Ninafikiri sio suala la kumshangaa na kumshambulia kuwa anatafuta cheap popularity. Ni vyema tukampa nafasi ya kusikia. hata kwa kusafiri na treni, naamini hata asiposema kitu, basi wenye mamlaka na walio katika wajibu huo tayari tumbo moto, kama ilikuwa hakuna usafi watasafisha, at least hilo pia ni hatua. Kwa hiyo suala la shangingi kwenda dodoma au la sio issue, hapo ni kutaka kuona uhalisi wa huduma tunazopata, ikifika mahali wakaleta watoto shule za kawaida, shule za kata, dispensary za vijijini basi huduma itaingizwa katika mjadala wa kuona nini kifanyike. Tusihukumu, tusubiri tusikie nini kitatoka katika safari hiyo, na hatua zitakazochukuliwa. Ndilo tunalosubiri...