Ni ufisadi wa Spika Samwel Sitta

Ni ufisadi wa Spika Samwel Sitta

ndiyo hivyo.. mtu atusaidie tu.. kwa sababu hofu yangu ni kuwa hili la Spika lina zaidi ya suala la matumizi. Kuna zaidi ya malipo ya dola 10,000 kwa mwezi au magari. I really want to know what is this about.. maana haya mapambano ya fronts nyingi kweli.

Kuanzia mshahara na marupurupu, Spika analipwa sawa na Jaji Mkuu.

Bila kujadili kiwango cha kodi ya nyumba (kwamba dola 8000 ni sahihi au hapana), ukweli ni kwamba Spika wa sasa hana nyumba (official residence) maana iliyokuwepo Dar aliuziwa Msekwa (kupitia mama Ana Abdala ambaye alikuwa Waziri) na iliyokuwepo Dodoma aliuziwa Msekwa kupitia yeye mwenyewe.

Baada ya kupata uspika, alipangiwa nyumba ya kukaa katika quota za manaibu mawaziri pale Kijitonyama. Wabunge (Kamati ya Uongozi) ikakataa na kuona ni udhalilishaji wa Bunge. Ikaamuliwa apangiwe nyumba.

Sheria ya manunuzi ndio hutumika katika kupata huduma kama hizo ambapo spika hahusiki katika zabuni. Kumlaumu Sitta katika hili sio sahihi. Suala la msingi ni kuangalia kama kuna 'value for money' katika huduma hiyo na nyumba ni ya nani? Ilipatikanaje? Sheria ya manunuzi ilifuatwa? Nyumba za jirani na nyumba hiyo 'rent' yake ni hiyo hiyo? Ninadhani hayo ndio masuala ya msingi ya kujiuliza badala ya kupeleka akili zetu zote kwa 'individual' anaeitwa Samwel Sitta.
 
Matumizi machafu ya serikali kumgharimia Spika? Ni kiasi gani cha matumizi ya serikali kwa spika tunaweza kuyakubali kuwa ni masafi?

Matumizi machafu ni yale yote ambayo kwa njia moja au nyingine yanaujumu uchumi wa nchi. Na hii aijali kama ni shilingi mbili au bilioni mbili ! Ni mtu Fisadi ndiye anayeweza kusema ya kuwa shilingi millioni mia mbili ni sahihi katika kununulia fenicha za spika.

Tusema kuwa angekuwa anapanga nyumba kwa dola 5000 kwa mwezi na kuendesha corolla au nissan altima tutasema ni masafi? Vipi kama tungeamua kumjengea nyumba sehemu fulani katikati mjini kwenye mitaa yetu walalahoi, itamleta karibu zaidi na wananchi siyo?

Kwanza lazima utambue kitu kimoja sio mandatory kwa serikali kumpatia huyu bwana nyumba, hata Spika mwenyewe anaweza kunisupport mimi katika hili. Yeye mwenyewe alisuport uuzwaji wa nyumba za serikali , kwani alijua ya kuwa hazina umuhimu.


Matumizi mabaya yapo lakini hadi hivi sasa sijaona hayo ya Spika kuingizwa katika ubaya huo. Matumizi mabaya ni yale ambayo hayajulikani kiasi chake, yanakwenda wapi, na yanatumiwa na nani. Matumizi mabaya ni ya mtu anayetumia fedha ya serikali kwa uamuzi wake mwenyewe kujinufaisha. Hadi hivi sasa sijaona mahali ambapo panasema Spika ndiye amejitengea fedha hiyo na kujilipa yeye mwenyewe.

Hii si kweli kabisa , matumizi kujulikana haimaanishi ya kuwa ni sahihi. Pili, sio lazima matumizi mabaya yamnufaishe mtu binafsi , yanaweza yakainufaisha familia au sometimes jamii. Tafadhali rejea mfano wangu wa yatch hapo juu.

Kama kweli tunataka kupunguza matumizi na kuleta nidhamu kwanini tusililie kile tunacholilia sisi wengine nacho ni kusitisha misaada ya kigeni ili hawa viongozi wajifunze kutumia kidogo tulichonavyo kwa umakini?

Sasa unajicontradict mwenyewe kumbe unajua ya kuwa wanatumia hela ovyo ovyo. Mimi nilidhani ya kuwa unakubaliana nao, na kama unakubalina nao then kwa nini wajifunze kutumia hela kwa makini. Halafu wewe unasema hivyo na wakati ho huo unadefend sheria inayohalalisha maisha ya kifahari. kwa nini wajifunze kutumia hela kwa makini wakati hawajavunja sheria ?



Hivi unafikiri tatizo la Tanzania ni fedha? Yaani, unaamini kuwa umaskini wetu sisi unasababishwa na ukosefu wafedha. Mnachozungumzia kwenye Spika ni dalili tu ya tatizo lenyewe.

Tunachozungumzia kwenye Spika ni bunge lililooza chini ya usimamizi wake duni. Bunge ambalo linalotetea maslahi ya wachache. Bunge ambalo linasema wabunge wasilipe kodi , despite the fact that they are being paid a lot of money.
 
Kuweka taarifa sawasawa, Sitta hakuwa Mbunge kati ya 1995 - 2005. Hivyo, wakati nyumba zinauzwa hakuwa Mbunge.

Pili, kuuzwa kwa nyumba hakukuidhinishwa na Bunge na ndio maana kuna azimio la Bunge la kutaka nyumba zirudishwe.

Ni kweli kabisa kuwa spika hakupew nyumba ile akiwa anfanya kaziTIC,kwa kuwa ole naiko aligoma kuiuza,bali alipewa mara baada ya kuchaguliwa kuwa spika na ilijengwa hoja na ofisi ya spika
 
Jamani!
Munafahamu kile kifungu 1001, mshahara wa waziri wa wizara, siku zote inatajwa at least billion 2.x sasa hizo kwa waziri ndogo kwa mwaka?
Wandugu wenzetu wanatumbua nchi mimi sina issue na spika, wapo dagaa wanakula sana tu.
 
Sheria ya manunuzi ndio hutumika katika kupata huduma kama hizo ambapo spika hahusiki katika zabuni. Kumlaumu Sitta katika hili sio sahihi. Suala la msingi ni kuangalia kama kuna 'value for money' katika huduma hiyo na nyumba ni ya nani? Ilipatikanaje? Sheria ya manunuzi ilifuatwa? Nyumba za jirani na nyumba hiyo 'rent' yake ni hiyo hiyo? Ninadhani hayo ndio masuala ya msingi ya kujiuliza badala ya kupeleka akili zetu zote kwa 'individual' anaeitwa Samwel Sitta.


hii ndiyo inaitwa crux of the matter.. kwangu mimi kama kuna kashfa basi imejikita katika mambo hayo.
 
sawa.. given

Unajua GDP ya Tanzania
Unajua hali mbaya ya maisha ya Watanzania
Unajua matatizo yetu ya kiuchumi n.k

Sasa tuseme unatoa pendekezo la kuonesha kuwa Spika hawi extravagant. Ni kipi kiwe anastahili kama spika na ni kipi kiwe ni pecks ambazo si za lazima, assuming kuwa hawajafanya lolote kuinua GDP?


a. Mshahara wa Spika uwe kiasi gani kwa mwezi?

$ 120. Hapa tunataka watu wenye nia ya service, na si kujitajirisha

b. Apewe gari/magari mangapi na ya aina gani?
Land rover 110 moja

c. Nyumba yake kama Spika iwe na thamani ya kiasi gani na iwe na ukubwa gani? na amenities gani?

$ 100,000 ya serikali, samani za JKT/ Magereza (bure) gardener wa kutoka magereza (bure)

d. Kama ni ya kukodi, iwe kati ya kiasi gani na maeneo gani?

Kikodi ni concept za kimagharibi ambazo kwetu ni gharama zaidi ya kumiliki

e. Je apewe ulinzi wa nyumba na binafsi na wa idadi gani ya walinzi?

Walinzi wawili wa Polisi (nyumbani) na mmoja usalama wa taifa (personal)na gardener mfungwa wa kosa lisilo violent crime anayemalizia muda wake.

f. Je awe na bima ya afya inayogharimiwa na serikali au la na yenye kiasi gani?

serikali impe posho ya afya $ 30 kwa mwezi itakayopanda kulingana na kupanda kwa GDP

g. Je akisafiri kwenda nje kikazi safari zake zisidi kiasi gani? Je aende na msaidizi yeyote?

Safari zisizidi $ 10,000, msaidizi mmoja na usalama wa taifa wake, ikibidi usalama wa taifa anakuwa msaidizi wake vile vile kubana matumizi.

La kuzingatia katika majibu yenu, naomba mhakikishe kuwa kitu chochote mnachompatia hakizidi hali ya maisha ya Mtanzania wa kawaida.

Breakdown yangu iliyo realistic na maisha ya mtanzania hiyo hapo.Itatupa mtu mwenye nia ya service, wenye uchu wa pesa hata hawatagombania hiyo nafasi.
 
Tunachozungumzia kwenye Spika ni bunge lililooza chini ya usimamizi wake duni. Bunge ambalo linalotetea maslahi ya wachache. Bunge ambalo linasema wabunge wasilipe kodi , despite the fact that they are being paid a lot of money.

Nadhani Bunge hili la Tisa ni moja ya mabunge yaliyofanya kazi kubwa sana kuhusu kupinga ufisadi na kutetea rasilimali za nchi. Nakubali kuwa kuna matatizo makubwa sana tu ambayo ni lazima tuyatatue kama suala la kodi nk, lakini sidhani kama Bunge hili limeoza. Changamoto kubwa ni kuondoa ukiritimba wa chama kimoja ndani ya Bunge. Tukifanikiwa hili, mambo mengi yatakwenda bomba. Mkiirudisha CCM na majority yake Bungeni kama hii, mtaendelea kulalama tu kwani masuluhisho ya kimfumo hayatawezekana.
 
Breakdown yangu iliyo realistic na maisha ya mtanzania hiyo hapo.Itatupa mtu mwenye nia ya service, wenye uchu wa pesa hata hawatagombania hiyo nafasi.

sorry.. mapendekezo yako yote yanamfanya asifanane na Mtanzania wa kawaida. Mtu mwingine ataona ni kumtengenezea maisha ya anasa. Labda umodify ili yote utakayoyapendekeza yasimfanye aonekane ana maisha ya kifahari. Kutumia dola 10,000 kwa safari watu wachache sana wanaweza kutumia hizo.

Halafu dola 120 kwa mwezi ni chini ya kiwango anacholipwa Polisi, daktari, n.k sasa siyo tu umemfananisha na watu wa kawaida, bali umemshusha mno. Na kama ana watoto wadogo au walio shule atamudu kweli hata kama ana wito? Siyo kwamba tutamtengenezea mazingira ya kutafuta "fedha ya ziada pembeni"..
 
Hapa tunazungushana maneno tu. Tunajaribu kufanya ionekane kuwa hili la Spika ndilo limesababisha hali mbaya ya maisha ya wananchi wetu.

Mwanakijiji hapa huwatendei haki hata kidogo watu usikubaliana nao. Tunachojaribu kufanya ni kuonyesha jinsi Ufisadi wa tuliowapa madaraka unavyosababisha hali mbaya ya maisha ya wananchi wetu, Spika akiwa moja kati ya hao viongozi. Tumeshuhudia spika huyo huyo siku moja anatoa machozi ya mamba eti nchi inaendeshwa vibaya na siku ya pili yeye anakaa kimya na kukubali kutapanywa kwa mali za Watanzania kwa kisingizio cha stahili ya spika.

Tunataka (kwa makosa) kubebesha mzigo wa lawama wa matatizo ya wananchi wetu kwenye mgongo wa nyumba ya Spika wa Jamhuri ya Muungano. Kwamba madawati hayatoshi sababu ni nyumba ya spika, n.k

Dr. Slaa alipopiga kelele kuhusu malipo makubwa wanayopata wabunge, Mh. Samwel Sitta kama Spika aliwaongoza walafi wenzie bungeni kumlaani. Spika Sitta kama kiongozi wa Bunge alikaa kimya siku wabunge wa CCM, ambao ni asilimia kubwa, walipokuwa wanashauriwa kutanguliza maslahi ya chama mbele ya taifa. Bunge ni taasisi muhimu na linapopwaya, mihimili mingina lazima nayo itapwaya.

Sasa mimi naomba wale ambao wanaona kuwa this is extravagant watupe angalau mchanganuo wao wa kile anachostahili Spika. Lets assume siyo mtu anaitwa Samuel Sitta.

Yale yale.

a. Mshahara wa Spika uwe kiasi gani kwa mwezi?
b. Apewe gari/magari mangapi na ya aina gani?
c. Nyumba yake kama Spika iwe na thamani ya kiasi gani na iwe na ukubwa gani? na amenities gani?
d. Kama ni ya kukodi, iwe kati ya kiasi gani na maeneo gani?
e. Je apewe ulinzi wa nyumba na binafsi na wa idadi gani ya walinzi?
f. Je awe na bima ya afya inayogharimiwa na serikali au la na yenye kiasi gani?
g. Je akisafiri kwenda nje kikazi safari zake zisidi kiasi gani? Je aende na msaidizi yeyote?

Tuna watu tumewachagua na wanalipwa kushughulikia haya maswali kwa kuzingatia hali halisi ya nchi yetu. Hivi kweli tunaomba msaada ili Spika wetu alipiwe pango USD 8.000, anunuliwe gari USD 30,000 na anunuliwe samani USD 20,000 wakati watoto wetu wanakufa kwa malaria. Kama mamlaka tulizonazo haziwezi kufanya tathmini na kutoa majibu kwa maswali haya, basi hazitufai - iwe serikali, bunge au mahakama.

La kuzingatia katika majibu yenu, naomba mhakikishe kuwa kitu chochote mnachompatia hakizidi hali ya maisha ya Mtanzania wa kawaida.

Hoja yako inakosa nguvu kwa kujikita zaidi kwa mtu moja - hata hivyo kwa nini tuna wawakilishi bungeni na kwa nini tuna serikali. Halafu tunaambiwa Raisi ndiye aliridhia hayo malipo, je ina maana angeweza kukataa ? Mwanakijiji kuna kamtindo hapa ka kutetea majina fulani fulani eti wanapiga vita ufisadi huku vitendo vyao na maisha yao wamepiga kambi kwenye bonde la ufisadi. Kama Spika Sitta hayuko kwenye kundi la mafisadi basi kumbe twajidanganya - hakuna fisadi Bongo.
 
Hapa tunazungushana maneno tu. Tunajaribu kufanya ionekane kuwa hili la Spika ndilo limesababisha hali mbaya ya maisha ya wananchi wetu. Tunataka (kwa makosa) kubebesha mzigo wa lawama wa matatizo ya wananchi wetu kwenye mgongo wa nyumba ya Spika wa Jamhuri ya Muungano. Kwamba madawati hayatoshi sababu ni nyumba ya spika, n.k

Sasa mimi naomba wale ambao wanaona kuwa this is extravagant watupe angalau mchanganuo wao wa kile anachostahili Spika. Lets assume siyo mtu anaitwa Samuel Sitta.


a. Mshahara wa Spika uwe kiasi gani kwa mwezi?

b. Apewe gari/magari mangapi na ya aina gani?

c. Nyumba yake kama Spika iwe na thamani ya kiasi gani na iwe na ukubwa gani? na amenities gani?

d. Kama ni ya kukodi, iwe kati ya kiasi gani na maeneo gani?

e. Je apewe ulinzi wa nyumba na binafsi na wa idadi gani ya walinzi?


f. Je awe na bima ya afya inayogharimiwa na serikali au la na yenye kiasi gani?

g. Je akisafiri kwenda nje kikazi safari zake zisidi kiasi gani? Je aende na msaidizi yeyote?

La kuzingatia katika majibu yenu, naomba mhakikishe kuwa kitu chochote mnachompatia hakizidi hali ya maisha ya Mtanzania wa kawaida.

MMJ,

Kitu kikubwa kinachopigiwa kelele hapa ni matumizi makubwa ya pesa ambayo si ya lazima yanayofanywa na viongozi wetu katika nchi masikini Tanzania. Hili suala la spika limekuwa ni mwanga wa kuonesha kwamba wakuu wetu wanatuumiza kwa kiasi kikubwa sana. Hapa nikiwa na maana mawaziri, makatibu wakuu, Raisi, wakuu wa mikoa nk wamekuwa na matumizi makubwa ya pesa yasiyo kuwa ya lazima katika nchi masikini kama Tanzania. Kumshambulia spika ni kwa sababu matumizi yake yamejulikana hadharani na bila shaka JF pia haitasita kumshambulia kiongozi yeyote matumizi yake yakijulikana na kama hayaendani na maisha na uwezo wetu.

Hatumaanishi kwamba matumizi makubwa ya spika pekee yake ndiyo chanzo cha ukosefu wa madawati, madawa na huduma nyingine muhimu kwa jamii bali yanachangia kwa namna moja ama nyingine kuleta madhara hayo na bila kuona haya wala kuchelewa ni muhimu kuyapigia kelele.
Hizi kelele ni kengele ya kuwaamsha viongozi wetu ili waanze kuangalia upya matumizi yao na wala si za spika pekee yake.

Elewa kuwa kila sherehe (Ngoma) ina mwanzo wake. Tumeanza kwa kuchambua suala la matumizi ya spika kwa kulinganisha na hali halisi ya kipato chetu na bila shaka tutafikia katika kuchambua matumizi ya wakuu wetu wengi na tutapata picha kamili nini kinaendelea na tutaweza kutoa ushauri kwa wahusika. Na hilo tunaweza lianza kwa yeyote si lazima awe spika, lakini kwa sababu ambazo mimi na wewe hatuzijui suala la spika limewekwa mezani.
 
Matumizi mabaya ya fedha za serikali NI PAMOJA NA HILI!udhalilishaji wa bunge?....tena kuishi kijitonyama?

WANGEWEZA KUTUMIA HATA MILIONI MBILI,hizo nane zinaelekezwa kwenye mikopo ya wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu!mkwa mwaka ni milioni 96,ambayo itasomesha wanafunzi hata 12 kwa mwaka mzima

udhalilishaji wabunge?...........THERE IS NO POINT!
 
Invisible na mwanakijiji,hapa ninazo picha za nyumba ya spika aliohamia,tangu jana nashindwa kiziweka humu.nani nimtumie kwa email now aweke.nangojea jibu lenu
 
Baada ya kupata uspika, alipangiwa nyumba ya kukaa katika quota za manaibu mawaziri pale Kijitonyama. Wabunge (Kamati ya Uongozi) ikakataa na kuona ni udhalilishaji wa Bunge. Ikaamuliwa apangiwe nyumba.

Nashukuru sana kwa majibu yako , ambayo kiasi fulani yamenihuzunisha sana ! Kwa hiyo kamati ya bunge iliona ni kuzalilishwa kwa Spika kupangiwa nyumba hapo Kijitonyama ! Hivi watu wakifika hapo Bungeni mbona wanajichukulia too serious, Spika ana tofauti gani na naibu waziri. Na bunge litadhalilishwa vipi kwa yeye kuishi kwenye hizo nyumba. Mimi naona tatizo ni low self esteem !

Sheria ya manunuzi ndio hutumika katika kupata huduma kama hizo ambapo spika hahusiki katika zabuni. Kumlaumu Sitta katika hili sio sahihi. Suala la msingi ni kuangalia kama kuna 'value for money' katika huduma hiyo na nyumba ni ya nani? Ilipatikanaje? Sheria ya manunuzi ilifuatwa? Nyumba za jirani na nyumba hiyo 'rent' yake ni hiyo hiyo? Ninadhani hayo ndio masuala ya msingi ya kujiuliza badala ya kupeleka akili zetu zote kwa 'individual' anaeitwa Samwel Sitta.


Tunamlaumu Spika kwa sababu when it comes to our parliament issues, THE BUCK STOPS WITH HIM. Mwanasiasa yoyote makini angependa kujua ni kiasi gani kimetumika katika kulipia gharama mbali mbali zinazomhusu yeye.
 
Mijadala yetu watanzania wakati mwingine huwa ninapata nayo shida sana. Mara kwa mara tunaangalia mtu na kuachana na hoja kabisa. Hebu nije kwenu kwa kuangalia mtu. Lengo ni kupanua tu mjadala ili mjaribu kuona kuwa suala la malipo au stahili za dhamana ya kikatiba ni suala la kuliangalia kwa mapana yake.

Agalia mifano ifuatayo.

1. Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania mshahara wake ni 16,000,000 kwa mwezi
2. Kamishna Mkuu wa TRA analipwa sh 18,000,000 kwa mwezi
3. Mkurugenzi Mkuu wa TBC analipwa sawa na Gavana wa Benki Kuu.
4. Orodha ni ndefu na hao wote mshahara wao (mshahara tu bila marupurupu mengine) ni zaidi ya ule anaopata Rais wa Nchi (Rais analipwa 5.4m kwa mwezi).

Turudi kwenye hoja, malipo ya nyumba ile yanaendana na soko? Taratibu zilifuatwa? Lakini kama lengo lenu ni kumsulubu Sitta, mnaweza kuendelea na wala hamtapata suluhisho maana kesho akiwa Spika Slaa au Hamad Rashid au Marmo nk, atalipiwa nyumba hivyo hivyo kama hatutamaliza tatizo la Nyumba kwa viongozi wa Kikatiba.

Fenicha za 200m zilizonunuliwa kwa ajili ya nyumba ya Spika, ndizo hizo hizo na thamani hiyo hiyo ambayo amenunuliwa Jaji Mkuu na ni zaidi ya hapo alizonunuliwa Waziri Mkuu amara alipoteuliwa maana PM anaetoka hutoka na kila kitu alichokuwa anatumia (wanasema ndio commonwealth tradition)
 
Hoja yako inakosa nguvu kwa kujikita zaidi kwa mtu moja - hata hivyo kwa nini tuna wawakilishi bungeni na kwa nini tuna serikali. Halafu tunaambiwa Raisi ndiye aliridhia hayo malipo, je ina maana angeweza kukataa ? Mwanakijiji kuna kamtindo hapa ka kutetea majina fulani fulani eti wanapiga vita ufisadi huku vitendo vyao na maisha yao wamepiga kambi kwenye bonde la ufisadi. Kama Spika Sitta hayuko kwenye kundi la mafisadi basi kumbe twajidanganya - hakuna fisadi Bongo.


Mag3.. una miss pointi kubwa sana; Ukisoma hiyo makala ya Tanzania Daima unaweza kuona jinsi gani imemlenga mtu na siyo hasa tatizo lenyewe. Na mwitikio wa watu wengi umekuwa ni hivyo hivyo wa kuangalia Sitta zaidi na siyo tuhuma au madai yenyewe.

Lengo langu la kuuelekeza mjadala ni ili tuweze kufikia mahali tujue hasa tatizo ni nini.

a. Je Sitta ametumia cheo chake vibaya: Hili hatuwezi kulisema hivi hivi bila kujua nyumba hiyo inapangishwa wapi na ni ya nani?

b. Je gharama ya nyumba hiyo ni kubwa mno? Hilo nalo hatuwezi kujua kwa uhakika hadi tujue imepangishwa wapi na kulinganisha bei ya kupangisha eneo hilo ikoje.

c. Je kiasi kilichotumika ni kikubwa mno? Hilo nalo ni gumu kulielewa hadi tuweze kulinganisha na jinsi tunavyowahudumia viongozi wengine wa kitaifa. Wabunge wanalipwa vipi, mawaziri, wakuu wa mikoa n.k and then tuna factor ya Spika.

Mwisho wa siku tukiuliza maswali sahihi tutaona kuwa tatizo siyo kwa Spika tu. And that is my point. Kwamba kwa kuangalia spika tu tunakwepa kuangalia kiini hasa cha tatizo. Tuna tatizo katika usimamizi wa fedha, tuna tatizo katika matumizi ya fedha, tuna tatizo katika matumizi mabaya ya madaraka n.k Hili la Spika ni kiduchu tu na yawezekana lisiwe kubwa kama tatizo lenyewe.

HII ndiyo sababu I'm trying to move hoja kutoka kwa mtu kuelekea mfumo na muundo wetu wa utawala.

Katika hili umemiss kunipata mkuu. Sitetei mtu yeyote ambaye ni fisadi; lakini vile vile siharakishi kuhukumu bila ya kupata taarifa za kutosha. Nimejifunza kwenye masuala kadhaa ya huko nyuma.
 
Spika ana tofauti gani na naibu waziri. Na bunge litadhalilishwa vipi kwa yeye kuishi kwenye hizo nyumba. Mimi naona tatizo ni low self esteem !

Duh! sasa kama hujui tofauti kati ya Spika na Naibu Waziri.. tutakuwa na mjadala mrefu kweli.

Tunamlaumu Spika kwa sababu when it comes to our parliament issues, THE BUCK STOPS WITH HIM.

NO it does not! He is not the King of the Parliament!
 
Back
Top Bottom