Nimeanza maisha mapya kama Vegan

Nimeanza maisha mapya kama Vegan

Kiukweli kila nikitazama maana ya mahusiano sioni umuhimu wake au sioni maana yake na kila nikitazama mahusiano najawa na maswali zaidi. Sio kwa baba yangu au kwa mama aliyetangulia hibernation.
Ila ujue kama sio mahusiano wewe usingekuwepo
 
Hongera,
Kuna vitu nataka niachane navyo kabisa ila kwa wakati fulani natumia japo kwa kiasi sana kutokana na mazingira
[emoji736]Soda naweza kumaliza hata miezi sita sijanywa,nakunywa napolazimika tu
[emoji736]Nina miaka mingi situmii majani ya chai/kahawa
[emoji736]Nataka niachane kabisa na sukari ya kiwandani ila sijapata mbadala kwa hio natumia japo kwa kiwango kidogo sana
[emoji736]Natamani niache kunywa dawa za viwandani nitumie herbs tu japo bado nakumbana na vikwazo fulani.

Hili la kuachana kabisa na sukari kama kuna mtu kafanikiwa atuambie amewezaje?
Kuhusu sukari ni kwamba, utatumia asali kwenye chai badala ya sukari
 
Hebu nipe shule...yanii naogopa Hadi kufanya mazoezi cuz Kuna kipindi nlikua nafanya nikawa napungua tu😣 ikabd niache
Ukianza kufanya mazoezi inabidi na lishe uongeze kwani unapoteza kiasi kikubwa zaidi cha energy
 
Kweli Kila mwanadamu na upande aliochagua , hii ndio maana halisi ya kuwa wanadamu tunatofautiana pa kubwa kwenye hali na Mambo kadha wa kadha,inawezekana ulivyo ndiyo njia rahisi ya kusaidia wengine mbali na binadamu...
 
Habari 👋🏾

Siku ya leo nikiwa natimiza miaka kadhaa nimekuwa VEGAN rasmi. Hatua hii nimekwisha ianza muda toka 28 January, hivi sasa naendeleza nadhiri hii rasmi katika mfumo wa maisha yangu.

Nimekuwa nikijiuliza utajiita vipi mwenye upendo, heshima au mtu unayejali hisia na kuheshimu wengine ikiwa umeshindwa kuheshimu uwepo wa viumbe wengine kama wanyama, ndege na wengineo?

Kwa kujali na kuona umuhimu wa kila kiumbe nimekuwa nikivijali viumbe vyote mfano, huwatengea waramba sukari kiasi chao pasi ya kuwapatia bugdha, uhifadhi mayai ya kuku na kutotoa wengine kuendeleza uzao wao, hutembea na wanyama mbalimbali katika maeneo kadhaa waweze kijihisi umiliki nk.

Leo nimepanda miti 28 maeneo yayonizunguka na miti 21 maeneo ya umma katika shule 2, hospitali, eneo la jeshi, kituo cha wasiojiweza na watoto waishio mazingira hatarishi na katika ofisi za wilaya.


Nikiwa kama kijana anayezingatia maisha halisi leo ni wazi sitotumia tena bidhaa zinazotokana na wanyama na viumbe mbalimbali. Hili linaambatana na masuala kadhaa katika mfumo wangu wa maisha ninaoendelea kuufuata ikiwa ni pamoja na;-
  • Sishiriki mapenzi (Sex)
  • Situmii vinywaji kemikali (Processed Drink's)
  • Situmii bidhaa zenye sukari ongezwa (Candy's)
  • Situmii bidhaa zinafanywa majaribio kwa wanyama
  • Nimejiweka mbali na uovu na negativity ya aina yoyote
  • Sifungamani na upande wowote
Najihisi mwenye furaha na amani, najiona mshindi. 😊

Sergio
nakuunga mkono kwa yote.
karibu kwenye kanisa la kisabato maana hayo ndo mafundisho yetu. ila sex inaruhusiwa ndani ya ndoa
 
Wewe hufanyi sex lakini hao viumbe unaowatetea na kutembea nao, wanafanya sex na kuendeleza uzao wao.
Nalogoff
 
Back
Top Bottom