Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

hebu nisaidie:

a. Tumepata Uhuru 1961
b. Wakati huo huo tunakabiliwa na njaa 1962 na mapungufu makubwa ya chakula
c. Tunaungana 1964 na maasi ya 1964
d. Kujenga Taifa lililoungana
e. Inapofika 1967 watu wachache wameanza kujilimbikizia mali kwa kiasi kikubwa, weusi walioingia madarakani wameanza kujifanya miungu watu.
f. Azimio la Arusha linatangazwa kama jitihada ya kwanza na ya wazi ya kupambana na ufisadi. Mirija ikanyang'anywa.
g. 1970 upungufu wa mafuta kimataifa
h. Njaa ya 1974 (ambayo Nyerere aliileta according to Koba)
i. Hali mbaya ya kisiasa Uganda, na kutuweka katika hali ya wasiwasi
j. 1977 Kuvunjika kwa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki (kisa Nyerere)
k. 1978 Vita na Uganda
j. 1979 Vita inakwisha tunabakia na jukumu la kulinda amani na kuhakikisha Uganda inanusurika.By 1981 naamini wanajeshi waliobakia wote wanarudi nyumbani
h. 1983 tunaanza kupata mapungufu mengine ya chakula (kumbuka we go through this circle every 10 or so years)
i. 1984 IMF na WB wanaendelea kutoa masharti magumu ya mikopo, Mwalimu anawatolea nje
j. KUtokana na kugongana kwake mawazo na vyombo vya fedha na kuweza kuona mgogoro wa huko mbeleni, na akiwa na haja ya kuweza kuona Mtanzania mwingine atafanya nini, Nyerere kwa hiari yake anang'atuka.

Sasa, niambie with all those odds, ambazo Kenya haikuingia, tulifanikiwa kiasi gani? Nadhani tungekuwa na hali mbaya sana kama Taifa kuliko tulivyo sasa, don't you agree?

Mwanakijiji:

More than 75% za odds ulizoweka hapo ni MAN MADE. Kabla sijakubali au kupinga, je kulikuwa hakuna uwezekano wa kuondoka na hizo odds?
 
Nationalization of schools and quota prog ilisaidia mikoa iliyokuwa nyuma nayo kupata nafasi ktk elimu! Hii imesaidia kupunguza gap pia kati ya maskini na matajiri!

Wengi wetu hapa JF tuko hapa kutokana na sera za Mwal. ktk free na quota education.

Nakubaliana na wewe kabisa kuwa ulifaidika na hiyo quota. Je katika mchango wako wa taifa umesharudisha angalau 10% ya gharama zilizotokea.

Kumbuka kuwa kulikuwa na watu tayari wana taasisi zao. Na kuchukuliwa kwa taasisi zao kukusomesha wewe ilifanya wao warudi nyuma.
 
Nakubaliana na wewe kabisa kuwa ulifaidika na hiyo quota. Je katika mchango wako wa taifa umesharudisha angalau 10% ya gharama zilizotokea.

Kumbuka kuwa kulikuwa na watu tayari wana taasisi zao. Na kuchukuliwa kwa taasisi zao kukusomesha wewe ilifanya wao warudi nyuma.

Bin Maryam,

Mchango wangu ni kuwa na taifa moja na kutohisi kutopewa opportunity kwa kutoka mkoa uliokuwa nyuma kielimu! Faida zake ni kubwa- haya unayoyaona Kenya leo hii Nyerere alishayaona na kujaribu kuwapa nafasi wote kupitia quota!

Je wewe unashauri- mimi nilipeje kwa kupata elimu kama jamii ya mkoa uliokuwa nyuma na maskini?

Everything has a price- but in a large picture as a nation the policy was a plus!

Sasa sii unaona ni watoto wa matajiri tu ndo wanasoma shule nzuri? Is this healthy?
 
Bin Mariam,

Nimekusikia sana mkuu ukitoa mlolongo wa maelezo kuhusu kufanikiwa ama kutofanikiwa kwa Nyerere kiasi kwamba sasa hivi itakuwa kazi kubwa sana sisi kuweza kuelewana kwani unachodai wewe yawezekana kuna ukweli na kile wanachosema waandishi wengine kina ukweli vile vile, hivyo basi sielewi hicho kipimo cha mafanikio mnachojaribu kukiangalia kinatokana na factors zipi?...
Kisha sintapenda kubishana kwa sababu mtu fulani alisema hivi ama habari za kusikia kuwa Tanzania tulikopa fedha mahala fulani wakati hatuna ushahidi huo zaidi ya maneno yanayofumba akili za watu. Na tukashindwa kuelewa mtu hukopa kwa nini na mkopeshaji huitoa fedha kwa kuangalia vitu gani!...

Ebu turudi nyuma kidogo wakati huo wa Nyerere ambao umedai kuwa Elimu ilikuwa chini, Maradhi na Umaskini ndio yakajenga maskani...
Nakuomba unipe kipimo cha madai hayo kama unalinganisha na nchi nyinginezo ama Umechukua wapi tulikuwa kabla ya Uhuru na tulifikia wapi baada ya Nyerere kushika na kujiondoa madaraka...kwani navyofahamu, wengi hapa hawafahamu kabisa kipimo cha Tanzania kabla ya Uhuru ktk fani zote ulizozitaja hapo juu na tulipiga hatua gani mbele ama nyuma.
Halafu kumbuka kama unalinganisha na nchi nyinginezo sidhani kama utakuwa unamtendea haki mwalimu kwani wengi wa hawa jamaa waliachiwa mirathi ya Utajiri huo, nchi Kama Kenya, Msumbiji, Malawi, Zambia, Zimbabwe na kadhalika zilikuwa na uchumi bora (nafasi yao ktk mataifa) wakati wa mkoloni kuliko walivyo leo hii.. Je tunaweza sema viongozi wao walishindwa kuleta mafanikio!.
2. Swala jingine la kujiuliza ni kuwa nchi kama China na India ndizo zilikuwa super Power wa Uchumi duniani toka karne ya kwanza hadi ya 18, leo hii wameshuka daraja.. Je, viongozi wao wameshindwa Kiuchumi hivyo hakuna mafanikio?...
Leo hii China na India wanakuja juu vibaya sana kuliko hata nchi za Ulaya - Je, kuna uwezekano kuwa viongozi wa nchi hizo za Ulaya na Amerika wanashindwa kuleta mafanikio ktk nchi zao...

Nikirudi nyuma ktk swala la Afya na Umaskini - Mkuu wangu unaelewa kabisa kuwa Tanzania hatukuwahi kusikia Maleria as an epidemic...aghalabu kumsikia mtu kafa kwa Maleria labda tu kwa bahati mbaya alichelewa kwenda Hospital. Magonjwa kama Matende.TB na Ukoma vilikomeshwa kabisa only yamekuja jitokeza tena sasa hivi. Ugonjwa mkubwa wakati wa Nyerere ulikuwa Kipindu pindu na mara zote kilipojitokeza tu mkakati uliwekwa na hivyo watu wachache sana walipoteza maisha yao.
Wakati wa Nyerere ahtujawahi kusikia watu wakifa njaa hata kama tulikuwa ktk hali mbaya kiuchumi.. swala la kufa njaa halikuwepo kabisa lakini leo hii kufa njaa kunakubalika na ni umaskini wa kawaida kabisa kwa nchi zote za Kiafrika, Usipokufa njaa utakufa vitani...Na swala la kusema Elimu na afya bure ni makosa mbona hapa mjomba tunazipata huduma hizo bure?... Je Canada wana kasoro gani ama unachukulia maendeleo ya kitu ni kufanianisha na mfumo wa Marekani tu.

Mwisho nitarudia kusema ya kuwa hivyo vichache mwalimu alivyoweza kujenga nina hakika hakuna kiongozi hata mmoja sii Tanzania ama nchi za Kiafrika ameweza vijenga ndani ya Utawala wake. Reli ya Uhuru, viwanja vya ndege na shirika lake from scratch..viwanda vya kisawasawa visinyopungua 1000 na mashirika ya uzalishaji kila wilaya huu ulikuwa msingi bora ambao hauwezi kupita bure bila pongezi...As a fact jumlisha vitu vyote walivyojenga Mwinyi, Mkapa na JK as infrastructure bado hawawezi kumfikia mwalimu kwa hesabu yake acha mbali kuhesabu fedha kwani bila shaka hawa jamaa watashinda ktk matumizi ya fedha...
Nitakuacha na swali moja tu... Ikiwa mwalimu aliturithisha nyenzo za Ualishaji, majumba, vitega Uchumi, madini na kadhalika tukashindwa sisi kuviendelea ati tutazame aliacha ngapi benki, kweli huu ni uchumi bora jamani?... Hata mimi mfanyabiashara uchwara natazama utajiri wangu kwa assets nilizokuwa nazo, soko lililokuwepo pamoja na uwezo wa kutoa huduma ama kuzalisha kulingana na soko hilo badala ya kutaama ninazo dollar ngapi Benki kama akiba. Hata napotaka kuuza kijikampuni changu hakuna mteja atakaye taka kujua nina kiasi gani Benki ili apate kunipa mshiko wa kiuhakika badala ya kutazama vitu muhimu. Ni kwa mtaji huo wa assets aliotuachia Nyerere ndio tuliweza pata mikopo kwa utrahisi zaidi, Tanzania pamoja na kuwa na madeni yetu tulionekana kuwa nchi yenye kila nafasi ya kuendelea na uwezo wa kulipa ulikuwepo hii haitokani na sura ya Mwinyi kwenda kuomba msaada ama grant. Hakuna mtu atakayekupa fedha kwa huruma ati maskini na huna kitu benki!...fedha zinakopwa kutokana na uhakika wa kupipa yaani credit yako ni nzuri... Mwalimu ndiye mjeni wa credit hiyo, uhakika wa nchi kurudisha fedha hizo. Nakuuliza tena ni kiasi gani cha fedha ktk mikopo hiyo Mwl. Nyerere alipata kusamehemewa?....Je, kama hawa kina Mwinyi na Mkapa wangekuwa hawapati msamaha mkubwa wa fedha hizo za mikopo kwa masharti magumu hivi leo tungekuwa na deni la kiasi gani?..Huko Hazina kungekuwa na kitu gani!...na ebu tutazame nyuma hivi hawa jamaa wamejenga kitu gani haswa kwa hiyo mikopo?.. Nambieni vitu vilivyojengwa worth kujivunia kuwa leo hii tumepiga hatua kama sio hilo Daraja la huko Kusini (bila barabara ya maana) na huo Uwanja wa Mpira.. (tukiwa na timu mbuvu)..as a fact tunalipa fedha zaidi kwa makocha, zawadi kwa wachezaji na viongozi wake kuliko mfuko mzima wa budget ya mkoa wa Dar ktk Elimu. Na hadi leo hatujafikia record aloiacha mwalimu ktk micheo na sidhani kama tutaweza ifikia hata siku moja tukarudi na Medali Olympic games kwa mfuko wa serikali...
 
Damn it Mkandara, kila siku wadai wapata shule kumbe wewe ndiye Kungwi Mkuu!

Kula hamsini za haraka!
 
Rev. Kishoka,
Mkuu wangu mimi najua kushukuru, mara nyingi sisi waswahili hata ukipewa kitanda kulala ni lazima ushukuru lakini wapo ambao wanaweza sema kitanda sii lazima ktk kupata usingizi unaweza lala chini ya mti!...Hapo unajiuliza tena ikiwa unaweza lala chini ya mti, than why hawakulala chini ya mti?...
Hata hivyo nachopenda mjadala huu ni kuwa hawa wote wanaozungumza humu ni mavuno ya Mwalimu! - Incl. Bin Marium) nina hakika mtu wa Mwinyi ama Mkapa hauwezi mjadala kama huu kwa sababu wametengenezwa kama vile program za komputa i.e Excel...sote sisi ni ktk kundi la BTDT....
 
Bin Mariam,

Nimekusikia sana mkuu ukitoa mlolongo wa maelezo kuhusu kufanikiwa ama kutofanikiwa kwa Nyerere kiasi kwamba sasa hivi itakuwa kazi kubwa sana sisi kuweza kuelewana kwani unachodai wewe yawezekana kuna ukweli na kile wanachosema waandishi wengine kina ukweli vile vile, hivyo basi sielewi hicho kipimo cha mafanikio mnachojaribu kukiangalia kinatokana na factors zipi?...
Kisha sintapenda kubishana kwa sababu mtu fulani alisema hivi ama habari za kusikia kuwa Tanzania tulikopa fedha mahala fulani wakati hatuna ushahidi huo zaidi ya maneno yanayofumba akili za watu. Na tukashindwa kuelewa mtu hukopa kwa nini na mkopeshaji huitoa fedha kwa kuangalia vitu gani!...

Ebu turudi nyuma kidogo wakati huo wa Nyerere ambao umedai kuwa Elimu ilikuwa chini, Maradhi na Umaskini ndio yakajenga maskani...
Nakuomba unipe kipimo cha madai hayo kama unalinganisha na nchi nyinginezo ama Umechukua wapi tulikuwa kabla ya Uhuru na tulifikia wapi baada ya Nyerere kushika na kujiondoa madaraka...kwani navyofahamu, wengi hapa hawafahamu kabisa kipimo cha Tanzania kabla ya Uhuru ktk fani zote ulizozitaja hapo juu na tulipiga hatua gani mbele ama nyuma.
Halafu kumbuka kama unalinganisha na nchi nyinginezo sidhani kama utakuwa unamtendea haki mwalimu kwani wengi wa hawa jamaa waliachiwa mirathi ya Utajiri huo, nchi Kama Kenya, Msumbiji, Malawi, Zambia, Zimbabwe na kadhalika zilikuwa na uchumi bora (nafasi yao ktk mataifa) wakati wa mkoloni kuliko walivyo leo hii.. Je tunaweza sema viongozi wao walishindwa kuleta mafanikio!.
2. Swala jingine la kujiuliza ni kuwa nchi kama China na India ndizo zilikuwa super Power wa Uchumi duniani toka karne ya kwanza hadi ya 18, leo hii wameshuka daraja.. Je, viongozi wao wameshindwa Kiuchumi hivyo hakuna mafanikio?...
Leo hii China na India wanakuja juu vibaya sana kuliko hata nchi za Ulaya - Je, kuna uwezekano kuwa viongozi wa nchi hizo za Ulaya na Amerika wanashindwa kuleta mafanikio ktk nchi zao...

Nikirudi nyuma ktk swala la Afya na Umaskini - Mkuu wangu unaelewa kabisa kuwa Tanzania hatukuwahi kusikia Maleria as an epidemic...aghalabu kumsikia mtu kafa kwa Maleria labda tu kwa bahati mbaya alichelewa kwenda Hospital. Magonjwa kama Matende.TB na Ukoma vilikomeshwa kabisa only yamekuja jitokeza tena sasa hivi. Ugonjwa mkubwa wakati wa Nyerere ulikuwa Kipindu pindu na mara zote kilipojitokeza tu mkakati uliwekwa na hivyo watu wachache sana walipoteza maisha yao.
Wakati wa Nyerere ahtujawahi kusikia watu wakifa njaa hata kama tulikuwa ktk hali mbaya kiuchumi.. swala la kufa njaa halikuwepo kabisa lakini leo hii kufa njaa kunakubalika na ni umaskini wa kawaida kabisa kwa nchi zote za Kiafrika, Usipokufa njaa utakufa vitani...Na swala la kusema Elimu na afya bure ni makosa mbona hapa mjomba tunazipata huduma hizo bure?... Je Canada wana kasoro gani ama unachukulia maendeleo ya kitu ni kufanianisha na mfumo wa Marekani tu.

Mwisho nitarudia kusema ya kuwa hivyo vichache mwalimu alivyoweza kujenga nina hakika hakuna kiongozi hata mmoja sii Tanzania ama nchi za Kiafrika ameweza vijenga ndani ya Utawala wake. Reli ya Uhuru, viwanja vya ndege na shirika lake from scratch..viwanda vya kisawasawa visinyopungua 1000 na mashirika ya uzalishaji kila wilaya huu ulikuwa msingi bora ambao hauwezi kupita bure bila pongezi...As a fact jumlisha vitu vyote walivyojenga Mwinyi, Mkapa na JK as infrastructure bado hawawezi kumfikia mwalimu kwa hesabu yake acha mbali kuhesabu fedha kwani bila shaka hawa jamaa watashinda ktk matumizi ya fedha...
Nitakuacha na swali moja tu... Ikiwa mwalimu aliturithisha nyenzo za Ualishaji, majumba, vitega Uchumi, madini na kadhalika tukashindwa sisi kuviendelea ati tutazame aliacha ngapi benki, kweli huu ni uchumi bora jamani?... Hata mimi mfanyabiashara uchwara natazama utajiri wangu kwa assets nilizokuwa nazo, soko lililokuwepo pamoja na uwezo wa kutoa huduma ama kuzalisha kulingana na soko hilo badala ya kutaama ninazo dollar ngapi Benki kama akiba. Hata napotaka kuuza kijikampuni changu hakuna mteja atakaye taka kujua nina kiasi gani Benki ili apate kunipa mshiko wa kiuhakika badala ya kutazama vitu muhimu. Ni kwa mtaji huo wa assets aliotuachia Nyerere ndio tuliweza pata mikopo kwa utrahisi zaidi, Tanzania pamoja na kuwa na madeni yetu tulionekana kuwa nchi yenye kila nafasi ya kuendelea na uwezo wa kulipa ulikuwepo hii haitokani na sura ya Mwinyi kwenda kuomba msaada ama grant. Hakuna mtu atakayekupa fedha kwa huruma ati maskini na huna kitu benki!...fedha zinakopwa kutokana na uhakika wa kupipa yaani credit yako ni nzuri... Mwalimu ndiye mjeni wa credit hiyo, uhakika wa nchi kurudisha fedha hizo. Nakuuliza tena ni kiasi gani cha fedha ktk mikopo hiyo Mwl. Nyerere alipata kusamehemewa?....Je, kama hawa kina Mwinyi na Mkapa wangekuwa hawapati msamaha mkubwa wa fedha hizo za mikopo kwa masharti magumu hivi leo tungekuwa na deni la kiasi gani?..Huko Hazina kungekuwa na kitu gani!...na ebu tutazame nyuma hivi hawa jamaa wamejenga kitu gani haswa kwa hiyo mikopo?.. Nambieni vitu vilivyojengwa worth kujivunia kuwa leo hii tumepiga hatua kama sio hilo Daraja la huko Kusini (bila barabara ya maana) na huo Uwanja wa Mpira.. (tukiwa na timu mbuvu)..as a fact tunalipa fedha zaidi kwa makocha, zawadi kwa wachezaji na viongozi wake kuliko mfuko mzima wa budget ya mkoa wa Dar ktk Elimu. Na hadi leo hatujafikia record aloiacha mwalimu ktk micheo na sidhani kama tutaweza ifikia hata siku moja tukarudi na Medali Olympic games kwa mfuko wa serikali...


Mkandara:

Nitajibu posti yako nitoka kazini. Unaua inzi kwa rungu !!!!!!
 
Bin Mariam,

Nimekusikia sana mkuu ukitoa mlolongo wa maelezo kuhusu kufanikiwa ama kutofanikiwa kwa Nyerere kiasi kwamba sasa hivi itakuwa kazi kubwa sana sisi kuweza kuelewana kwani unachodai wewe yawezekana kuna ukweli na kile wanachosema waandishi wengine kina ukweli vile vile, hivyo basi sielewi hicho kipimo cha mafanikio mnachojaribu kukiangalia kinatokana na factors zipi?......................................................
.Huko Hazina kungekuwa na kitu gani!...na ebu tutazame nyuma hivi hawa jamaa wamejenga kitu gani haswa kwa hiyo mikopo?.. Nambieni vitu vilivyojengwa worth kujivunia kuwa leo hii tumepiga hatua kama sio hilo Daraja la huko Kusini (bila barabara ya maana) na huo Uwanja wa Mpira.. (tukiwa na timu mbuvu)..as a fact tunalipa fedha zaidi kwa makocha, zawadi kwa wachezaji na viongozi wake kuliko mfuko mzima wa budget ya mkoa wa Dar ktk Elimu. Na hadi leo hatujafikia record aloiacha mwalimu ktk micheo na sidhani kama tutaweza ifikia hata siku moja tukarudi na Medali Olympic games kwa mfuko wa serikali...

C'mon Mkandara!!

You really squashed it!!! Big UP!
 
Bob,
....Mkuu hayo, ulikuwa umeficha wapi mkuu, Kula tano mkuu
 
Wengi wanahadithiwa Tanzania iliyokuwepo wakati wa Mwalimu na hawakuiona LIVE!

Watabisha lakini ndio ukweli wenyewe.
 
Dua, ndio hapo sasa maana unaweza kuelemisha mtu kumbe mnatoka sehemu tofauti sana. Mtu anabishana kwa sababu "babu alinyang'anywa ng'ombe".. sasa utadhani katika Tanzania nzima ni babu yake tu aliyetoa sadaka kubwa katika mabadiliko tuliyoyafanya.
 
Bin Mariam,

Nimekusikia sana mkuu ukitoa mlolongo wa maelezo kuhusu kufanikiwa ama kutofanikiwa kwa Nyerere kiasi kwamba sasa hivi itakuwa kazi kubwa sana sisi kuweza kuelewana kwani unachodai wewe yawezekana kuna ukweli na kile wanachosema waandishi wengine kina ukweli vile vile, hivyo basi sielewi hicho kipimo cha mafanikio mnachojaribu kukiangalia kinatokana na factors zipi?...
Kisha sintapenda kubishana kwa sababu mtu fulani alisema hivi ama habari za kusikia kuwa Tanzania tulikopa fedha mahala fulani wakati hatuna ushahidi huo zaidi ya maneno yanayofumba akili za watu. Na tukashindwa kuelewa mtu hukopa kwa nini na mkopeshaji huitoa fedha kwa kuangalia vitu gani!...

Ebu turudi nyuma kidogo wakati huo wa Nyerere ambao umedai kuwa Elimu ilikuwa chini, Maradhi na Umaskini ndio yakajenga maskani...
Nakuomba unipe kipimo cha madai hayo kama unalinganisha na nchi nyinginezo ama Umechukua wapi tulikuwa kabla ya Uhuru na tulifikia wapi baada ya Nyerere kushika na kujiondoa madaraka...kwani navyofahamu, wengi hapa hawafahamu kabisa kipimo cha Tanzania kabla ya Uhuru ktk fani zote ulizozitaja hapo juu na tulipiga hatua gani mbele ama nyuma.
Halafu kumbuka kama unalinganisha na nchi nyinginezo sidhani kama utakuwa unamtendea haki mwalimu kwani wengi wa hawa jamaa waliachiwa mirathi ya Utajiri huo, nchi Kama Kenya, Msumbiji, Malawi, Zambia, Zimbabwe na kadhalika zilikuwa na uchumi bora (nafasi yao ktk mataifa) wakati wa mkoloni kuliko walivyo leo hii.. Je tunaweza sema viongozi wao walishindwa kuleta mafanikio!.
2. Swala jingine la kujiuliza ni kuwa nchi kama China na India ndizo zilikuwa super Power wa Uchumi duniani toka karne ya kwanza hadi ya 18, leo hii wameshuka daraja.. Je, viongozi wao wameshindwa Kiuchumi hivyo hakuna mafanikio?...
Leo hii China na India wanakuja juu vibaya sana kuliko hata nchi za Ulaya - Je, kuna uwezekano kuwa viongozi wa nchi hizo za Ulaya na Amerika wanashindwa kuleta mafanikio ktk nchi zao...

Nikirudi nyuma ktk swala la Afya na Umaskini - Mkuu wangu unaelewa kabisa kuwa Tanzania hatukuwahi kusikia Maleria as an epidemic...aghalabu kumsikia mtu kafa kwa Maleria labda tu kwa bahati mbaya alichelewa kwenda Hospital. Magonjwa kama Matende.TB na Ukoma vilikomeshwa kabisa only yamekuja jitokeza tena sasa hivi. Ugonjwa mkubwa wakati wa Nyerere ulikuwa Kipindu pindu na mara zote kilipojitokeza tu mkakati uliwekwa na hivyo watu wachache sana walipoteza maisha yao.
Wakati wa Nyerere ahtujawahi kusikia watu wakifa njaa hata kama tulikuwa ktk hali mbaya kiuchumi.. swala la kufa njaa halikuwepo kabisa lakini leo hii kufa njaa kunakubalika na ni umaskini wa kawaida kabisa kwa nchi zote za Kiafrika, Usipokufa njaa utakufa vitani...Na swala la kusema Elimu na afya bure ni makosa mbona hapa mjomba tunazipata huduma hizo bure?... Je Canada wana kasoro gani ama unachukulia maendeleo ya kitu ni kufanianisha na mfumo wa Marekani tu.

Mwisho nitarudia kusema ya kuwa hivyo vichache mwalimu alivyoweza kujenga nina hakika hakuna kiongozi hata mmoja sii Tanzania ama nchi za Kiafrika ameweza vijenga ndani ya Utawala wake. Reli ya Uhuru, viwanja vya ndege na shirika lake from scratch..viwanda vya kisawasawa visinyopungua 1000 na mashirika ya uzalishaji kila wilaya huu ulikuwa msingi bora ambao hauwezi kupita bure bila pongezi...As a fact jumlisha vitu vyote walivyojenga Mwinyi, Mkapa na JK as infrastructure bado hawawezi kumfikia mwalimu kwa hesabu yake acha mbali kuhesabu fedha kwani bila shaka hawa jamaa watashinda ktk matumizi ya fedha...
Nitakuacha na swali moja tu... Ikiwa mwalimu aliturithisha nyenzo za Ualishaji, majumba, vitega Uchumi, madini na kadhalika tukashindwa sisi kuviendelea ati tutazame aliacha ngapi benki, kweli huu ni uchumi bora jamani?... Hata mimi mfanyabiashara uchwara natazama utajiri wangu kwa assets nilizokuwa nazo, soko lililokuwepo pamoja na uwezo wa kutoa huduma ama kuzalisha kulingana na soko hilo badala ya kutaama ninazo dollar ngapi Benki kama akiba. Hata napotaka kuuza kijikampuni changu hakuna mteja atakaye taka kujua nina kiasi gani Benki ili apate kunipa mshiko wa kiuhakika badala ya kutazama vitu muhimu. Ni kwa mtaji huo wa assets aliotuachia Nyerere ndio tuliweza pata mikopo kwa utrahisi zaidi, Tanzania pamoja na kuwa na madeni yetu tulionekana kuwa nchi yenye kila nafasi ya kuendelea na uwezo wa kulipa ulikuwepo hii haitokani na sura ya Mwinyi kwenda kuomba msaada ama grant. Hakuna mtu atakayekupa fedha kwa huruma ati maskini na huna kitu benki!...fedha zinakopwa kutokana na uhakika wa kupipa yaani credit yako ni nzuri... Mwalimu ndiye mjeni wa credit hiyo, uhakika wa nchi kurudisha fedha hizo. Nakuuliza tena ni kiasi gani cha fedha ktk mikopo hiyo Mwl. Nyerere alipata kusamehemewa?....Je, kama hawa kina Mwinyi na Mkapa wangekuwa hawapati msamaha mkubwa wa fedha hizo za mikopo kwa masharti magumu hivi leo tungekuwa na deni la kiasi gani?..Huko Hazina kungekuwa na kitu gani!...na ebu tutazame nyuma hivi hawa jamaa wamejenga kitu gani haswa kwa hiyo mikopo?.. Nambieni vitu vilivyojengwa worth kujivunia kuwa leo hii tumepiga hatua kama sio hilo Daraja la huko Kusini (bila barabara ya maana) na huo Uwanja wa Mpira.. (tukiwa na timu mbuvu)..as a fact tunalipa fedha zaidi kwa makocha, zawadi kwa wachezaji na viongozi wake kuliko mfuko mzima wa budget ya mkoa wa Dar ktk Elimu. Na hadi leo hatujafikia record aloiacha mwalimu ktk micheo na sidhani kama tutaweza ifikia hata siku moja tukarudi na Medali Olympic games kwa mfuko wa serikali...

First thing first. Inabidi niweke sawa maana bado una-perpetuate myth. Wakati wa Nyerere, Tanzania katika michezo ya Olympic ilikuwa ni kichwa cha mwendawazimu tu.

Tulishinda medali mbili za fedha mwaka 1980 kwa sababu nchi nyingi ziligomea michezo hiyo iliyofanya Urusi. Ziligomea kwa sababu Urusi ilivamia Afghanistan. Na nchi zilizoshiriki zilikuwa za kijamaa na hivyo tulipata medali za dezo.

Mwaka 1980 tuliposhinda medali hizo Tanzania ilikuwa ina uchumi mbaya kuliko wakati wowote hule wa kuwepo kwa Taifa letu. Njaa kila kona, ukosefu wa bidhaa na miundo mibovu ya usafiri. Hivyo acha kuongeza chumvi kuwa tulikuwa tunazoa medali. Na zawadi walizopewa walioleta medali hizo ni radio kaseti zenye thamani ya shillingi 3000 kwa wakati hule. Na hilo lilifanya wanamichezo wetu kuachana na mambo ya kuwakilisha taifa.

Baada ya kuweka data sawa turudi kwenye mada. Hatupo hapa kulinganisha awamu. Na mnaofanya hivyo mnafanya makosa na hamlisaidii taifa. Taifa linakwenda na wakati. Pamoja na kwenda na wakati, kuna matukio ya ndani na nje ya nchi ambayo yana-influence mafanikio na matatizo ya nchi.

Matatizo ya nchi yanaweza kutatuliwa kwa njia mbili muhimu. Njia ya kwanza ni jumuia ya nchi hiyo kufanya intervention kwa kutumia uongozi, utaalamu na juhudi za wananchi. Na njia ya pili ni self-healing au adaptation. Katika njia hii ya pili utatuzi wa matatizo unategemea sana na juhudi za jumuia husika kuwa wavumilivu mpaka matatizo yatakapojiongoa yenyewe. Hivyo bajeti zinakatwa na matumizi mingine yanapunguzwa.

Katika posti yake moja MWANAKIJIJI alinitajia matatizo mbalimbali ambayo Nyerere alipambana nayo. Na nikamwambia kuwa 75% ya matatizo aliyotaja ni MAN MADE. Na kama hayo matatizo ni MAN MADE basi njia nilizotaja hapo ni lazima zitatue matatizo hayo. Na kama njia hizo zinashindikana basi aliye-SET PACE atakuwa alifanya makosa fulani. Katika kipindi chake cha uongozi hakuna matatizo yaliotatuliwa kwa kutumia moja ya njia nilizotaja hapo juu. Na misingi aliyojenga haikuweza kuwasaidia waliokuja baada yake.


Maendeleo ya ku-engineer ni tofauti na maendeleo ya evolution kama yaliotokea Ulaya. Maendeleo ya ku-engineer ni sawa na mbio za kupokezana vijiti. Ushindi wa mbio hizi zinategemea sana na mkimbiaji wa kwanza anaye-set pace. Hivyo ARI MPYA KASI MPYA haina maana kama spidi ya mkimbiaji wa mwanzo ilikuwa haina pumzi.

Na mwisho kumbuka kuwa Tanzania itaendelea kwa maendeleo ya ku-engineer tu. Maendeleo hayo yanataka vizazi vipya kurudi kwenye ubao wa michoro (drawing board) pale mambo yanapokwenda mrama. Na vilevile ni mapungufu makubwa kwetu kufuata maelezo ya Nyerere aliyotoa kwenye CNN juu ya kushindwa kwa siasa zake (michoro yake). Siku zote yeye anakuwa BIAS na kazi zake na hii ni kawaida kwa mwanafalsafa yoyote kwa sababu huwezi kuwa mwanafalsa kama huna shule ya mawazo (school of thoughts). Na wanafalsa ni extremist katika school of thoughts. Na nchi inajengwa kwa ku-balance skuli za mawazo.

Na vilevile ni makosa makubwa kwa watanzania kuzitupa kazi za Nyerere bila kuzipitia kwa makini ni kitu gani kilifanya twende mrama.

Now my hair hurts.
 
Bin Marium,
Kwana nilikuuliza kuhusu upimaji wa hayo mafanikio umeuchukua kwa kutumia mzani gani! umeshindwa kunielea lakini umekuja na haya mapya ambayo nitakufahamisha vizuri yaonyesha uncle kuwa huna kumbukumbu...

Hivyo basi labda nianze na kipengele kimoja baada cha kimoja...
Tulishinda medali mbili za fedha mwaka 1980 kwa sababu nchi nyingi ziligomea michezo hiyo iliyofanya Urusi. Ziligomea kwa sababu Urusi ilivamia Afghanistan. Na nchi zilizoshiriki zilikuwa za kijamaa na hivyo tulipata medali za dezo.

Mwaka 1980 tuliposhinda medali hizo Tanzania ilikuwa ina uchumi mbaya kuliko wakati wowote hule wa kuwepo kwa Taifa letu. Njaa kila kona, ukosefu wa bidhaa na miundo mibovu ya usafiri. Hivyo acha kuongeza chumvi kuwa tulikuwa tunazoa medali. Na zawadi walizopewa walioleta medali hizo ni radio kaseti zenye thamani ya shillingi 3000 kwa wakati hule. Na hilo lilifanya wanamichezo wetu kuachana na mambo ya kuwakilisha taifa.

Kwanza umesema tu kuwa nchi zilisusia Mashindano ya Urusi bila kueleza sababu za ushindani ambazo ningeweza kuzichukulia kama ni kigezo cha sisi kutoshinda hizo Medali... Labda kwa taarifa fupi nikwambie ya kwamba Filbert Bay alikuwa Bingwa wa mbio metre 1500 na hakushiriki pia ktk mashindano ya Montreal mwaka 1976 (nchi za kiafrika tuli boycot vile vile), hakuna mtu anayezungumzia hili kwa ushindi wa wanamichezo wengine. Bingwa wa mbio hizo za Steeplechase duniani alikuwa M Polland ambaye ndiye alimpita Filbert Bay ktk hatua ya mwisho kabisa na kabla ya mashindano hayo Bay alikwisha mshinda huyu jamaa huko miezi michache tu kabla ya mashindano hayo huko Stockholm... So, F. Bayi alikuwa na nafasi, uwezo, sababu ya kushinda sio kama kabahatisha na hakuna mshindani ambaye unaweza kumtaja jina hapa kusema kuwa angeweza kumzuia... ktk kila mashindani kuna contender sasa nambie ni kina nani hao badala ya kutumia kigezo cha nchi...Ni sawa na kusema ati Carl Lewis asingeweza kushinda mbio za mita 100 kwa sababu nchi 40 za kiafrika hatukushiriki...
Mbali na hayo yote Filbert Bay na Nyambui waliweza shinda mashindano mengine mbali na hiyo Olympic wakishiriki mabingwa wote wa michezo hiyo hivyo kujipatia ranking za kwanza hadi tatu na kuna wakati F. Bayi aliweka record ya dunia ambalo sii jambo dogo kabisa wala sidhani kama linaweza tokea tena..Kifupi kama hawakuwa wa kwanza basi pili ama Tatu... Yaani walikuwa contender na walipotegemewa kushinda -walishinda... Olympic ni kila baada ya miaka minne!
Filbert Bayi at his Peak aliwahi kumshinda Kipchoge Keino wa Kenya ambaye Kenya wenyewe wanamheshimu na kudai hakuna mwanariadha atakayewea heshimika Kenya kama yeye..

Mbali na hawa jamaa kuna majina ya kimataifa ambayo tuliweza yajenga kina Alredo Shahanga, Kidamus Shahanga, Titus Simba, Habib Kinyogoli, Lucas Msomba, Nassor Michael Willy Isangura..
Acha Mkuu huo mpango wa kusema Tanania ilikuwa na njaa kuliko wakati wowote una maanisha kitu gani hasa?... tazama uchumi wa Marekani mwaka huo huo chiuni ya Reagan ulikuwa umesimama wapi?.. Je, Reagan was a failure na kama ndio how come Marekani wanamheshimu sana wakati kazi aliyoifanya ndiyo ile ile aliyoifanya Nyerere kwa Tanzania na Afrika...
Haya mwaswala ya kutazama CCN mjomba vipi nawe huoni kama hawa jamaa ni mtandao ambao kazi yao ni kubrain wash watu wasiokuwa na access ya matukio halisi. Wewe kama ulikuwepo Tanzania miaka ya Nyerere kuna haja gani kusikiliza CCN upate kuelewa ni wapi Nyerere alikwama?..
Ikiwa taifa linajengwa na wakati how come wewe unatuletea mzani wa sasa kupima mambo ya wakati wa Nabii Mussa?...
 
Bin Marium,
Kwana nilikuuliza kuhusu upimaji wa hayo mafanikio umeuchukua kwa kutumia mzani gani! umeshindwa kunielea lakini umekuja na haya mapya ambayo nitakufahamisha vizuri yaonyesha uncle kuwa huna kumbukumbu...

Hivyo basi labda nianze na kipengele kimoja baada cha kimoja...


Kwanza umesema tu kuwa nchi zilisusia Mashindano ya Urusi bila kueleza sababu za ushindani ambazo ningeweza kuzichukulia kama ni kigezo cha sisi kutoshinda hizo Medali... Labda kwa taarifa fupi nikwambie ya kwamba Filbert Bay alikuwa Bingwa wa mbio metre 1500 na hakushiriki pia ktk mashindano ya Montreal mwaka 1976 (nchi za kiafrika tuli boycot vile vile), hakuna mtu anayezungumzia hili kwa ushindi wa wanamichezo wengine. Bingwa wa mbio hizo za Steeplechase duniani alikuwa M Polland ambaye ndiye alimpita Filbert Bay ktk hatua ya mwisho kabisa na kabla ya mashindano hayo Bay alikwisha mshinda huyu jamaa huko miezi michache tu kabla ya mashindano hayo huko Stockholm... So, F. Bayi alikuwa na nafasi, uwezo, sababu ya kushinda sio kama kabahatisha na hakuna mshindani ambaye unaweza kumtaja jina hapa kusema kuwa angeweza kumzuia... ktk kila mashindani kuna contender sasa nambie ni kina nani hao badala ya kutumia kigezo cha nchi...Ni sawa na kusema ati Carl Lewis asingeweza kushinda mbio za mita 100 kwa sababu nchi 40 za kiafrika hatukushiriki...
Mbali na hayo yote Filbert Bay na Nyambui waliweza shinda mashindano mengine mbali na hiyo Olympic wakishiriki mabingwa wote wa michezo hiyo hivyo kujipatia ranking za kwanza hadi tatu na kuna wakati F. Bayi aliweka record ya dunia ambalo sii jambo dogo kabisa wala sidhani kama linaweza tokea tena..Kifupi kama hawakuwa wa kwanza basi pili ama Tatu... Yaani walikuwa contender na walipotegemewa kushinda -walishinda... Olympic ni kila baada ya miaka minne!
Filbert Bayi at his Peak aliwahi kumshinda Kipchoge Keino wa Kenya ambaye Kenya wenyewe wanamheshimu na kudai hakuna mwanariadha atakayewea heshimika Kenya kama yeye..

Mbali na hawa jamaa kuna majina ya kimataifa ambayo tuliweza yajenga kina Alredo Shahanga, Kidamus Shahanga, Titus Simba, Habib Kinyogoli, Lucas Msomba, Nassor Michael Willy Isangura..
Acha Mkuu huo mpango wa kusema Tanania ilikuwa na njaa kuliko wakati wowote una maanisha kitu gani hasa?... tazama uchumi wa Marekani mwaka huo huo chiuni ya Reagan ulikuwa umesimama wapi?.. Je, Reagan was a failure na kama ndio how come Marekani wanamheshimu sana wakati kazi aliyoifanya ndiyo ile ile aliyoifanya Nyerere kwa Tanzania na Afrika...
Haya mwaswala ya kutazama CCN mjomba vipi nawe huoni kama hawa jamaa ni mtandao ambao kazi yao ni kubrain wash watu wasiokuwa na access ya matukio halisi. Wewe kama ulikuwepo Tanzania miaka ya Nyerere kuna haja gani kusikiliza CCN upate kuelewa ni wapi Nyerere alikwama?..
Ikiwa taifa linajengwa na wakati how come wewe unatuletea mzani wa sasa kupima mambo ya wakati wa Nabii Mussa?...


Kaka:

Hiyo ya michezo nilikuwa nachokoza nyoka kutoka shimoni tu. Lakin nili-mind sana kwanini wawakilishi wa Tanzania walikuwa hawatambuliki enzi zile. Mtu anailetea zawadi taifa na anachopata ni radio ya 277 tu wakati wa mei mosi. Ndio maana watu wameanza kuwa mafisadi.
 
Bin Marium,
Lakin nili-mind sana kwanini wawakilishi wa Tanzania walikuwa hawatambuliki enzi zile.

Hapana mkuu Ufisadi upo rohoni mwa watu kwa sababu leo hii hawa jamaa wanazipata siufa hizo na ndio wamekuwa mafisadi...
Wakati wa Nyerere pamoja na 277 watu walikuwa wazalendo na sifa ni ya Taifa zima, wao wakapewa ELIMU kwani walikuwa vijana wadogo sana...tena kweli unajua leo hii huwezi kupata redio kama 277 ambayo uliweza kusikia hata redio BBC vizuri kabisa...vitu kama hivyo adimu leo...
Leo hii pamoja na na kuwepo misifa yote ya Taifa stars na wanamichezo mbuzi , utakuta wanaoiba fedha zetu sio wachezaji ila ni viongozi....Wachezaji wanatumika kama watumwa ama njia za kuiba serikalini.
Binafsi nilidhani kuwepo kwa Utandawazi na soko huria tukiongozwa hna UWAZI pengine tungekuwa tukiugawa Utajiri wetu kwa wale wanaiostahiri badala yake kina Patel wamerudi.... sasa huwezi kumsikia mwana michezo wala kiongozi bora ila kina Patel. Wee kama huamini tazama magazeti yetu...
 
Pamoja na mapungufu yake, makala hii inavuta hisia kali na ilitoka siku ya Februari mosi, 2008 katika gazeti la KULIKINI ukurasa wa katikati.

Nyerere analia, Kikwete
angalia, uamuzi ni wako

MBARAKA ISLAM
Dar es Salaam

KWA kawaida ndoto hutafsiriwa kwa maana nyingi kulingana na hisia, imani na msimamo wa mtu anayewasilisha ama kupokea ujumbe husika, lakini kwa hili naandika nikiamini kwamba kuna ujumbe mzito ndani yake.

Hii ni mara ya pili kwa Baba wa Taifa, Marehemu Julius Kambarage Nyerere, kunijia katika ndoto na mara zote hutokea wakati kuna jambo zito linalohusu hatima ya Tanzania, taifa aliloliasisi kuanzia miaka ya hamsini. Nitaeleza baadaye ili kwa sasa nieleze ya sasa.

Nilishituka katika usingizi na kujisikia mzito kupita kiasi na ghafla nikajikuta niko katika katika nyumba moja ya kawaida kabisa mahali ambako nikaaminishwa kwamba ndipo makazi halisi ya Baba wa Taifa.

Kwa kuwa kazi yangu ni kutafuta habari, nilihitaji sana maoni ya Baba wa Taifa, mtu ambaye anaujua kwa dhati uchungu wa Tanzania, watu wake na rasilimali zake na mara moja nikamkabili mzee huyo ambaye alikuwa anaonekana kuwa mwenye mawazo mengi na huzuni iliyomfanya kuwa na uso uliochoka.

Nilisita kumuuliza kuhusu kilichokuwa kikinikera kwani alianza kulia aliponiona hali iliyonifanya nami nishindwe kujizuia kububujikwa na machozi.

Nilianza kulia naye alinikumbatia na kuniambia, “Nalilia Tanzania yangu, najutia yaliyotokea. Sikujua kwamba niliyemuamini amefanya yale niliyoyapinga kwa nguvu zangu zote.”

Nilipata ujasiri na kutoa kijitabu changu cha kuchukua dondoo za habari ili nianze kunukuu maneno yake. Kwa bahati mbaya nilikuta kijitabu hicho kimejaa, hakina nafasi kubwa ya kuandika.

Nikaokota vipande vya karatasi jirani na tulipokuwa tumekaa na kuanza kuandika maneno hayo. Katika mazungumzo yetu nilijiona mpumbavu kwa kutokuwa na kaseti ndogo ya kurekodi, baada ya kuona mazungumzo yananoga.

Nilitaka kujua undani wa maneno yake, na kwa kweli hakuwa na mengi ya kuzungumza na mahojiano yalikuwa mafupi mno, kiasi cha kunifanya nipate maneno machache kutoka kwake.

Baada ya kusema analilia Tanzania yake, Mwalimu alisema, “Zimwi la ajabu lenye mapembe ya rushwa, kulindana na matumizi mabaya ya madaraka, limeimeza Tanzania yangu. Msikate tamaa, pambaneni. Mwambie Jakaya (Rais Jakaya Kikwete) aangalie.”

Baada ya maneno hayo nilipoteza ujasiri maana nilipoteza mwelekeo na sikuweza kuendelea na mahojiano yake kwa kina. Katika hali ya kawaida, mimi sio mtu wa kushindwa kufanya mahojiano na mtu yeyote, hasa nikipata nafasi lakini kwa Mwalimu nilikwama.

Kabla sijaondoka aliniomba nimsindikize akapumzike kwa kuwa alikuwa amechoka. Nilimshika mkono na kumpeleka hadi chumbani kwake, ambako kulikuwa na vitanda vitatu na kabla hajalala akasema, “Nilimzuia Jakaya mwaka 1995 nikijua mwenzetu amekomaa na ni msafi kumbe amekuja kuniaibisha kabisa.”

Hayo ni maneno machache na pengine kutokana na kuguswa nayo, ndiyo niliyoweza kuyanukuu nilipozinduka huku uso wangu ukiwa umetapakaa machozi.

Nimejiuliza na kuwauliza watu wa karibu nami kuhusiana na ndoto hiyo, lakini nimepata majibu mchanganyiko ndio sababu hasa nimeamua kuwapa nafasi Watanzania wa Mwalimu Nyerere nao wapate maneno hayo. Sio lazima wayaamini, lakini wapate ujumbe.

Mara baada ya Mwalimu kufariki, nilipata kuota ndoto ambayo alinieleza huku akitembea kwamba niwaambie ‘jamaa zangu’ kwamba hajapendezwa kabisa na kuuzwa ama kubinafsishwa kwa iliyokuwa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), jambo ambalo nakumbuka aliwahi kuliweka wazi wakati wa uhai wake tulipokuwa mjini Arusha.

Siku hiyo ilikuwa ni ziara ndefu ya kuanzia Dar es Salaam, Iringa mjini na hatimaye vijijini na baadaye Arusha, safari ambayo nilibaini ukakamavu wa Mwalimu katika umri wa utu uzima na hiyo ilikuwa miezi michache kabla ya kwenda nchini Uingereza kwa matibabu, safari iliyokuwa ya moja kwa moja. Hakurejea tena akiwa hai. Alipoteza maisha yake akiwa huko baada ya kusumbuliwa na ugonjwa wa saratani ya damu.

Lakini, hadi sasa sifahamu kinachonisukuma kuwa na hisia kali na Mwalimu Nyerere, kwani kabla hata ya kutangazwa kuugua kwake, nilipata kuwaeleza wakubwa wangu wa kazi wakati ule, Salva Rweyemamu, aliyekuwa Mhariri Mtendaji wangu ambaye tulikubaliana kuwa na subira kabla ya kuandika habari hiyo.

Ilikuwa ni gazeti moja litolewalo kwa wiki kwa lugha ya Kiingereza ndilo lililotusukuma kuanza kuandika habari za ugonjwa wa Mwalimu, kwani liliandika habari ikielezea kwamba Mwalimu amezidiwa na amesafirishwa kwenda nje ya nchi, jambo ambalo halikuwa sahihi wakati huo. Tukaandika ukweli kwamba anaumwa, lakini yupo nchini.

Tuliendelea kufuatilia habari zake hadi siku ambayo alikuwa akiondoka nchini kwa Ndege ya Shirika la Ndege la Uswisi (Swiss Air), siku ambayo ni waandishi watatu tu ndio tulikuwapo uwanja wa ndege, Absalom Kibanda, ambaye sasa ni Mhariri wa Tanzania Daima na mpiga picha Emmanuel Herman, ambaye amerejea tena Habari Corporation.

Siku hiyo nakumbuka, uwanjani hapo kulikuwa na kundi la waandishi wa habari waliofika kupokea wanamichezo waliofika Dar es Salaam kwa ndege ya Swiss Air iliyomchukua Mwalimu, lakini baada ya kuwapokea wanamichezo waliondoka bila kujua Baba wa Taifa anaondoka kwa mara ya mwisho kwenda Uingereza.

Nakumbuka baada ya makosa kadhaa ya kitaaluma kutokea, nilimwambia Kibanda kwamba Mwalimu hatarudi. Sikuwa na sababu zozote za kusema maneno hayo na hakuna aliyezingatia maneno hayo na ndio maana hata mpiga picha wetu Herman hakupiga picha za kutosha katika tukio hilo. Niliumia sana.

Nakumbuka hata waliomsindikiza hawakuwa watu wazito kwani alikuwapo aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Temeke, John Chiligati na upande wa Polisi, alikuwapo aliyekuwa Mkuu wa Usalama Barabarani mkoa wa Dar es Salaam, Salum Mkwama, na pia ofisa mmoja wa Wizara ya Mambo ya Nje, ambaye alikuwa pale kusimamia itifaki.

Hata aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Andrew Chenge, alikutana na Mwalimu pale VIP akiwa katika safari zake na hakuwa katika orodha ya waliofika kumsindikiza Mwalimu na mkewe Maria, huku familia ikiwakilishwa na mabinti wawili ambao walionekana wakiipungia mkono ndege ikiwa angani.

Hisia hizo zinanipeleka siku ya kifo chake, nilipojikuta nikianguka mara baada ya kuona sura ya Baba wa Taifa pale nyumbani kwake Msasani na haikuishia hapo kwani nilitoka nyumbani kwenda kusindikiza mwili Uwanja wa Ndege kwenda Butiama, lakini nilijikuta nikidandia ndege ya jeshi la Afrika Kusini kwenda Musoma na hatimaye Butiama.

Halikuwa jambo la kawaida, kwani sikuwa na chochote zaidi ya nguo nilizokuwa nimevaa hata niliponyeshewa na mvua tukiwa katika msafara wa mwili wa marehemu sikuwa na nguo za kubadili na huko nilimkuta mwandishi mwenzangu aliyekwenda huko kama muongoza kwaya, Ansbert Ngurumo, ambaye naye “alizamia” kufika Butiama; hakuwa ameaga ofisini. Tulivutwa na mzimu wa Nyerere.

Hata Benjamin Mkapa, akiwa Rais aliyekuwa madarakani, alisema mbele ya kaburi la Mwalimu kwamba watakaofanya mambo kinyume na wosia wa Baba wa Taifa, “jinamizi lake litawashukia,” na kwa hakika inaelekea sasa “jinamizi” linaelekea kumshukia yeye.

Hakuna ubishi kwamba mambo mengi ambayo Mwalimu aliyapinga kwa nguvu zake zote hadi anakata roho, Mkapa ameyakiuka ikiwa ni pamoja na sio tu kushindwa kabisa kupambana na rushwa, bali pia yeye binafsi kujihusisha na rushwa na ufisadi.

Mwalimu alipinga kabisa Ikulu kutumika kujinufaisha, lakini mara tu alipoaga dunia, Mkapa alianzisha kampuni akitumia rasilimali za umma, ikiwa ni pamoja na majengo, magari, wataalamu na hata kuamua kabisa bila aibu kushirikiana na waziri wake, Daniel Yona kufanya biashara wote wakiwa madarakani.

Pamoja na kufahamu wazi kwamba Baba wa Taifa alipinga kabisa kuuzwa kwa NBC, Mkapa alijenga uhusiano wenye utata mkubwa na wamiliki wa benki hiyo, uhusiano ambao ulimuwezesha kuendelea kujineemesha yeye na familia yake na kujitanua kwa kujipatia nyumba nyingine jirani na ile aliyokuwa akiishi pale Sea View, Dar es Salaam.

Ni Mkapa huyo huyo ambaye sasa tunaambiwa kwamba kwa baraka zake, Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imefanya ‘madudu’ ya ajabu ambayo kwa hakika ndiyo yaliyofanya Baba wa Taifa, aniijie katika ndoto baada ya kubaini kwamba nimekuwa nikiumia sana kwa jinsi Tanzania yetu ilivyotumbukizwa katika “janga la kujitakia”.

Hakuna asiyefahamu kwamba Mkapa alitetewa kwa nguvu zote na Baba wa Taifa, wakati huo akionekana kama mtu pekee msafi katika kundi kubwa la wanasiasa walioomba kuwania urais mwaka 1995, mwalimu huko aliko sasa anajuta, lakini anamwambia Jakaya aangalie.

Mwalimu analia Jakaya angalia, Tanzania na Watanzania kwanza mambo mengine baadaye, tuko nyuma yako ukiamua.

Kuamua kwa Kikwete kutatokana na utashi wake binafsi na sio wa mashabiki wala watu wanaojikomba kwake.

Ni kuamua ndiko kutampa sifa na baraka tele kutoka kwa Mungu Mkuu baada ya kutovaa sura ya aibu kwa watu ambao wanamkwamisha kutekeleza azma yake.

Azma kubwa ya Kikwete ni maisha bora kwa kila Mtanzania, lakini sasa anaonekana kushindwa na wengi tunaamini kuwa anaweza, isipokuwa anaangushwa na hao wapambe wanaomzunguka.

Wapambe wake ni wengi wakiwamo marafiki zake, wasaidizi wake wa karibu serikalini ambao kila jambo wao wanaona ni hewala, wakati ukweli ni kwamba Watanzania wanateketea na kutomuamini rais wao waliyemchangua kwa kura nyingi.

Ni vyema, sasa Kikwete akaamua kabla muda haujawa mwingi, akawatosa wote wanaomuangusha na kumfanya kukosa thawabu.

Nakumbuka Simba wa Vita, Waziri Mkuu mstaafu, Rashidi Mfaume Kawawa aliwahi kukieleza kikao kimoja cha Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi, kwamba ni vyema mtu anayetoboa jahazi akatoswa mapema, kwani kulelewa na kushangilia huku akiendelea na hujuma zake, mwisho wake ni abiria wote, pamoja na nahodha kuzama na kupoteza maisha.

Kikwete, wakati wa kuwatosa wote wanaokuangusha ni sasa na usijali urafiki, uswahiba au undugu na watu wa aina hiyo na hapo utakuwa umeokoka na kulitendea haki taifa la Watanzania.

Source: KULIKONI, Februari 1, 2008
 
Maneno mazito haya ta ndugu Mbaraja Islam .Machozi yamenitoka maana anaye ambiwa huwa haelewi yeye Chama kwanza Tanzania baadaye baada ya marafiki zake .
 
Back
Top Bottom