Ni choyo tu wabongo hamna chengine ,mmeimaliza Zanzibar sasa mwageukiana wenyewe kwa wenyewe ,ivi dola 8000 ndio zinawatoa roho ,sasa napata akili kwanini kuna majambazi wengi na vibaka wa simu za mkononi.
Yaani dola alufu nane ndio tayari watu wengine wameanza kuona jamaa anafaidi ? Mnashindwa kufahamu kuwa nchi yetu si masikini ya kumlipa mtu dola hizo na haswa kutokana na cheo chake ,mnaacha mambo muhimu ya kujadili na kutafakari ,mnaenda kumvamia spika ,kweli umasikini kitu kibaya , sijui kama kuna mtu amewahi kushikwa na njaa ya kula na hana matumaini ya kupata mlo ,tabu yake unatamani ukimuona mtu anakula hungojei hata kukaribishwa unatamani umpokonye ule wewe na hapo ndipo walipo baadhi kama tuonavyo humu.
Ni njaa na umasikini wa kuona fulani anapata kingi , kama ni hivyo fanyeni siasa ili muwaondoe na kubadilisha yote hayo ,kwa maana kukaa na kusema mna mabo peke yake haitoshi wala haisaidii chochote ,toka yalikuwa mambo makubwa ya wananchi kuyaona ya ajabu mpaka sasa inaonekana ni nyimbo tu kama nyimbo zingine za kwenye redio au unaweza kufananisha na ze comedy tu,hayana mvuto kabisa ,maana hayasaidii chochote kile.
Fanyeni siasa sio kumuonea mtu kijicho ,sasa ingekuwa wewe ungetaka upunguziwe ? Timeona hapa sijui mbenge gani ameenda kuvamia ,eti wabunge wanalipwa mshahara mkubwa ? Sasa kama mshahara ni mkubwa na yeye unamkereketa basi angekuwa wa mwanzo kuukataa na kumwomba spika ampunguzie ,lakini wapi ,unabaki kupiga mayowe ,mshahara wa wabunge mkubwa huku unaisabu tarehe.
Siasa si mchezo wa kuigiza ni mambo kwa vitendo ,omba upunguziwe,jiuzulu ,wachia ngazi ,hio ndio siasa ,unapoona jambo haliendani na msimamo wako ni lazima uonyeshe kwa vitendo sio unakaa na kupiga makelele tu ,hio sio siasa itakuwa ni uchoyo kwamba kuna wengine nao wanapata fedha pengine baada ya muda kwa akili zao wakakupita kwenye maslahi na wao wakaendeleza zaidi wakakuwacha pale ulipo.
Spika aendelee kupata hiyo hela na mwengine nae pia aendelee ,siku nyie mlioko mstari wa mbele hapa mkifanikiwa kuukwaa utawala wa Nchi tuwaone mkikatakata mishahara yote ya waserikali ,ila msije mkaongeza zaidi ,tutashindwa kuwaelewa.