Tumeanza kulazimisha mabasi na abiria kwenda kupakia stendi kuu?

Rufaro

JF-Expert Member
May 7, 2022
222
340
Sijui niseme ni kukosa hekima au ni makusudi.

Baadhi ya makampuni ya mabasi waliamua kukodi ama kujenga vituo vyao binafsi vya mabasi kwa ajili ya urahisi kwa abiria wao na kuepuka usumbufu usio wa lazima kutoka kwa wapiga debe huko stendi na hata wizi.

Na naamini kama ni kukodisha ina mana wanalipa kodi ya mtu binafsi na serikali, kama kuna huduma zinaendelea kama mgahawa na mengineyo ina mana kuna risiti za efd na kodi inalipwa. Je, kutaka kulazimisha mabasi hayo pamoja na abiria wapande usafiri wa daladala waende kupandia stendi kuu ni HAKI?

Ni kwamba serikali inaona wivu au chuki kwa wananchi hao hawapati usumbufu?

Katika hali ya kustaajabisha, leo katika moja ya kituo binafsi cha mabasi yanayoenda mikoani, abiria wameshushwa kwenye gari na kulazimishwa kupanda daladala tena kwa garama zao na kwenda stendi kuu, na basi kulazmishwa kwenda kupakilia stendi kuu, na hio imepelekea abiria kuchelewa sana kuondoka ..je hii ni sawa? Tumefikia huku? Mbona kama akili za kihayawani hizi?

Waacheni wawekezaji WAZAWA wa usafirishaji wafanye biashara zao alimradi wanalipa kodi na tozo zenu, waacheni wawajali abiria wao na kuwatengenezea mazingira mazuri, nalaani sana kitendo hicho kilichofanyika.
 
Hivi haiwezekani kuwadhibiti wapiga debe na matapeli pale Mbezi Louis au ni uzembe wa mamlaka husika.
 
Nikiambiwa kuchagua stand. Heri stand ya zamani Ubungo kuliko Magufuli. Mbwembwe nyiiiingi lakini haina lolote.
 
Siamini unachokisema. Imagine mtu anayeishi Masaki, Tegeta, Mbezi beach, Mabagala, Temeke na sehemu zoote ambazo kiungo chao kikuu kilikuwa Ubungo, sasa wabebeshwe mzigo wa kukodi taxi, kupanda boda au bajaji mpaka huko wanakosema kiwe kituo pendwa? Kwanza tujiulize wakati wazo linatolewa, kullikuwa hakuna washauri upande wa barabara, mawasiliano na uchukuzi? Ni mahesabu yapi yalitumika kujenga kituo huko Mbezi?

Nchi hii inaendeshwa kwa mihemko na kuridhisha waliomadarakani. Hakuna kujali raia wala utu wao na uwezo wao.
 
Kituo chenyewe cha Mbezi ni HATARISHI KWA AFYA YA WATUMIAJI. Mabasi yanayokuwa chini na yote yanakuwa yanewashwa asubuhi, kuna moshi mwingi sana.

Moshi unazuiwa na paa na hivyo usambaa kwenye mabasi yote ya ayokuwa chini na wakati huo yote yanakuwa tayari yamepakia abiria. Kituo hiki kitakuwa chanzo cha magonjwa mengi ikiwemo kansa ya mapafu. Naomba wataalam waangalie upya
 
Moja ya kero kubwa San awamu ya tano ilifanya ni kuamisha stand kongwe na kuzipeleka nnje ya mji mfno stand ya iringa na ddm pmj na babati ziko nnje ya mji kuja mjini kutoka huko Ni elf nne mkp tano imagine.

Ni kero kwa kweli.

Ila pia hzi stand bubu zimezidi Happ shekilango ziko nyingi mnoo sioni sababu kuwepo stand pale labda chanika mbaga na kigamboni ni sawa.

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Siamini unachokisema. Imagine mtu anayeishi Masaki, Tegeta, Mbezi beach, Mabagala, Temeke na sehemu zoote ambazo kiungo chao kikuu kilikuwa Ubungo, sasa wabebeshwe mzigo wa kukodi taxi, kupanda boda au bajaji mpaka huko wanakosema kiwe kituo pendwa? Kwanza tujiulize wakati wazo linatolewa, kullikuwa hakuna washauri upande wa barabara, mawasiliano na uchukuzi? Ni mahesabu yapi yalitumika kujenga kituo huko Mbezi?

Nchi hii inaendeshwa kwa mihemko na kuridhisha waliomadarakani. Hakuna kujali raia wala utu wao na uwezo wao.
HAWA WANASIASA... WAMEPUNGUZA MSONGAMANO NA FOLENI MJINI...UNAAMBIWA ZAMANI STEND ILIKUWA MNAZI MMOJA... BAADAE WAKAIHAMISHIA UBUNGO(zamani ilikuwa ndio nje ya mji)... JUST FOR THEM NOT YOU... KUPUNGUZA KERO...

NA HAPO UBUNGO NAPO PAMEKUWA KERO... MKAPELEKWA MBEZI LUIS...

HIVI ILE DARAJA YA MFUGALE PALE TAZARA... WALISEMA YAPUNGUZA FOLENI... FOLENI GANI PALE IMEPUNGUZA? TUSEME NI FOLENI YA VIONGOZI, WANASIASA YA WAGENI WANAOTOKA AIRPORT TO CITY CENTER...

THOSE MIKOPO NA MISAADA KUTOKA NJE NDIO HELA INAYOHAKIKISHA MISHAHARA YA WANASIASA... HALAFU HIZO KODI MNAZOTOZWA ZINATUMIKA KULIPIA MADENI... ILI NCHI IENDELEE KUAMINIKA KWENYE KUKOPESHEKA...

THOSE SO CALLED MAENDELEO... NOT FOR YOU... JUST FOR THEM "WANASIASA"...
 
Stand ya Magufuli Mbezi ni kichefuchefu wala siwezi kuingia kule, kumejaa wezi na matapeli
Yani acha tu mkuu..yan mimi tajiri nimewekeza nchi hii nalipa kodi kila siku na kwa wakati haalafu unasumbua abiria wangu bila sabab za msingi..ni ujinga!
 
Yule kambale na wasaidizi wake walijenga likituo mahali sio rafiki, pesa imemwagikia chini sasa ndiyo viongozi bongolala wanalazimisha ili wapate ushuru
hakuna asiyejua ile ilikua project ya watu flan flan ya kulazmisha, hua siku zote wanawaza kupiga hela na sio kuangalia future
 
Stand inatakiwa iwe katikati ya mji. Mtu unaishi Chanika. Ukapande basi la kwenda Mwanza mbezi mwisho. Duh
 
Stand inatakiwa iwe katikati ya mji. Mtu unaishi Chanika. Ukapande basi la kwenda Mwanza mbezi mwisho. Duh
Wanawachezea hawa matajiri, hii lazima italeta shida tu..mimi nina lipa kodi ya mabasi kama 20 halafu unaninyanyasia abiria wangu
 
Back
Top Bottom