Mwakyembe apanda treni kwenda Bungeni Dodoma

Mwakyembe apanda treni kwenda Bungeni Dodoma

Mimi nakataa unafiki na sifa za kijinga. Huyu jamaa aache maigizo. Siku zote anakwenda kwao Mbeya,huwa anatumia treni za TAZARA?
kweli tunastahili umaskini tulio nao. kama tunamponda mwakyembe kwa kupanda treni hii ni hatari
 
kupanda tren sio hoja
labda atuambie ana mpango gani wa kununua mabehewa mapya,tren mpya na reli iboreshwe
sii hivo tu nini shuluhisho la usugu wa usafiri ktk miji mikubwa
na tuone kama waziri wa uchukuzi anakuwa mfano wa kukataa shangingi
na pia awe mfano wa kubana matumizi ya serikali
kwa kuuza magari ya kifahari na kununua ya bei nafuu kwa mawaziri na viongozi.
naona hapa ni changa la mcho. TUTAONA VITUKO VINGI SANA VYA MAWAZIRI HADI OCTOBER 2015
 
Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Kwa hili Mwakyembe anastahili sifa kwa sababu hii itamsaidia kujua adha na matatizo yanayoikumba sector ya reli moja kwa moja.
 
Hakuna tofauti na ziara za Jakaya Kwenye ofisi za wizara. Matatizo ya hizo treni yako kwenye ofisi huku makao makuu, muache atafute cheap popularity, atapoteza vyote viwili, mtoto na mbeleko.

Umenishangaza. Cheap popularity? Ninamfahamu Mwaakyembe, personally, lakini sio sana. Ilitosha kukutana naye MARA MOJA TU ili kumwelewa. Ni msikivu, anasikiliza ushauri wa watu, hata kama hakufahamu. Jaribu kumtafuta, uone atakujibu nini. Unadhani kulishwa sumu ni mchezo?

Cheap popularity indeed! Yaani kiongozi anawajibika ipasavyo kusimamia RASILMALI ZETU, we unamwona anatafuta umaarufu? Hao wanaokwiba hizo RASILMALI kwako sio shida?

Duh! Kaka AIBU!
 
Mimi nakataa unafiki na sifa za kijinga. Huyu jamaa aache maigizo. Siku zote anakwenda kwao Mbeya,huwa anatumia treni za TAZARA?

Amepanda treni kwenda Dodoma KIKAZI. Anasimamia Wizara yake. Kuhusu TAZARA, alikwenda kukesha na abiria mpaka treni ilipoondoka. Amesema ataifumua TAZARA, uozo wote nje.

UNATAKA AFANYE NINI ZAIDI?
 
hahahahhaa,,,,nadhan si kwa mawaziri tu,hata

Nadhani nchi hii imekumbwa na tatizo lingine kubwa la watu wake kutojua na kuweka umhimu wa mda.

Najua watu watasema ni njia ya kujiridhisha kwa kuangalia miradi iliyo chini ya wizara, lakini je matatizo ya TRL yamemalizika ya kimikataba ambayo was a serious issue?

Navyojua mimi safari ya treni hadi Dodoma ni zaidi ha masaa 14, mda huu unatosha kwa waziri kuwa amefanya kazi nyingi sana na kuwa amefanya maamuzi mengi sana ofisini tena yenye tija zaidi kuliko hili la kusafiri na teni.

Kama Waziri anaweza kufanya kazi ya kuhesabu madaraja kwenye njia ya treni je watendaji wako wapi? Au ndo kutowaamini na kufikiri wanawapinga/wahujumu mawaziri ili washindwe kufanya kazi zao za kiwaziri na waondolewe ili waje maswahiba zao?

Mtizamo wangu mimi katika hili simuungi mkono waziri Mwakyembe na kutumia usafiri wa treni hadi Dom kwa sababu moja nimesema kuhusu matumizi mabaya ya mda, pili risk kama ambavyo baadhi wamesema kuharibika kwa treni porini hivyo kuhitaji rescue, tatu hujuma ambazo zinaweza kufanyika juu yake ukizingatia yaliyomtokea huko nyuma.

Mhe Mwakyembe has emerged to be a popularist minister who uses whatever it is as a political platform, I guess he has a hidden agenda, watu kama hawa hawafai kabisa katika uongozi ambao wananchi maskini wanawategemea, mwisho wa siku akipata uongozi mkubwa nchi anaweza kuwa kama JK kama alivyoanza na anakoishia uongozi wake ambsko ni kubaya by losing popularity.
 
Sawa. Lakini tusijesikia ananalamika mara ooh ugonjwa wangu umerudi baada ya kuvuta hewa yenye sumu, sijui ugoro wa kigogo kule kwenye treni, au behewa haikuwa na hewa ya kutosha, mara nipelekeni India. Hatuna pesa ya mchezo kwa haya mambo ya kisanii.
 
Mzizi wa Mbuyu kumbuka pia kwamba Naibu waziri ana limitations zake; anapangiwa kazi na waziri wake. Sijui kama kuna suala la kuogopana hapa nadhani ni suala tu la kuheshimu mipaka ya kazi yako.
 
Last edited by a moderator:
ili ukubalike na walalahoi lazima ufanye anachofanya mwakiembe
 
Ni kweli huyu jamaa alikuwa chini ya Magufuri, na hakuweza kupanda treni hiyo haimanishi kuwa yeye ni mwoga bali hakutaka kuingilia kazi wizara nyingine. Kumbuka kuwa wao walikua ujenzi.

..............................


Baba,

Naona hujaelewa!

Nasema kule kwa Magufuli kulikuwa/kuna uozo mwingi tu...

kama vile barabara kujengwa kwa gharama kubwa kuliko nchi yoyote ile Afrika Mashariki....

kitu ambacho alikiri yeye mwenyewe!

Sasa kwanini alikuwa hachukui hatua za kudhibiti uozo wa aina ile kule kwa spidi hii??

Kama bda hujaelewa, ntakulipia uende darasani.


au vipi?
 
Umenishangaza. Cheap popularity? Ninamfahamu Mwaakyembe, personally, lakini sio sana. Ilitosha kukutana naye MARA MOJA TU ili kumwelewa. Ni msikivu, anasikiliza ushauri wa watu, hata kama hakufahamu. Jaribu kumtafuta, uone atakujibu nini. Unadhani kulishwa sumu ni mchezo?

Cheap popularity indeed! Yaani kiongozi anawajibika ipasavyo kusimamia RASILMALI ZETU, we unamwona anatafuta umaarufu? Hao wanaokwiba hizo RASILMALI kwako sio shida?

Duh! Kaka AIBU!

Msimamo wangu uko pale pale, huyu Jamaa ni Mmoja kati ya wanasiasa waongo katika Taifa hili, ni mmoja kati ya wanasiasa wanaotafuta sifa zisizo na msingi wowote ule, na katika hili anatafuta cheap popularity.

Mpaka sasa kitu pekee nachojua anaweza kukifanya kwa ufanisi mkubwa ni kutengeneza uongo na kuchafua watu wengine, Mpaka siku atakapoliambia Taifa ni mambo gani kamati yake ya Richmond iliyaficha kwenye report yake ndio naweza nikaanza kumsikiliza.

Mtu yeyote makini ni lazima ajiulize, kwa nini CCM inashindwa kumfukuza Lowasa with all the damage kamati ya mwakyembe ilimfanyia ni lazima aquestion credibility ya huyu jamaa.
 
According to Clouds FM,
Dr Harrison Mwakyembe amefanya supprise visit na kusafiri kwa treni kutoka Dar kuelekea Dodoma kuhudhuria kikao cha bunge. Mud si mrefu tutafahamu alichokusudia kufanya hiyo suprise.

Inabidi na Waziri wa Nishati na madini akalale kwenye nyumba ambayo haina umeme ajue jinsi ambavyo Tanesco inasumbua wateja wake kuwaunganishia umeme, na pia waziri wa kilimo anende KANTALAMBA akalime. Kwa simple analysis sidhani kama Mwakyembe angehitaji kufanya hivyo pamoja na kwamba inaweza kumjenga kisiasa kwani matatizo ya reli na treni hayahitaji upande uende Dodoma.
 
Msimamo wangu uko pale pale, huyu Jamaa ni Mmoja kati ya wanasiasa waongo katika Taifa hili, ni mmoja kati ya wanasiasa wanaotafuta sifa zisizo na msingi wowote ule, na katika hili anatafuta cheap popularity.

Mpaka sasa kitu pekee nachojua anaweza kukifanya kwa ufanisi mkubwa ni kutengeneza uongo na kuchafua watu wengine, Mpaka siku atakapoliambia Taifa ni mambo gani kamati yake ya Richmond iliyaficha kwenye report yake ndio naweza nikaanza kumsikiliza.

Mtu yeyote makini ni lazima ajiulize, kwa nini CCM inashindwa kumfukuza Lowasa with all the damage kamati ya mwakyembe ilimfanyia ni lazima aquestion credibility ya huyu jamaa.

Akishakuambia hicho unachodai alificha katika ripoti ya Richmond utafanya nini wewe kajamba nani? Mnapiga kelele tu wakati hamna uwezo wa kubadilisha chochote hata kama mngeambiwa the so called ukweli!! Suppose wewe ndio ungekuwa kwenye hiyo kamati ungesema?? au kazi kupiga kelele zisizo na maana. Mlipoambiwa ya Mzee wa vijisenti mlichukua hatua gani?? mbona mmeishia kuimba nyimbo zisizo na kiitikio?? Fikiri kabla ya kuongea siyo unaropoka ovyo tu kama mtu anayeharisha chooni.
 
Hapa ni uraisi unatafutwa hakuna kingine, wanao mfahamu mwakyembe hawashangai ila waio mjua watashangaa sana, HUYU JAMAA NI ZAIDI YA SITA KATIA KUTAFUTA SIFA,

Tatizo si kupanda tren kwa sababu hata Yule Raisi wa Korea kaskazini mpaka mautu yanamkuta alikuwa kwenye tren ya nch yake,


E KUPAJNDA KUTAFUFUA TREN? JE KUTAFUFUA RELI YA TANGA ARUSHA?



...Good Questions Comrade, So why not give the Guy the benefit of doubt and see what comes after his 'Train Tour'....???
 
Back
Top Bottom