Mkono Mmoja
JF-Expert Member
- Jan 26, 2019
- 1,932
- 4,086
Kero ya usafiri Kimara Termina ni kubwa sana muda wa kuanzia asubuhi mpaka saa 6 mchana.
Msongamano wa watu ni mkubwa sana na mabasi yenu ni machache.
Toeni tenda watu binafsi waingize mabasi kwenye hii njia yenu, maana inaonekana kazi imewashinda.
Msongamano wa watu ni mkubwa sana na mabasi yenu ni machache.
Toeni tenda watu binafsi waingize mabasi kwenye hii njia yenu, maana inaonekana kazi imewashinda.
Leo tena inajirudia karaha ya siku zote, abiria wanasota vituoni korogwe na Kimara kwa zaidi ya masaa mawili wakisubiri gari yenye nafasi wapande waingie katika uzalishaji mali na kuliendeleza taifa.
Binafsi nimefika kituoni saa moja asubuhi mpaka saiz saa tatu na nusu sijaweza kupanda kwenye gari. Hii sio mara ya kwanza. Ni Bora kama wenye dhamana ya kutatua kero hii wakae pembeni wanatukwamisha katika maendeleo kama taifa.
Wanafunzi wanafika shuleni saa 4 kisa usafiri tabu, wananchi wanashindwa kuwahi kazini. Hivi ni kweli kabisa hili haliwezekani kutaftiwa ufumbuzi?