GoldDhahabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2023
- 4,695
- 6,398
Asemacho mkubwa ni "Sheria"Nao ni binadamu tuu, wanaghafilika.
P
Asemacho mkubwa ni "Sheria"Nao ni binadamu tuu, wanaghafilika.
P
Jukumu la kuulinda huu muungano wetu adhimu, sio la watu fulani na kutuita nyie, ni jukumu la kila Mtanzania mzalendo wa kweli wa taifa lake.
It's very unfortunately, tuna Watanzania wenzetu ni mamluki wanatamani huu muungano wetu adhimu kuvunjika hata leo!.
Mamluki hawa watasubiri sana!.
P
Tusiume ume maneno!Naunga mkono hoja, mimi ni Mnyerere naamini kwenye serikali moja! Kama kweli nia ya dhati ni kuimarisha Muungano, then "Twende kwenye Serikali Moja!" na hili la serikali mbili nililipinga since day 1 Tahadhari ya hatari: CCM Imepania Kufanya Kinyume cha Maumbile! na hapa Chonde Chonde Rais Kikwete: Msimamo wa CCM wa Serikali Mbili ndio utauvunja Muungano
Naunga mkono hoja
Tunaona na tumewashauri Wanzanzibar amueni moja, ama acheni kelele za muungano!, ama pigeni Kura ya Maoni, muamue moja
P
Ni usipoziba ufa, utajenga ukuta.USIPOJENGA UFA UTAJENGA NYUMBA!
.........
Hakuna anae kataa Muungano! Ilaha huu mfumo wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ndio haukubaliki ni pasua kichwa!Wazanzibari ni Watanganyika pia,maana hapo zamani kabla ya watu kuishi zanzibar hapakuwa na watu,waliogundua Kisiwa cha Zanzibar ni Watanganyika kama vile wanyamwezi,wamakonde,wadigo,wahaya,wazramo nk,hawa ndio waliogundua kuwa kuna Visiwa vikubwa vya kuweza kuishi watu,na ndio wakaanza maisha yao huko.Wakoloni wa kiarabu na wengineo walipofika zanzibar waliwakuta Watanganyika washaanza kuzaliana na kuwa na tamaduni zao,kwa vile wakoloni lengo lao ni lilikuwa kuongeza makoloni ndio wakaanza kuwaoa na kuwapa watoto ,na hapo ndio machotara na rangi mbali mbali wakazaliana na kuwaambukiza utamaduni wao kule zanzibar,na ndio mpk sasa athari za wakoloni na waarabu waliotawala zanzibar.
Hivyo baada ya mapinduzi na kuondolewa wakoloni ndio Viongozi wetu Nyerere na Karume kuamua kuunganisha Zanzibar na Tanganyika,hivyo kuungana kwao ni muunganiko wa kiudugu wa kidamu,maana wazanzibari asili yao ni Watanganyika pia,hivyo ni muunganiko wa kiudugu au ni Mjumuiko wa Kiuddugu wa damu kabisa,sasa wewe kijana wa leo uliyekulia miaka ya 2020 hujui hii historia unapelekeshwa na udini na ukabila kichwani mwako ndio unawaza kuandika huu uzi,na kusema muungano hauna faida kweli uko serious wewe kijana?leo watu washazaliana kila mkoa na mchanganyiko ni mkubwa sana kati ya watu wa miji hii,kule zenji mahotelini kote wanaendesha hoteli sio watu wenye ASILI YA ZANZIBAR NI wazaramo ,wahaya ,wachaga nk.leo ukitaka kusema muungano uvunjike au muunganiko uenguliwe utakuwa haujaitendea haki nchi yako,kumbuka hilo kuwa WAZANZIBARI NI WATANGANYIKA na ndio maana muungano wa namna hii haupatikani kokote kule duniani kwasababu hizi nchi 2 ni za udugu wa damu,ni mtu na kaka yake,dada yake,bibi yake,mama yake,mjomba wake,shangazi yake,ami yake,rafiki yake,jirani yake,nk
Nawasalimu katika jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na kuwatumia salaam zangu za kuadhimisha kumbukumbu ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, tutayalinda kwa gharama yoyote.
Nawatakia maadhimisho mema ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
Japo sasa Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yanaelekea miaka 60, Miaka 50 Ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, Bado Kuna Maswali Bila Majibu -1
Kazi Iendelee!.
Paskali
Wazanzibari ni Watanganyika pia,maana hapo zamani kabla ya watu kuishi zanzibar hapakuwa na watu,waliogundua Kisiwa cha Zanzibar ni Watanganyika kama vile wanyamwezi,wamakonde,wadigo,wahaya,wazramo nk,hawa ndio waliogundua kuwa kuna Visiwa vikubwa vya kuweza kuishi watu,na ndio wakaanza maisha yao huko.Wakoloni wa kiarabu na wengineo walipofika zanzibar waliwakuta Watanganyika washaanza kuzaliana na kuwa na tamaduni zao,kwa vile wakoloni lengo lao ni lilikuwa kuongeza makoloni ndio wakaanza kuwaoa na kuwapa watoto ,na hapo ndio machotara na rangi mbali mbali wakazaliana na kuwaambukiza utamaduni wao kule zanzibar,na ndio mpk sasa athari za wakoloni na waarabu waliotawala zanzibar.
Hivyo baada ya mapinduzi na kuondolewa wakoloni ndio Viongozi wetu Nyerere na Karume kuamua kuunganisha Zanzibar na Tanganyika,hivyo kuungana kwao ni muunganiko wa kiudugu wa kidamu,maana wazanzibari asili yao ni Watanganyika pia,hivyo ni muunganiko wa kiudugu au ni Mjumuiko wa Kiuddugu wa damu kabisa,sasa wewe kijana wa leo uliyekulia miaka ya 2020 hujui hii historia unapelekeshwa na udini na ukabila kichwani mwako ndio unawaza kuandika huu uzi,na kusema muungano hauna faida kweli uko serious wewe kijana?leo watu washazaliana kila mkoa na mchanganyiko ni mkubwa sana kati ya watu wa miji hii,kule zenji mahotelini kote wanaendesha hoteli sio watu wenye ASILI YA ZANZIBAR NI wazaramo ,wahaya ,wachaga nk.leo ukitaka kusema muungano uvunjike au muunganiko uenguliwe utakuwa haujaitendea haki nchi yako,kumbuka hilo kuwa WAZANZIBARI NI WATANGANYIKA na ndio maana muungano wa namna hii haupatikani kokote kule duniani kwasababu hizi nchi 2 ni za udugu wa damu,ni mtu na kaka yake,dada yake,bibi yake,mama yake,mjomba wake,shangazi yake,ami yake,rafiki yake,jirani yake,nk
Karibuni Tunguu
Imekuwa ni jadi na utamaduni kufurahia sikukuu hii na kuwaenzi waasisi wa Muungano wetu Mwalimu Nyerere na Mzee Abeid Karume kwa matamasha, gwaride na shangwe kebekebe.
Lakini imekuwa ni dhambi, tena yenye sumu kali kwa mtu yeyote kuhoji au kutaka kuuchambua Muungano huu.
Lengo langu si kuuliza historia au kudadisi uhalali wa Muungano wa Tanzania bali ni faida zake na manufaa yake kutokana na mfumo wa Muungano kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania, mamlaka zilizoko kama vile Mahakama, Bunge, Baraza la Wawakilishi na ni vitu gani ambavyo ni kwa ajili ya Muungano na vipi si kwa ajili ya Muungano.
Je, kwa nini tuliweka vipengele fulani viwe masuala ya muungano na vingine visiwe?
Je, Muungano huu una maana gani ikiwa vipengele ilivyoko vinakingana na azma kuu ya kuunda Taifa lenye nguvu na umoja?
Je, Wananchi wa Tanzania, wananufaika vipi na Muungano huu na wanaathirika vipi kutokana na Muungano huu na mfumo wake?
Je, kuna haja ya kuupitia Muungano na ama kupangua vipengele fulani au kuunganisha kila kitu na kuwa na sura moja bila kutofautisha ya hili la Watanganyika au Watanzania Bara na lile ni la Wazanzibari?
BAADHI YA MICHANGO ILIYOTOLEWA NA WADAU KUHUSU MADA HII
---
---
---
---
---
---
---
ZAIDI UNASHAURIWA KUSOMA MADA HIZI:= > Lipo wapi tatizo kwenye muungano wa Tanganyika na Zanzibar? Tafakari!
= > Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni sawa na Muungano wa Siria na Ejibti walioungana 1958
= > Waliohoji uhalali wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar wafikia hatua gani?
Kwa taarifa yako Mzanzibari hahitaji msaada wa mtu, Kabla ya uvamizi Hao wote uliowataja walikuja huku Zanzibar kutafuta maisha , hata Leo hii Watanganyika wamejaa wakidavia davia japo dagaa. Lakini wengi wamekosa utu na ustaarabu wameichafua nchi pamoja na majeshi ya Tanganyika na usalama wa Taifa wao waliovalia rubega za kimasai ni aibu tupu. Tuacheni tuijenge nchi yetuWazenj was0me kut0ka Uingereza! Hivi sasa wataka wapige kura tena warudi EU! Utajiri m0dhani mtaupata baada ya kujitenga ni myth. Kama Mwarabu asaidia 0vy 0vy angeisaidia Yemen, Sudan au hata wafanyakazi wa ndani ku0tka nchi za Kiislamu!
Muundo mzuri pengine tungalikuwa na Rais wa JMT, akiwa na mawaziri wake wakuu wawili kwa upande wa Tanganyika na Zanzibar. Hawa wawili ndio wangalikuwa ni viongozi wa shughuli za kiserikali katika upande husika.Hakika Watanganyika tumekuwa Wajinga kwa Miaka Mingi sana na UJINGA wetu umetengenezwa na CCM kwa muda wote huo.Kwa hesabu za kawaida tu Nchi mbili zikiungangana na kuzaa nchi ya 3 basi zile Nchi mbili zilizoungana zinapotea au zote mbili zinaendelea kuwepo.Tanganyika na Zanzibar (Nchi 2) zilizoungana na Kuizaa TANZANIA.Nilitegemea Tanganyika na Zanzibar zingefutika kabisa au zote 2 zingeendelea kuwepo.AJABU ya Tanzania Nchi ya TANGANYIKA haiopo kabisa na ukiwauliza VIONGOZI ipo wapi hata Wao hawajui kama ipo au imekwenda wapi cha kushangaza zaidi ni Uwepo wa Nchi ya Zanzibar ikiwa na RAIS wake Bendera yake na Wimbo wake wa Taifa.
JE huu ni MUUNGANO wa AINA GANI hapa Duniani?
WaTanganyika ktk Rasmu ya JAJI WARIOBA walitaka MUUNGANO wetu uwe na SERIKALI 3 ,Serikali ya TANGANYIKA Serikali ya ZANZIBAR na Serikali ya Jamhuri ya Muungano ya TANZANIA .Kutokuwepo kwa Nchi ya TANGANYIKA na RAIS wake ni KUWAONEA watu Wa TANGANYIKA kwanini Watu wa ZANZIBAR wamependelewa pekee yao bila Mshiriki mwenza Tanganyika?
CCM ,Wananchi wa TANGANYIKA tuna Haki yetu kama ZANZIBAR walivyopewa HAKI yao na sisi TANGANYIKA tuwe na NCHI yetu na RAIS wetu.
Huwa nawashangaa sana CCM wakati wa kukumbuka UHURU wa TANGANYIKA utakuta Vyombo vya habari na Vioeperushi Vimesambazwa vikiwa na MAANDISHI yasemayo MIAKA 62 ya UHURU wa TANZANIA BARA"
Hivi kweli Nchi ya Tanzania bara ipo wapi?Je huo mwaka 1961 Alimkabidhi NYERERE UHURU wa TANZANIA BARA?
Mtanzania yeyote mwenye sifa stahili anaweza kuwa Rais wa eneo lolote, umefika wakati sasa mambo ya uzanzibar na utanganyika yakawekwa pembeni kwani hayana tija kwa maendeleo yetu.