No matter how sweet it is......

No matter how sweet it is......

Heri ya mwaka mpya waungwana...
Mapendo daima...
Asee kuna mda unampata mtu au unakuwa na mtu unampenda balaa na ukiwa nae ni raha tu ila kila ukitafakari mazingira yake na yako inabidi umuachilie tu aendee no matter how sweet it is.... yani unamwambia kabisa kwamba mazingira tuliyo nayo haiwezi kuwork out na hivyo baba au mama byebye.....inaumaaa sema ndo hivyo tena bora ukweli mchungu.

Vipi waungwana mshawahi kutana na hali hizii?
Natakiwa kuchukua uamuzi kama huu ila I am very deeply in love with her, shida bado mtoto sana kwangu enough to be my daughter. I am in love with wrong person
 
Natakiwa kuchukua uamuzi kama huu ila I am very deeply in love with her, shida bado mtoto sana kwangu enough to be my daughter. I am in love with wrong person
Thanks God nimechukua hatua japo nipo kwenye maumivu makali but I am moving. Mm ni aina ya wanaume ambao hupata shida sana inapofika suala la kuachana. Ila huwa nikiondoka naondoka polepole lakini kwa uhakika na bila makelele. Huyu nimeanza kwa kupunguza mawasiliano but inside me nateketea coz nlikuwa nampenda to the core, nitakata huduma hapa namsubiria tarehe za mshahara zifike ila hpa ndo pagumu maana mtoto yule huwa siwezi kumwona anashida nikavumilia hata kama tumegombana akilia kidogo tu huwa namtumia hela sasa mwezi huu sijui nitumie mbinu gani.
Naomba Mungu nipate mwingine mapema sana atanisaidia kumove on haraka maana nisipopata basi pengine nikajikuta nimerudi coz anakuja likizo mwisho wa mwezi wa 2 najua tu nikituma nauli ni mgeni wangu kwa wiki 1 ama 2 kabla hajaenda kwao
 
Upo sahihi kabisa ,kila mwanamke ninaedate nae nikija kuchunguza vizuri nagundua single mama yaani imekuwa kama mkosi.
 
Depal uko sahihi 100%

Baada ya yeye wamekuja wengi sana na kwa baadhi yao nilikuwa muwazi kuwa kuna mtu kichwani na wakanikubali hivyo hivyo na mapenzi niliyoishi sikuwa na moyo i had so much fun nila hisia

Mpka nilipokutana na Cousin wangu, kiboko yangu, Ex wangu huyu ndiyo nataka niweke mambo sawa nimsahau yule

Maana walau Cousin ndiye anafanana naye,

ila ma cousin bana lazima waende mbingun wanajua kuishika mioyo
 
Inatokea sana Manzi mmoja tulifall vibaya mno ila me mwenyewe nikajitoa kwa sababu asee nilimdanganya vitu vingi sana !! Vingi mno kiasi kwamba tungeingia kwenye ndoa tulikaa kama mwaka hivi ! Alikua mzuri sana na anapenda maisha fulani hivi unyamwezi sana !! Alikua mwaminifu sana , niliamua kumpotezea tu maana nilikua muongo mno !!! Na sijawahi kukutana kama yeye 😂😂😂 Yan nakutana na mavimpire unyama unyama nisingekua Nakaza wangeshanitoa roho !! Sasa nataka kurudi kwa mtoto mzuri hadi leo anaelewa ila mauongo dadeki
Uongo haujawahi kumwacha mtu salama 🤣🤣🤣
 
Nakadori umeniquote hapo juu .mkuu unajua ilikuwaje???

Kuna mwanamke so beautiful. unajua beautiful wewe basi ndio yule anaitwa Naomi .
yule mwanamke hatukutongozana ila ni love at first sight. hiyo ni 2020.
Alikuwa bikra kabisa. Alisema kawabania wote kanipa mimi hiyo chance. sikufanya ajizi .Alinipenda sana nilimpenda kwani alinitoa katika stress za mapenzi ndio akawa tiba yangu.
maisha yakaenda nimemaliza chuo mambo hayaendi mtoto yuko na mimi tu. imefika stage mwaka Jana wa kumi nikamuweka chini

nikamuambia mama maisha yangu naona kutoboa kwa sasa ni ngumu najua hujawa influenced na chchte kuwa na me ila pesa ni muhimu pia kwenye mapenzi ila please ona hadi ninashindwa kukununulia jezi ya Yanga . kweli hii sio sawa najua itafika Kipindi utanichoka .

kwanza wakuu nilifikiria sana kbla ya kufikia uamuzi huo. ila nikawa sina jinsi ila nikawa na hope mambo yanaenda pouwa imani nilikuwa nayo na bado ninayo kuwa kutoboa hakuko mbali.
,
basi alinielewa lakini mimi nikijisema kwamba akikataa kuniacha na kunivumilia basi once nikitoboa siji spend maisha na mwanamke mwingine zaidi yake.
Lakini Ndyo hivyo alienda huku nampenda.

Guess what November nimeitwa job baada ya kupass certain i nterview baada ya kuwa jobless kwa miaka kadhaa.
natamani ningekuwa na Wewe Naomi muda huu nikununulie raba nyeupe na jersey ya Yanga kama nilivokuahidi maana sahivi Mambo yangu yamenyooka .

inapain ila sina jinsi .
Jamani natamani Naomi wako arudi kwako
 
Back
Top Bottom