![]()
Vyama vya upinzani bado sana..
Kunyoosha kidole au kukosoa si kazi kubwa kama kuendesha nchi. Baada ya kusema hivyo, napenda kusema ya kwamba, hizi zote ni kazi zinazoitaji kwenda sambamba. CCM pamoja na yote yanayotokea hivi sasa, bado ni chama madhubuti zaidi kuongoza nchi yetu kwa sasa. Tusijidanganye na mapenzi yetu ya vyama vya siasa, upizani (Chadema ,CUF nk..) hawako tayari kuchukua madaraka ya nchi kwa sasa. Ukweli ni kwamba vyama vya upinzani viko katika hali nzuri zaidi kujijenga na kuleta changamoto zaidi kwenye bunge letu katika hiki kipindi na kipindi kijacho.
Kukosolewa na kujirekebisha kwa chama ndiko kuna imarisha chama, kwa hiyo wale wana JF ambao hawataki kusikia vyama vyao vinakosolewa wanavidhoofisha vyama vyao.
Kuna mambo mengi tu tunayoweza kujivunia sisi watanzania, haya mambo yameletwa na wananchi chini ya uongozi wa CCM. Leo tunazungumzia ufisadi ambao ni pigo kubwa sana kwa jamii. Vyombo vya habari vimefanya kazi nzuri kuhamasisha wanachi kwa ujumla katika hili jambo. Sasa umefika wakati wa kuangalia mambo mengine muhimu pia. Wana JF na waandishi wa habari msijisahau mkawa kama nchi za magharibi na utangazaji wa habari mbaya tu(negative publicity) kuhusu Afrika au Tanzania (specifically). Au ni kwasababu ya kuishi au kusoma magharibi? Wana JF tuchambue mambo kwa uwazi zaidi kwa faida ya Jamii na sio vyama vya siasa.
Kuongoza nchi sio lelemama, nitatoa mfano mfupi tu wa HAMAS kule Palestine, hawa wamekua nguzo muhimu sana katika mapambano ya kivita zidi ya waisraeli, lakini walikua hawako tayari kutawala, sasa hivi,HAMAS wameshikilia GAZA na wanashindwa kuiendesha na kuendeleza mapambano vizuri kama zamani, wanapoteza wafuasi wao wengi (well this is another issue). Je ni kweli tuko tayari kumpa nchi jini huyu tusiyemjua??🙂
Let this stand on its own!!