hahahahhaa,,,,nadhan si kwa mawaziri tu,hata
Nadhani nchi hii imekumbwa na tatizo lingine kubwa la watu wake kutojua na kuweka umhimu wa mda.
Najua watu watasema ni njia ya kujiridhisha kwa kuangalia miradi iliyo chini ya wizara, lakini je matatizo ya TRL yamemalizika ya kimikataba ambayo was a serious issue?
Navyojua mimi safari ya treni hadi Dodoma ni zaidi ha masaa 14, mda huu unatosha kwa waziri kuwa amefanya kazi nyingi sana na kuwa amefanya maamuzi mengi sana ofisini tena yenye tija zaidi kuliko hili la kusafiri na teni.
Kama Waziri anaweza kufanya kazi ya kuhesabu madaraja kwenye njia ya treni je watendaji wako wapi? Au ndo kutowaamini na kufikiri wanawapinga/wahujumu mawaziri ili washindwe kufanya kazi zao za kiwaziri na waondolewe ili waje maswahiba zao?
Mtizamo wangu mimi katika hili simuungi mkono waziri Mwakyembe na kutumia usafiri wa treni hadi Dom kwa sababu moja nimesema kuhusu matumizi mabaya ya mda, pili risk kama ambavyo baadhi wamesema kuharibika kwa treni porini hivyo kuhitaji rescue, tatu hujuma ambazo zinaweza kufanyika juu yake ukizingatia yaliyomtokea huko nyuma.
Mhe Mwakyembe has emerged to be a popularist minister who uses whatever it is as a political platform, I guess he has a hidden agenda, watu kama hawa hawafai kabisa katika uongozi ambao wananchi maskini wanawategemea, mwisho wa siku akipata uongozi mkubwa nchi anaweza kuwa kama JK kama alivyoanza na anakoishia uongozi wake ambsko ni kubaya by losing popularity.