Nimeanza maisha mapya kama Vegan

Nimeanza maisha mapya kama Vegan

Faida ni nyingi hakika maradhi ya sukari, shinikizo la damu, inflammation, matatizo ya ngozi, hali ya umakini, kutokuwa/kupunguza stress and so many more. Kiroho ni nguvu zaidi baina ya roho, nafsi, nature na muumba hakuna doubt wala vikwazo.
Sawa mkuu,kila la kheri,ila kuna hicho cha kwanza kama ukikiweza kujiepusha nacho itakuwa vizuri sana,ina maana sasa hutaoa kabisa...?
 
Nakutamania, maisha mazuri hayo ila usijinyime sana ukatenda dhambi..mie nisipokula nyama 3dys roho hua inataka kutoka!

Soda nisipokunywa Coca sifanyi kitu nakua zoba.

Hapa niko sehem nasubiria mishikaki kwanza.

All the best
Ati! Niache nyama choma laini, ndizi na kachumbari kwa pembeni, ukiteremshia na kinywaji baridiii nitakuwa nafanya kazi kwa ajili gani sasa!
 
Hivi miti na mimea si ni viumbe hai navyo mkuu? Huvionei huruma navyo? Kwanini unakula mchicha au spinachi wakati ili uukule lazima uuchume (Ndio kuua kwenyewe huko)?

We jilie tu vyote vinavyoruhusiwa ila mengine fanya kama ulivyoamua.

Nje ya mada, hautashiriki sex ndio kusema hautaoa wala nini? Vipi puchu?
Mkuu ,ukiuchuma mchicha huuui mkuu Ila ukiung'oa ndo unauua
 
Kwa Nini majani huyaonei huruma? Na yenyewe yana hisia usiyale.
 
Hongera,
Kuna vitu nataka niachane navyo kabisa ila kwa wakati fulani natumia japo kwa kiasi sana kutokana na mazingira
[emoji736]Soda naweza kumaliza hata miezi sita sijanywa,nakunywa napolazimika tu
[emoji736]Nina miaka mingi situmii majani ya chai/kahawa
[emoji736]Nataka niachane kabisa na sukari ya kiwandani ila sijapata mbadala kwa hio natumia japo kwa kiwango kidogo sana
[emoji736]Natamani niache kunywa dawa za viwandani nitumie herbs tu japo bado nakumbana na vikwazo fulani.

Hili la kuachana kabisa na sukari kama kuna mtu kafanikiwa atuambie amewezaje?
 
Nakutamania, maisha mazuri hayo ila usijinyime sana ukatenda dhambi..mie nisipokula nyama 3dys roho hua inataka kutoka!

Soda nisipokunywa Coca sifanyi kitu nakua zoba.

Hapa niko sehem nasubiria mishikaki kwanza.

All the best

Wanasayansi walimfanyia majaribio panya wakamuwekea cocaine na sukari kwa mwezi mzima,aliishia kulamba sukari tu alionja cocaine akaona haina inshu.

Point ni kwamba Sukari ni addiction mbaya kabisa,na mwisho wa hizo Coca za kila siku ni kisukari kinakusubiri.
 
Vipi huvai viatu unapekua kama mjomba Mpoto
🤣 Na zile dawa wanajaribiwa panya nazo hataki, mambo mengine ya kuiga hii nature hata huko porini wanyama wanakulana na Mungu katupa barka hii ndio maana unaona mbuzi au Ng'ombe wanachinjwa kila siku lakini hawaishi ila paka wanazaana dozen hakuna anaowala lakini wako wachache na hawana thamani.
 
Nakutamania, maisha mazuri hayo ila usijinyime sana ukatenda dhambi..mie nisipokula nyama 3dys roho hua inataka kutoka!

Soda nisipokunywa Coca sifanyi kitu nakua zoba.

Hapa niko sehem nasubiria mishikaki kwanza.

All the best
Haya endelea kula mishikaki
IMG-20210428-WA0003.jpg
 
Mkuu hongera sana, hakika ni commitment ya juu sana.

Mi nina swali hapo kuhusu sex, na ukaongeza kuwa huna tatizo lolote la uzazi. Swali langu ni kuwa je, hiyo kitu yako inasimama? Kama ilivyo ada kwa rijali kila siku asubuhi na occasionally unapotamani? au huwa hautamani? Na ikitokea hivyo unafanyaje kuiondoa hali hiyo.

Je haujawahi kabisa kufanya au umewahi na kwa sasa umeamua kuacha? unaacha sex tu au unaacha kabisa kufanya mapenzi ya aina yoyote ile?

Je kwenu ninyi watu wa aina hiyo, au kwako wewe ninini maana ya maisha? na ninini kinakupa furaha?

Kuhusu chakula na vinywaji Hongera sana, binafsi nimejipima nikaona siwezi kuacha kula kuku na nyama choma.

Otherwise, Kila la heri ndugu.
 
Back
Top Bottom