Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

Nyerere: The Man, The Myth and the Legend

=

Mwalimu hakuwa na tatizo na sisi watu wa Pwani, isipokuwa yalikuwa ni matatizo ya uvivu wetu! Ni wavivu mno wa viuongo mpaka akili, ndio maana mfano hauko mbali, hata awamu ya nne imekwama, ndio jadi yetu watu wa Pwani sio siri! Tunajua kunywa gahawa, na kashata, na kuongelea ngoma ya mwali, baada ya mpira wa Yanga na Simba, ambazo hata ubingwa wa East Africa ni matatizo, watu wa pwani tuamke tuache kulaumu watu wengine kwa ujinga wetu, sisi Pwani ndio kina Ditopile, kazi kuangushana na hadithi nyingi! Watu wa bara wanakuja na treni, wanatuacha baho tu, kazi kucheza ngoma ya mwali tu!

ukisikia stereotype ndio hiii

sawa na wazungu leo ku clam that African Americans are lazy

mjomba i beg to disagree

je unaweza kujibu kwa nini NYERERE aliamuru reli ya DAR-MTWARA inglewe?
 
DrWho,
Kama Nyerere aliwakandamiza watu wa PWANI au MWAMBAO, basi na ndugu zangu Wachagga, Wahaya, Wasukuma nao wanaweza kutoa madai kama hayo hayo. Hawa walikuwa wameendelea zaidi lakini ili kuleta hali ya mlingano ilibidi wapige maktaimu wakati wale waliokuwa chini yao wakipewa "upendeleo."

jiulize kwa nini kambi za jsh zimejazana mkoa ya Pwani? na kwa nini kila anayetaka kuendeleza ardhi anaambiwa kuwa ohhhh hiyo ni Hifadhi ya Taifa!!!! wakati upuuuzi huo hawaupeleki mikoa ya juu?
 
Mzee ES ameandika: Mwalimu hakuwa na tatizo na sisi watu wa Pwani, isipokuwa yalikuwa ni matatizo ya uvivu wetu! Ni wavivu mno wa viuongo mpaka akili, ndio maana mfano hauko mbali, hata awamu ya nne imekwama, ndio jadi yetu watu wa Pwani sio siri!

Hapana mzee ES, watu wa pwani sio wavivu wa viungo, vinginevyo wasingeoa wake wengiwengi na kuzaana vya kutosha! Nilitaka tu kusahihisha hili!
 
JokaKuu: data kali hizo mzee; ila Ibrahimu Kaduma sio mwislamu, aliacha uislamu siku nyingi sana alipokuwa kijana na kabla hajashika hayo madarka uliyoyataja. Huyu ni mlokole wa kutupa anayechapa injili ile mbaya!
 
Habari zilizotolewa hapo juu sio sahihi zote. Kuna kubadili dini. Kati ya waliotajwa, wapo waliobadili dini. Sio kosa. Wapo vile vile Wakristu wanaobadili na kuwa Waislamu.

Namshukuru sana Rais Mkapa kwa kuwapa Waislamu Chuo cha Tanesco ili waanzishe chuo kikuu pale. Lakini mbona chuo walichoanzisha hakiwiki? Kuna tatizo gani?

Augustine Moshi

Ndio maana namkubali Mkapa japo si msafi hiiiivyo alikubali kuna tatizo na akawa INTERESTED kukwepo kwa solutions

sasa chuo tangu kimepewa waislam UNATAKA MAAJAB baada ya MWAKA MMOJA mjomba university haijatoa hata graduate mmoja wewe unataka matokeo sasa kama siyo ubuli huo ni nini?

kwa mtu mwenye calibre yako you can do better than that
 
DrWHO

Unafahamu mara ya kwanza nilipofika Dar es Salaam na mikoa ya pwani kwa ujumla mtu akikwambia ana shamba - mipaka yake yote utaiona wakati umesimama sehemu moja na huyu mtu atakwambia ni shamba. Kule bara nikikupeleka kukuonyesha shamba jasho litakutoka mwenyewe - ni shamba haswa ambalo litakidhi mahitaji yako kwa mwaka mzima hili halina ubishi ndio watu wanaposema watu wa mwambao ni wavivu. Bara ukienda shambani unaondoka asubuhi sana kabkla jua kuchomoza na unarudi baada ya jua kuzama - chakula unaletewa shamba - hakuna desturi hii pwani.

Uvivu huu ndio unachangia hata awamu hii ya JK ambaye hana tofauti kiuchapaji kazi na Mzee Ruksa. Matatizo tuliyonayo ni fundisho kwa TZ ukichagua uozo utapata uozo. Sifikirii kama muda wa kubadili mambo umekwisha - Rais ameshasema wala rushwa ni ruksa ati Richmond wanatumia fedha zao? What a joke! Utaona sio muda mrefu atajiunga kwenye mdundiko?
 
nenda kajaribu kulima pale Kazimzimbu kamajamaa hajakukomala rohoni achilia mbali ha JWTZ
 
Naona hapa tukubaliane hatutakubaliana
 
swali:

je ni jukumu la nani kupeleka maendeleo katika maeneo fulani katika nchi?
 
DrWho,

Naona msemo wangu kwamba sikisikii chuo kikuu kilichoanzishwa pale kilipokuwepo Chuo Cha Tanesco imekuudhi. Nimekuwepo Dar kwa wiki tatu tu, na inawezekana chuo kinasikika. Kumradhi.

Ningependa kiwe chuo imara sana. Hivi jina lake kamili ni nini? Kinaweka matangazo ya ajira, wanafunzi waliochaguliwa, tenda, etc. kwenye magazeti yetu mara kwa mara?

Ili kiwe chuo chenye ufanisi kwa Waislamu na kwa taifa kwa ujumla, itabidi kiwe secular. Kiwe na kitivo cha dini, ndiyo, lakini kiweze vile vile kufundisha elimu dunia vizuri na kuchangia tafiti za kitaifa za aina zote. Website ya hicho chuo ni ipi? Nataka niingalie kama ipo.

Tuko Watanzania wengi wenye uzoefu wa kufundisha vyuo vikuu. Tunakubalika au lazima kuwa wa dini fulani?

Chuo kinapashwa kuwa na PR ya kutosha, na si lazima kikae miaka mingi kabla hatujasikia michango ya walimu na wanafunzi wake katika shughuli na mijadala ya kitaifa. Tell me a little about the curriculum, for I am mightly interested. Na Chancellor, na VC ni akina nani?

Augustine Moshi
 
mwanasiasa wrote:
JokaKuu: data kali hizo mzee; ila Ibrahimu Kaduma sio mwislamu, aliacha uislamu siku nyingi sana alipokuwa kijana na kabla hajashika hayo madarka uliyoyataja. Huyu ni mlokole wa kutupa anayechapa injili ile mbaya!

mwanasiasa,
nafahamu kwamba mzee kaduma sasa hivi anaitwa abraham. yuko mtu aliniambia kwamba alibadili dini wakati mzee ruksa akiwa madarakani. inasemekana kitendo cha kaduma kubadili dini kilimuudhi alhaji mwinyi kiasi cha kumfuta kazi kaduma kama mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya katani.

sijui kama habari hizo ni za kweli au uongo. ila nina uhakika kwamba kuna kipindi alikuwa akiitwa ibrahim, na miaka ya 90 akaamua kuitwa abraham.

Mzee ES,
kipindi cha Nyerere kujitambulisha kama muumini mkubwa wa siasa za ujamaa ilikuwa njia ya kujipatia madaraka. wote waliojaribu kukosoa "imani" ya ujamaa na muelekeo wake kiuchumi walipoteza nafasi zao ktk chama.

watu kama edwin mtei, cleopa msuya,..ambao walijaribu kumshauri mwalimu abadilishe muelekeo wa uchumi kabla ya hali haijaharibika kabisa waliitwa wasaliti. edwin mtei alilazimika kujiuzulu, na cleopa msuya aliondolewa katika kamati kuu ya ccm. mkapa naye nasikia alikuwepo ktk kundi hilo alitupwa ubalozini kanada!

wakati wa awamu ya mwinyi siasa za ujamaa zilipoteza mvuto wake. wanasiasa wakaanza kutafuta mbinu mbadala ya kuwa karibu na raisi. kwasababu raisi alikuwa muumini safi wa dini basi wako waliotumia uislamu kama advantage ya kuwa karibu na mzee mwinyi.

Mzee ES, mimi nadhani kilichokuwa kikiendelea ni usanii na mbinu za ku-survive kisiasa ndani ya awamu ya juliasi, na ile ya alhaji mwinyi.
 
Mkandara, thanks for the master piece, put more!
Hapa najiuliza kwa nini kuna gap kubwa kuhusu hawa ma Rais waliokuja baada ya nyerere. Ukisoma hizi hotuba au interview unaona ile intelligence, hata anapojibu maswali. Let this him rest, he did his [own] best!
 
DrWHO,
Kambi za jeshi kujazana mkoa wa pwani tulirithi kwa wakoloni. Polepole Mwalimu akaanza kujenga nyingine Tabora, Kiabakari na kule kusini wakati wa mapambano na Mreno Msumbiji. Kama unataka kusema Mwalimu alijaza kambi za wanajeshi pwani ili kuwazibiti Wapwani,basi sema tu!
 
Mzee ES,
Mwalimu hakutaka udini na ukabila. Ndio maana hata viongozi waliomzunguka hawakuvaa udini/ukabila wao mbele yake. Mwinyi alikuwa Mdini. Alipokuwa balozi pale Cairo, niliarifiwa, kila wakati kunafanyika mabadiliko katika baraza la mawaziri alikuwa anataja mbele ya maafisa wake akihesabu kuna Waislamu wangapi. Kwa hiyo sishangai kuwa alipoingia mamlakani hata wale waislamu ambao hawakuona umuhimu wa uislamu wao ilibidi wauvae kimbelembele. Unakumbuka alimwambia nini Harun Mahundi alivyomteua kuwa mkuu wa polisi?
 
Tatizo letu kubwa huwa tunatafuta every reason kuonyesha kuwa Nyerere alikuwa na udini au upendeleo; maswahili ya Mzee ES yajibiwe kwa nini haya mambo ya udini yaliibuka tu baada ya Mwinyi na vile vile tulianza kuwajua nani ni nani? Interesting!
 
Mzee Mushi, Mzee wangu katika kupigania umuhimu wa elimu,

Machache niyajuayo kuhusu hicho Chuo:

Jina kamili ni Chuo Kikuu cha Waislam cha Morogoro. Kinamilikiwa na Taasisi ya Maendeleo ya waislamu, chini ya uenyekiti wa Kitwana Kondo.

VC ni mama Mwantumu Malale, katibu mkuu mstaafu wa wizara ya elimu, na wizara nyinginezo ikiwemo wizara ya maendeleo ya jamii, wanawake na watoto.

Chuo ni secular, wanasoma wanafunzi wa dini zote na walimu hali kadhalika.

Kwa sasa kinaoffer 3 courses: LAW, EDUCATION na MASS COMMUNICATION. Mipango ya kuwepo vitivo vingine iko mbioni.

Kitivo cha dini nasikia kitakuwepo pia, lakini si priority kwa sasa.

Sijawahi kufika chuoni hapo, but I am told there is a lot of room for expansion.

Mengineyo uliyouliza siyafahamu, labda DrWHO alieulizwa atakuwa na majibu.

Nachukua nafasi hii kutoa shukrani zangu za dhati kwa Rais mstaafu, Mh. B W Mkapa kwa ushirikiano wake mkubwa kufanikisha kuwepo kwa chuo hiki, si tu kwa kutoa majengo, bali pia kuongoza kwake ile fund raising kuliwatoa woga matajiri wengi ambao kawaida huhofia kuchangia projects kiislamu.. zikapatikana more than 3 billions within a few hours, na pledges nyinginezo nyingi. That was great. Sasa kazi kwetu!
 
Kulikoni: Mama Mwantumu Malale sio VC; yeye ni Chancellor. VC ni profesa fulani jina limenitoka.

Nafikiri hiki chuo sio secular angalau kwa vigezo vya udahiri wa wanafunzi na wafanyakazi. Takwimu zilizopo zinaonesha kuwa katika udahiri wa kwanza chuo kilichukua wanafunzi wote wa kiislamu. Hata utawala, vigogo karibu wote (kama sio wote kabisa) ni waislamu! Naomba unisahihishe katika hili kama si kweli!
 
from ippmedia.com
Makamu wake, Professa Said ni bingwa wa misitu na maliasili na hivi sasa ni Mkurugenzi wa Wizara ya Maliasili na Utalii.

Chuo hicho pia kimefanikiwa kuwapata wajumbe 17 wa baraza hilo ambao ni Professa Bakary Lembariti, Professa Mwajabu Possi, Dk.Ramadhan Dau, Dk.Baanda Salim, Balozi Sulemain Hemed, Dk.Mussa Assad, Dk.Hamed Hikmany na Alhaj Adam Kimbisa.

Wengine ni Maalim Ameir H.Ameir, Bi.Hawa Mmanga, Sheikh Said El Maamry, Bw.Hashim Saiboko, Bw.Faraj Tamim, Bi.Zainab Vulu, Bw.Salim Zagar na Bi.Mwanaid Maajar.

Mnamo Mei 22 mwaka jana, Rais Benjamin Mkapa alizindua taasisi ya maendeleo ya waislam nchini, MDF pale Diamond Jubilee na baada ya uzinduzi huo, akakabidhi majengo ya Tanesco yaliyopo mkoani Morogoro kuwa sehemu ya chuo hicho.

Rais Mkapa pamoja na viongozi wengine wa Serikali walichangia taasisi hiyo ili kufanikisha maendeleo ya chuo hicho.
 
Radio Butiama, hicho kitabu kama walivyosema wachangiaji wengine kwa kweli kimejaa historical facts ambazo nampongeza Mohamed Said na hususan kwa vile namfahamu. Ila premises alizotumia ndiyo sikubaliani nae. Tukiacha hilo. Mimi hofu yangu ni kwamba historia ya nchi yetu inaelekea kusahaulika kama siyo kupotea. Wale waliozaliwa mwaka 1961 na kuendelea hawaifahamu sawa sawa. Lazima zitafutwe njia za kuhakikisha hii historia muhimu haipotei.
 
mwanasiasa,kulikoni,
kuna wilaya zimekuja na idea ya kuanzisha vyuo vya ualimu, halafu hapo hapo wanakuwa na shule ya sekondari. ni sawa na kuwa na medical university na teaching hospital. naamini hiyo ni idea nzuri sana na inapaswa kuigwa na maeneo mengine.

pamoja na kuunga mkono kuanzishwa kwa chuo kikuu cha waislamu, binafsi ningewasisitiza kuongeza juhudi ktk kuboresha elimu ya sekondari kwa vijana wao.

shule za sekondari zilizosajiliwa tanzania zinakadiriwa kufikia 500. wakatoliki wana shule za sekondari 120, walutheri wanazo 50. waislamu,waanglikana, na wasabato, wanazo shule ngapi?
 
Back
Top Bottom