Mkuu Mzizi wa Mbuyu Mwakyembe alikuwa mgonjwa muda mwingi wakati yupo Ujenzi. Nadhani si haki kumhukumu kwa hilo.
Huyo alikuwa akipanda treni kwa sababu ya shida ya usafiri,Mwakyembe ana shida ya Usafiri?
Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
Kwahiyo gari yake imeenda tupu au kapakia abria.
linasafiri na dereva!na allawonce yake atalipwa!kwa hiyo shangingi linabaki dar au?
jamani tuangalie tusije kuwa kama Ugiriki tukatangazwa bunkrupt!Mheshimiwa Mwakyembe atumia usafiri wa reli ya kati kuhudhuria kikao cha bunge la bajeti kilichoanza leo. Mbali na kuutumia usafiri huo kuhudhuria kikao hicho cha bunge, Mh. Mwakyembe atatumia fursa hiyo kujionea mwenyewe hali halisi ya reli hiyo na adha wanazopata wasafiri na hivyo kuwa katika nafasi ya kusaidia maboresho....
My Take
Wazo la Mheshimiwa ni zuri bila shaka, hata hivyo kwa mujibu wa taarifa toka katika mtandao wa Mh. Zitto Kabwe, naona ni ngumu sana kuleta mabadiriko katika reli hiyo kwa bajeti hii ya mwaka wa fedha wa 2012/2013 na hasa ukizingatia kuwa kiasi kikubwa cha bajeti kinaenda kulipia deni la taifa....Hebu angalia maelezo ya Mh. Zitto hapa chini....
Serikali inapendekeza Bajeti ya TZS 15 trilioni(USD 8.75 Billion) katika mwaka 2012/13. Uchambuzi wa vitabu vya Bajeti unaonesha kwamba mafungu ya juu 5 kwenye Bajeti ni Kama ifuatavyo;Bajeti ya Mwaka huu 2012/2013 ni Bajeti ya Madeni
1 Huduma kwa Deni la Taifa Tshs 2.7 trilioni(USD 1.69 Billion)
2 Wizara ya Ujenzi. Tshs 1 trilioni (USD 625 Million)
3 Wizara ya Ulinzi Tshs 920 bilioni (USD 575 Million)
4 Wizara ya Elimu Tshs 721 bilioni (USD 451 Million)
5 Wizara ya Nishati na Madini Tshs 641 bilioni (USD 400 Million)
TOTAL TZS 5.982 Trilioni(USD 3.74 Billlion)
Chanzo: Vitabu vya Bajeti kwa Wabunge
Jumla ya mafungu haya ni sawa na asilimia 40% ya Bajeti. Kwa hiyo asilimia 40% ya Bajeti yote imepangwa kwa mafungu 5 tu. Fungu lenye kiwango kikubwa zaidi ya Bajeti kuliko vyote ni fungu 22 ambalo ni malipo kwa Deni la Taifa. Pia sehemu kubwa ya fedha zilizotengwa kwa Ujenzi na Nishati ni madeni kwa wakandarasi wanaotekeleza miradi ya miaka ya nyuma.
Hii yaweza kuwa Bajeti ya kulipa madeni zaidi kuliko Bajeti ya kuchochea maendeleo. Bajeti hii pia yaweza pia kuwa ni Bajeti ya kukopa maana jumla ya TZS 5.1 trilioni(USD 3.19 Billion) zitachukuliwa kama mikopo kwa Serikali. Mikopo ya kibiashara ambayo ni mikopo ghali sana itachukuliwa kwa wingi zaidi kuliko mwaka wa fedha uliopita.
Wabunge wanapaswa kufanya uchambuzi zaidi wa Bajeti ya mwaka huu inayopendekezwa na Serikali. Kuna haja kubwa sana ya kuharakisha kuanzishwa kwa Ofisi ya Bajeti katika Bunge na Kamati ya Bunge ya Bajeti ili kuweza kufuatilia kwa karibu, kuchunguza na kutoa taarifa kwa wabunge ili kuwezesha kuboresha Bajeti.
Misamaha yote ya Kodi na Madeni yote ambayo Serikali inaingia inabidi sasa ithibitishwe na Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi ili kuongeza udhibiti na usimamizi wa Misamaha ya Kodi na pia Deni la Taifa.
Nisomesoma kwa masikitiko baadhi ya watu wakibeza hatua ya Mwakyembe kupanda treni. Wengine wamesema anatafuta urais! Waziri kupanda treni, ambayo wanapanda makwabwela, ni hatua ya kupigiwa mfano maana ataona shida zinazowakabili. Hata akilizungumza anakuwa na picha halisi! Fikiria kama mawaziri wote wangepanda dala dala, unadhani hali ingekuwa vile? Au kama watoto wao wangesoma shule za kata, unadhani zingekuwa hivyo? Tusiwakatishe watu wenye nia ya kuelewa shida zetu. Angekuwa Obama kafanya hivyo tungemsifia au tungemwabia anataka sifa?
Halafu tumuone eti ni mzalendo....ukiwa ndani ya gamba hamna kitu!!!linasafiri na dereva!na allawonce yake atalipwa!
Alikuwa wapi alipokuwa naibu waziri wa magufuri?
Mbona kuna madudu mengi tu kayaacha ? Inamaana alikuwa anamuogopa magufuri?
Kiongozi muoga ni dhaifu hatufai!