Mwakyembe apanda treni kwenda Bungeni Dodoma

tatzo ni kuwa v8 anatangulia nayo dreva kumpoka stesheni,apa sijua atakua amesevu nini?
 
Mkuu Mzizi wa Mbuyu Mwakyembe alikuwa mgonjwa muda mwingi wakati yupo Ujenzi. Nadhani si haki kumhukumu kwa hilo.

Kaka tuliza kichwa na ukumbuke vizuri alitumikia unaibu waziri mda gani?

alikuwa mgonjwa muda gani?

na ameanza makeke kwenye wizara mpya baada ya muda gani?

Utagundua ninachokisema kina kiasi fulani ya ukweli Mwakyembe, alikuwa anamuogopa Magufuri ......nadhani nae

anatiming zake!

Wanasiasa mkuu, wana mengi!
 
Tumedanganywa kiasi cha kutosha pia.Mimi siku ya kwanza kumfahamu Kitwana Kondo miaka ya 1990 aliingia kwenye daladala al maarufu chai maharage akashuka Makumbusho,japo niliambiwa watoto wake walikuwa wakitembelea M/benzi wakati huo huo.Mwakyembe anaingia kwenye rekodi ya Wachekeshaji wa CCM: Augustine Lyatonga Mrema alikamata VIGOGO Dar International Airport,hadi leo takribani miaka zaidi ya 20 hajataja jina!JK alisema wala rushwa na vigogo wa madawa ya kulevya anawajua kwa majina na hadi leo hajataja hata initials za jina la mmoja akiwa yeye ni Amiri Jeshi Mkuu!Mwakyembe alishajiuzulu Bodi ya NBC Ltd akitii pia DHAMIRI yake kabla ya kuwa MBUNGE.Mwenzie mtoto wa MKULIMA alikataa shangingi moja tu lililonunuliwa kwa indhini ya ofisi yake,akiwa pia ameidhinisha mengine mengi kwa ajili ya Waheshimiwa wengine,hii ni chini hata ya kiwango cha uchekeshaji,maana inatia huruma(soma aibu)
Kama anataka kuthibitisha kwamba ana uchungu na TAIFA HILI athubutu kufanya haya:
Aaachane na Serikali ya CCM ambayo kwa utafiti maarufu wa Kamati ya Bunge kuhusu Richmond,ilithibitishwa kuwa ya kifisadi kiasi cha kuanguka,ukiacha kwamba yeye na waheshimiwa wenzake ktk kamati ile waliamua kuficha(soma kudanganya) kuhusu mambo mazito zaidi yaliyohusu Richmond:
Apime wapi kuna wapambanaji wa kweli aungane nao siyo lazima kama mbunge ama kiongozi katika kudai haki za kimsingi ikiwemo katiba na miliki za nchi kwa uwezo mkubwa alionao akiwa mbobezi ma mzamivu kwenye maeneo hayo kisheria
Afanye kazi ya mzee wa falsafa SOCRATES,ARUDI UDSM au maeneo kama hayo ili aelimishe vijana na kuwasemea waliozibwa midomo wapate haki zao za msingi
Athubutu kumtaja hadharani kwa majina matatu aliyeunganisha mission ya yeye kutegeshewa sumu ma kuumia kimwili kiasi hicho,UKWELI huu utamweka yeyey na wananchi na huyo haramia huru!
Hii ya kukesha na wasafiri waliokwama TAZARA ama kupanda treni ya karne ya 17 Ulaya haitasaidia kuleta treni za kisasa ,bandari ya kisasa wala kuifufua ATCL,UDA,TRL, wala TAASISI za aina hiyo.NA JUU ya hayo haiwezi kuwa mbinu ya kuwadanganya watanganyika wote wakati wote kwamba yeye ni bora kuliko mfumo wa kifisadi uliomfikisha hapo alipo na ambao kwa ujasiri mkubwa wa.....ameamua kuutumikia hata kwa gharama ya kichwa chake!
 
Mheshimiwa Mwakyembe atumia usafiri wa reli ya kati kuhudhuria kikao cha bunge la bajeti kilichoanza leo. Mbali na kuutumia usafiri huo kuhudhuria kikao hicho cha bunge, Mh. Mwakyembe atatumia fursa hiyo kujionea mwenyewe hali halisi ya reli hiyo na adha wanazopata wasafiri na hivyo kuwa katika nafasi ya kusaidia maboresho....

My Take
Wazo la Mheshimiwa ni zuri bila shaka, hata hivyo kwa mujibu wa taarifa toka katika mtandao wa Mh. Zitto Kabwe, naona ni ngumu sana kuleta mabadiriko katika reli hiyo kwa bajeti hii ya mwaka wa fedha wa 2012/2013 na hasa ukizingatia kuwa kiasi kikubwa cha bajeti kinaenda kulipia deni la taifa....Hebu angalia maelezo ya Mh. Zitto hapa chini....


Bajeti ya Mwaka huu 2012/2013 ni Bajeti ya Madeni
Serikali inapendekeza Bajeti ya TZS 15 trilioni(USD 8.75 Billion) katika mwaka 2012/13. Uchambuzi wa vitabu vya Bajeti unaonesha kwamba mafungu ya juu 5 kwenye Bajeti ni Kama ifuatavyo;
1 Huduma kwa Deni la Taifa Tshs 2.7 trilioni(USD 1.69 Billion)
2 Wizara ya Ujenzi. Tshs 1 trilioni (USD 625 Million)
3 Wizara ya Ulinzi Tshs 920 bilioni (USD 575 Million)
4 Wizara ya Elimu Tshs 721 bilioni (USD 451 Million)
5 Wizara ya Nishati na Madini Tshs 641 bilioni (USD 400 Million)
TOTAL TZS 5.982 Trilioni(USD 3.74 Billlion)
Chanzo: Vitabu vya Bajeti kwa Wabunge

Jumla ya mafungu haya ni sawa na asilimia 40% ya Bajeti. Kwa hiyo asilimia 40% ya Bajeti yote imepangwa kwa mafungu 5 tu. Fungu lenye kiwango kikubwa zaidi ya Bajeti kuliko vyote ni fungu 22 ambalo ni malipo kwa Deni la Taifa. Pia sehemu kubwa ya fedha zilizotengwa kwa Ujenzi na Nishati ni madeni kwa wakandarasi wanaotekeleza miradi ya miaka ya nyuma.
Hii yaweza kuwa Bajeti ya kulipa madeni zaidi kuliko Bajeti ya kuchochea maendeleo. Bajeti hii pia yaweza pia kuwa ni Bajeti ya kukopa maana jumla ya TZS 5.1 trilioni(USD 3.19 Billion) zitachukuliwa kama mikopo kwa Serikali. Mikopo ya kibiashara ambayo ni mikopo ghali sana itachukuliwa kwa wingi zaidi kuliko mwaka wa fedha uliopita.
Wabunge wanapaswa kufanya uchambuzi zaidi wa Bajeti ya mwaka huu inayopendekezwa na Serikali. Kuna haja kubwa sana ya kuharakisha kuanzishwa kwa Ofisi ya Bajeti katika Bunge na Kamati ya Bunge ya Bajeti ili kuweza kufuatilia kwa karibu, kuchunguza na kutoa taarifa kwa wabunge ili kuwezesha kuboresha Bajeti.
Misamaha yote ya Kodi na Madeni yote ambayo Serikali inaingia inabidi sasa ithibitishwe na Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi ili kuongeza udhibiti na usimamizi wa Misamaha ya Kodi na pia Deni la Taifa.
 
Sitashangaa nikisikia anagombea urais maana kwa misifa tu huyu mzee nampa first class
 
Mheshimiwa Mwakyembe atumia usafiri wa reli ya kati kuhudhuria kikao cha bunge la bajeti kilichoanza leo. Mbali na kuutumia usafiri huo kuhudhuria kikao hicho cha bunge, Mh. Mwakyembe atatumia fursa hiyo kujionea mwenyewe hali halisi ya reli hiyo na adha wanazopata wasafiri na hivyo kuwa katika nafasi ya kusaidia maboresho....

My Take
Wazo la Mheshimiwa ni zuri bila shaka, hata hivyo kwa mujibu wa taarifa toka katika mtandao wa Mh. Zitto Kabwe, naona ni ngumu sana kuleta mabadiriko katika reli hiyo kwa bajeti hii ya mwaka wa fedha wa 2012/2013 na hasa ukizingatia kuwa kiasi kikubwa cha bajeti kinaenda kulipia deni la taifa....Hebu angalia maelezo ya Mh. Zitto hapa chini....


Bajeti ya Mwaka huu 2012/2013 ni Bajeti ya Madeni
Serikali inapendekeza Bajeti ya TZS 15 trilioni(USD 8.75 Billion) katika mwaka 2012/13. Uchambuzi wa vitabu vya Bajeti unaonesha kwamba mafungu ya juu 5 kwenye Bajeti ni Kama ifuatavyo;
1 Huduma kwa Deni la Taifa Tshs 2.7 trilioni(USD 1.69 Billion)
2 Wizara ya Ujenzi. Tshs 1 trilioni (USD 625 Million)
3 Wizara ya Ulinzi Tshs 920 bilioni (USD 575 Million)
4 Wizara ya Elimu Tshs 721 bilioni (USD 451 Million)
5 Wizara ya Nishati na Madini Tshs 641 bilioni (USD 400 Million)
TOTAL TZS 5.982 Trilioni(USD 3.74 Billlion)
Chanzo: Vitabu vya Bajeti kwa Wabunge

Jumla ya mafungu haya ni sawa na asilimia 40% ya Bajeti. Kwa hiyo asilimia 40% ya Bajeti yote imepangwa kwa mafungu 5 tu. Fungu lenye kiwango kikubwa zaidi ya Bajeti kuliko vyote ni fungu 22 ambalo ni malipo kwa Deni la Taifa. Pia sehemu kubwa ya fedha zilizotengwa kwa Ujenzi na Nishati ni madeni kwa wakandarasi wanaotekeleza miradi ya miaka ya nyuma.
Hii yaweza kuwa Bajeti ya kulipa madeni zaidi kuliko Bajeti ya kuchochea maendeleo. Bajeti hii pia yaweza pia kuwa ni Bajeti ya kukopa maana jumla ya TZS 5.1 trilioni(USD 3.19 Billion) zitachukuliwa kama mikopo kwa Serikali. Mikopo ya kibiashara ambayo ni mikopo ghali sana itachukuliwa kwa wingi zaidi kuliko mwaka wa fedha uliopita.
Wabunge wanapaswa kufanya uchambuzi zaidi wa Bajeti ya mwaka huu inayopendekezwa na Serikali. Kuna haja kubwa sana ya kuharakisha kuanzishwa kwa Ofisi ya Bajeti katika Bunge na Kamati ya Bunge ya Bajeti ili kuweza kufuatilia kwa karibu, kuchunguza na kutoa taarifa kwa wabunge ili kuwezesha kuboresha Bajeti.
Misamaha yote ya Kodi na Madeni yote ambayo Serikali inaingia inabidi sasa ithibitishwe na Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi ili kuongeza udhibiti na usimamizi wa Misamaha ya Kodi na pia Deni la Taifa.
jamani tuangalie tusije kuwa kama Ugiriki tukatangazwa bunkrupt!
 
Nisomesoma kwa masikitiko baadhi ya watu wakibeza hatua ya Mwakyembe kupanda treni. Wengine wamesema anatafuta urais! Waziri kupanda treni, ambayo wanapanda makwabwela, ni hatua ya kupigiwa mfano maana ataona shida zinazowakabili. Hata akilizungumza anakuwa na picha halisi! Fikiria kama mawaziri wote wangepanda dala dala, unadhani hali ingekuwa vile? Au kama watoto wao wangesoma shule za kata, unadhani zingekuwa hivyo? Tusiwakatishe watu wenye nia ya kuelewa shida zetu. Angekuwa Obama kafanya hivyo tungemsifia au tungemwabia anataka sifa?

Siamini kama kwa kupanda treni ndio Mwakyembe atakuwa anagundua matatizo ya usafiri huo? kwani wasaidizi wake wanafanya kazi gani? ina maana watu wanaofanya kazi chini yake hawafanyi kazi? na kama wanafanya,je hawaamini? na kama hawaamini anawezaje kuendelea kufanya nao kazi? this is too cheap for him
 
Alikuwa wapi alipokuwa naibu waziri wa magufuri?
Mbona kuna madudu mengi tu kayaacha ? Inamaana alikuwa anamuogopa magufuri?

Kiongozi muoga ni dhaifu hatufai!

Ni kweli huyu jamaa alikuwa chini ya Magufuri, na hakuweza kupanda treni hiyo haimanishi kuwa yeye ni mwoga bali hakutaka kuingilia kazi wizara nyingine. Kumbuka kuwa wao walikua ujenzi.
 
Waziri kupanda train Dar to Dodoma na kutumia masaa 10 wakati angepanda bus angetumia masaa matano tu ni kupoteza muda wa kulitumikia taifa. Hana tofauti na boss wake anayetumia muda mwingi wa utawala wake kwenye ndege akisafiri kuzunguka dunia. Anyway Mwakyembe tutampima kwa bajeti atakayotuletea na si kwa kupanda treni, cheap popularity
 
Back
Top Bottom