Nimeibiwa leo; jifunze na wewe usiibiwe kama mimi

Nimeibiwa leo; jifunze na wewe usiibiwe kama mimi

Pole sana sana aisee itabidi waliochangia thread hii tumchangie mwenzetu jamani. Nipe namba yako nikutumie 100,000
 
pole sana kiongozi wangu.hapo umejifunza siku nyingine huibiwi tena kuweni makini muda wote si ktk daladala tu
 
Pole sana sana aisee itabidi waliochangia thread hii tumchangie mwenzetu jamani. Nipe namba yako nikutumie 100,000

acha utani bwana,leo kwa mwenzetu kesho kwako unajua inauma sana!mimi hawa vibaka sijui tuwafanyeje
 
View attachment 117202
Ilikuwa hivi;
Ilikuwa leo majira ya saa moja na nusu jioni,Nimetoka kwenye mihangaiko nimefika Ubungo ili nipande Daladala nyingine kuelekea Nyumbani,Daladala niliyopanda nikafanikiwa kupata siti ya dirishani ili nipunge upepo.

Tukiwa bado tuko kwenye mataa ninauchovu wa mwili na roho,ikanibidi nitoe simu yangu aina ya Nokia N97,nikaweka Headphone ili nisikilize radio kujua yaliyojiri duniani.Nikiwa bado natafuta masafa ya Radio,ghafla nikaona bonge la mkono kutokea nje likamata simu yangu na mtu kukimbia nayo.Nikajua tayari nimesha fanyiwa kamchezo si kazuri,haraka sana nikapita dilishani kumfata mwizi,nyuma ya daladala niliyokuwa nimepanda kulikuwa na gari kubwa la mizigo ambapo kwenye gari lile kulikuwa na vijana wa ziada,walipoona nimeshuka haraka nao wakashuka kunisaidia tukamfukuzia mwizi umbali kazaa lakini hatukufanikiwa.

Maskini simu yangu NOKIA N97,ikawa imeniacha kimwili.

Wana JF nawaombeni mchukue tahadhari msije mkajikuta mmeingia kwenye hii janga kama lilonikuta leo.

RIP SIMU YANGU

kwenye daladala tena kwenye mataa ukiwa dirishani unatumia similar?!!!!!Ubishoo wa kijinga, usizungumze kabisa!!!!!!
 
Hiyo simu haijafa ila imepelekwa fundi akaseti masafa vzr!
 
kuna hawa wezi (supply side of the problem) na kuna hawa wanunuzi wa simu za moto(demand side of the problem) kuna wanao-flash na kutoa password(service providers of the problem) nahata raia wanaotizama wenzao wakiibiwa bila kusaidia hata kama inawezekana,kuna kampuni za simu zisizojali kuwekeza katika sayansi ya usalama kwa wateja wanaotumia simu na teknolojia ya kusaidia kupata simu zilizoibwa zikiwa na line iliyosajiliwa!Kuna Polisi ambao sina hata hamu ya kuwaongelea maana wananitia kichefuchefu kama maji ya mkondo wa baharini yaliyo tibuka!SASA WHERE DO WE GO FROM HERE?MABADILIKO POPOTE PALE NI WEWE!KILA MMOJA WETU AKIBADILIKA AMA AKIPIGANIA MABADILIKO MAJANGA HAYA YANAEPUKIKA!KWA WENZETU HUWEZI KUNUNUA SIMU YA MOTO!
 
Iliwai nitokea hii maeneo ya mwembe chai kuelekea usalama. Jamaaa kaingiza mkono aichukue simu yangu niliwai kumuona nikasogeza mbeleee mikono kisha nikambana mkono. Jamaa noma aiseee hata uvaaji wao hua ni balaaa utakuta kapiga bukta na singlend hapo hashikiki
 
Wacha nikupatie namba ya yule mganga anaeweza kurudisha simu iliyoibiwa...
 
View attachment 117202
Ilikuwa hivi;
Ilikuwa leo majira ya saa moja na nusu jioni,Nimetoka kwenye mihangaiko nimefika Ubungo ili nipande Daladala nyingine kuelekea Nyumbani,Daladala niliyopanda nikafanikiwa kupata siti ya dirishani ili nipunge upepo.

Tukiwa bado tuko kwenye mataa ninauchovu wa mwili na roho,ikanibidi nitoe simu yangu aina ya Nokia N97,nikaweka Headphone ili nisikilize radio kujua yaliyojiri duniani.Nikiwa bado natafuta masafa ya Radio,ghafla nikaona bonge la mkono kutokea nje likamata simu yangu na mtu kukimbia nayo.Nikajua tayari nimesha fanyiwa kamchezo si kazuri,haraka sana nikapita dilishani kumfata mwizi,nyuma ya daladala niliyokuwa nimepanda kulikuwa na gari kubwa la mizigo ambapo kwenye gari lile kulikuwa na vijana wa ziada,walipoona nimeshuka haraka nao wakashuka kunisaidia tukamfukuzia mwizi umbali kazaa lakini hatukufanikiwa.

Maskini simu yangu NOKIA N97,ikawa imeniacha kimwili.

Wana JF nawaombeni mchukue tahadhari msije mkajikuta mmeingia kwenye hii janga kama lilonikuta leo.

RIP SIMU YANGU

Hahaaha, hivi hizi mambo bado zipo? Nakumbuka kipindi cha ujana kidogo waniibie kepu yangu ya kacha, kuna kepu nzuri sana nilikuwa nazitoa mwanza sku moja nimekaa kwny dldl siti ya nyuma dirishani nilishtukia kono limepiga kichwani paa, bahati nzuri nilikuwa attention nikawahi kubamiza ule mkono kwenye ukingo wa dirisha nikaskia "yalaaa"...! Pia huwa wanatarget chain na hereni za wadada!
 
Unataka patashika nguo kuchanika eh?

nguo kuchanika tena...........??? pata-shika???? mmmhhhh bora uongee kingereza kumbe kiswahili kigumu zaidi
au uongee lugha ya kipepe ndo ntaelewa hapo nimetoka kapa hahahahaaaaaa kipeeeeee EMT looh
jioni njema.
 
Siku ingine ukiibiwa kwa namna hiyo usikimbize. wale jamaa huwa wako wengi na vizu pamoja na bisibisi. Utakimbiza na kujikuta umeishia mtaroni bisibisi kwenye utumbo au kisu. Achana kabisa na hao vijana
 
Siku ingine ukiibiwa kwa namna hiyo usikimbize. wale jamaa huwa wako wengi na vizu pamoja na bisibisi. Utakimbiza na kujikuta umeishia mtaroni bisibisi kwenye utumbo au kisu. Achana kabisa na hao vijana

Mkuu wewe una undugu na yule Mary Mwanjelwa, nguli wa kupitia mataulo ya hotelini kwa tiketi ya Ccm mkoani Mbeya?
Samahani lakini!
 
Last edited by a moderator:
Mkuu wewe una undugu na yule Mary Mwanjelwa, nguli wa kupitia mataulo ya hotelini kwa tiketi ya Ccm mkoani Mbeya?
Samahani lakini!

Yes dadangu yule. Kwa taarifa yako na wenzako wasioijua Dunia, Hotel zote za kimataifa Duniani uki-check out unaondoka na Taulo na vitukdhaa. Kitu cha kawaida. Sasa shida ya waswahili, mko too localized, yaani hata hapo nje kidogo tu kuchungulia hamuwezi! Mnaishia kujiaibisha na comments za ajabu ajabu. Nimeikuta hii issue ya Taulo kwenye blog ya Wacameroun. Wanshangaa sana wa TZ. Pole sana, ndiyo nchi yetu, tutafika hivi hivi
 
Bongo hata kuweka headphones masikioni hatari.

Kuna wataalam wana mikono mirefu hata siti ya kati wanaweza kukukwapua kama ulimi wa chura unavyomkwapua nzi hewani.
 
Back
Top Bottom