Nimeibiwa leo; jifunze na wewe usiibiwe kama mimi

Nimeibiwa leo; jifunze na wewe usiibiwe kama mimi

Jaribu kuipata, nenda ktuo cha polisi, fungua kesi yako, itapelekwa kwa vjana wa cyber, wataitafta, wiki mbili znaweza zisiishe unaweza ipata. Mhim ni kuwapa ushirikiano polisi hao. Na unatakiwa uwe makini nao, wapo wasiowaaminifu pia
 
kwani we uliyeibiwa dar umefkka lini? story z
ote we zilikuwa zinakupita kando? bongo daresalama baba
 
hawa walisema usajiri simu kutapunguza wizi sijui wamefikia wapi maana bado tunaibiwa simu na hakuna chochote
 
Nani bado anaweka simu exposed dirishani kwenye daladala?

Sema wewe ndio umejifunza, usituambie unatufundisha kitu ambacho hujui kama sisi hatukijui already.

Na ungeweza kugeuziwa kibao ukapigwa wewe mwizi trying to chase a kibaka down vichochoro roads.
Una mengi ya kujifunza, usijaribu kutufunza sisi.


Kweli kiongozi. Yeye ndio kajifunza sio sisi.
 
Dah pole mkuu...mie ubungo ziwezi pasahau niliuziwa sabuni ya mbunju yaan wale jamaa ni wezi hatari..sio ukwapuaji wala utapeli wa kubadilisha simu
 
Da pole sana mie mwenyewe nimetapeliwa leo

Sent from my BlackBerry 9380 using JamiiForums
 
View attachment 117202
Ilikuwa hivi;
Ilikuwa leo majira ya saa moja na nusu jioni,Nimetoka kwenye mihangaiko nimefika Ubungo ili nipande Daladala nyingine kuelekea Nyumbani,Daladala niliyopanda nikafanikiwa kupata siti ya dirishani ili nipunge upepo.

Tukiwa bado tuko kwenye mataa ninauchovu wa mwili na roho,ikanibidi nitoe simu yangu aina ya Nokia N97,nikaweka Headphone ili nisikilize radio kujua yaliyojiri duniani.Nikiwa bado natafuta masafa ya Radio,ghafla nikaona bonge la mkono kutokea nje likamata simu yangu na mtu kukimbia nayo.Nikajua tayari nimesha fanyiwa kamchezo si kazuri,haraka sana nikapita dilishani kumfata mwizi,nyuma ya daladala niliyokuwa nimepanda kulikuwa na gari kubwa la mizigo ambapo kwenye gari lile kulikuwa na vijana wa ziada,walipoona nimeshuka haraka nao wakashuka kunisaidia tukamfukuzia mwizi umbali kazaa lakini hatukufanikiwa.

Maskini simu yangu NOKIA N97,ikawa imeniacha kimwili.

Wana JF nawaombeni mchukue tahadhari msije mkajikuta mmeingia kwenye hii janga kama lilonikuta leo.

RIP SIMU YANGU

Kanunue simu nyingine! na kiherehere cha kucheza na masimu kwenye madirisha ya madaladala mkome! nyie ndo wale mnaotupigia kelele za manyimbo ya kina diamond kwenye daladala! Ingia kwenye hiace,tulia ufike unakokwenda ndo uanze kucheza na masimu yako.
Wewe lazima utakuwa ni kibaka anebisha aseme NO
Pole ila unge wasaka hao mateja wahapo ukajifanya unataka simu ya kanyanka ungeuziwa ileile simu yako
Nashukuru kwa ushauri but Sina muda,aisee!
Somo zuri....
Umeona eee,take care my friend
pole sana mkuu,wizi wa namna hiyo upo sana maeneo ya mwenge,manzese na bunju b (mahakama ya simu)
ee bwana nausikiaga tu lakini sasa nimejionea na kunipata siunajua tena ushamba wa daladala?
hawa wezi hawa...mie waliniibia sim yangu sina ham nao hataa pale Mwenge
yaanni natamani nikute wanapiga mwizi aisee
pole lakini huo ni ushamba, umekuja lini mjini? hiyo mbona ni style ya siku nyingi iliyokata wasichana masikio yao kwa kukwapuliwa heleni zao madirishani? Kaa na liushamba lako
Ushamba ndio nini mkuu?..hivi huo mdomo ndio unalia chakula au ndio unaendea haja kubwa?
Pole mkuu. Kwa mafundisho niliyowahi kupata sehemu fulani hiyo inaitwa GIVING (kutoa). Mtu utatoa kwa njia yoyote hata kwa kuibiwa. Jenga mazoea ya kutoa bila kulazimishwa.
aaa wapi si kweli nipe quote,yaani uibiwe et umetoa!...mbona utoaji kwangu si tatizo?
Ivi kuna watu bado wanapanda daladala??..
wewe wapanda guta?...wale madudu kama wewe mnaoishi chooni mnapanda uchafu sie watu tunapanda daladala n.k....ungejua wala usingesema hivyo

Hayo maeneonkumbe yana vibaka sana ee.. Pole kaka

Pole na hiyo inaitwa welcome to Dar es salaam!
its not true mkuu,thunk again
kwani we uliyeibiwa dar umefkka lini? story z
ote we zilikuwa zinakupita kando? bongo daresalama baba

hawa walisema usajiri simu kutapunguza wizi sijui wamefikia wapi maana bado tunaibiwa simu na hakuna chochote
wizi juu ya wizi kaka
Kweli kiongozi. Yeye ndio kajifunza sio sisi.
hata wewe ----- utakua umeeongeza kitu kwakua unadhani unajua wakati hujui na hujui kama hujui

R.i.p n97.
byebyebye!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
nunua gari ndo dawa ya hawa jamaa

Gari ninalo kaka,umesahau siku ya kufa nyani miti yote huteleza?
 
Asante kwa taarifa mkuu... Ulipotea sana! Karibu tena!
hujambi Cl mambo vip?..mi nipo tele

Na angekamatwa huyo
angejuta kuzaliwa;

Siku ukiwa na nafasi kula doria maeneo ya
ubungo uone wezi wanavyowaibia watu
then unaweza maliza hasira yako kwa kuwapa
kipigo kile kile cha kuleeee!.

Pole sana lakini.
mama mambo?..usijali within 3 days atakuwa mikononi mwangu si-unanijua zangi?
 
hahahaha, kiukweli nakuonea huruma, pole...lakini umenifurahisha sana..
 
Tumebaki kuibiana roho zetu sasa, kama ndo hivo huko dar siji na simu...

Usiache simu mkuu sema uwe makini sana kwani mdau ameeleza hali ilivyo na ni jambo la kawaida pale Mataa Kwa wale wa UDMS wanalijua hili wakitoka chuo jioni mara nyingi wadau huibiwa sana. usisahau hii tabia ipo pia Buguruni Sheri pale
 
View attachment 117202
Ilikuwa hivi;
Ilikuwa leo majira ya saa moja na nusu jioni,Nimetoka kwenye mihangaiko nimefika Ubungo ili nipande Daladala nyingine kuelekea Nyumbani,Daladala niliyopanda nikafanikiwa kupata siti ya dirishani ili nipunge upepo.

Tukiwa bado tuko kwenye mataa ninauchovu wa mwili na roho,ikanibidi nitoe simu yangu aina ya Nokia N97,nikaweka Headphone ili nisikilize radio kujua yaliyojiri duniani.Nikiwa bado natafuta masafa ya Radio,ghafla nikaona bonge la mkono kutokea nje likamata simu yangu na mtu kukimbia nayo.Nikajua tayari nimesha fanyiwa kamchezo si kazuri,haraka sana nikapita dilishani kumfata mwizi,nyuma ya daladala niliyokuwa nimepanda kulikuwa na gari kubwa la mizigo ambapo kwenye gari lile kulikuwa na vijana wa ziada,walipoona nimeshuka haraka nao wakashuka kunisaidia tukamfukuzia mwizi umbali kazaa lakini hatukufanikiwa.

Maskini simu yangu NOKIA N97,ikawa imeniacha kimwili.

Wana JF nawaombeni mchukue tahadhari msije mkajikuta mmeingia kwenye hii janga kama lilonikuta leo.

RIP SIMU YANGU


WE KILAZA BADO UNAKAAGA SITI ZA DIRISHANI NA LISIMU BILA KUFUNGA DIRISHA? WAmEKUPATIA
 
Back
Top Bottom