Mvutano wa NHIF na watoa huduma za afya ni kaburi la afya za Watanzania wengi

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Nov 28, 2013
10,129
35,153
Hizi heka heka za mivutano baina ya serikali kupitia NHIF na watoa huduma za afya wa vituo binafsi sio jambo lenye kheri, mwisho wake utakuwa mbaya sana.

Haijarishi nani ataibuka mshindi lakini mwisho wa siku afya za watanzania zinakwenda kupuputika vibaya.

Ni kweli NHIF inazilipa fedha nyingi taasisi binafsi za afya (hivyo huendeshaji wa hizo taasisi kwa zaidi ya 50% huenda unategemea pesa kutoka NHIF) lakini ukitazama malipo ya kitita kipya cha mafao cha NHIF umejaa kasoro kubwa zenye kuzinyonya kiasi cha kuelekea kuziua kabisa taasisi binafsi. Haijarishi taasisi binafsi zitaamua kuchukua mkondo gani (kugoma au kuendelea kutoa huduma), mwelekeo wa kufa utabakia pale pale. Na ili ziendelee kuwepo na huku zikiendelea kutoa huduma, ni lazima zijipange kutoa huduma duni sana kwa wagonjwa, na huo ndio msiba wa watanzania wengi ulipo.

Hekima ilikuwa ni kukaa mezani ili kufikia muafaka.
 
Wanashindwa kufahamu kwamba,UONGOZI BORA hupimwa kwenye nyakati NGUMU..Ummy maliza hili suala,wananchi WANATESEKA
 
Hizi heka heka za mivutano baina ya serikali kupitia NHIF na watoa huduma za afya wa vituo binafsi sio jambo lenye kheri, mwisho wake utakuwa mbaya sana.

Haijarishi nani ataibuka mshindi lakini mwisho wa siku afya za watanzania zinakwenda kupuputika vibaya.

Ni kweli NHIF inazilipa fedha nyingi taasisi binafsi za afya (hivyo huendeshaji wa hizo taasisi kwa zaidi ya 50% huenda unategemea pesa kutoka NHIF) lakini ukitazama malipo ya kitita kipya cha mafao cha NHIF umejaa kasoro kubwa zenye kuzinyonya kiasi cha kuelekea kuziua kabisa taasisi binafsi. Haijarishi taasisi binafsi zitaamua kuchukua mkondo gani (kugoma au kuendelea kutoa huduma), mwelekeo wa kufa utabakia pale pale. Na ili ziendelee kuwepo na huku zikiendelea kutoa huduma, ni lazima zijipange kutoa huduma duni sana kwa wagonjwa, na huo ndio msiba wa watanzania wengi ulipo.

Hekima ilikuwa ni kukaa mezani ili kufikia muafaka.
Hakika wanatengeneza shida kwa Wananchi, Tutunzeni afya zetu.
 
Back
Top Bottom