Mwakyembe apanda treni kwenda Bungeni Dodoma

Mwakyembe apanda treni kwenda Bungeni Dodoma

kweli tunastahili umaskini tulio nao. kama tunamponda mwakyembe kwa kupanda treni hii ni hatari

Mimi binafsi jana jioni niliona ITV, nilimpongeza kwa kitendo cha kijasiri.

Mtu akifanya jambo jema inabidi tumpe pongezi na siyo kumlaumu na kuweka itikadi mbele. Tunachohitaji ni mabadiliko tu.

HONGERA MWAKYEMBE TUNAOMBA na WENGINE WAFUATE MFANO HUU.

Mfano:

(1) Waziri wa Afya na familiya yake wakatibiwe Mwananyamala Hospital na wapange foleni kama wagonjwa wengine pasipo kupendelewa kwa chochote.
(2) Waziri wa Elimu watoto wake awahamishie shule za msingi za serikali na sekondari za Kata.
(3) Waziri wa Kilimo na Chakula akanunue chakula Tandale na soko la Mwananyamala, Kinondoni Hananasifu ili ajue mfumuko wa bei.
(4) Waziri Magufuli ahamie Kigamboni iliapande Pantoni kwenda Kigamboni na kurudi ili ajue uchungu wa kupandisha nauli.

Nk. Nk. Nk. Kila Waziri na kiongozi kwa nafasi yake.



MIZAMBWA
NABII MTARAJIWA!!!
 
Sion cha ajabu lamda angapanda tingatinga

labda ninafsi ningependa kufahamishwa kuwa ni Waziri yupi mwingine aliyewahi kupanda Treni???? kwa safari za kikazi.


MIZAMBWA
NABII MTARAJIWA!!!
 
According to Clouds FM,
Dr Harrison Mwakyembe amefanya supprise visit na kusafiri kwa treni kutoka Dar kuelekea Dodoma kuhudhuria kikao cha bunge. Mud si mrefu tutafahamu alichokusudia kufanya hiyo suprise.

Bado Raisi Kikwete na yeye atafanya Surprise kwa kupanda Daladala muda wa jioni kuotka POSTA MPYA hadi MWENGE, kisha atapanda Daladala la kwenda TEGETA, akifika Tegeta atapanda daladala la kwenda BUNJU, akifika Bunju atapanda la kwenda BAGAMOYO.

Na kesho yake asubuhi atarudi kwa madaladala tena kuja ofisini Magogoni.

Lengo ajionee jinsi usafiri wa jioni na asubuhi ulivyo pamoja na gharama anayotumia mfanyakazi kila siku kisha atafanya TAFAKARI YA KUBORESHA HUDUMA ZA USAFIRI NA KUONGEZA MISHAHARA WAFANYAKAZI.


BILA SHAKA NA KIKWETE NAYE ATAFANYA UAMUZI wa KUONYESHA MFANO KWA WATENDAJIA WAKE.


MIZAMBWA
NABII MTARAJIWA!!!
 
alilipa nauli? halafu mwambieni hiyo wizara hayuko peke yake bali kuna watendaji wengine ...wazee wa bandari wanamsubiri
 
Huyu baba naona watamkoma safari hii juzi kati alipanda daladala ta bungu kuanzia mwenge but konda na dereva kama kawaida yao wakaitisha tegeta kibaoni abiria wakashuka konda akatangaza bunju akapanda tena hadi bunju kisha akageuza na gari nyingine, alipofika bunju akamuuliza dereva kwanini ameitisha nauli mara2 wakati gari inasomeka mwenge/bunju yeye kapakia kibaoni halafu kufika kibaoni tena kapakia wa bunju akalipa nauli 1500/ na tiketi ya gari anayo na alisema atakwenda nazo dodoma kama kidhibitisho,amewaonya madereva na makonda kuacha tabia yakunyanyasa wananchi kuwatoza nauli kubwa zaidi ya ile iliopitishwa na sumatra.
 
Marehemu Mr.Ebo aliimba wimboo flani hivi sijui unasemaje ule, sijui unaitwa Sifa za Kijinga
Mpwa amepanda first class halafu sasa hiyo surprise ameitoa wapi na booking najua pale mpaka wiki 2 ndio unapata nafasi !
 
Sawa kabisa! Hii ndiyo tunaita on-the-spot leadership/guidance. Tabia ya umangimeza ndo imetifikisha hapa. Viongozi kukaa maofisini watajuaje kinachoendelea kwenye maeneo yao ya kazi? Dr Magufuli amekuwa akifanya hivi mara nyingi. Mtu mmoja aitwaye Mrema alikuwa akifanya hivi, faida zake ni kuelewa eneo lako ama wizara yako vilivyo.
Tatizo la Mwakyembe labda itakuwa alisafiri Daraja la kwanza, walimwandalia vizuri nk. Angesafiri pia Daraja la Tatu ajionee jinsi binadamu anavyosafirishwa kama mnyama, akutane na vibaka, panya, mende, viroboto, vyoo vichafu, hakuna maji, niishie hapo........
 
Shida ya wanasiasa hasa wa bongo usanii umezidi, tafakari yangu, nafikiri atakua amechoka kuapata kiyoyozi cha VX V8 au ndege, nikawaida starehe ikizidi binaadamu hutafuta karaha kwakua hua anikosa kukamilisha balansi.
 
urais unatafutwa kwa nguvu zote!

Kweli duniani hakuna jema! Mwakyembe akila kuku katika uwaziri wake mtasema ooh, mzembe huyu, wanapeana tu uwaziri hawa CCM. Akichapa kazi, oooh, huyu bwana anatafuta uraisi kwa nguvu zote!

Jamani Watanzania, hivi mnajua mnachotaka kweli? Mie nadhani mnataka mkoloni arudi atutawale, kila mtu akose. Maana sasa naanza kuhisi kama haya mambo yote ya CM Vs Chadema hakuna lolote bali ni fitina wivu na majungu tu, si uzalendo kwa ajili ya nchi yetu. Hamna jema litafanyika mkasifia, bali kutafuta visababu tu vya kumsema mtu. Nina uhakika hata Chadema wakichukua nchi nyie hao hao mnaoshabikia Chadema leo mtakuwa wa kwanza kupiga kelele!

Hebu msikie aibu mara nyingine kusema watu ili mradi basi tu mseme.
 
Shida ya wanasiasa hasa wa bongo usanii umezidi, tafakari yangu, nafikiri atakua amechoka kuapata kiyoyozi cha VX V8 au ndege, nikawaida starehe ikizidi binaadamu hutafuta karaha kwakua hua anikosa kukamilisha balansi.

Wewe unayesema hayo hapo juu sijui kama zimo zote. Unaonyesha katabia ka ushabiki usio na tija wa kutukana viongozi kama wafanyavyo wanasiasa walemavu walioibukia siasa siku hizi hapa Tz. Ukome!! Kwa kuwa katoka CCM basi hata hili zuri lenye tija kwako baya. Baya pia baya. Ama kweli tenda wema nenda zako... Kwani hata waanzilishi wa JF si ajabu wewe huwatukana.
 
Kweli duniani hakuna jema! Mwakyembe akila kuku katika uwaziri wake mtasema ooh, mzembe huyu, wanapeana tu uwaziri hawa CCM. Akichapa kazi, oooh, huyu bwana anatafuta uraisi kwa nguvu zote!

Jamani Watanzania, hivi mnajua mnachotaka kweli? Mie nadhani mnataka mkoloni arudi atutawale, kila mtu akose. Maana sasa naanza kuhisi kama haya mambo yote ya CM Vs Chadema hakuna lolote bali ni fitina wivu na majungu tu, si uzalendo kwa ajili ya nchi yetu. Hamna jema litafanyika mkasifia, bali kutafuta visababu tu vya kumsema mtu. Nina uhakika hata Chadema wakichukua nchi nyie hao hao mnaoshabikia Chadema leo mtakuwa wa kwanza kupiga kelele!

Hebu msikie aibu mara nyingine kusema watu ili mradi basi tu mseme.
Mkuu ulilolisema ni kweli kabisa, kweli kabisa, kweli kabisa, kweli kabisa,
kweli kabisa, Hawajui wanachokitaka
 
hapa mie naona wangi ya wana jf uitikadi umewazid badala ya uzalendo na inaonyesha chochote anachofanya wa chama kingne mbali na cdm hakitakua na maana hata kama ni cha maana, na chochote watachofanya cdm kitakuwa cha maana hatakama hakina maana. sijaona tatizo kwa mwakyembe kuamua kusafiri n train. Amemua kujionea kero wanazopata wadau usafiri wa tren! Tatizo ni nini? Tunataka wachapakaz na wala si chama fulani. Achen akili za matope!!
 
Nadhani ni wewe mwenye kukurupuka na hauko analytical enough kwa kutetea mambo ya ajabu, unapofikiria kitu hebu jaribu kuangalia na upande mwingine wa shilingi.

Kuna mtu katoa observation moja ndogo but very logical, kuwa je waziri wa nishati akalale ktk nyumba isiyo na umeme ndo ajue matatizo ya mgawo wa umeme? Na waziri wa afya je afanyeje kujua matatizo ya wagonjwa?

Kama unakuja na hoja ya kutembea usiku na hoja ya ndege wawili jiwe moja, that is a childish argument, je miradi inakaguliwa usiku kama madai ya kusafiri usiku? Unaweza ona nini usiku katika njia ya treni na ukizingatia sehemu kubwa ni pori?

Ili ndg yangu uwe effective ktk utawala try to specialize by doing one thing at a time, vinginevyo utakujapata stress ya kuwa na pending issues mana utakuwa na issues nyingi but all unfinished.

Do you know the pressure ya Budget kwa mawaziri kipindi hiki hadi apate mda wa kukagua mradi. Cheza na bunge hili wewe, nadhani wewe bado dogo ki umri kuweza jua mambo. But I believe one day u gonna know what exactly I mean.

Kama Mwakyembe angetaka kujua matatizo ya watanzania, kwa nini kipindi anaumwa alienda India Apolo hosp na si Mwananyamala? Ili aje atueleze matatizo ya tiba ya watanzania?
 
Msimamo wangu uko pale pale, huyu Jamaa ni Mmoja kati ya wanasiasa waongo katika Taifa hili, ni mmoja kati ya wanasiasa wanaotafuta sifa zisizo na msingi wowote ule, na katika hili anatafuta cheap popularity.

Mpaka sasa kitu pekee nachojua anaweza kukifanya kwa ufanisi mkubwa ni kutengeneza uongo na kuchafua watu wengine, Mpaka siku atakapoliambia Taifa ni mambo gani kamati yake ya Richmond iliyaficha kwenye report yake ndio naweza nikaanza kumsikiliza.

Mtu yeyote makini ni lazima ajiulize, kwa nini CCM inashindwa kumfukuza Lowasa with all the damage kamati ya mwakyembe ilimfanyia ni lazima aquestion credibility ya huyu jamaa.


Sangara

Kilichomponza Mwakyembe mpaka akalishwa sumu ni hicho unachokisemea. Aliweka wazi kila kitu kwenye ripoti ya Richmond, lakini kama wakubwa zaidi yake wanahusika, unadhani kwenye final copy hayo mazito yataonekana? Au umezisahau kauli za Lowassa kwenye Mkutano Mkuu wa CCM majuzi huko Chimwaga?

Umeisoma ripoti ya Ukaguzi wa Mwakyembe huko TRL? Abiria kulipishwa Shs. 29,000 wakati nauli ni Shs. 9,000?

Cheap popularity, indeed!

Na vipi kuhusu ile ndege (Airbus) iliyokodishwa na ATCL, ambayo haikuruka, na mpaka sasa bado tunadaiwa USD 200 million, na riba yaongezeka kila siku? Huo nao ni uongo? Hata Uganda Vision waliandika kuhusu hili. Kama ni uongo, basi akina Mwakyembe wako wengi.

Sina mbavu!
 
Back
Top Bottom