Nimeibiwa leo; jifunze na wewe usiibiwe kama mimi

Nimeibiwa leo; jifunze na wewe usiibiwe kama mimi

Ruhazwe JR

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2011
Posts
3,402
Reaction score
944
mobile.jpg
Ilikuwa hivi;
Ilikuwa leo majira ya saa moja na nusu jioni,Nimetoka kwenye mihangaiko nimefika Ubungo ili nipande Daladala nyingine kuelekea Nyumbani,Daladala niliyopanda nikafanikiwa kupata siti ya dirishani ili nipunge upepo.

Tukiwa bado tuko kwenye mataa ninauchovu wa mwili na roho,ikanibidi nitoe simu yangu aina ya Nokia N97,nikaweka Headphone ili nisikilize radio kujua yaliyojiri duniani.Nikiwa bado natafuta masafa ya Radio,ghafla nikaona bonge la mkono kutokea nje likamata simu yangu na mtu kukimbia nayo.Nikajua tayari nimesha fanyiwa kamchezo si kazuri,haraka sana nikapita dilishani kumfata mwizi,nyuma ya daladala niliyokuwa nimepanda kulikuwa na gari kubwa la mizigo ambapo kwenye gari lile kulikuwa na vijana wa ziada,walipoona nimeshuka haraka nao wakashuka kunisaidia tukamfukuzia mwizi umbali kazaa lakini hatukufanikiwa.

Maskini simu yangu NOKIA N97,ikawa imeniacha kimwili.

Wana JF nawaombeni mchukue tahadhari msije mkajikuta mmeingia kwenye hii janga kama lilonikuta leo.

RIP SIMU YANGU
 
hahahahahahahahahah..........mkuu huwezi amini jamaa kaingiza mkono ndani kama nusu mita,can you imagine kiasi gani jamaa alivyo professional kwenye fani
 
Pole sana. Ndo maana nikiona wanavalishwa tairi na kuchomwa siwahurumii.
Arusha hiyo ni kazi maalum inafanyika eneo la tengeru,mabasi hata ya mikoani yakifika pale abiria wanatangaziwa wafiche simu maana pale lazima ulizwe.
 
Pole sana. Ndo maana nikiona wanavalishwa tairi na kuchomwa siwahurumii.
Arusha hiyo ni kazi maalum inafanyika eneo la tengeru,mabasi hata ya mikoani yakifika pale abiria wanatangaziwa wafiche simu maana pale lazima ulizwe.

we acha tu!...ninahasira na mwizi yoyote yule!
 
Pole ndugu pole sana jamaa wanatiming mbaya ni aina ya wizi flani wakijinga sana hasa ukiibiwa!
 
Back
Top Bottom