not open for further replies.
Hii ni sawa sawa na Kumuua Yesu.. watu wanashangilia kumbe kuna mitume wamejibanza mahali.. wanasubiri time yao ifike waanze kumwaga neno!

Weweeee! Usimfananishe huyu mshenzi na YESU! Yesu alifia watu na huyu aliua watu! Jitahidi kuwa makini unapochangia humu usijeonekana mropokaji! Yesu afananishwi na yeyote hata kama ni mtu mwema kiasi gani. Tuko makini sana
 
Actually Wapakistani wanadai walishiriki, Wamarekani wanasema hawakuambiwa mpaka baada ya tukio so theory yako haileti maana yoyote.

Kama Pakistan inaogopa retaliation wasingedai wameshiriki.

Wamarekani gani wanasema hawakuambiwa
Nachokuambia ukweli kuwa taifa la pakistan livlivyo serikali au viongozi wa gazi ya juu ya pakistan haiwawezi kuweka wazi ushiriki wake. Labda ije wiki leak nyingine. Hao wapakistan wasema wameshiriki ni watu wa kawaida sio viongozi wa jeshi wala rais.

Same kama kamashambulizi yaliyokuwa yanafanyka Yemen. Theory haileti maana lakini ndo hivyo. zipo theory nyingi kama hizi inategema uko side gani
 

Sio kwamba hizo helikopter zime fly below radar. Ni kwamba wapakistan hawtaki kuonekana kama wameshiriki.

Eneo hilo kuna kitua cha kijeshi na pia sio mbali sana kuna ka kituo ka nyuklia. No way hata simple radar ishndwe kuona low flying helicopter.

Hii movie ni kwamba serikali ya pakistan wanaogopa kuonekana wanashirikiana na marekeni


Mkuu sidhani kama ni kweli usemayo. Kwa mujibu wa balozi wa pakistani nchini uingereza akihojiwa na CNN leo hii kasema waziwazi kua pakistani ni mshirika madhubuti katika vita dhidi ya ugaidi/al qaeda. Na kuthibitisha hilo kadai nchi yake imeshambuliwa mara nyingi zaidi kuliko nchi nyingine na magaidi. Wananchi wake (civilians)wengi zaidi wameuawa na wengi zaidi kujeruhiwa kuliko nchi nyingine. Wanajeshi wake wengi zaidi wameuawa na wengi kujeruhiwa kuliko wa nchi nyingine. Hivo kadai wao wako full committed na hiyo ndo price na sacrifice waitoayo kama matokeo ya ushiriki
 
Kama uliwaamini kwamba Osama bin Laden ana-exist kwa nini usiamini kwamba kauwawa? Or have you seen Osama face to face? Unataka uende kukagua maiti? If you did depend on the media from the start on all these information about Osama why hesitating today? Camon man...

Hongera sana Mgalanjuka kwa kugalanjula maelezo yenye mantiki. Umenifikirisha sana.
 
wanajidanganya wamewasha moto upyaaaaaaaaaaaaaaaaaa!

Hamna kitu. Alqaeeda wenyewe tuliobakia hata mhogo unatushinda kununua jamani. Angalia tu jinsi grafu ya misaada iliyokuwa ikitolewa na osama siku za karibuni ilivyoshuka tofauti na zamani. Waliobakia ni wahuni tu wenye shida ya kupewa misaada
 
we need credible sources.
There are thousands of those websites that are loaded up with full of crap.
 
Akili mgando!!
Kama Osama wako yupo basi si ajitokeze na awaumbue wakina Obama ama atoe CD/DVD ama vijitapes vyake?

Vuvuzela napingana na mtazamo wako kwa kiasi kikubwa. Lazima tufahamu Osam was a normal human being like us though dangerous, kuugua na kufa nae pia alipaswa ku-experience the same. Tell me " who knows kama Osama kisha kufa siku nyingi, wame-prove hilo na ndo wanakuja na uongo wao" kwa kujua hawezi kutoa CD/DVD au tape. Hukumbuki Bush aliwahi kutangaza hilo before?
 
Sijasema DNA ina-prove death. DNA ina prove identity! Waislamu wanazika ndani ya 24hrs. Hiyo ni ku-respect dini yao maana hawataki attack yeyote kutoka kwa waislamu kuwa hawaja heshimu dini yao, nk. Maana watu wanapenda kudandia kosa lolote ilimradi wapate sehemu ya kuponda na kushtumu!
wakibaki na mwili watapata faida gani?
Ku-respect dini yao ndio kutupa mwili baharini!?

Mi nilikuwa sijui kuwa Waislam ni kawaida yao na ni jambo la heshima kuzikwa baharini.
 
Ni uongo wa Serikali ya Obama kuwa Osama bin Laden eti wamemuwa na Maiti yake kuizika Baharini Wa Tanzania amkeni acheni Usingizi. Tunachotaka Ushahidi wa picha za Osama kama Bush alivyo Wauwa na kuonyesha Picha za Watoto wa SAADAM HUSSEIN walivyouliwa IRAQ, huo ni uongo wa Rais Obama kumuuwa Osama Bin Laden na kumzika eti Baharini Wabongo Amkeni jamani. Uongo wa Serikali ya Marekani kumuuwa Osama ni kama Uongo wa Mayahudi kumuwa Bwana Yesu Kristo na hawakuumuwa huyo YEsU hao Wayahudi.

Wee nawe khaaaa
 
Wakati Osama anafaidi 'bikra 72' ngoja wengine tuendelee na maisha yetu ya kila siku.

Bikra zitoke wapi? Huwa wanajidanganya! Kwa hiyo wanawake wao watakwenda kupata nini? Wanaume wenye maumbile makubwa au? Hizi imani zingine wala sizielewi kabisa kwa akili ya kibinadamu jamani! Aangalie asije jikuta anageuziwa yeye kibao, si unajua tabia za waarabu? Watafanywa hivyo hivyo.
 
Hamna kitu. Alqaeeda wenyewe tuliobakia hata mhogo unatushinda kununua jamani. Angalia tu jinsi grafu ya misaada iliyokuwa ikitolewa na osama siku za karibuni ilivyoshuka tofauti na zamani. Waliobakia ni wahuni tu wenye shida ya kupewa misaada

> America wanaufanya ulimwengu mzima bunch of fools lakini hebu waulizwe wamerekani how much has costed to secure bin Ladin, na huu ndio mwisho wa safari ?
 
Vuvuzela napingana na mtazamo wako kwa kiasi kikubwa. Lazima tufahamu Osam was a normal human being like us though dangerous, kuugua na kufa nae pia alipaswa ku-experience the same. Tell me " who knows kama Osama kisha kufa siku nyingi, wame-prove hilo na ndo wanakuja na uongo wao" kwa kujua hawezi kutoa CD/DVD au tape. Hukumbuki Bush aliwahi kutangaza hilo before?

Bush hakuwahi kusema Sheikh Osama kafa. alisema anamtaka dead or alive!
 
Interesting timing by Obama's feat. But I am afraid of the political consequences if it can play a winning card for the next presidential elections.
 
Unajua ukimiliki vyombo ya habari unamiliki na akili za watu wasiopenda kufikiri, bbc news wamesema kapigwa risasi ya kifua, jioni ya leo CNN NEWS wamesema kapigwa risasi za macho. The Sun wamesema alikuwa kalala ndani kwake elikopta ikamshambulia, habari zingine zinasema kazikwa na watu wachache baharini, Marekani walisema wanamtaka Osama akiwa hai au amekufa, Osama kauwawa usiku halafu kazikwa asubuhi. Ahahahaha..
.

Hii ni project ambayo imeandaliwa muda mrefu sana, vyombo vya habari viliandaliwa kueneza huu uongo na propaganda....for sure leo nimegundua pia umbumbumbu wa raia wa Marekani, kwa kushangilia kiini macho hiki. This is totally fabrication.
 
You can't fool great thinkers Straatkasyambe, do you see how Mkasika has reveal your silly post? Don't Try It again!

Okey, man this what you believe. But let me tell you comred,.. Obama during his compaign in last election he promised to Americans withdrow to all America soldiers fighting and closing Guantanamo Bay and now its fact that Obama will contest for next election. Do you think the decision of Obama to close Guantanamo and killing of Osama is by concidence or its just preparing somebody's issues for campaign?. But it depend on what you believe on such media comred, i can not force you on what you believe, but what i posted is a link from people who view things altenativery
 
Ajabu zaidi kuna picha imetumika kuonyesha kama ndio maiti yake, lakini baada ya wataalam kuiona wakagundua kuwa hiyo picha si kweli ya Usama Bin Laden.

Hapa chini ni picha iliyotumika kwenye magazeti makubwa duniani kama Mail, Times, Telegraph, Sun na Mirror. Lakini baadae waliziondoa picha zote baada ya kugundua kuwa si za kweli (fake pictures).

An-image-purporting-to-sh-004.jpg




It appears the fake picture was initially published by the Middle East online newspaper themedialine.org on 29 April 2009, with a warning from the editor that it was "unable to ascertain whether the photo is genuine or not".

NOTE: Niliwahi kusoma zamani kuwa huyu jamaa alisha fariki siku nyingi.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom