Mimi sina akili kuliko Allah ila nimetumia akili ambayo kanipa ALLAH kama alivyosema katika Quran
- Surah Al-Imran (Sura ya 3), aya ya 190-191:"إِنَّ فِي خَلْقِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَاخْتِلَافِ اللَّيْلِ وَالنَّهَارِ لَآيَاتٍ لِّأُولِي الْأَلْبَابِ"Tafsiri: "Hakika katika uumbaji wa mbingu na ardhi na tofauti ya usiku na mchana kuna ishara kwa wenye akili."
Hivyo, hapo utaona ALLAH katoa mfano wa usiku na mchana kuwa ni ishara kwa wenye akili, Vipi kuhusu Quran yenyewe ndio tuisome kibubusa? jibu ni hapana inabidi tutumie akili katika kuyaelewa mafundisho ya ALLAH, Kama alivyoseema mtukufu wa daraja Rasullullah Muhammad swalahu alaiy wasalam
"مَن لَا عَقْلَ لَهُ لَا دِينَ لَهُ"Tafsiri:
"Yeyote ambaye hana akili, hana dini.
Hata hivyo kwakuwa umeahidi kunifundisha nasubiri je wewe umeelewaje aya hizo. Asante.