Nimeibiwa leo; jifunze na wewe usiibiwe kama mimi

Nimeibiwa leo; jifunze na wewe usiibiwe kama mimi

View attachment 117202
Ilikuwa hivi;
Ilikuwa leo majira ya saa moja na nusu jioni,Nimetoka kwenye mihangaiko nimefika Ubungo ili nipande Daladala nyingine kuelekea Nyumbani,Daladala niliyopanda nikafanikiwa kupata siti ya dirishani ili nipunge upepo.

Tukiwa bado tuko kwenye mataa ninauchovu wa mwili na roho,ikanibidi nitoe simu yangu aina ya Nokia N97,nikaweka Headphone ili nisikilize radio kujua yaliyojiri duniani.Nikiwa bado natafuta masafa ya Radio,ghafla nikaona bonge la mkono kutokea nje likamata simu yangu na mtu kukimbia nayo.Nikajua tayari nimesha fanyiwa kamchezo si kazuri,haraka sana nikapita dilishani kumfata mwizi,nyuma ya daladala niliyokuwa nimepanda kulikuwa na gari kubwa la mizigo ambapo kwenye gari lile kulikuwa na vijana wa ziada,walipoona nimeshuka haraka nao wakashuka kunisaidia tukamfukuzia mwizi umbali kazaa lakini hatukufanikiwa.

Maskini simu yangu NOKIA N97,ikawa imeniacha kimwili.

Wana JF nawaombeni mchukue tahadhari msije mkajikuta mmeingia kwenye hii janga kama lilonikuta leo.

RIP SIMU YANGU
Bandugu utapata nzuri na ya kisasa badala yake "wala usikasirike na usiwe na hasira" Something good on the way!!
 
acheni tu, na mimi manzese niliibiwa sony yangu xperia-------------yaani niliumwa mwezi mzima
 
Hivi kuna watu bado wanabana cm? mbona Hawaibi tena siku hizi? Unajua kitu inaitwa IMEI? au cm yako ni nokia mchina? Nowdays wajanjaaaaa Hawaibi tena cm mkuu. Kama una receipt yenye particulars ya hiyo cm you can easily trace it, ila ka mchina hesabu .
 
Pole Mkuu! Umakini Unahitajika kila wakati na kila mahali! pia nikushukuru kwa kuwakumbusha watz wenzako kuchukua tahadhar wasije wakaibiwa kama wewe!
 
Nimepania kumuabisha Mmoja kwa kutmia toyi la simu.
Atakapo chukua, unamuitia Mwizi. Anakula kichapo kwa kukwapua toyi la simu.
 
Yes dadangu yule. Kwa taarifa yako na wenzako wasioijua Dunia, Hotel zote za kimataifa Duniani uki-check out unaondoka na Taulo na vitukdhaa. Kitu cha kawaida. Sasa shida ya waswahili, mko too localized, yaani hata hapo nje kidogo tu kuchungulia hamuwezi! Mnaishia kujiaibisha na comments za ajabu ajabu. Nimeikuta hii issue ya Taulo kwenye blog ya Wacameroun. Wanshangaa sana wa TZ. Pole sana, ndiyo nchi yetu, tutafika hivi hivi


Duh! Kwahiyo kuchukua mataulo na baadhi ya vitu vya hotel ni kawaida kwa wenzetu!?
Huku kwetu ni wizi Mkuu!
 
Pole sana ndg yangu.
Nakuelewa kabisa.Mimi nilimtumia mtu TZ simu iPhone4,AKAIDONDOSHA naiona lakini mtaa wenyewe na sehemu yenyewe ni Tandika Sokoni.Jamaa angebadilisha line tungemdaka,lakini naona anawasha na kuzima tu.Pale kuna watu na vibanda million.Tunaomba mungu wasii geuze spare,wezi wa siku hizi technology sijui wanaielewaje kwa haraka zaidi.
KUBWA KULIKO LOTE-SHARING OF RESOURCES,SIKU HIZI ASIYEFANYA KAZI ANAKULA,NA USAMEHE MARA 70 X70,la sivyo moto utakusubiri.Pole tena.
 
Huyo alishakuwa MZEE hata hivyo. Pole sana kwa kupoteza DATA na Namba za totoz kama zilikuwemo.

Muda sasa wa kuhamia walau Nokia E-7 kama unapenda simu zenye QWERTY (Keyboard). RIP Nokia N97.

10x0914nojar3ur5e7.jpg
 
Duh! Kwahiyo kuchukua mataulo na baadhi ya vitu vya hotel ni kawaida kwa wenzetu!?
Huku kwetu ni wizi Mkuu!

Nyumbani kwako wewe ndiyo wizi. Wenzako wameomba msamaha zamani. Aliye-report siku iyo ni kama wewe; hujui chochote. Nina brands kibao za Taulo za hotels za kimataifa nilizowahi kaa humu duniani
 
Aiseee! kumbe ndivyo ilivyotokea! dah pole sana mkuu Ruhazwe JR, halafu muda ule unapoporwa unahisi kama uko ndotoni vile! unapotahamaki kibaka anakuwa tayari ameshakuacha! hata hivyo wacha niseme RIP NOKIA ya Ruhazwe JR!
 
Mkuu MWanjelwa-hebu nieleze utamu wa hizo hotel ,nijitahidi siku moja.Huku Uswazi(DSM,NRB,MOM,ZNZ) zipo? Ninayo millioni 2 ya kulala siku 1, kesho yake nikimbie na taulo-ahaaaaaaaaaaha.
Kama hazipo pa karibu ulipokaa ni wapi,nijaribu nauli?Asante.
Nyumbani kwako wewe ndiyo wizi. Wenzako wameomba msamaha zamani. Aliye-report siku iyo ni kama wewe; hujui chochote. Nina brands kibao za Taulo za hotels za kimataifa nilizowahi kaa humu duniani
 
Back
Top Bottom