Ni ufisadi wa Spika Samwel Sitta

Ni ufisadi wa Spika Samwel Sitta

Salaam Wakuu wote,

- Eti hoja ni nini hasa hapa, kwamba Spika amejipangia namna ya kuishi kama Spika bila muongozo wa sheria, au what I do not get it?

Respect.

Kamanda Es!
 
Salaam Wakuu wote,

- Eti hoja ni nini hasa hapa, kwamba Spika amejipangia namna ya kuishi kama Spika bila muongozo wa sheria, au what I do not get it?

Respect.



...tatizo ni hizo milion kumi(10) kwa mwezi,usijidai huijui milioni 10 kwa bongo,wizi mtupu hapo na hakuna justification yeyote ya matumizi kama hayo kwa pesa za walipa kodi,cha ajabu unaweza kukuta hiyo nyumba ni yake au ya ndugu yake au fisadi mwezake au unaweza kukuta hata hizo pesa hazilipwi zipo kwenye makaratasi tuu zinaingia kwenye account yake...hawa mafisadi sijui lini watatuachia
 
Mwanakijiji,

Maneno yako yanachefua , mtu anaweza kutapika.

hilo halifanyi hoja yako kuwa na nguvu. Ni kulazimisha hoja.
Wewe umetoka kwenye nchi gani ambaye huoni tatizo kwa kiongozi wa bunge kutumia za nusu bilioni kwa mwaka , kwa ajili tuu ya hadhi yake.

Kwa kweli sijaona tatizo bado kwani hakuna aliyeonesha hasa tatizo ni NINI zaidi ya kutumia maneno ya kugusa vionjo, kejeli, na kujaribu kulazimisha hoja.

Narudia tena hoja, sio pango tuu bali samani alizonunuliwa na serikali , pamoja na msede unaoworth milioni 300.

So tatizo ni nini?
 
Salaam Wakuu wote,

- Eti hoja ni nini hasa hapa, kwamba Spika amejipangia namna ya kuishi kama Spika bila muongozo wa sheria, au what I do not get it?

Respect.

Kamanda Es!

Mkuu ES haya ndiyo matatizo thread za JF siku hizi, kuna page 4 za threads ktk hizo zote zenye maana thread 10 au pungufu. Kibaya zaidi kwenye jukwaa muhimu la siasa almost majungu na udini tu. Inaboa kinoma.

anyway karibu Kamanda ES.
 
Bado sijaelewa tatizo hasa ni nini? Ukiondoa kilio cha "nchi maskini".. what is the problem?

a. Ni spika?
b. Ni gharama kubwa? compared to whose na kwanini tuna compare na huyo?
c. Ni Sitta?
d. Ni mkataba wa upangaji?

b; compared to us wananchi, na kipato cha nchi. Kufanya hayo anayoyafanya huku akijtangaza kuwa naye yumo katika mapambano ya ufisadi ni KUFURU na UNAFIK kuliko maelezo. Kwamba yeye ameikuta kwenye sheria na taratibu is a lame excuse kwa sababu yeye kama kiongozi alipaswa kuona kwamba hilo ni tatizo na angeanzisha mchakato wa kubadilisha ujinga huo aliuokuta. Kwa maelezo haya yote sasa yanaingia-so all items above-a, b, c, and d- are a problem.
 




1. ...tatizo ni hizo milion kumi(10) kwa mwezi,

2. usijidai huijui milioni 10 kwa bongo,wizi mtupu hapo na hakuna justification yeyote ya matumizi kama hayo kwa pesa za walipa kodi,

3. cha ajabu unaweza kukuta hiyo nyumba ni yake au ya ndugu yake au fisadi mwezake

4. au unaweza kukuta hata hizo pesa hazilipwi zipo kwenye makaratasi tuu zinaingia kwenye account yake...hawa mafisadi sijui lini watatuachia

- Sheria ipi ya Jamhuri ambayo imevunjwa na hizo Millioni 10 za nyumba ya Spika? Na hata kama ningekuwa ninajua ninaweza vipi kuingilia sheria maofisa wetu nje wa ubalozi wanaishi kwenye nyumba za hela ngapi mpaka nishangae hizi hela ndogo sana?

- Spika wa bunge la kutunga sheria za taifa kisheria zetu anatakiwa aishi kwenye nyumba ya hela ngapi mbona maneno mengi bila facts? Wekeni facts Spika wa Kenya anaishi kwa hela ngapi? Wa Zambia anaishi kwa hela ngapi? as opposed na wetu ambaye anakiuka sheria ya Jamhuri kufungu kipi hicho na inasema nini hasa?

- Wakuu Tanzania tumeamua kufuata ubepari, katika ubepari serikali haimiliki nyumba za viongozi ikiwa ni moja ya sera za kuhakikisha hela zinazunguka katika kuboresha uchumi, kumilipia Spika na viongozi wote wa juu nyumba ni moja ya hatua muhimu sana katika kuboresha uchumi wa Taifa katika kuhakikisha kwamba wananchi wanaingiza pesa mifukoni mwao huku serikali ikikusanaya kodi katika hela hizo zake yenyewe, unless kuna ishus zingine separate zinazomhusu Spika na ufisadi ambazo mwenye facts anatakiwa kuziweka hapa tuzichambue, lakini la Millioni 10 na nyumba wakati tuna maofisa nje ya nchi wanaolipiwa more than this amount tena on monthly bases, binafsi sioni kuwepo na ishu hapa, Spika hawezi kwenda kuishi kwenye chamba cha kupanga na besides si kuna bajeti ya ofisi ya Spika inayopitishwa na wabunge wetu wa CCM na upinzani sasa hizi kelele ni kwa sababu Spika amepitisha bajeti ya matumizi ya ofisi yake or what?

- Can we talk facts badala ya emotions? I mean some ishus zinahitaji pure facts na hii ni mojawapo! Yaani the third leader on line to run our Government hatakiwi kuishi on $ 10,000 House tena only monthly tu? Aaaaaghhhhhhrrr!

Repsect.

Kamanda FMEs!
 
b; compared to us wananchi, na kipato cha nchi. Kufanya hayo anayoyafanya huku akijtangaza kuwa naye yumo katika mapambano ya ufisadi ni KUFURU na UNAFIK kuliko maelezo. Kwamba yeye ameikuta kwenye sheria na taratibu is a lame excuse kwa sababu yeye kama kiongozi alipaswa kuona kwamba hilo ni tatizo na angeanzisha mchakato wa kubadilisha ujinga huo aliuokuta. Kwa maelezo haya yote sasa yanaingia-so all items above-a, b, c, and d- are a problem.

I thought leaders should be ready to die for a cause. Well a fight without a martyr is not a fight.

By the way, what kind of accomodation does CHADEMA provide Dr. Slaa and Kabwe in order to protect them against these vicious Mafisadi?
 
b; compared to us wananchi, na kipato cha nchi. Kufanya hayo anayoyafanya huku akijtangaza kuwa naye yumo katika mapambano ya ufisadi ni KUFURU na UNAFIK kuliko maelezo. Kwamba yeye ameikuta kwenye sheria na taratibu is a lame excuse kwa sababu yeye kama kiongozi alipaswa kuona kwamba hilo ni tatizo na angeanzisha mchakato wa kubadilisha ujinga huo aliuokuta. Kwa maelezo haya yote sasa yanaingia-so all items above-a, b, c, and d- are a problem.


Mkuu Kitila heshima yako kwanza,

- As a nation na taratibu za usalama wa taifa kwa viongozi wetu wa juu, ni taifa ndio tunampangia kiongozi namna ya kuishi haamui mwenyewe, ndio maana hawasafiri kwenye Economy ingawa wengi wao wangependa hivyo kwa sababu ni wajibu wetu taifa kuwalinda kwa kufuata sheria za Jamhuri, Spika hawezi on his own kuamua mahali pa kuishi ni taifa ndilo tunamuamulia, hata singetaka hawezi kwa sababu hatuwezi ku-compromise usalama wake kwa sababu tu ya kujaribu ku-save peanuts,

- Kumlaumu Spika kwa sababu ya gharama ya nyumba anayoishi either ni ignorance au ni kukosa hoja za kuikosoa serikali, ndio maana sometimes tunajiuliza kwa wananchi wanaichagua CCM tu, off ocurse kwa hoja kama hizi ni clear kuwa wananchi hawana alternative na kama ipo basi ni very weak au iko kwenye political lifesupport somehwere!

Respect.

Kamanda FMEs!
 
I thought leaders should be ready to die for a cause. Well a fight without a martyr is not a fight.

By the way, what kind of accomodation does CHADEMA provide Dr. Slaa and Kabwe in order to protect them against these vicious Mafisadi?

They live like any other mwananchi using their salaries to finance their accommodation and other essentials.
 
- Sheria ipi ya Jamhuri ambayo imevunjwa na hizo Millioni 10 za nyumba ya Spika? Na hata kama ningekuwa ninajua ninaweza vipi kuingilia sheria maofisa wetu nje wa ubalozi wanaishi kwenye nyumba za hela ngapi mpaka nishangae hizi hela ndogo sana?

- Spika wa bunge la kutunga sheria za taifa kisheria zetu anatakiwa aishi kwenye nyumba ya hela ngapi mbona maneno mengi bila facts? Wekeni facts Spika wa Kenya anaishi kwa hela ngapi? Wa Zambia anaishi kwa hela ngapi? as opposed na wetu ambaye anakiuka sheria ya Jamhuri kufungu kipi hicho na inasema nini hasa?

- Wakuu Tanzania tumeamua kufuata ubepari, katika ubepari serikali haimiliki nyumba za viongozi ikiwa ni moja ya sera za kuhakikisha hela zinazunguka katika kuboresha uchumi, kumilipia Spika na viongozi wote wa juu nyumba ni moja ya hatua muhimu sana katika kuboresha uchumi wa Taifa katika kuhakikisha kwamba wananchi wanaingiza pesa mifukoni mwao huku serikali ikikusanaya kodi katika hela hizo zake yenyewe, unless kuna ishus zingine separate zinazomhusu Spika na ufisadi ambazo mwenye facts anatakiwa kuziweka hapa tuzichambue, lakini la Millioni 10 na nyumba wakati tuna maofisa nje ya nchi wanaolipiwa more than this amount tena on monthly bases, binafsi sioni kuwepo na ishu hapa, Spika hawezi kwenda kuishi kwenye chamba cha kupanga na besides si kuna bajeti ya ofisi ya Spika inayopitishwa na wabunge wetu wa CCM na upinzani sasa hizi kelele ni kwa sababu Spika amepitisha bajeti ya matumizi ya ofisi yake or what?

- Can we talk facts badala ya emotions? I mean some ishus zinahitaji pure facts na hii ni mojawapo! Yaani the third leader on line to run our Government hatakiwi kuishi on $ 10,000 House tena only monthly tu? Aaaaaghhhhhhrrr!

Repsect.

Kamanda FMEs!


FMS,

May be we should perform a simple math. 10,000 * 12 = 120,000. In 2 years, the amount goes up to 240,000 USD. For this money they could take a loan from a bank and then build a house with all security features needed.
 
b; compared to us wananchi, na kipato cha nchi.

Hapana huko siyo kulinganisha kwa haki kwani kunafanywa based on vionjo. Tukifuata hilo, ni gari gani kiongozi anatakiwa awe nalo ukilinganisha na usafiri wanaotumia wananchi wengi? Je mtumishi wa umma anastahili kitu gani kulinganisha na mwananchi mwingine?

hofu yangu ni kuwa mtu ambaye amefanikiwa anapokuja kwetu kijijini anatakiwa avae marapurapu, atembee kwa miguu tena avae makubanzi ili afanane na wananchi anaowaongoza.

Hivyo, msomi asijifanye msomi sana kwani kwa kufanya hivyo anakuwa tofauti na wananchi wengi ambao si wasomi. Mwenye uwezo wa kujenga nyumba ya kisasa asiijenge ikawa ya kutisha sana kwani haimfananishi na mamiliioni ya watu.

Suala la kipato cha nchi is debatable; je kipato cha nchi hakiakisi matumizi hayo ya ofisi ya Spika maana kwa kadiri nilivyosoma hiyo taarifa ni kuwa serikali ndio imeefanya iliyoyafanya ina maana wanajua kuna uwezo wa kufanya hivyo.

Kufanya hayo anayoyafanya huku akijtangaza kuwa naye yumo katika mapambano ya ufisadi ni KUFURU na UNAFIK kuliko maelezo.

Hilo si sahihi; ufisadi siyo mavazi, nguo, cheo, elimu au kuishi maisha ya fahari au afueni. Ufisadi NI vitendo. Ndio maana kwangu mimi kashfa hapa ingekuwa:

a. Nyumba yenyewe haistahili bei hiyo
b. Nyumba hiyo mmiliki wake ana uhusiano wa wa karibu na Spika na hivyo imepatikana nepotism ya aina fulani. Au ni nyumba yake mwenyewe!
c. Spika alijiamulia bila kuishirikisha serikali
d. Pesa zinalipwa kupitia akaunti yake binafsi na hazijulikani zinakwenda n.k
e. Kulinganisha na bei ya upangaji katika eneo lililoko nyumba hiyo haistahili kupangisha kwa zaidi ya dola 1000 kwa mwezi. Je katika eneo hilo (sijui wapi) nyumba nyingine zinapangishwa kwa kiasi gani kwa mwezi na baadhi ya wapangaji ni nani? - Kama nyumba nyingine katika eneo hilo hilo za watumishi wa kawaida zinapangishwa kwa kati ya dola 5000 na 12,000 kwa mwezi then sidhani kama itamshtua mtu.
f. kwamba utaratibu unasema kuwa gharama ya kumpangishia Spika au mtumishi wa serikali isizidi dola 5000 kwa mwezi na yeye ameenda mara mbili yake; so far sijaelewa ni taratibu gani imevunjwa.

Kwamba yeye ameikuta kwenye sheria na taratibu is a lame excuse kwa sababu yeye kama kiongozi alipaswa kuona kwamba hilo ni tatizo na angeanzisha mchakato wa kubadilisha ujinga huo aliuokuta.

Hilo hapo ni kweli kabisa; lakini ni wangapi ambao wako tayari kukata tawi ambalo wao wenyewe wamekalia? Ni wangapi ambao wanapewa magari ya serikali na wanajua ni ya gharama kubwa kuliko vinginevyo?

Lakini hapa kubwa ni kuwa kama Wabunge wanaona kuwa Spika hastahili nyumba hiyo au ni ya ghali ni wao ndio wabadilishe au kumpunguzia hayo yote. Kitu ambacho itabidi kitulete pia kwa waliowahi kuwa mawaziri wakuu, marais n.k

Hivi aliyekuwa Waziri Mkuu na Spika ni nani ana hadhi kubwa? Ni nani anastahili kupewa pecks za aina mbalimbali. Je Spika anastahili kuwa na msafara wa magari au ajiendeshe yeye mwenyewe? Je anahitaji ulinzi kwenye nyumba yake ? Je anatakiwa kukaa kwenye nyumba ya vyumba vinggapi? Je anapopata wageni wa kimataifa anaweza kuwakaribisha nyumbani kwake? na eneo la hiyo nyumba liwe na uwezo wa kuegesha magari mangapi? n.k


Kwa maelezo haya yote sasa yanaingia-so all items above-a, b, c, and d- are a problem.


maelezo yako ni mazuri lakini hayajagusa au kuonesha kiini cha tatizo hasa.
 
...sioni justification yeyote kwa spika wa nchi maskini kama Tanzania kutumia 10,000USD kama house rent na gari ya milioni 300,ni upumbavu na ufisadi wa hali ya juu!
 
Mkuu ES haya ndiyo matatizo thread za JF siku hizi, kuna page 4 za threads ktk hizo zote zenye maana thread 10 au pungufu. Kibaya zaidi kwenye jukwaa muhimu la siasa almost majungu na udini tu. Inaboa kinoma.

anyway karibu Kamanda ES.``

Mkulu Nziku, heshima mbele sana you always have my respect,

- Ninakuelewa sana maana kila ninapopata nafasi ya kuingia hapa maana siku hizi kwangu imekuwa adimu sana, ninayaona sana unayoyasema, na hasa nimesikitishwa sana na ishus za udini zilivyotawala JF ya leo,

- Otherwise, inaonekana ni njama za makusudi za kujaribu kutuvuruga lakini hazitafanikiwa kwa sababu soon JF itakuwa kwenye masafa makubwa na ya ajabu sana kwa taifa letu, nimesha karibia ingawa bado nipo likizo ni kwa sababu tu ya Mkulu wangu George, ndio maana ninachungulia sana in the last four days tena kwa mtandao wa kuazima usiokuwa wangu, inabidi nilipie kwa saa!

- Pamoja na yote JF ita-prevail tu tena big time na very soon maana sasa tumeanza hata kutoa candidates wa uongozi wa juu wa taifa, ingawa kama ulivyosema mengine yanaboa sana!

Respect.

Kamanda FMEs!
 
...sioni justification yeyote kwa spika wa nchi maskini kama Tanzania kutumia 10,000USD kama house rent na gari ya milioni 300,ni upumbavu na ufisadi wa hali ya juu!

It is not justication; tunachotaka kuelewa ni kuwa tunaposema Spika anagharimiwa sana, tujiulize nani hagharimiwi zaidi?

a. Makamu wa Rais anapata pecks gani
b. Waziri Mkuu
c. Manaibu
d. Mkuu wa Jeshi/Polisi, Usalama wa Taifa
e. Jaji Mkuu
f. Wakuu wa Mikoa
g. Wakuu wa Mashirika ya Umma

Tusitageti mtu kwa sababu ya mtu; Tujaribu kuyaweka yote katika perspective:


Kuna vyombo vitatu vya Serikali yetu na kila kimoja kina mkuu wake:

- Rais ni mkuu wa utendaji: = anapata pecks gani kama Rais, mshahara wake wa mwezi, kuentertain guests, safari, msafara n.k?


- Jaji Mkuu - mkuu wa Mahakama - vipi yeye?


- Spika - mkuu wa Bunge


Hawa watatu wanaongoza mihimili ya serikali. So.. naomba niambiwe ni kitu gani anastahili Spika kama mkuu wa Mhimili wa serikali ambao unatunga sheria mbalimbali na kusimamia serikali nzima?

a. Tumjengenee nyumba ya vyumba vitatu na kumpa gari Corolla? ili afanane na wananchi wengi? Tukifanya hivyo, vipi kuhusu Rais na Jaji Mkuu?
 
FMS,

May be we should perform a simple math. 10,000 * 12 = 120,000. In 2 years, the amount goes up to 240,000 USD. For this money they could take a loan from a bank and then build a house with all security features needed.

- Mkuu ya serikali kumiliki nyumba yamepitwa na wakati sasa hayapo tena, hizi hela lazima ziwe injected kwenye uchumi wetu kupitia mikononi mwa wananchi na ndicho kinachofanyika kufuatia ushauri wa World Bank, ndio maana pamoja na mapungufu yake yote Mkapa bado uchumi ulikuwa ni one his of strength,


- Huko upande wa pili wa glass mnashindwa kuelewa kwamba gaharama za namna ya kuishi kwa viongozi wetu wa juu sio uamuzi wao, ni bunge letu ndilo linaloamua, sasa kumlaumu Spika ni kutomtendea haki kabisa! Sikatai huenda Spika ana madhambi yake mengine lakini hili la nyumba kwa maoni yangu hapana mkuu hakuna enough facts za kumhukumu.

Respect.

Kamanda FMEs!
 
I thought that these are the ones should fear for their lives.
Mzuvendi,
Once again you are right. But according to FMES our spika deserves an expensive house because of security reasons while it is the same CCM government that sold our taxpayers houses which were already paid for and had adequate security arrangements to accomodate ministers and the house speaker. And by the way who are they renting the house from?
 
- Mkuu ya serikali kumiliki nyumba yamepitwa na wakati sasa hayapo tena, hizi hela lazima ziwe injected kwenye uchumi wetu kupitia mikononi mwa wananchi na ndicho kinachofanyika kufuatia ushauri wa World Bank, ndio maana pamoja na mapungufu yake yote Mkapa bado uchumi ulikuwa ni one his of strength,


- Huko upande wa pili wa glass mnashindwa kuelewa kwamba gaharama za namna ya kuishi kwa viongozi wetu wa juu sio uamuzi wao, ni bunge letu ndilo linaloamua, sasa kumlaumu Spika ni kutomtendea haki kabisa! Sikatai huenda Spika ana madhambi yake mengine lakini hili la nyumba kwa maoni yangu hapana mkuu hakuna enough facts za kumhukumu.

Respect.

Kamanda FMEs!
FMES,
Siyo lazima ushauri wote wa World Bank/IMF ufuatwe. Ndiyo maana tuna viongozi ambao wanatumainiwa kupima na kuamua kwa mujibu wa hali zetu.
 
Mkuu Kitila heshima yako kwanza,

- As a nation na taratibu za usalama wa taifa kwa viongozi wetu wa juu, ni taifa ndio tunampangia kiongozi namna ya kuishi haamui mwenyewe, ndio maana hawasafiri kwenye Economy ingawa wengi wao wangependa hivyo kwa sababu ni wajibu wetu taifa kuwalinda kwa kufuata sheria za Jamhuri, Spika hawezi on his own kuamua mahali pa kuishi ni taifa ndilo tunamuamulia, hata singetaka hawezi kwa sababu hatuwezi ku-compromise usalama wake kwa sababu tu ya kujaribu ku-save peanuts,

- Kumlaumu Spika kwa sababu ya gharama ya nyumba anayoishi either ni ignorance au ni kukosa hoja za kuikosoa serikali, ndio maana sometimes tunajiuliza kwa wananchi wanaichagua CCM tu, off ocurse kwa hoja kama hizi ni clear kuwa wananchi hawana alternative na kama ipo basi ni very weak au iko kwenye political lifesupport somehwere!

Respect.

Kamanda FMEs!

Not as simple as you would want us to believe. Kwamba anapangiwa na ameukuta huo utaratibu sio hoja kwa sababu kama angetaka angebadili, uwezo huo anao. Aliweza kubadilisha kanuni za bunge atashindwa vipi kubadilisha utaratibu wa ovyo wa kukufuru matumizi ya walipa kodi maskini?

Hoja iliyopo hapa ni je ni sawa kwa kiongozi maskini kama Tanzania, ambayo zaidi ya 50% ya watu wake wanaishi chini ya sh. 1,300 kwa siku (chini ya sh. 39,000 kwa mwezi na chini ya sh. 500,000 kwa mwaka), kuishi katika nyumba ambayo pango lake ni zaidi ya sh.9,000,000 kwa mwezi (zaidi ya sh. 108,000,000 kwa mwaka) na kutembelea gari la zaidi ya sh 300,000,000 na kununua fanicha za zaidi ya sh 200,000,000? Inawezekanaje spika wa bunge la wananchi la nchi ambayo watoto wa shule wanakaa chini kwa kukosa madawati ya sh. 200,000 akae katika nyumba yenye fanicha za thamani ya sh 200,000,000 ambazo zinalipwa kwa hela ya walipa kodi maskini wasio na uwezo wa kula mara tatu kwa siku? Kwani angetembelea gari la sh. 50,000,000 angepungukiwa vipi na hiyo unayoita security? Hivi akilala kwenye nyumba yenye fanicha za sh 5,000,000 anapungukiwa vipi na hiyo security? Yeye kulala kwenye nyumba ya kodi ya sh. 1,500,000 kwa mwezi inamfanya vipi asiwe spika mahiri? Yaani yote haya wewe hayakusumbui isipokuwa huo uspika na hizo sheria zilizoweka huo utaratibu wa aibu?

Sasa kama kuuliza haya maswali ni 'ignorance' acha mimi niwe kwenye hilo kundi, na kama kuuliza haya maswali yatatufanya wananchi wasituchague, acha tuendelea kuwa chama cha upinzani!
 
Mzuvendi,
Once again you are right. But according to FMES our spika deserves an expensive house because of security reasons while it is the same CCM government that sold our taxpayers houses which were already paid for and had adequate security arrangements to accomodate ministers and the house speaker. And by the way who are they renting the house from?

- Mkuu Jasusi, heshima mbele sana unajua sana mkuu kwamba ushauri wa kuuza nyumba za serikali haukuwa wetu, ni wa tabia za kibepari tunazofuata ikiwa ni pamoja na kuuza mashirika yetu kwa mara ya kwanza katika historia ya taifa letu toka tuwe huru sasa mashirika ya siagara na bia yanaingiza faida na kuliingizia taifa dola millioni nyingi sana through kodi, yaani baada ya kuuzwa,

- Now look at this, eti hizo nyumba zinamilikwa na nani unasema ni tatizo la wapangiwaji? Are you serious mkuu au?

Respect.

Kamanda FMEs!
 
Back
Top Bottom