Nani bado anaweka simu exposed dirishani kwenye daladala?
Sema wewe ndio umejifunza, usituambie unatufundisha kitu ambacho hujui kama sisi hatukijui already.
Na ungeweza kugeuziwa kibao ukapigwa wewe mwizi trying to chase a kibaka down vichochoro roads. Una mengi ya kujifunza, usijaribu kutufunza sisi.
Afadhali ume-back off sina utani mie.
Dah R.I.P simu yetu..........
Pole sana mkuu, huenda mambo mazuri yamekaribia
"......mateso yakizidi ujue saa ya wokovu imekaribia......." Ruhazwe JR
View attachment 117202
Ilikuwa hivi;
Ilikuwa leo majira ya saa moja na nusu jioni,Nimetoka kwenye mihangaiko nimefika Ubungo ili nipande Daladala nyingine kuelekea Nyumbani,Daladala niliyopanda nikafanikiwa kupata siti ya dirishani ili nipunge upepo.
Tukiwa bado tuko kwenye mataa ninauchovu wa mwili na roho,ikanibidi nitoe simu yangu aina ya Nokia N97,nikaweka Headphone ili nisikilize radio kujua yaliyojiri duniani.Nikiwa bado natafuta masafa ya Radio,ghafla nikaona bonge la mkono kutokea nje likamata simu yangu na mtu kukimbia nayo.Nikajua tayari nimesha fanyiwa kamchezo si kazuri,haraka sana nikapita dilishani kumfata mwizi,nyuma ya daladala niliyokuwa nimepanda kulikuwa na gari kubwa la mizigo ambapo kwenye gari lile kulikuwa na vijana wa ziada,walipoona nimeshuka haraka nao wakashuka kunisaidia tukamfukuzia mwizi umbali kazaa lakini hatukufanikiwa.
Maskini simu yangu NOKIA N97,ikawa imeniacha kimwili.
Wana JF nawaombeni mchukue tahadhari msije mkajikuta mmeingia kwenye hii janga kama lilonikuta leo.
RIP SIMU YANGU
View attachment 117202
ilikuwa hivi;
ilikuwa leo majira ya saa moja na nusu jioni,nimetoka kwenye mihangaiko nimefika ubungo ili nipande daladala nyingine kuelekea nyumbani,daladala niliyopanda nikafanikiwa kupata siti ya dirishani ili nipunge upepo.
Tukiwa bado tuko kwenye mataa ninauchovu wa mwili na roho,ikanibidi nitoe simu yangu aina ya nokia n97,nikaweka headphone ili nisikilize radio kujua yaliyojiri duniani.nikiwa bado natafuta masafa ya radio,ghafla nikaona bonge la mkono kutokea nje likamata simu yangu na mtu kukimbia nayo.nikajua tayari nimesha fanyiwa kamchezo si kazuri,haraka sana nikapita dilishani kumfata mwizi,nyuma ya daladala niliyokuwa nimepanda kulikuwa na gari kubwa la mizigo ambapo kwenye gari lile kulikuwa na vijana wa ziada,walipoona nimeshuka haraka nao wakashuka kunisaidia tukamfukuzia mwizi umbali kazaa lakini hatukufanikiwa.
Maskini simu yangu nokia n97,ikawa imeniacha kimwili.
Wana jf nawaombeni mchukue tahadhari msije mkajikuta mmeingia kwenye hii janga kama lilonikuta leo.
Rip simu yangu
ahaa kumbe!....najua sijafunga ndoa na ushamba iposiku utaishaa tu mkuu polepole ndio mwendo
Hahahaa..umenichekesha sana mkuu hasa hapo kwenye red..umenikumbusha pia pale ubungo kuna jamaa lilikwapua Bible ndogo ya mmama wa watu akienda kanisani..jamaa lilidhani ni pochi afu likajirusha darajani..kidogo likufeNakumbuka 2010 pale ESSO - ARUSHA tupo kwenye daladala majira kama ya saa 2 hv jioni, me nilikaa siti ya kwanza kabisa dirishani kule back beacher pembeni akiwa amekaa mama wa makamo na katoto kake huku kakichezea toy yake ya simu la kuwakawaka flani hv. Ghafla nikaona limkono lirefu kama shetani tokea nje ya dirisha kwenda kwa yule mama na kumnyang'anya mtoto toy yake..!
Nilibaki nimeduwaa na kushangaa jinsi yule kibaka alivyotoa mbio na lile toy.!
Yaani ni hatari sana.
mkuu,
si kila wakati ni hivyo ulivyosema wakati mwingine mateso yanazidi mwanzo mwisho na hakuna wokovu kabisa
Mimi jamaa alichukua simu yangu bila hata kunigusa,yaani sijui mafunzo wanachukulia wapi!hahahahahahahahahah..........mkuu huwezi amini jamaa kaingiza mkono ndani kama nusu mita,can you imagine kiasi gani jamaa alivyo professional kwenye fani
Pole sana. Ndo maana nikiona wanavalishwa tairi na kuchomwa siwahurumii.
Arusha hiyo ni kazi maalum inafanyika eneo la tengeru,mabasi hata ya mikoani yakifika pale abiria wanatangaziwa wafiche simu maana pale lazima ulizwe.