NHIF inachangia kuua Huduma za Afya kwa kutolipa madeni ya Hospitali

Hivi wewe hujui kupiga hesabu, kuna familia zetu wengine kubwa, wazazi wa pande zote mbili, watoto bado na mke wa pili, we peke yako utaweza kubeba. Mbona huoni fursa khaaa heheee.

ila kwann watanzania wanajichimbiaga mashimo wenyewe nimeamini.


Nisome vizuri sana huenda hujanielewa vizuri.

Mume na mke wote wanakatwa michango ya bima kuchangia watu wale wale .

Wakati inatakiwa mmojawapo tu ndiye achangie.

Hivi unaelewa lakini ?
 
Nisome vizuri sana huenda hujanielewa vizuri.

Mume na mke wote wanakatwa michango ya bima kuchangia watu wale wale .

Wakati inatakiwa mmojawapo tu ndiye achangie.

Hivi unaelewa lakini ?

We una familia umeoa na mke na ana kadi na ana nafasi nne za wategemezi na we nne.... wote mnafanya kazi. Niambie, wewe unaweza kuwabeba wazazi wote na watoto wote ........... peke yako?
 
We una familia umeoa na mke na ana kadi na ana nafasi nne za wategemezi na we nne.... wote mnafanya kazi. Niambie, wewe unaweza kuwabeba wazazi wote na watoto wote ........... peke yako?


Kwani hizo nafasi 4 ni pamoja na watoto?

Wazazi wana nafasi zao mbali na nafasi za watoto 4.

Isitoshe kwa wale ambao wana extend families mfano mitala n.k

Uwepo utaratibu wa wale ambao wanahitaji kukatwa wote mke na mume kwa sababu zao wakatwe na wale ambao kutokana na facts zao hawastahili kukatwa wasikatwe wote , achangie mmoja tu.

Yule ambaye hana mzigo wa wategemezi wengi asilazimishwe kuchangia mke na mume .

Kusiwepo na mazoea au kukariri kwenye hili.

Kuna wengi wamejikuta mke na mume wanakatwa kwa dependants wale wale , walioko kwa mume Ndiyo walioko kwa mke , sasa huoni kuna dhuluma?

Kama anaochangia mke na anaochangia mume ni dependants tofauti hapo inakuwa sawa na haki na siyo kuwa walewale.

Umenisoma vema sasa?
 
Kwani hizo nafasi 4 ni pamoja na watoto?

Wazazi wana nafasi zao mbali na nafasi za watoto 4.

Isitoshe kwa wale ambao wana extend families mfano mitala n.k

Uwepo utaratibu wa wale ambao wanahitaji kukatwa wote mke na mume kwa sababu zao wakatwe na wale ambao kutokana na facts zao hawastahili kukatwa wasikatwe wote , achangie mmoja tu.

Yule ambaye hana mzigo wa wategemezi wengi asilazimishwe kuchangia mke na mume .

Kusiwepo na mazoea au kukariri kwenye hili.

Kuna wengi wamejikuta mke na mume wanakatwa kwa dependants wale wale , walioko kwa mume Ndiyo walioko kwa mke , sasa huoni kuna dhuluma?

Kama anaochangia mke na anaochangia mume ni dependants tofauti hapo inakuwa sawa na haki na siyo kuwa walewale.

Umenisoma vema sasa?
Jaribu kutaka uelewa kwanza Mtanzania. Nafasi nne unaweza kuweka wazazi au watoto. Upo apo?
 
Actually hii imeshajidiriwa sana tena mara nyingi kwenye vikao rasmi vye kiofisi na hao jamaa wa NHIF na wanachama.

Jibu ambalo walitoa wakati fulani ni swala la udanganyifu toka kwa baadhi ya wanachama .

Lakini swala la udanganyifu wa wengine Ndiyo iwe fimbo ya kuwaadhibu wengine ambao siyo wadanganyifu?

Wanatakiwa waweke mifumo yao vizuri ili iwapo mwanachama atawadanganya wamtambue mapema na kumchukulia hatua kali za kisheria na siyo kuwakata mume na mke michango ambayo dependants ni wale wale.
 
Wanachama wanachangia kwa kukatwa mke na mume wakati inatakiwa achangie mmoja tu.

Kila mkiambiwa mkurugenzi Konga hili swala hulioni ni tatizo?

Hii ni dhuluma kubwa sana.

Kama mume na mke wako taasisi moja ambako unaweza kujiridhisha vyeti vya ndoa kwanini mnalazimisha wote wachangie?

Imarisheni namna yenu ya kusimamamia taarifa sahihi na kushindwa kufanya hivyo isiwe kisingizio cha kusema wengine hutoa taarifa za udanganyifu.

Watakaodanganya watambueni sheria ichukue mkondo wake na siyo kishindwa kwenu kusimamamia na kuweka mifumo ya utambuzi wa mapema muwakate mke na mume kwa wakati mmoja..

Bernard Konga na wenzio tafakarini hayo na kuyatolea ufumbuzi wa haraka.

Au mpaka tumwambie Madam President ndipo mtalifanyia kazi hili?
Kwanza tuwe waungwana kama misingi ya JamiiForums, moja ni kuheshimu nafasi za kazi/uteuzi au heshima tu kwa mtu - kutajana majina siyo jambo jema, tumia tu cheo - Mkurugenzi Mkuu, au "cheo-flani" inatosha kufikisha ujumbe..

Mbili, naona kama vile ume-divert ktk hoja ya vituo thread iliyoanzishwa na kuingia ktk specific issues - unrelated..

Okay, kujibu hoja yako ni hivi: ukipitia sheria ya NHIF ya 1999 na marekebisho yake 2002, 2005, 2009, 2010, 2015, inaongelea makato kwa mtumishi mwajiriwa. Yatosha ieleweke makato haya kisheria ndiyo msingi wa undugu wa kuchangiana matibabu. Ni kama ilivyo PAYE unakatwa lakini yawezekana nje ya nyumbani kwako barabara ni ya vumbi, yawezekana unataka lami; kupitia PAYE ya mwajiri na kodi nyinginezo mpaka za vinywaji/madukani ungetemea maji yakufikie ila labda bado - ila haimaanishi hiyo kodi haifanyi kazi, au haifikii wengine, au haitakufikia na wewe.

Vivyo hivyo, mchangiaji na mwenza wanakatwa kama sehemu ya kutimiza sheria, ila pia wanakatwa kama sehemu ya kutunisha Mfuko. Watanzania tunatakiwa tujifunze kuwa wazalendo, kuupenda Mfuko na kuona faida yake kwa jicho pana zaidi, na siyo kujiangalia kipekee (individualistic). Leo unaweza kuona unanyanyasika kukatwa wewe na mwenza; kesho akija ndugu yako kuomba laki 6 mfano kwa ajili ya matibabu ya mtoto wake, unampa Tsh. 50,400 na kumwambia akakate Toto Afya NHIF atapata matibabu yote - ila ngumu kumeza ni kusukumiza fikra nyuma ya ubongo hiyo difference inatoka kwa nani (600,000 - 50,400); kama siyo uzalendo wa uchangiaji? I can justify this point all over and over with different scenario ila kama jicho la kiuzalendo na undugu limefungwa ila lililo wazi ni individualistic we shall always be parting ways..

Yatosha ieleweke makato haya nayo ni akiba kwa lile usilolijua mbele:
i] Moja ya ukomo wa uchangiaji ni kifo, na hivyo huduma hukwama; sasa let us assume for a moment mwenza ulikuwa huchangii, unatengemea Bima ya mwenzako, alafu ikatokea akafariki - na wewe na watoto mkawa ktk immediate need ya medical service hapo hiyo taharuki unaiwekaje? Upande mmoja umetoka kuzika - na upande mmoja magonjwa/shida hazitatuliki bila pesa, kwa sababu huna Bima.

ii] Uchangiaji huu ni akiba ya credits kukusaidia upate fao la ustaafu; kwa macho ya kutoona mbele waweza sema hakuna msingi wa kuchangia uengemee kwa mume/mke; ila itakapotokea mwenza wako akapata ajali kazini/ulemavu akashindwa kufanya kazi; au akaachishwa au worse akafariki..piga picha miaka imeenda na credits umekosa za ustaafu, unajitengenezea ugumu wa maisha kwa sababu ambazo zingeepukika.

iii] Uchangiaji huu unakusaidia kuwaweka wategemezi: mwenza, watoto wako wa kuzaa, watoto wako wa kufikia, watoto wa kuasili (adopted children), wazazi, wakwe. Ni fursa pana ya kuwaweka hawa wategemezi. Wengi huingia ktk mkumbo wa kulalamika "mimi na mke tunakatwa" kwa kutokujua extent ya coverage aliyonayo. Mwingine anajua ila baada ya kuonja tunda la neema na akaitumia kuweka hawa wategemezi, anaona hakuna haja tena (unthankfulness & ignorance); na mwingine inatokea hana hawa wategemezi (unfortunate circumstance)..ila ktk jicho pana ni msaada wa kuweka wategemezi na kuondoa gharama za maisha.
 
Jaribu kutaka uelewa kwanza Mtanzania. Nafasi nne unaweza kuweka wazazi au watoto. Upo apo?


Wewe ni msemaji wa NHIF humu?

Kama siyo msemaji changia yako lakini usichangie kama msemaji ukapotosha watu.

Nikikwambia uweke ile copy yao ya wategemezi tuone Muundo wao utakuwanayo na kuweza kuiweka hapa?

Nazani kama wewe siyo msemaji wao usiwe jaji wa kuwahukunu wachangiaji wengine.
 
Kwanza tuwe waungwana kama misingi ya JamiiForums, moja ni kuheshimu nafasi za kazi/uteuzi au heshima tu kwa mtu - kutajana majina siyo jambo jema, tumia tu cheo - Mkurugenzi Mkuu, au "cheo-flani" inatosha kufikisha ujumbe..

Mbili, naona kama vile ume-divert ktk hoja ya vituo thread iliyoanzishwa na kuingia ktk specific issues - unrelated..

Okay, kujibu hoja yako ni hivi: ukipitia sheria ya NHIF ya 1999 na marekebisho yake 2002, 2005, 2009, 2010, 2015, inaongelea makato kwa mtumishi mwajiriwa. Yatosha ieleweke makato haya kisheria ndiyo msingi wa undugu wa kuchangiana matibabu. Ni kama ilivyo PAYE unakatwa lakini yawezekana nje ya nyumbani kwako barabara ni ya vumbi, yawezekana unataka lami; kupitia PAYE ya mwajiri na kodi nyinginezo mpaka za vinywaji/madukani ungetemea maji yakufikie ila labda bado - ila haimaanishi hiyo kodi haifanyi kazi, au haifikii wengine, au haitakufikia na wewe.

Vivyo hivyo, mchangiaji na mwenza wanakatwa kama sehemu ya kutimiza sheria, ila pia wanakatwa kama sehemu ya kutunisha Mfuko. Watanzania tunatakiwa tujifunze kuwa wazalendo, kuupenda Mfuko na kuona faida yake kwa jicho pana zaidi, na siyo kujiangalia kipekee (individualistic). Leo unaweza kuona unanyanyasika kukatwa wewe na mwenza; kesho akija ndugu yako kuomba laki 6 mfano kwa ajili ya matibabu ya mtoto wake, unampa Tsh. 50,400 na kumwambia akakate Toto Afya NHIF atapata matibabu yote - ila ngumu kumeza ni kusukumiza fikra nyuma ya ubongo hiyo difference inatoka kwa nani (600,000 - 50,400); kama siyo uzalendo wa uchangiaji? I can justify this point all over and over with different scenario ila kama jicho la kiuzalendo na undugu limefungwa ila lililo wazi ni individualistic we shall always be parting ways..

Yatosha ieleweke makato haya nayo ni akiba kwa lile usilolijua mbele:
i] Moja ya ukomo wa uchangiaji ni kifo, na hivyo huduma hukwama; sasa let us assume for a moment mwenza ulikuwa huchangii, unatengemea Bima ya mwenzako, alafu ikatokea akafariki - na wewe na watoto mkawa ktk immediate need ya medical service hapo hiyo taharuki unaiwekaje? Upande mmoja umetoka kuzika - na upande mmoja magonjwa/shida hazitatuliki bila pesa, kwa sababu huna Bima.

ii] Uchangiaji huu ni akiba ya credits kukusaidia upate fao la ustaafu; kwa macho ya kutoona mbele waweza sema hakuna msingi wa kuchangia uengemee kwa mume/mke; ila itakapotokea mwenza wako akapata ajali kazini/ulemavu akashindwa kufanya kazi; au akaachishwa au worse akafariki..piga picha miaka imeenda na credits umekosa za ustaafu, unajitengenezea ugumu wa maisha kwa sababu ambazo zingeepukika.

iii] Uchangiaji huu unakusaidia kuwaweka wategemezi: mwenza, watoto wako wa kuzaa, watoto wako wa kufikia, watoto wa kuasili (adopted children), wazazi, wakwe. Ni fursa pana ya kuwaweka hawa wategemezi. Wengi huingia ktk mkumbo wa kulalamika "mimi na mke tunakatwa" kwa kutokujua extent ya coverage aliyonayo. Mwingine anajua ila baada ya kuonja tunda la neema na akaitumia kuweka hawa wategemezi, anaona hakuna haja tena (unthankfulness & ignorance); na mwingine inatokea hana hawa wategemezi (unfortunate circumstance)..ila ktk jicho pana ni msaada wa kuweka wategemezi na kuondoa gharama za maisha.


Weeee nawe buana!

Wanatajwa majina ya wahemishimiwa Marais kwa majina yao, wakuu wa majeshi na vyombo vya usalama kwa vyoo na majina yao, IGPs n.k itakuwa huyo CEO wa NHIF?

Halafu wewe utakuwa ni ndiye Konga mwenyewe!

Asitajwe kwanini sasa wakati ni Mtumishi wa Umma ?

Yani ukubali kuteuliwa na kuwa Mtumishi wa Umma Tena sehema nyeti ya matibabu halafu hutaki ujulikane wala kutajwa jina ?

Chukua kile tunachikisema kifanyie kazi achana na hofu wala mashaka.

Wewe naanza kutilia shaka kiwango chako cha ufahamu?!

Tafakari.
 
Wewe ni msemaji wa NHIF humu?

Kama siyo msemaji changia yako lakini usichangie kama msemaji ukapotosha watu.

Nikikwambia uweke ile copy yao ya wategemezi tuone Muundo wao utakuwanayo na kuweza kuiweka hapa?

Nazani kama wewe siyo msemaji wao usiwe jaji wa kuwahukunu wachangiaji wengine.
Na wewe usiwe Jaji msaidizi
 
1.0 Maelezo ya awali
Kwa mujibu wa Mikataba kati ya NHIF na watoa huduma malipo yanapaswa kufanyika ndani ya siku 60 (miezi 2), ili kuongeza ufanisi Mfuko umejiwekea malengo ya kulipa ndani ya siku 30 pale tu madai (claims) yanapokuwa hayana shida. Changamoto zinazosababisha madai kuchelewa kulipwa ni pale dai likiwa na shida ikiwemo kuwa na viashiriana vya udanganyifu wenye lengo la kuuhujumu Mfuko na kutofuata miongizo ya tiba pamoja na masharti ya mkataba. Dai likikatwa ni pale Mfuko umejiridhisha bila shaka, ila kuna utaratibu wa makubaliano/mapatano (reconciliation) ambapo mtoa huduma na Mfuko hujadili maeneo mbalimbali na kufikia makubaliano rasmi.

Mlango wa reconciliation upo wazi – ila vituo vya afya haswa vile vya binafsi hukwepa kwa wingi wao (siyo wote) kukaa na Mfuko, yote ikiwa ni viashiria vya kutokubali makosa kwa makusudi au tabia endelevu ya kupika madai. Mfuko hupata ushirikiano sana kutoka vituo vya afya vya Serikali – na ni mfano wa kuigwa.

Kama sehemu ya kutolea hasira kwa vituo vingi vya binafsi ni kupitia mitandao ya jamii – taarifa za lawana ambazo ni za upande mmoja; na ambazo zimechujwa kujilinda wao. Hii siyo haki, kama unakuja mtandaoni elezea pande zote mbili, na weka wazi wajibu wa kituo, na kile kisichofanyika kuelekea kukatwa madai.

Kuhusu mikopo ya vituo vya afya; Mfuko unatoa mikopo ya ukarabati wa vituo (facility improvement loan); mikopo ya Tehama (ICT facility loan); mikopo ya vifaa tiba (medical equipment loan); na mikopo ya dawa (medicine and medical consumable loan); marejesho ya mikipo hii inafika hadi miaka 5 kwa kukatwa kidogo kidogo kutoka katika madai yao. Vituo vinakatwa asilimia ndogo, isiyozidi 40% ya madai husika. Mikopo imekuwa mkombozi kwa vituo vya afya katika kuboresha huduma. Hoja ya kuzorota huduma kwa sababu ya mikopo, ni hoja ambayo inahitaji maelezo zaidi, shida ni nini. Ni sawa na kuilaumu benki marejesho ya mkopo wa biashara, wakati uliomba mwenyewe kupanua biashara/mtaji; sasa uovu upo wapi?

2.0 Ukataji madai na Wajibu wa Watoa Huduma

2.1 CAG Report

Turejee muhtasari wa ripoti za mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za Serikali kwa mwaka wa fedha 2019/20 ulioishia tarehe 30/06 iliyowasilishwa tarehe 8/04/2021; *pitia kurasa 56; Hasara itokatokanayo na kukataliwa kwa madai ya fedha za Bima ya Afya Kiasi cha Sh. bilioni 4.46 “Tathmini niliyofanya katika zahanati, vituo vya afya, na hospitali katika Mamlaka 60 za Serikali za Mitaa nilibaini uwepo wa madai yaliyokataliwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ikiwa ni gharama za matibabu kwa wagonjwa wanaotumia huduma za bima ya kiasi cha Sh. bilioni 2.28 na sh.bilioni 2.18 kwa Hospitali za Rufaa 26 kutokana na makosa katika ujazaji wa taarifa za wagonjwa pamoja na kutozingatia taratibu kama vile idhini batili, kutozingatia miongozo ya matibabu, kutoonesha vipimo vya utambuzi, na kuingizwa kwa huduma ambazo hazikuwa katika Mfuko. Madai yaliyokataliwa yanaathiri uwezo wa zahanati, vituo vya afya na hospitali katika kutoa huduma za afya kwa jamii kwani hii ni sawa na kutoa huduma za matibabu bure.”

Kadiri unavyosoma ripoti zaidi utagundua Halmashauri ambazo zinasimamia vituo mbalimbali vya afya kwa kutokuwa makini kutunza pesa, au ufujaji zimeshindwa kuhudumia huduma za msingi za jamii kiufanisi ikiwemo manunuzi ya dawa, vifaa tiba n.k; ukweli huu upo pia katika kurasa:

*pitia kurasa 42, matokeo ya ukaguzi wa mamlaka za serikali za mitaa, mapato ya shs. Bilioni 18.769 yalikusanywa lakini hayakupelekwa benki.

*pitia kurasa 44, matokeo ya ukaguzi wa mamlaka za serikali za mitaa, mapato ambayo hayajakusanywa kutoka kwenye vyanzo mbalimbali shs. Bilioni 30.86.

*pitia kurasa 47, matokeo ya ukaguzi wa mamlaka za serikali za mitaa, fedha za mapato ya ndani bilioni 33.96 hazikupelekwa kwenye miradi ya maendeleo

*pitia kurasa 60, Halmashauri ya Manispaa ya Buboka: kutopokelewa kwa vifaatiba kutoka Bohari ya Dawa (MSD) vyenye thamani ya shs. Bilioni 1.08

*pitia kurasa 64, Halmashauri ya jiji la DSM: kutokamilika ujenzi wa zahanati katika kata ya kipunguni kutokana na upotevu wa fedha Sh. 74,093,000

*pitia kurasa 70, Halmashauri ya jiji la Tanga: Vifaatiba Vilivyolipiwa Lakini Havijafikishwa Kituo cha Afya Duga Sh. 175,679,500

Hivyo basi hoja ya Mfuko kutolipa vituo na kusababisha kudhorota kwa huduma haina mashiko. Vituo binafsi ukweli unaweza usiwe mbali pia, tabia za mwanadamu zinafanana, yaweza kuna changamoto za ukaribu kama vituo vya serikali – ukweli ni ngumu kuupata maana CAG hapiti huko!

2.2 Makato ya Vituo
Makato mengi ni kwa sababu ya kutofuata miongozo ya matibabu iliyotolewa na Wizara ya Afya; mf. Muongozo wa STG, muongozo wa magonjwa ya uzazi, muongo wa malaria, etc..

Sababu kubwa nyingine ni kutofuata mkataba wa utoaji huduma (service provision agreement), ambapo ndani yake kuna price list. Yote haya ni kutokujua, kutokuwepo na wafanyakazi walio serious/competent, pia udanganyifu katika madai – uchomekaji wa madai hewa, kupika madai, n.k. Saa nyingine kituo kinaajiri wafanyakazi wapya, orientation hawapati ya kutosha, elimu duni juu ya kushughulikia madai na miongozo ya Wizara, hivyo hujaza sivyo ndivyo madai!

Watoa huduma wana wajibu wa kumuhakiki mwanachama (member verification) kupitia portal ya Mfuko na kutoa authorization number – kinyume na hapo wanaweza kutibu mwanachama asiye hai, hivyo dai hukataliwa iwapo halijafuata utaratibu huu. Watoa huduma wana wajibu wa kuingiza taarifa vizuri katika fomu za madai na katika eClaims system; na hapo inategemewa physical folio na electronic folio zisipishane. Kuna masuala mengine kama signature, attendance date, stamp ya kituo, disease code na namba ya kadi ni muhimu zionekane katika fomu ya madai. Baadhi ya hoja kusema hivi ni vitu vidogo ila kama vinavyoonekana kutofuatwa ni mwanzo wa mwanya wa madai ya kupikwa au udanganyifu; sawa sawa na bank-teller au supervisor aandike cheque alafu afute kwa mkato asahau kusaini (ni jambo dogo ndio ila haitakiwi); au ushawahi ona mhasibu anatumia correction fluid ktk risiti zake? (ni jambo dogo ila hairuhusiwi) – hivyo Mfuko huchukulia kila eneo serious kwa lengo la kulinda uhai na uendelevu wake. La sivyo Mfuko ukifirisika hapa hapa mtaanza kuandika na kuwalaumu Mfuko kuwa walikuwa wapi mpk Mfuko unafirisika!! Ila kama awali nilivyoelezea Mfuko una nafasi ya kukaa na vituo kwa ajili ya mapatano/reconciliation – itumiwe hiyo na huo ndio uungwana, kukaa na kutafuta suluhu ya

1.0 Maelezo ya awali
Kwa mujibu wa Mikataba kati ya NHIF na watoa huduma malipo yanapaswa kufanyika ndani ya siku 60 (miezi 2), ili kuongeza ufanisi Mfuko umejiwekea malengo ya kulipa ndani ya siku 30 pale tu madai (claims) yanapokuwa hayana shida. Changamoto zinazosababisha madai kuchelewa kulipwa ni pale dai likiwa na shida ikiwemo kuwa na viashiriana vya udanganyifu wenye lengo la kuuhujumu Mfuko na kutofuata miongizo ya tiba pamoja na masharti ya mkataba. Dai likikatwa ni pale Mfuko umejiridhisha bila shaka, ila kuna utaratibu wa makubaliano/mapatano (reconciliation) ambapo mtoa huduma na Mfuko hujadili maeneo mbalimbali na kufikia makubaliano rasmi.

Mlango wa reconciliation upo wazi – ila vituo vya afya haswa vile vya binafsi hukwepa kwa wingi wao (siyo wote) kukaa na Mfuko, yote ikiwa ni viashiria vya kutokubali makosa kwa makusudi au tabia endelevu ya kupika madai. Mfuko hupata ushirikiano sana kutoka vituo vya afya vya Serikali – na ni mfano wa kuigwa.

Kama sehemu ya kutolea hasira kwa vituo vingi vya binafsi ni kupitia mitandao ya jamii – taarifa za lawana ambazo ni za upande mmoja; na ambazo zimechujwa kujilinda wao. Hii siyo haki, kama unakuja mtandaoni elezea pande zote mbili, na weka wazi wajibu wa kituo, na kile kisichofanyika kuelekea kukatwa madai.

Kuhusu mikopo ya vituo vya afya; Mfuko unatoa mikopo ya ukarabati wa vituo (facility improvement loan); mikopo ya Tehama (ICT facility loan); mikopo ya vifaa tiba (medical equipment loan); na mikopo ya dawa (medicine and medical consumable loan); marejesho ya mikipo hii inafika hadi miaka 5 kwa kukatwa kidogo kidogo kutoka katika madai yao. Vituo vinakatwa asilimia ndogo, isiyozidi 40% ya madai husika. Mikopo imekuwa mkombozi kwa vituo vya afya katika kuboresha huduma. Hoja ya kuzorota huduma kwa sababu ya mikopo, ni hoja ambayo inahitaji maelezo zaidi, shida ni nini. Ni sawa na kuilaumu benki marejesho ya mkopo wa biashara, wakati uliomba mwenyewe kupanua biashara/mtaji; sasa uovu upo wapi?

2.0 Ukataji madai na Wajibu wa Watoa Huduma

2.1 CAG Report

Turejee muhtasari wa ripoti za mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za Serikali kwa mwaka wa fedha 2019/20 ulioishia tarehe 30/06 iliyowasilishwa tarehe 8/04/2021; *pitia kurasa 56; Hasara itokatokanayo na kukataliwa kwa madai ya fedha za Bima ya Afya Kiasi cha Sh. bilioni 4.46 “Tathmini niliyofanya katika zahanati, vituo vya afya, na hospitali katika Mamlaka 60 za Serikali za Mitaa nilibaini uwepo wa madai yaliyokataliwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ikiwa ni gharama za matibabu kwa wagonjwa wanaotumia huduma za bima ya kiasi cha Sh. bilioni 2.28 na sh.bilioni 2.18 kwa Hospitali za Rufaa 26 kutokana na makosa katika ujazaji wa taarifa za wagonjwa pamoja na kutozingatia taratibu kama vile idhini batili, kutozingatia miongozo ya matibabu, kutoonesha vipimo vya utambuzi, na kuingizwa kwa huduma ambazo hazikuwa katika Mfuko. Madai yaliyokataliwa yanaathiri uwezo wa zahanati, vituo vya afya na hospitali katika kutoa huduma za afya kwa jamii kwani hii ni sawa na kutoa huduma za matibabu bure.”

Kadiri unavyosoma ripoti zaidi utagundua Halmashauri ambazo zinasimamia vituo mbalimbali vya afya kwa kutokuwa makini kutunza pesa, au ufujaji zimeshindwa kuhudumia huduma za msingi za jamii kiufanisi ikiwemo manunuzi ya dawa, vifaa tiba n.k; ukweli huu upo pia katika kurasa:

*pitia kurasa 42, matokeo ya ukaguzi wa mamlaka za serikali za mitaa, mapato ya shs. Bilioni 18.769 yalikusanywa lakini hayakupelekwa benki.

*pitia kurasa 44, matokeo ya ukaguzi wa mamlaka za serikali za mitaa, mapato ambayo hayajakusanywa kutoka kwenye vyanzo mbalimbali shs. Bilioni 30.86.

*pitia kurasa 47, matokeo ya ukaguzi wa mamlaka za serikali za mitaa, fedha za mapato ya ndani bilioni 33.96 hazikupelekwa kwenye miradi ya maendeleo

*pitia kurasa 60, Halmashauri ya Manispaa ya Buboka: kutopokelewa kwa vifaatiba kutoka Bohari ya Dawa (MSD) vyenye thamani ya shs. Bilioni 1.08

*pitia kurasa 64, Halmashauri ya jiji la DSM: kutokamilika ujenzi wa zahanati katika kata ya kipunguni kutokana na upotevu wa fedha Sh. 74,093,000

*pitia kurasa 70, Halmashauri ya jiji la Tanga: Vifaatiba Vilivyolipiwa Lakini Havijafikishwa Kituo cha Afya Duga Sh. 175,679,500

Hivyo basi hoja ya Mfuko kutolipa vituo na kusababisha kudhorota kwa huduma haina mashiko. Vituo binafsi ukweli unaweza usiwe mbali pia, tabia za mwanadamu zinafanana, yaweza kuna changamoto za ukaribu kama vituo vya serikali – ukweli ni ngumu kuupata maana CAG hapiti huko!

2.2 Makato ya Vituo
Makato mengi ni kwa sababu ya kutofuata miongozo ya matibabu iliyotolewa na Wizara ya Afya; mf. Muongozo wa STG, muongozo wa magonjwa ya uzazi, muongo wa malaria, etc..

Sababu kubwa nyingine ni kutofuata mkataba wa utoaji huduma (service provision agreement), ambapo ndani yake kuna price list. Yote haya ni kutokujua, kutokuwepo na wafanyakazi walio serious/competent, pia udanganyifu katika madai – uchomekaji wa madai hewa, kupika madai, n.k. Saa nyingine kituo kinaajiri wafanyakazi wapya, orientation hawapati ya kutosha, elimu duni juu ya kushughulikia madai na miongozo ya Wizara, hivyo hujaza sivyo ndivyo madai!

Watoa huduma wana wajibu wa kumuhakiki mwanachama (member verification) kupitia portal ya Mfuko na kutoa authorization number – kinyume na hapo wanaweza kutibu mwanachama asiye hai, hivyo dai hukataliwa iwapo halijafuata utaratibu huu. Watoa huduma wana wajibu wa kuingiza taarifa vizuri katika fomu za madai na katika eClaims system; na hapo inategemewa physical folio na electronic folio zisipishane. Kuna masuala mengine kama signature, attendance date, stamp ya kituo, disease code na namba ya kadi ni muhimu zionekane katika fomu ya madai. Baadhi ya hoja kusema hivi ni vitu vidogo ila kama vinavyoonekana kutofuatwa ni mwanzo wa mwanya wa madai ya kupikwa au udanganyifu; sawa sawa na bank-teller au supervisor aandike cheque alafu afute kwa mkato asahau kusaini (ni jambo dogo ndio ila haitakiwi); au ushawahi ona mhasibu anatumia correction fluid ktk risiti zake? (ni jambo dogo ila hairuhusiwi) – hivyo Mfuko huchukulia kila eneo serious kwa lengo la kulinda uhai na uendelevu wake. La sivyo Mfuko ukifirisika hapa hapa mtaanza kuandika na kuwalaumu Mfuko kuwa walikuwa wapi mpk Mfuko unafirisika!! Ila kama awali nilivyoelezea Mfuko una nafasi ya kukaa na vituo kwa ajili ya mapatano/reconciliation – itumiwe hiyo na huo ndio uungwana, kukaa na kutafuta suluhu ya pamoja.
Usiweke fact za uongo hapa hospitali zote kuanzia vituo vya afya mpaka National hospital wanadai malipo yao zaidi ya miez 5 ,Mwisho mlilipa Mwaka jana November Mpaka leo hospitali zinajiendesha kihasara, Wagonjwa wanapata shida vifaa tiba vinapohitajika inafika sehemu Mgonjwa anaambia akanunue gloves, crep bandage, p.o.p hospitali hazina kitu harafu mnatwambia mkataba miez miwili wapi hiyo
Hii Bodi ni bora ifumuliwe tu....
Ovyo kabisa Dawa zingine Mara zinatolewa
 
S
No research, No right to speak!
Kasome muhtasari wa ripoti za mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za Serikali kwa mwaka wa fedha 2019/20 ulioishia tarehe 30/06 iliyowasilishwa tarehe 8/04/2021; *pitia kurasa 56; Hasara itokatokanayo na kukataliwa kwa madai ya fedha za Bima ya Afya Kiasi cha Sh. bilioni 4.46 “Tathmini niliyofanya katika zahanati, vituo vya afya, na hospitali katika Mamlaka 60 za Serikali za Mitaa nilibaini uwepo wa madai yaliyokataliwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ikiwa ni gharama za matibabu kwa wagonjwa wanaotumia huduma za bima ya kiasi cha Sh. bilioni 2.28 na sh.bilioni 2.18 kwa Hospitali za Rufaa 26 kutokana na makosa katika ujazaji wa taarifa za wagonjwa pamoja na kutozingatia taratibu kama vile idhini batili, kutozingatia miongozo ya matibabu, kutoonesha vipimo vya utambuzi, na kuingizwa kwa huduma ambazo hazikuwa katika Mfuko. Madai yaliyokataliwa yanaathiri uwezo wa zahanati, vituo vya afya na hospitali katika kutoa huduma za afya kwa jamii kwani hii ni sawa na kutoa huduma za matibabu bure.”

Halmashauri ambazo zinasimamia vituo mbalimbali vya afya kwa kutokuwa makini kutunza pesa, au ufujaji zimeshindwa kuhudumia huduma za msingi za jamii kiufanisi ikiwemo manunuzi ya dawa, vifaa tiba n.k; ukweli huu upo pia katika kurasa:
*kurasa 42, matokeo ya ukaguzi wa mamlaka za serikali za mitaa, mapato ya shs. Bilioni 18.769 yalikusanywa lakini hayakupelekwa benki.
*kurasa 44, matokeo ya ukaguzi wa mamlaka za serikali za mitaa, mapato ambayo hayajakusanywa kutoka kwenye vyanzo mbalimbali shs. Bilioni 30.86.
*kurasa 47, matokeo ya ukaguzi wa mamlaka za serikali za mitaa, fedha za mapato ya ndani bilioni 33.96 hazikupelekwa kwenye miradi ya maendeleo
*kurasa 60, Halmashauri ya Manispaa ya Buboka: kutopokelewa kwa vifaatiba kutoka Bohari ya Dawa (MSD) vyenye thamani ya shs. Bilioni 1.08
*kurasa 64, Halmashauri ya jiji la DSM: kutokamilika ujenzi wa zahanati katika kata ya kipunguni kutokana na upotevu wa fedha Sh. 74,093,000
*kurasa 70, Halmashauri ya jiji la Tanga: Vifaatiba Vilivyolipiwa Lakini Havijafikishwa Kituo cha Afya Duga Sh. 175,679,500

Hoja ya Mfuko kutolipa vituo na kusababisha kudhorota kwa huduma haina mashiko. Vituo binafsi navyo vina shida ya kiutendaji sehemu moja au nyingine, ni basi tu utendaji wake hauanikwi kama ilivyo upande wa vituo vya serikalini - ama sivyo tungesikia changamoto zake kama CAG angekuwa anapita!

Makato ya Vituo
Makato mengi ni kwa sababu ya kutofuata miongozo ya matibabu iliyotolewa na Wizara ya Afya; mf. Muongozo wa STG, muongozo wa magonjwa ya uzazi, muongo wa malaria, etc..

Sababu kubwa nyingine ni kutofuata mkataba wa utoaji huduma (service provision agreement), ambapo ndani yake kuna price list. Yote haya ni kutokujua, kutokuwepo na wafanyakazi walio serious/competent, pia udanganyifu katika madai – uchomekaji wa madai hewa, kupika madai, n.k. Saa nyingine kituo kinaajiri wafanyakazi wapya, orientation hawapati ya kutosha, elimu duni juu ya kushughulikia madai na miongozo ya Wizara, hivyo hujaza sivyo ndivyo madai!

Watoa huduma wana wajibu wa kumuhakiki mwanachama (member verification) kupitia portal ya Mfuko na kutoa authorization number – kinyume na hapo wanaweza kutibu mwanachama asiye hai, hivyo dai hukataliwa iwapo halijafuata utaratibu huu. Watoa huduma wana wajibu wa kuingiza taarifa vizuri katika fomu za madai na katika eClaims system; na hapo inategemewa physical folio na electronic folio zisipishane. Kuna masuala mengine kama signature, attendance date, stamp ya kituo, disease code na namba ya kadi ni muhimu zionekane katika fomu ya madai. Baadhi ya hoja kusema hivi ni vitu vidogo ila kama vinavyoonekana kutofuatwa ni mwanzo wa mwanya wa madai ya kupikwa au udanganyifu; sawa sawa na bank-teller au supervisor aandike cheque alafu afute kwa mkato asahau kusaini (ni jambo dogo ndio ila haitakiwi); au ushawahi ona mhasibu anatumia correction fluid ktk risiti zake? (ni jambo dogo ila hairuhusiwi) – hivyo Mfuko huchukulia kila eneo serious kwa lengo la kulinda uhai na uendelevu wake. La sivyo Mfuko ukifirisika hapa hapa mtaanza kuandika na kuwalaumu Mfuko kuwa walikuwa wapi mpk Mfuko unafirisika!! Ila kama awali nilivyoelezea Mfuko una nafasi ya kukaa na vituo kwa ajili ya mapatano/reconciliation – itumiwe hiyo na huo ndio uungwana, kukaa na kutafuta suluhu ya pamoja.
Shida zenu Mnajibu kwa kutumia Makaratasi mkiwa ofisini mnakunywa kahawa ndio maana hii nchi inawatu wa ovyo sijawahi pata kuona, Sisi tunaowaeleza ukweli tunaojionea tunapokwenda kutibiwa mahospitalini na kuona hali halisi
Nyinyi mnajiona mnaelewa sana kumbe ni uelewa fake
Nendeni field mkajionee hali halisi
Vile vile tuambie mwisho kulipa madai ya hospitali ni lini
 
Usiweke fact za uongo hapa hospitali zote kuanzia vituo vya afya mpaka National hospital wanadai malipo yao zaidi ya miez 5 ,Mwisho mlilipa Mwaka jana November Mpaka leo hospitali zinajiendesha kihasara, Wagonjwa wanapata shida vifaa tiba vinapohitajika inafika sehemu Mgonjwa anaambia akanunue gloves, crep bandage, p.o.p hospitali hazina kitu harafu mnatwambia mkataba miez miwili wapi hiyo
Hii Bodi ni bora ifumuliwe tu....
Ovyo kabisa Dawa zingine Mara zinatolewa
Uongo wako Konki aisee ... safi kabisa ...
 
Hapa anahitajika adjudicator. Huyu awe independent. Ni go between ya huduma hasa hawa NHIF na hizi private. Aweze hata kutoza penalty kwa NHIF au facilities danganyifu. Ikiwepo penalty ya kuchelewa kulipa vituo au hospital.
 
Huu uzi umeleta wageni wengi watetezi.
Kawatuma Boss wao lakini ukweli ni kwamba tunakoelekea hili shirika bila mipango mikakati madhubuti litaua huduma za afya kwa kasi ya hatari
Ikumbukwe kwa sasa wananchi wengi wanajiunga na Bima
Itafika Mahala wagonjwa wa cash watapungua
Bima wanachelewesha malipo, Je Hospitali zitajiendeshaje?
 
Serikali itoe tamka kwenye hili swala ni aibu kuwa na mfuko wenye matatizo makubwa namna hii wao viongozi wako kimya
 
Back
Top Bottom