Ni ufisadi wa Spika Samwel Sitta

Natamani kuanzisha thread nyingine kuuliza JF imekutwa na janga gani? Toka tumeanza huu mjadala, imechukua zaidi ya siku 2 kupata picha za nyumba ya Sitta inayojadiliwa. Pia hatuna undani wa mchakato mzima na hata mwenye nyumba hatujamjua. Mbaya zaidi hatuoni hata ka-inzi ka kutuletea data za jinsi viongozi wetu wengine wanavyofuja na kula nchi. Je JF imefulia?
 

HAPANA. Nimeangalia picha tu, naweza nisiwe sahihi.

Labda kuta zake hata ukipiga na SCUD hazivunjiki, hilo linaweza kuongeza thamani na nalikubali hasa ukizingatia kuna mijangili na ma jasusi wanaomwinda Spika Six kila siku!!

Pia doors zake na windows zinaweza kuwa bullet proof hili pia linaongeza bei.

Inaweza kuwa na kamera na mfumo wa ulinzi unaoonyesha kuanzia "NIA" ya mvamiaji au jasusi anapofikiri kuja kuvamia, leave alone kuanza kuja kuvamia. Hilo pia linaweza kuongeza thamani.

Ila bado nasema kwa Masaki.....sijuiiii.

Alamsik
 


Hold on.......Mheshimiwa Zitto, hivi umesema kuna mtumishi wa umma kama kamishna wa TRA anapokea mshahara mkubwa kuliko wa Rais? Sasa inakuwaje kwenye maagizo? Rais anakuwa na 'nguvu' zipi dhifi ya kwa mfano gavana wa BoT nk? Mishahara imapishana mbali mno jamani! sasa ina maana mkuu wa TRA anapokea almost 216,000millioni kwa mwaka, bado marupurupu mengine, na hii ni sawa au zaidi ya wakubwa kabisa wa kule white house marekani.....

Something must be very wrong here!
 

sio very tu.
 
kwani spika kama anaishi nyumba ya thamani ya shilingi milioni kumi kwa mwezi anapokea mshahara wa shilingi ngapi kwa mwezi?itakuwa ni kichekesho kama gharama ya pango ni kubwa kuliko mshahara. wake

Zaidi ya hapo viongozi wawe wazaledno sio mambo yakijulikana wanarusha mpira kwa watu wengine . kwa upeo wa elimu yao na uazalendo wao wana wajibu wa kukataa mambo kila kitu wanachoshauriwa. Na kwa style hii unaweza kukuta hata hiyo nyumba ni ya mtoto au mwanafamilia wa kigogo fulani basi irimradi ilimradi utajiri unaendelea kugawanywa kwa matajiri.
 
Tanzania itajengwa na wenye moyo na kuliwa na wenye meno...
 
Mimi nasema kuwa Samwel Sitta ni mbadhirifu kw kuwa nyumba yenyewe wameikodisha kisanii kw mkenya kupitia third party ambaye ni Rupia investment.....nafasi ya uwanja ni ndogosana hata gari 5 haziwezi kupaki yani hakuna hata eneo la kukaa nje ya nyumba...kutoka kwenye ukuta mpaka kwenye nyumba ni less than 3 metres.haina wimming pool wala nyumba ya nje ya walinzi na umbali wake kutoka bahalini ni zaidi ya mita mia 5
 
Kwani waajiriwa gani wa serikali wanalipwa mshahara wa mkia wa mbuzi ?
 
wa kulaumiwa hapa ni ROSTAM maana ndiye aliyempa hiyo kazi

hahaha! Ukimkamata mwizi utamlaumu mzazi wake?

Tatizo linamwangukia spika kwa maana yeye ndio mtumiaji wa hizo pesa. Is he blind to notice such extravagant usage of money?


Naona kajijibu mwenyewe hapa...


okay, point taken. Lakini i would imagine point of view yako na wewe imekuwa distorted kidogo kutokana na kuwa mmoja wa walaji wa pesa za umma - aka: mishahara iliyozidi kiwango. Sidhani kama watu wanamsulubu Sitta, bali wanasulubu ujinga wake. Ukisoma article inaanza kwa kuzungumzia statement zake za kupingana na ufisadi. Then it leads to lavish expenditure za pesa ya umma. Link the two, then there is your problem. Kamishna wa TRA kulipwa million kadhaa ingekuwa ishu kama na yeye angekaa na kudai anapambana na ufisadi. Lakini kakaa kimya, na hivyo tumemweka kando kwa sasa.
A good point uliyoweka ni hilo la kuangalia mfumo mzima. Hapo nakubaliana na wewe 100%. Sijui kama nyie Waheshimiwa mmeliongelea bungeni. Mishahara ya watumishi wa umma - ilingane na hali ya umma, that is the main cry from JF!

Zitto.. hivi Gen. Mboma amewahi kushika wadhifa wa Meremeta baada ya kutoka JWTZ?

I would have thought hii ingekuwa covered by the 50 paged report!!
 

Kumbe nyumba yenyewe ipo Dar? My thought it is in Dodoma! Then where he is staying in Dodoma? In hotel? And its not the headquarter of Bunge in Dodoma?...
 
Tukishakubali kwamba tumeshatoka rasmi kwenye siasa za ujamaa na kujitegemea, itakua rahisi zaidi kuielewa hii picha. Hapa tunapiga kelele wakati tunayoyataka tunajua kabisa hayatawezekana, eti nini... mkuu wa TRA alipwe laki 5 kwa mwezi sababu nchi ni masikini...subuutu!

People lets stop dreaming... Kutambua reality of our times ni first step ya kuusuka upya mfumo mzima. Lakini hii ya spika, spika, spika napingaaa.
 
Lazima tukubali ya kuwa viongozi wetu ndio wanaotuangusha sisi wananchi, mimi nadhani hili la spika ni kipande kidogo sana cha ubadhirifu unaoendelea (It is just the tip of the iceberg). Kuna vitu vingi sana sisi wananchi hatuelewi especially inapokuja kwenye masuala ya malipo ya viongozi wetu walio madarakani na wale ambao wamestaafu. Ni lazima vitu viwekwe wazi jamani, kwani hapa tunazungumzia hela za walipa kodi wote wa Tanzania. Ni haki ya kila mtanzania kujua Rais, Waziri, Naibu Waziri au Jaji Mkuu et al wanalipwa kiasi gani , kiasi gani kinakuwa taxed, Posho zao wanalipwa vipi, Nyumba zao wanazokodiwa zinatakiwa ziwe kwenye price range gani and so forth. Wakati huo huo malipo yao ni lazima ya reflect hali yetu ya uchumi !

Kusema ya kuwa tutapigana na vita mnavyoita vya fikra, wakati sheria zetu pamoja na chombo cha kutunga sheria vimejaa ufisadi itakuwa ni naivety. Ukitaka kujua ni jinsi gani hii ishu imejaa ufisadi jiulize swali moja tuu, Mheshimiwa sana Spika amenunuliwa fenicha zenye thamani ya shilingi millioni 200. Per jumuia ya common wealth tradition (according to Hon. Zitto) hizi fenicha atapewa kama akistaafu au asipochaguliwa tena kuwa spika. Kwa maana nyingine spika alijua kabisa wakati akinunuliwa hizi fenicha ya kuwa hizi fenicha mwisho wa siku zitakuwa zake. Kwa hiyo Spika kama Mwanadamu mwingine angependa kununuliliwa kitu kizuri na chenye thamani, kwa maneno mengine ni kuwa indirectly tumempa spika open check tunamwambia kanunue kitu utakachopenda ambacho kitakuwa chako ! You don't have to be a neurosurgeon to realize this issue is encroached with ufisadi.

Sasa hapa tunazungumzia spika tu, bado hatujaenda kwa mzee mwenyewe wa Magogoni, tukisikia matumizi yake pamoja na waziri mkuu, Makamu wa Rais nadhani itakuwa hatari !
 
Lakini hapa unasahau kuwa rais ana marupurupu kibao.
 
..nimesikia pia hiyo imeidhinishwa na Rais? ambaye aliutangazia umma kuwa kuna mtikisiko wa kiuchumi? Hii ni sawa na baba kutangaza matatizo ya kiuchumi nyumbani, nyama hakuna (kama nyumba ya wapenda nyama) wakati yeye anachoma nyama baa!! Kumbe siasa za kwenye majukwaa hazina ukweli wowote katika maisha halisi? Hiyo nyumba sio ya kulipiwa milioni kumi kwa mwezi nakataa kuamini kuwa ni kweli.
 
Kwani Ubepari maana yake ni Ufujaji? Au kuwa na mali bila daftari? china a former commuist with capitalism on Chinese "socialist" charateristics. USA and Eorpean capitalists. Sasa hapo unaiweka wapi Tanzania? Ufujaji hauna ideology!!
 
Hivi wakulu, heshima mbele, maadamu sisi ni 'mabingwa' wa kuiga 'sera' za wenzetu wa nje huko na kujilinganisha, hli la mishahara hawakumsikia Obama alivopunguza punguza mishahara/marupurupu ya watu wake wa ikulu? au hilo haliwezi kuigwa, maadamu na sisi 'mdororo' wa kiuchumi umetukumba? au hii hawakuisikia?
 
Kwani Ubepari maana yake ni Ufujaji? Au kuwa na mali bila daftari? china a former commuist with capitalism on Chinese "socialist" charateristics. USA and Eorpean capitalists. Sasa hapo unaiweka wapi Tanzania? Ufujaji hauna ideology!!

Now you are talking, manake umeshaanza kufikiria kimfumo mfumo badala ya ki Sitta Sitta. Tukishakubaliana tuna tatizo la kimfumo basi tunaelekea pazuri. Safi sana...
 
Unajua watanzania sisi ni watu wa ajabu sana.
Vyama vya upinzani wakijaribu kulipeleka kwa wananchi hawa hawa wa Tanzania, utasikia wakibezwa kwamba hawana hoja nyingine bali hii hii tena wanabezwa na watanzania wenyewe hawa hawa.
Sijui tumelogwa!
 
...naomba kuuliza;

Iwapo spika anaishi kwenye hili jumba na marupurupu hayo, mkewe (Bi Margaret Sitta) anastahiki marupurupu na nyumba nyingine kwa wadhifa wake wa uwaziri wa jamii, jinsia na watoto au ndio serikali imejumuisha mafao yao wote wawili?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…