Muungano wa Tanganyika na Zanzibar: Una faida gani na kwa manufaa ya nani?

Rev. Kishoka

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
4,526
1,529
1599643531292.png

Imekuwa ni jadi na utamaduni kufurahia sikukuu hii na kuwaenzi waasisi wa Muungano wetu Mwalimu Nyerere na Mzee Abeid Karume kwa matamasha, gwaride na shangwe kebekebe.

Lakini imekuwa ni dhambi, tena yenye sumu kali kwa mtu yeyote kuhoji au kutaka kuuchambua Muungano huu.

Lengo langu si kuuliza historia au kudadisi uhalali wa Muungano wa Tanzania bali ni faida zake na manufaa yake kutokana na mfumo wa Muungano kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania, mamlaka zilizoko kama vile Mahakama, Bunge, Baraza la Wawakilishi na ni vitu gani ambavyo ni kwa ajili ya Muungano na vipi si kwa ajili ya Muungano.

Je, kwa nini tuliweka vipengele fulani viwe masuala ya muungano na vingine visiwe?

Je, Muungano huu una maana gani ikiwa vipengele ilivyoko vinakingana na azma kuu ya kuunda Taifa lenye nguvu na umoja?

Je, Wananchi wa Tanzania, wananufaika vipi na Muungano huu na wanaathirika vipi kutokana na Muungano huu na mfumo wake?

Je, kuna haja ya kuupitia Muungano na ama kupangua vipengele fulani au kuunganisha kila kitu na kuwa na sura moja bila kutofautisha ya hili la Watanganyika au Watanzania Bara na lile ni la Wazanzibari?

BAADHI YA MICHANGO ILIYOTOLEWA NA WADAU KUHUSU MADA HII
Baada ya Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Jamhuri yetu kutamka bayana katika Bunge kuwa Zanzibar sio nchi, kulikuwa na mjadala mkali kutoka kwa wadau mbalimbali kuhusu usahihi wa kauli yake hiyo.

Wako watu wengi walioona kuwa kauli ya Mheshimiwa wetu huyu aliyoitamka mbele ya kadamnasi ya waheshimiwa wenzake ni sahihi kwa misingi ya katiba zetu. Aidha kumekuwa na watu wengine, wakiwamo baadhi ya Mawaziri wa SMZ na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi, waliyoyatizama mambo kwa upande wa pili wa sarafu. Kwao wao hawa, Zanzibar ni nchi kamili na kamwe haiwezi kusemwa vyenginevyo. Kila moja ya makundi haya limekuwa na sababu zake ambazo baadhi zimetolewa kwa hoja zenye mashiko na nyengine zimekuwa ni hoja za kibubusa ambazo hazina mashiko yoyote ya kielimu zaidi ya kutolewa kwa misingi ya ushabiki au jazba. Kwa maoni ya Wazanzibari waliowengi, hata Rais Kikwete hakuongeza jipya lolote pale alipolihutubia bunge na kuzungumzia kadhia hii zaidi ya kuongeza petroli katika moto unaowaka au kupigilia msumari katika kidonda kibichi kinachovuja damu!

Vyovyote iwavyo, Katiba ya Jamhuri ya Muungano inatamka bayana kuwa Zanzibar ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hata hivyo, Katiba hii haikutamka hili kwa bahati mbaya au kwa kukosewa kama baadhi ya watu wanavyoamini. Katiba hii imetungwa; na walioiandika walijua lengo lao tangu mwanzo wa uandishi wao na walihakikisha wanalikamilisha. Ikitathminiwa tangu awali inaweza kubainika wazi kuwa hakukuwa na nia njema kutoka upande wa Tanganyika katika kuunda na kuuendeleza Muungano huu wa Tanganyika na Zanzibar.

Mwalimu Nyerere mwenyewe katika miaka ya mwisho wa 1950 aliwahi kunukuliwa akisema kuwa lau angeweza kuvisukuma nje ya bahari ya hindi visiwa vya Zanzibar basi angefanya hivyo kwa jinsi vinavyomkera na asivyopenda kuviona vinastawi na kunawiri (Smith, William E. 1973 uk 121). Kwa vile ni dhahiri kuwa asingeweza kutekeleza kusudio lake hilo, ndipo alipotafuta kila mbinu ili angalau basi Zanzibar isiwe nchi huru yenye mamlaka yake inayojitegemea. Katika kukamilisha azma yake hiyo, ndipo alipobuni mpango wa kuifanya Zanzibar kuwa ni sehemu ya Tanganyika chini ya kitambaa cha Muungano. Kwa bahati mbaya sana Mzee Karume kwa wakati ule hakuweza kung'amua haraka nia mbaya hii ya Tanganyika na viongozi wake kwa Zanzibar na hivyo akajikuta anacheza ngoma asiyoitambua kwa kuiweka rehani Zanzibar na maslahi yake .

Watu wanaweza kushangaa ni kwa vipi Mwalimu Nyerere, kiongozi anayeonekana 'mtakatifu' mbele ya macho ya baadhi ya watanganyika asemwe kuwa hakuwa na nia njema na Zanzibar hasa pale suala la muungano linapohusika. Ukweli huu unadhihirika wazi iwapo itatathminiwa ushiriki wa Nyerere tangu mwanzo wa harakati za muungano hadi pale alipofariki. Historia inajionyesha wazi kuwa kabla ya Muungano Zanzibar ilikuwa ni nchi inayojitegemea na yenye mamlaka yake kamili ' independent and sovereign state'.

Makubaliano ya Muungano ‘Articles of Union' yaliyosainiwa mwaka 1964 ni mkataba wa kimataifa ‘international treaty' unaotambuliwa na Vienna Convention on the Law of Treaties. Makubaliano hayo ya Muungano yalikuwa juu ya mambo kumi na moja tu ambayo ndiyo yaliyokubaliwa kuwa mambo ya muungano. Mihimili ya utendaji na kutunga sheria ya Zanzibar (Zanzibar Executive and Legislature) ilikosa mamlaka ya kisheria juu ya mambo hayo kumi na moja tu. Nje ya mambo yale kumi na moja Zanzibar ilikuwa na mamlaka yake kamili ya kusimamia na kushughulikia mambo yote mengineyo. Hii ndiyo sababu Makubaliano ya Muungano yalibakisha separate executive and legislature kwa Zanzibar zilizotakiwa kuundwa kwa mujibu wa sheria za Zanzibar na ambazo zina mamlaka ya kusimamia na kushughulikia mambo yote ambayo si ya muungano kwa Zanzibar. Mambo haya yanamaanisha kuwa Makubaliano ya Muungano yamebakisha kiwango fulani cha utaifa ‘sovereignty' kwa Zanzibar juu ya mambo yake yote yasiyo ya muungano.

Mashaka yote katika Muungano huu unaoweza kufananishwa na muungano wa paka na panya yameanzia katika Sheria ya Muungano yaani 'Acts of Union, No. 22 of 1964'. Ikilenga kuridhia na kurasimisha Makubaliano ya Muungano, Sheria hiyo ya Muungano ilitoa mwanya wa kuvurugwa Muungano na kuonewa aliye dhaifu na mdogo. Kwa hakika Sheria hii imeweka jiwe la msingi kwa mipasuko yote ya kikatiba iliyofuatia katika muungano wetu. Ni sheria hii ndiyo iliyodhihirisha bayana nia mbaya ya Tanganyika na viongozi wake kwa mustakabali wa Zanzibar. Sikusudii kuonyesha kila jambo lililokwenda kinyume na spiriti ya Makubaliano ya Muungano katika sheria hii.

Bali kwa mukhtasari, kifungu cha 8 cha sheria hii kwa mfano kilimpa mamlaka Rais wa Jamhuri ya Muungano kupitisha na kutoa ‘Decrees'. Ijapokuwa ni kweli kuwa Ibara (III) ya Makubaliano ya Muungano inaelezea kuwa wakati wa kipindi cha mpito Jamhuri ya Muungano ingeongozwa kwa Katiba ya Tanganyika iliyorekebishwa ili kukidhi matakwa ya Makubaliano ya Muungano lakini kwa vyovyote vile Ibara hii haikumpa madaraka yoyote Rais kupitisha na kutoa Decrees. Rais alikuwa na madaraka kwa mujibu wa Ibara (V) (b) ya Makubaliano ya Muungano kutoa ‘oder' ya kuifanya itumike hadi Zanzibar sheria yoyote iliyohusu jambo la muungano. Haikubaliki kulitafsiri neno ‘order' lililotumika katika Ibara (V)(b) ya Mapatano ya Muungano kumaanisha ‘Decree' hasa kwa vile Decree zilizotolewa na Rais zilikuwa na hadhi ya kikatiba wakati presidential order zingekuwa na hadhi ya azimio la kiutendaji yaani 'executive declaration' tu.

Kufuatia kifungu 8, Rais wa Jamhuri wa wakati ule (Nyerere) alipitisha Decrees chungu nzima ambazo hazikuwiva pamoja wala kwenda sambamba na makubaliano ya Muungano. Kwa mfano, katika G.N. 245 ya 1964 Nyerere alitoa Decree iliyoitwa Transitional Provisions Decree ambayo iliibatiza Serikali yote ya Tanganyika na kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano. Athari ya kwanza ya ‘Decree' hii ni kuviza muundo wa shirikisho uliotazamiwa na kukusudiwa na Makubaliano ya Muungano. Lakini pia, kuichanganya Serikali ya Tanganyika ndani ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano kumeyachanganya mambo yasiyo ya Muungano ya Tanganyika ndani ya eneo la Jamhuri ya Muungano na, hivyo, kuifanya Tanganyika na Jamhuri ya Muungano kuwa ni pande mbili za sarafu moja!

Mhimili wa utoaji haki (mahkama) mathalan kamwe haukuingizwa wala kufanywa kuwa ni jambo la muungano (haumo kwenye Makubaliano ya Muungano) na hivyo kuufanya kila upande wa Muungano uwe na mfumo wake wa sheria na mahkama yake iliyo huru kutoka nyenziwe. Bali kutokana na kuchanganywa mambo kimakosa kile kilichopaswa kuwa Mahkama kuu ya Tanganyika sasa kinaitwa Mahkama kuu ya Jamhuri ya Muungano. Hili ni koseo kubwa hasa kwa kuwa kila inapotajwa Mahkama ya Jamhuri ya Muungano katika sheria mbalimbali imekuwa ikitafsiriwa kuwa ni Mahkama ya Tanzania Bara na kwamba Mahkama za Zanzibar hazina mamlaka mlingano au 'concurrent jurisdiction' kushughulikia jambo hilo.

Mfano uliowazi upo katika kesi ya Jina Khatib Haji v Juma Sleiman Nungu [1986] L.R.C ambapo ilielezwa na Mahkama kuwa kwa vile sheria ya Uchaguzi ya Jamhuri ya Muungano imeipa mamlaka Mahkama kuu ya Jamhuri ya Muungano kusikiliza petition za uchaguzi hivyo Mahkama kuu ya Zanzibar haina mamlaka ya kusikiliza kesi hizo hata kama itahusu uchaguzi wa wabunge katika majimbo ya Zanzibar!

Kama kwamba haitoshi, Transitional Provisions Decree pia imeeleza kuwa kila mtu aliyekuwa anashikilia Afisi katika ajira ya Jamhuri ya Tanganyika atahesabika kuwa anashikilia Afisi inayofanana na hiyo katika Jamhuri ya Muungano. Athari ya hili ni kuwa watumishi wote wa Serikali ya Tanganyika wakawa ni watumishi wa Jamhuri ya Muungano hata kama Afisi zao hazihusu mambo ya Muungano. Hata sheria zilizosimamia mambo ya ajira na utumishi serikalini ambazo awali hazikuwa za muungano nazo kinyemela zikawa ni sheria za muungano kwa kuwa utumishi katika serikali ya Jamhuri ya Muungano sasa limepewa hadhi ya kuwa jambo la Muungano.

Hata Wizara ambazo si za mambo ya Muungano kwa upande wa Tanganyika nazo sasa zaitwa kuwa Wizara za Jamhuri ya Muungano. Jambo hili limewapa madaraka kwa mlango wa nyuma Mawaziri wanaosimamia Wizara zisizo za Muungano kwa Tanganyika kushughulikia baadhi ya mambo ambayo si ya Muungano hadi Zanzibar! Kwa Mfano Waziri anayeongoza Wizara ambayo si ya Muungano kwa upande wa Tanganyika anapokwenda katika mikutano ya kimataifa kuiwakilisha Tanzania hivi huwa anaiwakilisha Tanganyika au Tanzania nzima ikiwemo Zanzibar. Maana wawapo kule ughaibuni hujinasibu kuwa wao ni Mawaziri katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano kwa mfano Mimi ni Waziri wa Kilimo na Mifugo wa Jamhuri ya Muungano wakati mambo hayo siyo katika mambo ya Muungano.

Halkadhalika, kuosekana kwa Mfuko Mkuu tofauti kwa mambo yasiyo ya muungano kwa Tanganyika nalo limekuwa ni tatizo jengine. Kwa msingi huu, hata tanganyika inapotaka kutumia fedha kwa idara na taasisi zake zisizo za muungano basi fedha hizo hutolewa kutoka katika hazina na Mfuko Mkuu wa Muungano. Jambo hili linaipa Zanzibar unfair advantage kwa kuwa yenyewe hairuhusiwi kutumia fedha kutoka mfuko huu kwa mambo yasiyo ya muungano kwa Zanzibar. Kwa bahati mbaya, fedha zote za ruzuku na misaada zinazokuja kwa jina la Tanzania kutoka nje huhifadhiwa katika mfuko huu ambao Zanzibar hainufaiki nawo na badala yake tanganyika kwa kujifanya wajanja wanazitafuna mara mbili.

Itaendelea………View attachment 21575
---
Heshima kwako Rev Kishoka,

Muungano una fadia zaid kwa Wazanzibar kuliko Watanzania bara.

Zanzibar waliungana na Tanzania bara kwaajili ya usalama wao kipindi cha vita baridi.Mazingira ya wakati huu siasa za vita baridi hazipo tena na pengine ndiyo maana tunashuhudia wazanzibar wakitaka sauti zaidi kwa kutambua kitisho cha miaka ya sitini na sabini hakipo tena.

Muungano wa Tanzania bara yenye idadi ya watu 44 milioni na eneo lenye ukubwa wa 945,087 sq km dhidi ya Zanzibar yenye watu 1 milioni na ukubwa wa eneo 2,461 sq km tu ni baadhi ya chamgamoto kubwa zinazosumbua muungano.Ukizingatia ukubwa wa Tanzania bara na idadi ya watu wake ukilinganisha na ukubwa wa Zanzibar na idadi ya watu wake tayari mgongano wa kimaslahi [kisiasa,kiuchumi na kijamii] ni sababu tosha za kuyumbisha muungano.

Muundo wa muungano wa serekali mbili uliandaliwa na Mwl J Nyerere kwaajili ya kuaccomaodate kanchi kadogo sana "Zanzibar" [hakana ukubwa wa mkoa wa Tanga au Mbeya] ndani ya muungano wa nchi mbili moja kubwa "Tanzania bara".Kinachotokea sasa ni nchi moja ndogo kutaka usawa na nchi moja kubwa sana kugawana madaraka ya kisiasa na kiuchumi.Zanzibar ina wabunge zaidi ya sabini [70] ndani ya bunge la JMT, mkoa wa Dar es Salaam hakuna zaidi ya wabunge kumi [10] lakini ina idadi ya watu zaidi ya 3 milioni amabayo ni idadi ya watu mara tau zaidi ya Zanzibar.Mkuu hiki nikipengele kimoja tu, ukijaribu kuangalia vipengele vingine utabaki kinywa wazi ni kwanini tulazimishe muungano.

Mkuu wazanzibar wanatumia fursa kubwa za kiuchumi zinazopatikana Tanzania bara.Ushahidi uko wazi kabisa siku ikatokea wapemba wakaambiwa wafungashe warejee kwao hakika wangewalaumu sana wapinga muungano.Zanzibar haina rasilimali nyingi kama Tanzania bara bado wanaota mafuta amabyo mpaka sasa hakuna dalili za kuwepo mafuta ya kutosha kwaajili ya biashara.

Zanzibar haichagii uendeshaji wa serekali ya JMT,Mahakama ya rufaa na Bunge la JMT.Utashangaa wazanzibar wanadai nyongeza ya mgao wa mapato ya misaada lakini wanasahau hawachangii senti tano ya uendeshaji wa serekali ya JMT.

Ipo hasara moja kubwa sana iwapo Tanzania itaamua kuvunja muungano leo hii au siku za usoni,Ni rahisi sana magaidi kujipenyeza Zanzibar isoyopenda kufanya kazi ya kuwakomboa wananchi wake kiuchumi na badala yake inajikita kuota uwepo wa mafuta kwenye pwani yake.Tanzania itajikuta ikipokea wakimbizi wa kizanzibar maelfu kwa malaki kama ilivyotokea Burundi na Rwanda.Zanzibar wakijitenga leo tujiandae kukaa na Somalia nyingine kilometa chache kutoka Dar es Salaam na Tanga.
---
  • Hoja binafsi kwa wazalendo ipo mezani!
  • Operesheni megua muungano Zanzibar kuanza jimbo kwa jimbo!
Na: Malik Nabwa
Zamani mtoto akilia sana usiku tukimchombeza kwa nyimbo. Tukianza na nyimbo za kuchezea watoto kuanzia makwaya kwaya kamndindiliya, adi adi. Tukiona hanyamazi tunaimba nyimba za Samba. Kisha msewe, tarazia, kibandiko, boso, mbware, na kama mtoto bado hanyamazi tukimpiga ubeleko. Ndani ya mbeleko akiendelea kulia tukimuoshakwa maji maana tukidhani ana joto. Yakishindwa yote haya mtoto bado hasikii dawa na anaendelea kulia sasa tukimtisha kwa babu mduma. Zote hizi ni juhudi tu za kumreburebu mtoto anyamaze maana kilio ni ghasia na hunyima watu raha.

Na muungano wetu wa Tanzania ni mithai ya mtoto mlizi. Tumekwisha kila rai kuutaka Muungano huu ama uondoke, au basi angalau urekebishwe ili unufaishe sehemu zote mbili sawasawa lakini wapi?. Juhudi hizi zimeshindikana. Tulitaka muungano uangaliwe upya, tukaonekana tunabwabwaja tu. Tukataka tupunguziwe mambo ya Muungano yasio na faida bado kimya. Baya zaidi Raisi wetu aliepo madarakani kila jambo analoletewa na wasaidizi wake husema hilo ni la Muungano kwanza nalipitie bara huko ndio lijadiiwe hapa. Tumeona hivi karibuni jinsi mamilioni ya Brunei yalivyorudishwa hivi hivi kwa Rais kukataa nchi hiyo kuisaidia Zanzibar kama nchi akisisitiza kupitia Muunganoni kwanza. Kwa haya machache na mengine mnayoyajua na kuyaona kwa mato yenu ni dalili tosha kuwa njia mbadala ya kujinasua haipo.

Kumwaga damu haina haja na si katika njia nzuri ya kudai haki iwapo haina ulazima. Tulishajaribu ikashindikana mara moja hiyo. Lakini kwa sasa kuna njia mbadaa ya kuutumia umma wa Zanzibari kuitatua hili. Ninaposema nguvu ya umma sikusudii tuandamane, la hasha. Katika Operesheni Megua muungano visiwani hatukusudiii kabisa kuingia barabarabani. Bali tutatumia utaratibu sahihi wa sheria na katiba ya nchi na tukishikamana kiukwei basi tutafanikiwa muda si mrefu. Wazalendo wenzangu, kampeni MEGUA haina nia ya kuuvunja muungano. Neno MEGUA maana yake kuunyofoa nyofoa kidogokidogo mpaka tukajua moja. Kupata haki yetu au kuufanyia marekebisho Muungano huo ukawa wa manufaa zaidi kwa kila mmoja wetu. Ikishindikana hivyo tutaendelea kuumegua hadi tuumalize. Nyumba isiyo nguzo haisimami, na hii ndio falasafa ya Operesheni MEGUA. Na ili tuuangushe huu ni kuumegua nguzo zake muhimu.

Operesheni megua itaendeshwa na wazaendo wenyewe. Haitagharimu hata senti kumi lakini itahitajai umakini na kujitolea kulikotukuka. Operesheni hii itafanyika katika kila jimbo.Zanzibar ina majimbo hamsini na wawakilishi hamsini pia. Shida yetu juu ya hili sio wabunge bali ni Wawakilishi. Kwa vile katiba ya Zanzibar inaruhusu wananchi kupiga kura ya maoni juu ya kila mabadiliko ya katiba Operesheni MEGUA itakitumia kipengee hiki kukusanya maoni ya wananchi katika kila Jimbo kuhusu jambo moja moja la Muunagano ambalo wananchi hawalitaki. Tutaandaa barua rasmi (Muundo na kiambatisho kitawekwa hapa baada ya wazo hili kupitishwa na wazalendo) itakayaopelekwa kwa mwakilishili wa kila jimbo baada ya kupata ridhaa za wanajimbo na sahihi zao kuhusu kukubali au kukataa jambo Fulani la Muungano.

Baada ya maoni ya wananchi katika kila jimbo yakipata kuungwa mkono barua hiyo na dodoso yenye orodha ya wanajimbo walio wengi kutia saini kutokubali suali hilo kinachofuata hapo ni kumpa barua hiyo na dodoso Mwakilishi na kumtaka alifikishe wazo lile au hoja hile jumba la kutungia sheria huko Mbweni; yaani Baraza la wawakilishi. Zoezi hili litakuwa gumu lakini likisimaiwa vizuri linaweza kuleta athari kubwa sana katika jamii zetu. Itakapofikia hatua tukapata angalau majimbo 30 tu yakafanikisha zoezi hili na barua hizo kuwasilishwa mikononi mwa Wawakilishi huku baadhi ya kopi zikiwekwa kama kumbukumbu kwa taasisis za kiraia na zile za Kimataifa basi utakuwa tumefanya kazi kubwa. Kitakachobakia ni kwa Wawakilishi kusuka au kunyoa. Ni juu yao kuamua kuyafikisha maoni yetu kunakohusika au kuyakalia na kutoyafanyia kazi, ili kusubiri tuwaoneshe hasira zetu kwa kutowachagua au hata kuwaengua nyadhifa zao kwa kushindwa kutufikishia matakawa yetu kunakohusika.

Katika fomu hiyo tutaorodhesha baadhi ya mambo ya muungano ambayo kwa sasa lazima yaondolewe kama mambo ya Muungano na kuachwa kuwa chini ya nchi husika; Zanzibar na Tanganyika. Mambo kama vile TRA, bandari, Mafuta, NECTA, na Mambo ya Nje n.k yatakuwemo katika dodoso atakayoulizwa mwana jimbo na kutoa maoni yake.Lakini kabla ya huko ni nafasi yako mzalendo kutoa maoni yako juu ya hili.
Wazalendo, mnaonaje wazo hili? Linafaa? Tutaweza? Nasubiri maoni yenu. Sina mengi leo!
Wakatabahu
Nabwa
---
Zanzibar is a time bomb!.
Tena wenye akili, waushukuru Muungano vinginevyo baada ya Mapinduzi, wangeendelea kuchinjana mwanzo mwisho!.

Naifuatilia kwa keen interest hii GNU ya CCM na CUF, juzi nimetoka huko nikawa surprised, kumbe viongozi wa CUF ndani ya GNU wanatekeleza sera za CCM!.

CUF ni kama mtoto aliyekuwa akilia kwa makelele sana ndipo baba CCM akampa peremende ya GNU alambe anyamaze. CUF kalamba kanyamaza, nasubiria utamu wa peremende utakapoisha kama mwana ataendelea kunyamaza!.

Hata hao Wanzazibari wanaolalama humu kuhusu muungano hawajui watendalo kwa vile ni muungano ndio unaowapa fursa za kuyafanya wanayoyafanya kwa kukohoa na kelele nyingi, nje ya muungano hawa wange vanish into thin air (wangeshafungwa mawe shingoni na kutoswa baharini).

Wazanzibari wenye muono wa mbali, wanamshukuru Julius vinginevyo wangeachwa walivyo hawa, zamani pale pangekuwa ndio ngome ya Osama na Wamarekani wangevizamishia mbali kabisa visiwa hivi vifutike kwenye uso wa dunia! Thanks to Muungano.
---
Rugemeleza/ Chamajani Big Up bros, I cant thank you more.
To add more insult on the bleeding wound, Sosshi and Mdoandoaji have come up with evidence to deny Zanzibar Revolution. Basically, they say, Okello was sent by Christian to stop the Islam movement in Zanzibar. They further said, the overthrown of Sultan was a well orchestrated move by the western. I should admit though, the duo presented articles from different sources to substantiate their allegations, something good in any intellectual discourse. Unfortunate the evidence was biased and did not take an account that the authors are human being perhaps with their own interest.

It is a custom and tradition to celebrate Mapinduzi on 12 January since 1964. The architects of Mapinduzi some are still alive and active socially and politically, Mzee Mwinyi, Jumbe, Natepe etc few to mention. There is no doubt these old guards are committed Moslems as we have witness times and again. In this context our friends are suggesting that the 12 members of revolution council are traitors. The question is, should we celebrate Mapinduzi or not! Pandemonium 1.

Mdondoaji and Sosshi are charging with allegation that, Zanzibar could be better outside the Union Government. They may have a point so as to speak, unfortunate they fail short to answer the basic question Zanzibarian never want to answer , ' What Tanganyika is going to lose if the Union collapse today''! Pandemonium 2.

We all have an obligation to be candid when discussing issues touching our society. Babel and pandemonium is not an answer iota. If European are coming together for the common purpose we need to find a formula to excel the already milestone we have made.
The onus to nurture or kill the union remains to Zanzibar as the big loser. Whether the referendum or new constitution in the offing will answer the question, we have to wait and see
---
Baada ya Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Jamhuri yetu kutamka bayana katika Bunge kuwa Zanzibar sio nchi, kulikuwa na mjadala mkali kutoka kwa wadau mbalimbali kuhusu usahihi wa kauli yake hiyo.

Wako watu wengi walioona kuwa kauli ya Mheshimiwa wetu huyu aliyoitamka mbele ya kadamnasi ya waheshimiwa wenzake ni sahihi kwa misingi ya katiba zetu. Aidha kumekuwa na watu wengine, wakiwamo baadhi ya Mawaziri wa SMZ na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi, waliyoyatizama mambo kwa upande wa pili wa sarafu. Kwao wao hawa, Zanzibar ni nchi kamili na kamwe haiwezi kusemwa vyenginevyo. Kila moja ya makundi haya limekuwa na sababu zake ambazo baadhi zimetolewa kwa hoja zenye mashiko na nyengine zimekuwa ni hoja za kibubusa ambazo hazina mashiko yoyote ya kielimu zaidi ya kutolewa kwa misingi ya ushabiki au jazba. Kwa maoni ya Wazanzibari waliowengi, hata Rais Kikwete hakuongeza jipya lolote pale alipolihutubia bunge na kuzungumzia kadhia hii zaidi ya kuongeza petroli katika moto unaowaka au kupigilia msumari katika kidonda kibichi kinachovuja damu!

Vyovyote iwavyo, Katiba ya Jamhuri ya Muungano inatamka bayana kuwa Zanzibar ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hata hivyo, Katiba hii haikutamka hili kwa bahati mbaya au kwa kukosewa kama baadhi ya watu wanavyoamini. Katiba hii imetungwa; na walioiandika walijua lengo lao tangu mwanzo wa uandishi wao na walihakikisha wanalikamilisha. Ikitathminiwa tangu awali inaweza kubainika wazi kuwa hakukuwa na nia njema kutoka upande wa Tanganyika katika kuunda na kuuendeleza Muungano huu wa Tanganyika na Zanzibar.

Mwalimu Nyerere mwenyewe katika miaka ya mwisho wa 1950 aliwahi kunukuliwa akisema kuwa lau angeweza kuvisukuma nje ya bahari ya hindi visiwa vya Zanzibar basi angefanya hivyo kwa jinsi vinavyomkera na asivyopenda kuviona vinastawi na kunawiri (Smith, William E. 1973 uk 121). Kwa vile ni dhahiri kuwa asingeweza kutekeleza kusudio lake hilo, ndipo alipotafuta kila mbinu ili angalau basi Zanzibar isiwe nchi huru yenye mamlaka yake inayojitegemea. Katika kukamilisha azma yake hiyo, ndipo alipobuni mpango wa kuifanya Zanzibar kuwa ni sehemu ya Tanganyika chini ya kitambaa cha Muungano. Kwa bahati mbaya sana Mzee Karume kwa wakati ule hakuweza kung'amua haraka nia mbaya hii ya Tanganyika na viongozi wake kwa Zanzibar na hivyo akajikuta anacheza ngoma asiyoitambua kwa kuiweka rehani Zanzibar na maslahi yake .

Watu wanaweza kushangaa ni kwa vipi Mwalimu Nyerere, kiongozi anayeonekana 'mtakatifu' mbele ya macho ya baadhi ya watanganyika asemwe kuwa hakuwa na nia njema na Zanzibar hasa pale suala la muungano linapohusika. Ukweli huu unadhihirika wazi iwapo itatathminiwa ushiriki wa Nyerere tangu mwanzo wa harakati za muungano hadi pale alipofariki. Historia inajionyesha wazi kuwa kabla ya Muungano Zanzibar ilikuwa ni nchi inayojitegemea na yenye mamlaka yake kamili ' independent and sovereign state'.

Makubaliano ya Muungano ‘Articles of Union' yaliyosainiwa mwaka 1964 ni mkataba wa kimataifa ‘international treaty' unaotambuliwa na Vienna Convention on the Law of Treaties. Makubaliano hayo ya Muungano yalikuwa juu ya mambo kumi na moja tu ambayo ndiyo yaliyokubaliwa kuwa mambo ya muungano. Mihimili ya utendaji na kutunga sheria ya Zanzibar (Zanzibar Executive and Legislature) ilikosa mamlaka ya kisheria juu ya mambo hayo kumi na moja tu. Nje ya mambo yale kumi na moja Zanzibar ilikuwa na mamlaka yake kamili ya kusimamia na kushughulikia mambo yote mengineyo. Hii ndiyo sababu Makubaliano ya Muungano yalibakisha separate executive and legislature kwa Zanzibar zilizotakiwa kuundwa kwa mujibu wa sheria za Zanzibar na ambazo zina mamlaka ya kusimamia na kushughulikia mambo yote ambayo si ya muungano kwa Zanzibar. Mambo haya yanamaanisha kuwa Makubaliano ya Muungano yamebakisha kiwango fulani cha utaifa ‘sovereignty' kwa Zanzibar juu ya mambo yake yote yasiyo ya muungano.

Mashaka yote katika Muungano huu unaoweza kufananishwa na muungano wa paka na panya yameanzia katika Sheria ya Muungano yaani 'Acts of Union, No. 22 of 1964'. Ikilenga kuridhia na kurasimisha Makubaliano ya Muungano, Sheria hiyo ya Muungano ilitoa mwanya wa kuvurugwa Muungano na kuonewa aliye dhaifu na mdogo. Kwa hakika Sheria hii imeweka jiwe la msingi kwa mipasuko yote ya kikatiba iliyofuatia katika muungano wetu. Ni sheria hii ndiyo iliyodhihirisha bayana nia mbaya ya Tanganyika na viongozi wake kwa mustakabali wa Zanzibar. Sikusudii kuonyesha kila jambo lililokwenda kinyume na spiriti ya Makubaliano ya Muungano katika sheria hii.

Bali kwa mukhtasari, kifungu cha 8 cha sheria hii kwa mfano kilimpa mamlaka Rais wa Jamhuri ya Muungano kupitisha na kutoa ‘Decrees'. Ijapokuwa ni kweli kuwa Ibara (III) ya Makubaliano ya Muungano inaelezea kuwa wakati wa kipindi cha mpito Jamhuri ya Muungano ingeongozwa kwa Katiba ya Tanganyika iliyorekebishwa ili kukidhi matakwa ya Makubaliano ya Muungano lakini kwa vyovyote vile Ibara hii haikumpa madaraka yoyote Rais kupitisha na kutoa Decrees. Rais alikuwa na madaraka kwa mujibu wa Ibara (V) (b) ya Makubaliano ya Muungano kutoa ‘oder' ya kuifanya itumike hadi Zanzibar sheria yoyote iliyohusu jambo la muungano. Haikubaliki kulitafsiri neno ‘order' lililotumika katika Ibara (V)(b) ya Mapatano ya Muungano kumaanisha ‘Decree' hasa kwa vile Decree zilizotolewa na Rais zilikuwa na hadhi ya kikatiba wakati presidential order zingekuwa na hadhi ya azimio la kiutendaji yaani 'executive declaration' tu.

Kufuatia kifungu 8, Rais wa Jamhuri wa wakati ule (Nyerere) alipitisha Decrees chungu nzima ambazo hazikuwiva pamoja wala kwenda sambamba na makubaliano ya Muungano. Kwa mfano, katika G.N. 245 ya 1964 Nyerere alitoa Decree iliyoitwa Transitional Provisions Decree ambayo iliibatiza Serikali yote ya Tanganyika na kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano. Athari ya kwanza ya ‘Decree' hii ni kuviza muundo wa shirikisho uliotazamiwa na kukusudiwa na Makubaliano ya Muungano. Lakini pia, kuichanganya Serikali ya Tanganyika ndani ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano kumeyachanganya mambo yasiyo ya Muungano ya Tanganyika ndani ya eneo la Jamhuri ya Muungano na, hivyo, kuifanya Tanganyika na Jamhuri ya Muungano kuwa ni pande mbili za sarafu moja!

Mhimili wa utoaji haki (mahkama) mathalan kamwe haukuingizwa wala kufanywa kuwa ni jambo la muungano (haumo kwenye Makubaliano ya Muungano) na hivyo kuufanya kila upande wa Muungano uwe na mfumo wake wa sheria na mahkama yake iliyo huru kutoka nyenziwe. Bali kutokana na kuchanganywa mambo kimakosa kile kilichopaswa kuwa Mahkama kuu ya Tanganyika sasa kinaitwa Mahkama kuu ya Jamhuri ya Muungano. Hili ni koseo kubwa hasa kwa kuwa kila inapotajwa Mahkama ya Jamhuri ya Muungano katika sheria mbalimbali imekuwa ikitafsiriwa kuwa ni Mahkama ya Tanzania Bara na kwamba Mahkama za Zanzibar hazina mamlaka mlingano au 'concurrent jurisdiction' kushughulikia jambo hilo.

Mfano uliowazi upo katika kesi ya Jina Khatib Haji v Juma Sleiman Nungu [1986] L.R.C ambapo ilielezwa na Mahkama kuwa kwa vile sheria ya Uchaguzi ya Jamhuri ya Muungano imeipa mamlaka Mahkama kuu ya Jamhuri ya Muungano kusikiliza petition za uchaguzi hivyo Mahkama kuu ya Zanzibar haina mamlaka ya kusikiliza kesi hizo hata kama itahusu uchaguzi wa wabunge katika majimbo ya Zanzibar!

Kama kwamba haitoshi, Transitional Provisions Decree pia imeeleza kuwa kila mtu aliyekuwa anashikilia Afisi katika ajira ya Jamhuri ya Tanganyika atahesabika kuwa anashikilia Afisi inayofanana na hiyo katika Jamhuri ya Muungano. Athari ya hili ni kuwa watumishi wote wa Serikali ya Tanganyika wakawa ni watumishi wa Jamhuri ya Muungano hata kama Afisi zao hazihusu mambo ya Muungano. Hata sheria zilizosimamia mambo ya ajira na utumishi serikalini ambazo awali hazikuwa za muungano nazo kinyemela zikawa ni sheria za muungano kwa kuwa utumishi katika serikali ya Jamhuri ya Muungano sasa limepewa hadhi ya kuwa jambo la Muungano.

Hata Wizara ambazo si za mambo ya Muungano kwa upande wa Tanganyika nazo sasa zaitwa kuwa Wizara za Jamhuri ya Muungano. Jambo hili limewapa madaraka kwa mlango wa nyuma Mawaziri wanaosimamia Wizara zisizo za Muungano kwa Tanganyika kushughulikia baadhi ya mambo ambayo si ya Muungano hadi Zanzibar! Kwa Mfano Waziri anayeongoza Wizara ambayo si ya Muungano kwa upande wa Tanganyika anapokwenda katika mikutano ya kimataifa kuiwakilisha Tanzania hivi huwa anaiwakilisha Tanganyika au Tanzania nzima ikiwemo Zanzibar. Maana wawapo kule ughaibuni hujinasibu kuwa wao ni Mawaziri katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano kwa mfano Mimi ni Waziri wa Kilimo na Mifugo wa Jamhuri ya Muungano wakati mambo hayo siyo katika mambo ya Muungano.

Halkadhalika, kuosekana kwa Mfuko Mkuu tofauti kwa mambo yasiyo ya muungano kwa Tanganyika nalo limekuwa ni tatizo jengine. Kwa msingi huu, hata tanganyika inapotaka kutumia fedha kwa idara na taasisi zake zisizo za muungano basi fedha hizo hutolewa kutoka katika hazina na Mfuko Mkuu wa Muungano. Jambo hili linaipa Zanzibar unfair advantage kwa kuwa yenyewe hairuhusiwi kutumia fedha kutoka mfuko huu kwa mambo yasiyo ya muungano kwa Zanzibar. Kwa bahati mbaya, fedha zote za ruzuku na misaada zinazokuja kwa jina la Tanzania kutoka nje huhifadhiwa katika mfuko huu ambao Zanzibar hainufaiki nawo na badala yake tanganyika kwa kujifanya wajanja wanazitafuna mara mbili.

Itaendelea………View attachment 21575
---
Maelezo yafuatayo yana historia nzuri sana ya muungano wetu. tafadhali tuchukue muda wetu kuyasoma:

KATIKA sehemu ya kwanza ya makala haya, tuliona jinsi Muungano wa Tanzania ulivyofikiwa kati ya Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar kuunda Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar iliyokuja kujulikana baadaye kama Tan-zan-ia, miezi sita tangu nchi hizo ziungane.

Tuliona pia mgawanyo wa madaraka chini ya Muungano huo kati ya Serikali ya Muungano na serikali za Tanganyika na Zanzibar kwa kuzingatia Hati [Mkataba] ya Muungano ya Aprili 22, 1964.

Mwisho, tuligusia juu ya malalamiko yaliyoanza kujitokeza miongoni mwa baadhi ya Watanzania juu ya marekebisho ya 10 ya Katiba ya Zanzibar yakiwamo mawili; moja ni lile la Katiba hiyo kutaja Zanzibar kuwa ni nchi yenye mipaka na yenye Serikali yake. Lingine ni lile linalompokonya Rais wa Jamhuri ya Muungano mamlaka na uwezo wa kuigawa Zanzibar katika majimbo na mamlaka ya kuteua wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya Visiwani aliyokuwa nayo, kwamba yana lengo la kubomoa na kudhoofisha Muungano.

Katika sehemu hii ya pili ya makala, tutaona kama Zanzibar ni nchi au la, yenye mamlaka ya kufanya marekebisho iliyofanya, na kama imekiuka Katiba na matakwa ya Muungano.
Kipi kiliungana, Jamhuri au nchi?

Ibara ya kwanza ya Mkataba wa Muungano na utangulizi wa Sheria ya Muungano, Namba 22 ya 1964 ziko wazi kwa hili kwa maneno yafuatayo:

..It is therefore AGREED between the Government of the Republic of Tanganyika and of the Peoples Republic of Zanzibar as follows:-

(i) The Republic of Tanganyika and the Peoples Republic of Zanzibar shall be united in ONE SOVEREIGN REPUBLIC.
Kwamba, Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar zimekubaliana kuungana kuwa Jamhuri kuu [sovereign] moja kwa jina la [Jamhuri ya] Tanganyika na Zanzibar, na kwa masharti yaliyofafanuliwa kwenye Mkataba wa Muungano, mkataba ambao ndio msingi wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano.

Sheria mbili zilizoridhia Muungano za 1964; yaani Sheria ya Tanganyika ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar Namba 22, na Sheria ya Zanzibar ya Muungano wa Zanzibar na Tanganyika, zilitambua na kuhalalisha Muungano huo kwa Masharti ya Mkataba wa Muungano ili kuupa nguvu ya kisheria kuweza kutumika katika nchi hizo.

Zilichojivua Tanganyika na Zanzibar [kama nchi huru] na kutoa kwa Muungano pekee, ni ile hadhi ya kuwa Jamhuri ili kuunda Jamhuri Kuu chini ya Mkataba wa Muungano. Kuanzia hapo hazikujulikana tena kwa jina la Jamhuri ya Tanganyika au Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, bali kama Tanganyika au Zanzibar tu, kama inavyothibitishwa na baadhi ya ibara za Mkataba huo na Sheria za Muungano; zikiwamo ibara ya 5 [Mkataba] na 2 [Sheria] zenye kusomeka: Sheria za Tanganyika [sio Jamhuri ya Tanganyika] na zile za Zanzibar [sio Jamhuri ya Watu wa Zanzibar kama zamani] zilizopo zitaendelea kuwa na nguvu katika nchi hizo; au ile ibara ya 7 iliyompa mamlaka Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kuitisha Mkutano wa Katiba wenye Wajumbe kutoka Tanganyika na Zanzibar. Hakuna mahali inapotajwa ama katika Mkataba wa Muungano, au katika Sheria za Muungano kwamba baada ya kuundwa kwa Jamhuri ya Muungano, Tanganyika na Zanzibar zitafutwa au zitajifuta.

Nchi inaweza kuwa huru lakini si lazima iwe Jamhuri. Nchi huru bila kuwa Jamhuri maana yake ni kuwa chini ya himaya/uongozi au usimamizi wa Taifa au Serikali nyingine ya juu yenye nguvu zaidi.

Kwa mfano, Tanganyika ilipata uhuru Desemba 9, 1961 chini ya Katiba ya Uhuru ya 1961 iliyotungwa kwenye Ofisi ya Makoloni nchini Uingereza [London], na kutiwa sahihi na Malkia wa Uingereza. Chini ya Katiba hiyo, Tanganyika huru iliongozwa na Waziri Mkuu chini ya Gavana wa Uingereza akimwakilisha Malkia wa Uingereza kusimamia mambo kadhaa ambayo Serikali ya Wazalendo haikupewa mamlaka, lakini bado iliitwa nchi huru.

Ni pale tu ilipopigania haki ya kuwa Jamhuri, kwa maana ya Serikali na utawala wa nchi kuwa chini ya wazalendo kikamilifu chini ya Katiba ya Jamhuri ya 1962; ndipo Tanganyika ilipopata hadhi ya kuwa Jamhuri ya Tanganyika, na Gavana, Richard Turnbull, akaondoka nchini.

Vivyo hivyo kwa Zanzibar. Nchi hii ilipata uhuru wake Desemba 9, 1963 chini ya Serikali [ya mseto] iliyoundwa na Vyama vya Zanzibar Nationalist Party [ZNP] na Zanzibar and Pemba Peoples Party [ZPPP] ikiongozwa na Waziri Mkuu, kwa kuzingatia Katiba ya Uhuru kwa misingi ya makubaliano ya Lancaster House kabla ya uhuru.

Kwa misingi hiyo hiyo kama ilivyokuwa kwa Tanganyika, Zanzibar huru haikuwa Jamhuri mpaka yalipofanyika Mapinduzi, Januari 12, 1964, yaliyongoa Serikali mpya madarakani na Sultani ambaye alikuwa bado mtawala wa kilele, kama alivyokuwa Malkia wa Uingereza kwa Tanganyika huru kabla ya Jamhuri. Kufuatia Mapinduzi hayo, Zanzibar ilipata hadhi ya kuwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar.

Kwa hiyo, wakati zinaungana, Tanganyika na Zanzibar zilikuwa nchi huru na zenye Jamhuri, na pale zilipokamilisha Muungano kwa kutoa sadaka hadhi yake ya Jamhuri kwa Muungano, zilibakia nchi huru bila Jamhuri, zikajiongoza kwa Sheria zake pamoja na Katiba, huku dola ikihamia kwenye Serikali ya Jamhuri ya Muungano.

Muundo huu wa Serikali si mpya, hususan, kwa nchi za Jumuiya ya madola [Commonwealth]. Mfano mwingine mzuri ni nchi za Canada na Australia ambazo licha ya kuwa na Serikali zenye mamlaka chini ya Waziri Mkuu, lakini ziko chini ya Malkia wa Uingereza kwa sababu hazijawa Jamhuri.

Hata nchi kama Kenya; baada ya kupata Uhuru 1963, Rais wake, hayati Jomo Kenyatta, alipenda sana nchi yake isiwe Jamhuri, bali ibakie kama nchi huru chini ya Malkia wa Uingereza na yeye akiwa Waziri Mkuu na kiongozi wa Serikali ya Kenya. Alibadili mawazo na msimamo huo baada ya kushinikizwa na wanamapinduzi/wanaharakati kama hayati Tom Mboya, ndipo Kenya ikawa Jamhuri, na yeye [Kenyatta] akawa Rais Mtendaji wa Kenya.

Kwa mfumo huo, kulikuwa [hadi sasa] na Serikali tatu: Serikali ya Jamhuri ya Tanganyika na Zanzibar [ibara ya 1 na 4, ya Mkataba wa Muungano], Serikali ya Tanganyika [ibara ya 3 na 5], na serikali ya Zanzibar [ibara ya 3 (a) na 5]. Tofauti na Serikali za Tanganyika na Zanzibar, Serikali ya Jamhuri ya Muungano iko juu ya zote kwa sababu ni Jamhuri; na ndiyo pia inayobeba dola kuu kwa kuzipokonya Serikali hizo uwezo wa kujiamlia baadhi ya mambo makuu ya ndani, yanayojulikana kama Mambo 11 ya Muungano, tuliyoyataja katika sehemu ya kwanza ya makala haya, ambayo ndiyo yanayounda mamlaka ya Jamhuri ya Muungano.

Muundo upi wa Muungano uliokusudiwa?
Kwa kuwa Muungano haukuvunja Serikali za Tanganyika na Zanzibar, ni upi kati ya miundo minne inayotatiza, uliokusudiwa: Muungano wenye Serikali moja, Serikali mbili, Serikali tatu au Shirikisho?

Jibu la swali hili linaweza kupatikana kwa kutazama tu dhamira ya Waasisi wa Muungano kabla ya kuungana.

Dhamira kuu ya jumla kwa Viongozi wote wa nchi za Afrika Mashariki Tanganyika, Kenya na Uganda kabla na baada ya uhuru, ilikuwa ni kuunda Shirikisho la Afrika Mashariki kama hatua moja ya kufikia Shirikisho la Afrika. Mtetezi mkubwa wa Umoja wa Afrika kwa njia au mfumo wa kuanza na miungano ya kikanda [Shirikisho la nchi] alikuwa Mwalimu Julius K. Nyerere, akichuana vikali na Rais wa Ghana, Dakta Kwame Nkrumah, aliyeona Miungano midogo midogo ya kikanda au Shirikisho, ilikuwa ni kupoteza muda na kutaka Afrika iungane mara moja kabla Viongozi wa Afrika mpya hawajanogewa madaraka wakaona vigumu kuachia ngazi kwa Shirikisho.

Kuthibitisha kwamba aliamini alichotetea, Nyerere alinukuliwa wakati mmoja akisema, alikuwa tayari kuchelewesha uhuru wa Tanganyika [1961] hadi Kenya na Uganda zipate uhuru ili waweze kuungana kuunda Shirikisho la Afrika Mashariki.

Dhamira ya Nyerere juu ya aina ya Serikali ya Muungano aliyotaka ilijitokeza wazi kwenye Mkutano wa pili wa nchi huru za Afrika [OAU] mjini Cairo, Julai 1964 alipokataa kata kata kwa nguvu ya hoja, Muundo wa Serikali moja kuwa haufai kwa nchi za Kiafrika.

Miezi michache baadaye, alielezea msimamo wake huo kwa njia ya makala ndefu katika jarida la African Forum [The Nature and Requirements of African Unity in Africa] Vol.1, 1965 pg. 46, na kunukuliwa pia katika kitabu chake Freedom and Unity, uk. 300 304, akisema:

Muungano unaotakiwa si wa kuunda Taifa [state] moja lenye Serikali kuu moja yenye nguvu; bali ni kuunda Serikali ya Muungano yenye mamlaka ya pekee katika maeneo kadhaa ya msingi. Zaidi ya hayo, kunaweza kuwa na Serikali zingine zenye mamlaka ya pekee madogo kuliko yale ya Serikali ya Muungano, yatokanayo na Katiba za nchi hizo, na siyo kutoka Serikali kuu [ya Muungano].

Mwalimu aliendelea kufafanua: Hii, kwa tafsiri rahisi, ni muundo wa Serikali aina ya Shirikisho, ambalo madaraka yake yamegawanyika kati ya mamlaka kuu na sehemu [nchi] zinazounda Muungano huo kwa mujibu wa matakwa ya waasisi na kwa vizazi vijavyo.

Mapema kabla ya hapo, dhamira na utashi wa Wakuu wa nchi za Afrika Mashariki juu ya aina ya Muungano wa Shirikisho kuliko aina nyingine yoyote, ulidhihirika kwa njia ya TAMKO la pamoja kwenye Kikao kilichofanyika mjini Nairobi, Juni 5, 1963, kwa maneno yafuatayo:

Sisi, Viongozi wa Watu na Serikali za Afrika Masharikitunajifunga kwa kiapo [pledge] kuunda Shirikisho la kisiasa la Afrika Mashariki. Mkutano wetu wa leo unaongozwa na hamasa na utashi wa Afrika moja na sio kwa ubinafsi na matakwa ya kikanda [soma: Azimio la Shirikisho la Serikali za Afrika Mashariki, Kumb. Na. 13/931/63 PDT/1/1]
Zanzibar haikuwamo, kwa sababu wakati huo ilikuwa ikijiandaa kwa ajili ya uchaguzi Mkuu wa Julai 1963, kuelekea kupata uhuru. Lakini hata hivyo, Wakuu hao hawakuisahau Zanzibar, licha ya kwamba ilikuwa bado kwenye mchakato kuelekea Uhuru; TAMKO hilo lilisema: Ingawaje Zanzibar haikuwakilishwa katika Mkutano huu, hili tunaliweka wazi kwamba, nchi hiyo inakaribishwa kushiriki kikamilifu katika Mkutano wetu wa kuunda Shirikisho mara tu itakapomaliza uchaguzi wake mwezi ujao, Serikali yake itaalikwa kushiriki kama mshirika katika kuunda Shirikisho tunalokusudia kuunda.

Mapinduzi Zanzibar yalitibua Shirikisho
Ukweli ni kwamba, wakati Mapinduzi ya Zanzibar yakifanyika Januari 12, 1964, Wakuu wa nchi za Tanganyika, Kenya, Uganda na Zanzibar [Serikali ya ZNP/ZPPP] walikuwa mjini Nairobi kuendeleza mazungumzo ya mradi wa kuunda Shirikisho la Afrika Mashariki.

Hapa, tunaweza kuelewa kwa nini Rais Nyerere alimkaribisha mjini Dar Es Salaam, Sultani wa Zanzibar aliyepinduliwa, baada ya kukataliwa na Serikali ya Kenya kutia nanga Mombasa alikotaka kukimbilia. Inawezekana kabisa Nyerere, kwa dhamira thabiti ya kukamilisha mchakato wa Shirikisho la Afrika Mashariki, alikuwa amemkubali Sultani kama sehemu ya utawala Zanzibar, na kwamba kupinduliwa kwake lilikuwa pigo kwa mchakato huo.

Tunaweza kuelewa pia ni kwa nini Nyerere alikataa kuitambua Serikali ya Mapinduzi [hadi baada ya siku tano kupita], wakati Kenya na Uganda ziliitambua siku mbili tu kufuatia Mapinduzi. Nyerere alikataa kuitambua Serikali mpya kwa madai kwamba, hakuwa na uhakika kama ni kweli Karume alikuwa amechukua madaraka, jambo ambalo ama huenda halikumwingia kichwani, au alitaka kuhakikisha Karume ameshika madaraka badala ya Field Marshal John Okello aliyekuwa akitangaza redioni mara kwa mara kwamba yeye ndiye alikuwa Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi.

Nyerere alimkaribisha Sultani aliyepinduliwa mjini Dar es Salaam, Jumatano Januari 15, 1964 kwa kile alichokiita huruma ya kibinadamu, wakati huo wanamapinduzi Zanzibar wakiwa wameapa Sultan huyo kutokanyaga tena ardhi ya Zanzibar. Alikaa Dar Es Salaam kwa siku sita hadi Januari 20, 1964 alipokamilisha mipango yake ya kukimbilia uhamishoni London, Uingereza.

Hebu tujikumbushe kidogo jinsi tukio la Mapinduzi lilivyotibua kwa muda programu ya Mwalimu kuhusu Shirikisho kwa kukosa uhakika ni kiongozi yupi wa Mapinduzi Zanzibar ashirikiane naye kuweka mambo sawa. Kwa hili, inaonyesha dhahiri kwamba, Mwalimu hakujua mpango huo wa Mapinduzi hadi yalipotokea, vinginevyo angemtambua Karume au John Okello mara moja; na asingemkaribisha Dar es Salaam Sultan aliyepinduliwa.

Vivyo hivyo, niharakishe kutamka kwamba, Sheikh Abeid Karume hakujua mpango huo kwa sababu wanaharakati wa Mapinduzi [wa Umma Party na ASP] walimficha, kwa kuhofia kwamba angeyazuia kwa vile alikuwa mwoga na mtu asiyependa umwagaji damu. Ndiyo maana risasi ya kwanza ilipofyatuliwa usiku huo wa Mapinduzi aliogopa kwa kutojua kilichokuwa kinatokea na kukimbilia Dar es Salaam usiku huo.

Karume na Okello walijikabidhi kwa Nyerere
Jumapili usiku, Januari 12, 1964, Karume alikwenda kwa Nyerere Ikulu, naye [Nyerere] akamshauri [aache woga] arudi Unguja mara moja. Nyerere ndiyo tu alikuwa amerejea siku hiyo kutoka Nairobi kwenye kikao cha Shirikisho.
Kwa kukerwa na yaliyokuwa yakitokea Zanzibar, Jumanne, Januari 14 1964, Mwalimu alienda Nairobi kuonana na Waziri Mkuu wa Kenya, Jomo Kenyatta juu ya matukio ya Zanzibar na athari zake kwa mchakato wa Shirikisho, na kurejea Dar es Salaam siku hiyo hiyo na kumkaribisha Sultan wa Zanzibar aliyezuiwa kutia nanga Mombasa na Serikali ya Kenyatta.

Huko Zanzibar, Kiongozi wa Wapiganaji wa Mapinduzi, Field Marshall John Okello, tayari alikuwa ameunda Serikali yake na kujiteua Mkuu/Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi, na akamteua Karume kuwa Rais wa Zanzibar asiye Mtendaji. Na kupitia Redio Zanzibar ambayo alikuwa ameiteka na kuiweka chini yake, alimwita Karume bila kujua alikokuwa, akisema: Karume, popote ulipo, rudi Zanzibar haraka kuchukua nafasi yako.

Alhamis, Januari 16, 1964, Karume alikwenda kwa Nyerere mara ya pili kuomba msaada wa ulinzi wa muda, na akaahidiwa askari 300 wa Kikosi cha Kuzuia Ghasia [FFU] waliofika Zanzibar Jumamosi Januari 18, 1964 ili kurudisha amani Visiwani, na pia kumlinda dhidi ya wanaharakati waliokuwa wamepania kumwondoa madarakani kwa sababu ya kushindwa kudhibiti madaraka.

Jumapili usiku, Januari 19, 1964, huko Ikulu Dar es Salaam, Mwalimu alikuwa na mazungumzo mazito na Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibari, Field Marshal John Okello, aliyedai kwenda Dar es Salaam kwa ajili ya kupumzika kidogo, na katika mazungumzo hayo Mwalimu akamshauri afanye kazi kwa imani pamoja na Karume. Kwa maelezo hayo, bila shaka Mwalimu alimtambua Okello kama Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi, na Karume kama Rais.

Saa chache baadaye usiku huo, saa 7.50 kuamkia Januari 20, 1964 Jeshi la Tanganyika [Tanganyika Rifles TR] liliasi dhidi ya Serikali ya Nyerere; na kwa siku mbili mfululizo, Serikali hiyo ilikuwa mikononi mwa Waasi. Haielezwi ni vipi au kama wakati maasi hayo yakitokea Okello alikuwa bado [alilala] Ikulu na vipi aliweza kutoka wakati askari walioasi wakiwa tayari wameizingira Ikulu.

Maasi ya Januari 20, 1964 yaliyoitikisa Serikali ya Tanganyika, yalizikumba pia Kenya na Uganda kwa askari wake kuasi, siku hiyo hiyo, wakati huo huo wa maasi ya Tanganyika na kwa staili hiyo hiyo. Hata hivyo, maasi yote yalizimwa kwa nyakati tofauti, lakini kwa gharama kubwa kisiasa.

Nimelazimika kuelezea matukio haya kwa kirefu kutokana na mazingira yaliyojenga na hatimaye kubadili hoja na mchakato mzima wa Shirikisho la Afrika Mashariki, na badala yake kuzaa hoja ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Kwa vipi?

Mpango wa kuunda Shirikisho la Afrika Mashariki ulibuniwa na kusimamiwa na Marekani na Uingereza wakati wa harakati za Uhuru wa Tanganyika, Kenya, Uganda na Zanzibar kwa lengo la kuziweka nchi hizo ndani ya kapu moja, kuweza kuzidhibiti kwa njia ya rimoti, japo zingeendelea kujiita nchi huru.

Moja ya hofu iliyotawala Mataifa hayo makubwa enzi hizo hata kubuni mchakato huo, ni pamoja na Zanzibar kuwa kitovu cha Ukomunisti Afrika Mashariki, ambapo China na Cuba ziliweza kupenyeza sumu ya Ukomunisti kupitia wanaharakati wa Kimapinduzi wa Chama cha Zanzibar Nationalist Party [ZNP], na baadaye Chama cha Umma Party [UP], wakiwamo kina Abdulrahman Mohammed Babu, Kassim Hanga wa ASP na wengine.


Kwa hiyo, madhumuni ya kuunda Shirikisho la Afrika Mashariki yalikuwa ni pamoja na kuhakikisha kwamba, Zanzibar inajiunga na kumezwa ndani ya tumbo kubwa la Shirikisho na kukoma kuwa tishio kwa mataifa makubwa ya Kimagharibi nyakati hizo za vita baridi, kati ya mataifa ya Magharibi na mataifa ya Mashariki.

Jomo Kenyatta [Kenya] na Milton Obote [Uganda] walizigundua njama hizi za Marekani na Uingereza, na miezi miwili tu kufuatia Mapinduzi ya Zanzibar, walijitoa hima kwenye mchakato wa Shirikisho na kumwacha Nyerere mpweke, akiangalia mchakato huo ukimfia mikononi hatua za mwisho. Kenyatta alinukuliwa mahali fulani akisema, hakuwa tayari kumpigia magoti Nyerere.

Haijulikani kwa nini Kenyatta alisema maneno hayo, yenye kuashiria kwamba Nyerere alitaka kuongoza kwa nguvu Shirikisho hilo. Inawezekana hisia zake zilikuwa sahihi au hapana; lakini Mwalimu amekaririwa katika mahojiano kati yake na Mhariri Mkuu wa jarida la Africa Forum [Vol.1, No. 1] la 1991, Ad Obe Obe akisema, hakuwa na tamaa ya kuwa Kiongozi wa Tanganyika; ila alitamani kuiwakilisha Afrika Mashariki kama nchi kwenye Umoja wa Mataifa. Je, hilo ndilo lililomkoroga Kenyatta, ikizingatiwa kwamba Kenyatta huyo huyo, ambaye siku chache tu, ndiye aliyeonesha nia ya nchi yake huru kuendelea kuwa chini ya himaya ya Uingereza?

Na kwa kuwa azma ya Marekani na Uingereza, ya kuona Zanzibar inamezwa ndani ya tumbo kubwa ilikuwa pale pale, mpango na mkakati mbadala wa kuziunganisha Tanganyika na Zanzibar ukasukwa chini ya uratibu wa Mataifa hayo mawili.

Kwa kuanzia, Mwalimu Nyerere alituma Zanzibar ujumbe wa watu wawili Bibi Titi Mohamed [Mjumbe wa NEC ya TANU na Naibu Waziri] na Oscar Kambona [Waziri wa Mambo ya Nje], kwenda kumuomba Karume akubali nchi zao ziungane; lakini Karume alikataa kata kata kwa madai kwamba, alitaka kuweka kwanza nyumba [nchi] yake sawa kabla ya kufikiria jambo kama hilo.

Kabla ya kuondoka Zanzibar, Kambona na Bibi Titi walionana na Viongozi wa Zanzibar wenye ushawishi mkubwa Visiwani, Saleh Saadallah na Kassim Hanga, na kuwaachia jukumu la kumshawishi Karume akubali Muungano.

Ujumbe huo ulifuatiwa na ujumbe wa pili, wa Mawaziri Tewa Said Tewa na Job Lusinde. Hatujui Mawaziri hao walirudi na ujumbe gani kwa Nyerere kutoka kwa Karume; lakini Aprili 21, 1964, Karume, baada ya mazungumzo kwa njia ya simu na Nyerere siku hiyo, aliondoka ghafla Zanzibar kwa siri kwenda Dar Es Salaam kukutana na Nyerere, akifuatana na Maafisa Usalama wawili tu na Msaidizi wake, bila Wazanzibari wengi kujua, na kurejea Zanzibar siku hiyo hiyo.
Mara tu baada ya kurejea, Karume alimwagiza Msaidizi wake, Ali Mwinyigogo, kuandaa mapokezi ya Mwalimu Nyerere aliyetarajiwa kutua Zanzibar siku iliyofuata, Aprili 22, 1964.

Licha ya kwamba madhumuni ya safari, na mambo yaliyozungumzwa kati ya Nyerere na Karume alipokwenda Dar Es Salaam Aprili 21, hayakuwa wazi; lakini taarifa za uhakika zinaonyesha kwamba, Nyerere alimtaka Karume akubali Muungano, na alipoendelea kukaidi, Nyerere alitishia kuondoa askari 300 aliompa Karume kusaidia kurejesha hali ya amani Visiwani; naye [Karume], kwa kuona kwamba usalama wa Serikali yake na yeye mwenyewe ungekuwa mashakani, alisalimu amri na kukubali kuungana.

Itakumbukwa kwamba, siku tatu kabla ya Karume kuitwa na Nyerere, Dar Es Salaam, Nyerere alikuwa amemwita Mwanasheria wake Mkuu [AG], Roland Brown, na kumwagiza aandae kwa siri kubwa, rasimu ya Mkataba wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwa Muundo wa uhusiano kama ule kati ya Uingereza na Ireland; naye [Brown] akafanya hivyo.

Huo ndio Mkataba wa Muungano ambao Nyerere na ujumbe wake, alitua nao mkononi Zanzibar, Aprili 22, 1964; na kutiwa sahihi kati yake na Karume siku hiyo hiyo kuashiria kuundwa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Walioshuhudia wino ukimwagwa kuthibitisha fungate ya ndoa hiyo, walikuwa ni pamoja na Mawaziri Bhoke Munanka, Job Lusinde na Oscar Kambona, kwa upande wa Tanganyika; na Abdallah Kassim Hanga, Abdulaziz Twala na Ali Mwinyigogo, kwa upande wa Zanzibar.

Mambo muhimu Yaliyomo katika Mkataba, pamoja na Katiba iliyozaliwa kwa msingi wa Mkataba huo, nimeyaelezea mapema katika makala haya. Ni kwa kuzingatia matakwa ya Mkataba huo wa Muungano, sasa Wazanzibari wameweza kufanyia marekebisho Katiba yao ya 1984, huku baadhi ya marekebisho yakizua tafrani miongoni mwa Watanzania kwamba yamekiuka matakwa na Katiba ya Muungano. Ni yapi hayo? Kuna ukweli gani kwamba marekebisho hayo yamedhihaki misingi ya Muungano?
---
Wakuu

Kwa sisi tuliofika pemba na Unguja wala sio siri Wazanzibar hawauhitaji Muungano huu maana hauna faida kwao
Na ukisema leo hii wapige kura hakuna mzanzibar ambae anauhitaji muungano huu tulionao
Naona kwa afya ya Taifa kifanyike kitu ili kunusuru hii hali maana sina imani ya amani yetu miaka ijayo.

Labda tuunde katiba mpya ambapo bara mkuu wa serikali awe waziri mkuu na visiwani mkuu wa serikali awe waziri mkuu wa kutokea huko halafu tuwe na Rais wa Jamhuri ambae atakua kiongozi tu kiprotokali lakini kila nchi iwe na mamlaka kamili bila kuingiliwa na zanzibar iwe na kiti umoja wa mataifa. Na iwe mwanachama wa mashirika ya kimataifa hii naona itasaidia sana.


ZAIDI UNASHAURIWA KUSOMA MADA HIZI:
= > Lipo wapi tatizo kwenye muungano wa Tanganyika na Zanzibar? Tafakari!

= > Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni sawa na Muungano wa Siria na Ejibti walioungana 1958

= > Waliohoji uhalali wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar wafikia hatua gani?
 
Mimi naona yalikuwa ya kale na sasa hatuna faida kabisa

Tuliambiwa kuwa Tanzania ina mikoa 25 yaani 20 bara na mitano visiwani. hili jambo siku hizi halisikiki, nadhani mkoa wa Manyara ulisha ongezeka. Labda tukumbushane kwa sasa Tanzania ina mikoa mingapi. Ila nachojua mambo ya mikoa kwa sasa sio deal maana yake
  • Wana wimbo wa taifa
  • Wana bendera yao
  • Wana Jeshi
Nashindwa kujua, kwanini tunaendelea kudanganyika wakati mambo yamebadilika bila kutuhusisha sisi wadau?
Ninachojua wameamua kufaidi mambo ya muungano wakati ya kwao wanakula wenyewe. Subiri baada ya uchaguzi ndiyo utasikia Mbunge wa CCM ameshinda kwa kura 36 kati ya kura 40 zilizo pigwa. kwanini uwakilishi usiwe sawia na ule wa Tanzania bara?

Kweli twaliwa kwa muungano. Mie siu-mind kabisa.
 
Muungano una faida zake na nyingi zimekwishapatikana na kuonekana

Muungano una matatizo yake mengine yanajulikana na yanawezekana kumalizwa

Muungano upelekwa kwa wenye nchi, mkataba uchunguzwe upya kwa maslahi ya pande mbili

wakati ni huu,
 
Tunahitaji kutafakari sana kwa hili, Mzee wetu aliwahi kusema kuwa muungano umesaidia usalama kwa bara.
Kwa sasa jama hawa mamwinyi wana kila kitu chao kuanzia bendera, wimbo, rais, na mambo mengine mengi. In Short if we were to vote today then i would vote for a big NO. na sitabadili huu msimamo. Tuachane nao tu manake maandamano kibao hasa ule ugonvi wa deposits za mafuta yalogunduliwa. Katika bajeti ya taifa nadhani wanapata mgao mara mbili kutoka muunganoni na mapinduzini!
 
Muungano una faida zake na nyingi zimekwishapatikana na kuonekana

Muungano una matatizo yake mengine yanajulikana na yanawezekana kumalizwa

Muungano upelekwa kwa wenye nchi, mkataba uchunguzwe upya kwa maslahi ya pande mbili

wakati ni huu,

Wanashindwa kutafakari huu muungano, waulize huo wa EAC itakuwaje? Nchi hii inaongozwa na vilaza yaani hawafahamu 1+1=2 or more.
 
Rev. Kishoka, faida za muungano zipo nyingi sana kuliko hasara.siku zote umoja ni nguvu. Lakini hatuwezi kuona faida kubwa za muungano hadi kwa bahati mbaya tutengane, wajerumani ukiwauliza leo watakwambia faida nyingi sana za muungano .sikatai kuna baadhi ya viongozi wetu hawasimamii ipasavyo mambo ya muungano na baadhi ya vipengele vya muungano vyahitaji kurekebishwa.haya ni mawazo yangu binafsi.
 
Inaukuwaje mnakuwa na majibu yasiyo na hoja wala kujenga hoja, bali ni majibu alimradi umejibu?

Kama kuna Faida, zitaje hizo faida kwa kina si kusema kuna faida nyingi sana, maana kama kuna faida nyingi sana, kwa nini mpaka leo hii kuna kero za muungano na hakuna mwenye kuthubutu kuzifanyia kazi?
 
Muungano umejengwa asilimia mia moja kwa msingi wa serikali MBILI ZA CCM, lakini toka lini CCM ikawa na ufanisi wa mambo ya wananchi. CCM yenyewe imejengwa ktk misingi ya ubinafsi, ufisadi na ubabaishaji. Muungano haiwekani ukawa mzuri chini CCM, labda ondoa hiyo kitu CCM. Hata ukaunganisha ikawa nchi moja na serikali moja badala ya ilivyo sasa nchi moja na serikali mbili, bado choko choko toka wanaCCM wa mkoa wa UNGUJA NA PEMBA hazitakoma.
 
Baada ya Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Jamhuri yetu kutamka bayana katika Bunge kuwa Zanzibar sio nchi, kulikuwa na mjadala mkali kutoka kwa wadau mbalimbali kuhusu usahihi wa kauli yake hiyo.

Wako watu wengi walioona kuwa kauli ya Mheshimiwa wetu huyu aliyoitamka mbele ya kadamnasi ya waheshimiwa wenzake ni sahihi kwa misingi ya katiba zetu. Aidha kumekuwa na watu wengine, wakiwamo baadhi ya Mawaziri wa SMZ na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi, waliyoyatizama mambo kwa upande wa pili wa sarafu. Kwao wao hawa, Zanzibar ni nchi kamili na kamwe haiwezi kusemwa vyenginevyo. Kila moja ya makundi haya limekuwa na sababu zake ambazo baadhi zimetolewa kwa hoja zenye mashiko na nyengine zimekuwa ni hoja za kibubusa ambazo hazina mashiko yoyote ya kielimu zaidi ya kutolewa kwa misingi ya ushabiki au jazba. Kwa maoni ya Wazanzibari waliowengi, hata Rais Kikwete hakuongeza jipya lolote pale alipolihutubia bunge na kuzungumzia kadhia hii zaidi ya kuongeza petroli katika moto unaowaka au kupigilia msumari katika kidonda kibichi kinachovuja damu!

Vyovyote iwavyo, Katiba ya Jamhuri ya Muungano inatamka bayana kuwa Zanzibar ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hata hivyo, Katiba hii haikutamka hili kwa bahati mbaya au kwa kukosewa kama baadhi ya watu wanavyoamini. Katiba hii imetungwa; na walioiandika walijua lengo lao tangu mwanzo wa uandishi wao na walihakikisha wanalikamilisha. Ikitathminiwa tangu awali inaweza kubainika wazi kuwa hakukuwa na nia njema kutoka upande wa Tanganyika katika kuunda na kuuendeleza Muungano huu wa Tanganyika na Zanzibar.

Mwalimu Nyerere mwenyewe katika miaka ya mwisho wa 1950 aliwahi kunukuliwa akisema kuwa lau angeweza kuvisukuma nje ya bahari ya hindi visiwa vya Zanzibar basi angefanya hivyo kwa jinsi vinavyomkera na asivyopenda kuviona vinastawi na kunawiri (Smith, William E. 1973 uk 121). Kwa vile ni dhahiri kuwa asingeweza kutekeleza kusudio lake hilo, ndipo alipotafuta kila mbinu ili angalau basi Zanzibar isiwe nchi huru yenye mamlaka yake inayojitegemea. Katika kukamilisha azma yake hiyo, ndipo alipobuni mpango wa kuifanya Zanzibar kuwa ni sehemu ya Tanganyika chini ya kitambaa cha Muungano. Kwa bahati mbaya sana Mzee Karume kwa wakati ule hakuweza kung'amua haraka nia mbaya hii ya Tanganyika na viongozi wake kwa Zanzibar na hivyo akajikuta anacheza ngoma asiyoitambua kwa kuiweka rehani Zanzibar na maslahi yake .

Watu wanaweza kushangaa ni kwa vipi Mwalimu Nyerere, kiongozi anayeonekana ‘mtakatifu' mbele ya macho ya baadhi ya watanganyika asemwe kuwa hakuwa na nia njema na Zanzibar hasa pale suala la muungano linapohusika. Ukweli huu unadhihirika wazi iwapo itatathminiwa ushiriki wa Nyerere tangu mwanzo wa harakati za muungano hadi pale alipofariki. Historia inajionyesha wazi kuwa kabla ya Muungano Zanzibar ilikuwa ni nchi inayojitegemea na yenye mamlaka yake kamili ' independent and sovereign state'.

Makubaliano ya Muungano ‘Articles of Union' yaliyosainiwa mwaka 1964 ni mkataba wa kimataifa ‘international treaty' unaotambuliwa na Vienna Convention on the Law of Treaties. Makubaliano hayo ya Muungano yalikuwa juu ya mambo kumi na moja tu ambayo ndiyo yaliyokubaliwa kuwa mambo ya muungano. Mihimili ya utendaji na kutunga sheria ya Zanzibar (Zanzibar Executive and Legislature) ilikosa mamlaka ya kisheria juu ya mambo hayo kumi na moja tu. Nje ya mambo yale kumi na moja Zanzibar ilikuwa na mamlaka yake kamili ya kusimamia na kushughulikia mambo yote mengineyo. Hii ndiyo sababu Makubaliano ya Muungano yalibakisha separate executive and legislature kwa Zanzibar zilizotakiwa kuundwa kwa mujibu wa sheria za Zanzibar na ambazo zina mamlaka ya kusimamia na kushughulikia mambo yote ambayo si ya muungano kwa Zanzibar. Mambo haya yanamaanisha kuwa Makubaliano ya Muungano yamebakisha kiwango fulani cha utaifa ‘sovereignty' kwa Zanzibar juu ya mambo yake yote yasiyo ya muungano.

Mashaka yote katika Muungano huu unaoweza kufananishwa na muungano wa paka na panya yameanzia katika Sheria ya Muungano yaani ‘Acts of Union, No. 22 of 1964'. Ikilenga kuridhia na kurasimisha Makubaliano ya Muungano, Sheria hiyo ya Muungano ilitoa mwanya wa kuvurugwa Muungano na kuonewa aliye dhaifu na mdogo. Kwa hakika Sheria hii imeweka jiwe la msingi kwa mipasuko yote ya kikatiba iliyofuatia katika muungano wetu. Ni sheria hii ndiyo iliyodhihirisha bayana nia mbaya ya Tanganyika na viongozi wake kwa mustakabali wa Zanzibar. Sikusudii kuonyesha kila jambo lililokwenda kinyume na spiriti ya Makubaliano ya Muungano katika sheria hii.

Bali kwa mukhtasari, kifungu cha 8 cha sheria hii kwa mfano kilimpa mamlaka Rais wa Jamhuri ya Muungano kupitisha na kutoa ‘Decrees'. Ijapokuwa ni kweli kuwa Ibara (III) ya Makubaliano ya Muungano inaelezea kuwa wakati wa kipindi cha mpito Jamhuri ya Muungano ingeongozwa kwa Katiba ya Tanganyika iliyorekebishwa ili kukidhi matakwa ya Makubaliano ya Muungano lakini kwa vyovyote vile Ibara hii haikumpa madaraka yoyote Rais kupitisha na kutoa Decrees. Rais alikuwa na madaraka kwa mujibu wa Ibara (V) (b) ya Makubaliano ya Muungano kutoa ‘oder' ya kuifanya itumike hadi Zanzibar sheria yoyote iliyohusu jambo la muungano. Haikubaliki kulitafsiri neno ‘order' lililotumika katika Ibara (V)(b) ya Mapatano ya Muungano kumaanisha ‘Decree' hasa kwa vile Decree zilizotolewa na Rais zilikuwa na hadhi ya kikatiba wakati presidential order zingekuwa na hadhi ya azimio la kiutendaji yaani ‘executive declaration' tu.

Kufuatia kifungu 8, Rais wa Jamhuri wa wakati ule (Nyerere) alipitisha Decrees chungu nzima ambazo hazikuwiva pamoja wala kwenda sambamba na makubaliano ya Muungano. Kwa mfano, katika G.N. 245 ya 1964 Nyerere alitoa Decree iliyoitwa Transitional Provisions Decree ambayo iliibatiza Serikali yote ya Tanganyika na kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano. Athari ya kwanza ya ‘Decree' hii ni kuviza muundo wa shirikisho uliotazamiwa na kukusudiwa na Makubaliano ya Muungano. Lakini pia, kuichanganya Serikali ya Tanganyika ndani ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano kumeyachanganya mambo yasiyo ya Muungano ya Tanganyika ndani ya eneo la Jamhuri ya Muungano na, hivyo, kuifanya Tanganyika na Jamhuri ya Muungano kuwa ni pande mbili za sarafu moja!

Mhimili wa utoaji haki (mahkama) mathalan kamwe haukuingizwa wala kufanywa kuwa ni jambo la muungano (haumo kwenye Makubaliano ya Muungano) na hivyo kuufanya kila upande wa Muungano uwe na mfumo wake wa sheria na mahkama yake iliyo huru kutoka nyenziwe. Bali kutokana na kuchanganywa mambo kimakosa kile kilichopaswa kuwa Mahkama kuu ya Tanganyika sasa kinaitwa Mahkama kuu ya Jamhuri ya Muungano. Hili ni koseo kubwa hasa kwa kuwa kila inapotajwa Mahkama ya Jamhuri ya Muungano katika sheria mbalimbali imekuwa ikitafsiriwa kuwa ni Mahkama ya Tanzania Bara na kwamba Mahkama za Zanzibar hazina mamlaka mlingano au ‘concurrent jurisdiction' kushughulikia jambo hilo.

Mfano uliowazi upo katika kesi ya Jina Khatib Haji v Juma Sleiman Nungu [1986] L.R.C ambapo ilielezwa na Mahkama kuwa kwa vile sheria ya Uchaguzi ya Jamhuri ya Muungano imeipa mamlaka Mahkama kuu ya Jamhuri ya Muungano kusikiliza petition za uchaguzi hivyo Mahkama kuu ya Zanzibar haina mamlaka ya kusikiliza kesi hizo hata kama itahusu uchaguzi wa wabunge katika majimbo ya Zanzibar!

Kama kwamba haitoshi, Transitional Provisions Decree pia imeeleza kuwa kila mtu aliyekuwa anashikilia Afisi katika ajira ya Jamhuri ya Tanganyika atahesabika kuwa anashikilia Afisi inayofanana na hiyo katika Jamhuri ya Muungano. Athari ya hili ni kuwa watumishi wote wa Serikali ya Tanganyika wakawa ni watumishi wa Jamhuri ya Muungano hata kama Afisi zao hazihusu mambo ya Muungano. Hata sheria zilizosimamia mambo ya ajira na utumishi serikalini ambazo awali hazikuwa za muungano nazo kinyemela zikawa ni sheria za muungano kwa kuwa utumishi katika serikali ya Jamhuri ya Muungano sasa limepewa hadhi ya kuwa jambo la Muungano.

Hata Wizara ambazo si za mambo ya Muungano kwa upande wa Tanganyika nazo sasa zaitwa kuwa Wizara za Jamhuri ya Muungano. Jambo hili limewapa madaraka kwa mlango wa nyuma Mawaziri wanaosimamia Wizara zisizo za Muungano kwa Tanganyika kushughulikia baadhi ya mambo ambayo si ya Muungano hadi Zanzibar! Kwa Mfano Waziri anayeongoza Wizara ambayo si ya Muungano kwa upande wa Tanganyika anapokwenda katika mikutano ya kimataifa kuiwakilisha Tanzania hivi huwa anaiwakilisha Tanganyika au Tanzania nzima ikiwemo Zanzibar. Maana wawapo kule ughaibuni hujinasibu kuwa wao ni Mawaziri katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano kwa mfano Mimi ni Waziri wa Kilimo na Mifugo wa Jamhuri ya Muungano wakati mambo hayo siyo katika mambo ya Muungano.

Halkadhalika, kuosekana kwa Mfuko Mkuu tofauti kwa mambo yasiyo ya muungano kwa Tanganyika nalo limekuwa ni tatizo jengine. Kwa msingi huu, hata tanganyika inapotaka kutumia fedha kwa idara na taasisi zake zisizo za muungano basi fedha hizo hutolewa kutoka katika hazina na Mfuko Mkuu wa Muungano. Jambo hili linaipa Zanzibar unfair advantage kwa kuwa yenyewe hairuhusiwi kutumia fedha kutoka mfuko huu kwa mambo yasiyo ya muungano kwa Zanzibar. Kwa bahati mbaya, fedha zote za ruzuku na misaada zinazokuja kwa jina la Tanzania kutoka nje huhifadhiwa katika mfuko huu ambao Zanzibar hainufaiki nawo na badala yake tanganyika kwa kujifanya wajanja wanazitafuna mara mbili.

Itaendelea………

asset.php.jpg
 
Waheshimiwa JF..

Nimekuwa nikifuatilia sana masuala ya muungano. Nilichogundua ni kwamba viongozi wa Bara ndio wanaong'ang'ania huu Muunguno uendelee kuwepo, pasipo kuwa na faida yoyote kwa wakazi wa bara! Sijaona Mzanzibar hata mmoja anayeutaka huu muungano. Kwa kuthbitisha hilo angalia matukio ya kuchoma maeneo ya biashara wa watu wa bara huko Zanzibar.

Ukiangalia JK amewaweke waznz weng mno kwenye serikali yake (sisemi kwa ubaya) ili kuuridhsha upande wa pili..

Swali, Wazanzibar wanaonyesha vipi kwamba wanauhtaji muungano huu? Je, matukio ya kuchoma bar za wabara, serkal imechukua hatua gani? Je muungano una umuhmu gani, au ni kuendeleza urafiki wa Nyerere na Karume?
 
Wana JF tukiwa kama wananchi wanaohitaji kuchangia hoja nzito na zenye maslahi kwa nchi yetu, tunao wajibu wa kufahamu kwa undani jambo hili kuhusu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Kwangu mimi naona Muungano huu ni mzuri kwa malengo yaliyotafsiriwa na waasisi, LAKINI pia ni kiini macho kwa Watanganyika. Kwa sababu:

1. Zanzibar inatambulikana kimataifa kimichezo kama nchi.
2. Zanzibar ina Rais, na anaheshimika ndani na nje ya mipaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
3. Zanzibar ina Bendera ya Taifa.
4. Zanzibar ina Wimbo wa Taifa.
5. Wazanzibar wanavitambulisho kama Wazanzibar na siyo Watanzania.
6. N.k

Je, Nchi yetu Watanganyika iko wapi? Haki zetu za uraia kama watanganyika ziko wapi? Nini kifanyike hasa katika mchakato wa Katiba Mpya?

Je Muungano huu si Kiini macho kwa watanganyika? Kwanini?
JE,
 
Hata ukiwa na sifa zote hizo ulizozitaja, lakini kama hauna vyombo vya dola vya ulinzi na usalama, wewe sio dola!.

Pasco, nakubaliana na wewe lakini hoja yangu inasimamia pale muonekano na mwendelezo wa Wazanzibar katika kujaribu kujenga Taifa lao upya. Karibia haya yote niliyoyataja hapo juu, yamefanywa na Rais mstaafu wa Zanzibar Abeid Aman Karume. Kwa nini tusitarajie mengine kufanywa na hilo " ulinzi na usalama" likiwemo?

Unakumbuka wakati Karume alisusia kuhudhuria sherehe za Muungano eti kwa kisingizo cha mvua? Unakumbuka kuwa Mwafaka wa Zanzibar uliaasisiwa na Wazanzibar chini ya Rais wao wakati huo Karume kwa kukaa meza moja na upinzani kwa mazungumzo ya ... kwa nini kugombana huku sote wazanzibar? Tuungane tutawale pamoja nchi ni yetu sote. Wamefanikiwa. Kwa nini usifikiri na mengine kujitokeza? Ikiwa hivyo sisi Watanganyika tutabaki tunaitwaje?

Maana Katiba yao haitutaji!!
 
Kuna mtu aliwahi kusema wananchi wa Tanzania Bara ni Wadanganyika!! Ukitafakari sana utaona maana iliyojificha. Tatizo tulilo nalo watanzania, hatutaki kuumiza vichwa kufikiri na kubaini kitakachotokea mbeleni kwa kutumia historia za wakati uliopo na uliopita. Hii ni hatari sana.

Tutaishia kutatua mambo ambayo yasingetufika kama tungeyabaini mapema. Tabia hii ndiyo inatufanya hata sisi wanaJF tusichangie mada kama hizi. Tafadhali njooni tuchangie post hii na pengine mniodolee dukuduku nilizonazo kwa hatma ya Taifa la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania - Watanganyika na Wazanzibar.
 
Faida ya Muungano ni Wazanzibari kuishi Tanganyika na kumiliki ardhi bila Bughdha
Kujibebesha mzigo usio wa lazima.
Muungano ufe hata kesho maisha yataendelea tu.

Nijuavyo mimi, Muungano ukifa, Katiba yetu inabadilishwa. Jina la nchi na Muundo wa Serikali lazima vibadilishwe. Kwa maana nyingine, tunabadili usajili wa Jina la Taifa letu katika Ofisi za Umoja wa Mataifa. Au si hivyo??!!
 
Hata ukiwa na sifa zote hizo ulizozitaja, lakini kama hauna vyombo vya dola vya ulinzi na usalama, wewe sio dola!.
Mkuu Zanzibar ni nchi tena iliyokamilika! Lakini kweli nadhani wawe na NECTA yao bwana! kama hii ya wote bure kabisa si bora wawe na yao wanaweza kuboresha elimu yao
 
PMNBuko,

Yaani inasikitisha huku bara wanaotuongoza wasivyo kuwa na maono, kwa mfano kiongozi katika bunge ambaye anatoka Tanganyika anatangaza kwenye ukumbi wa bunge la JMT tangazo akisema wabunge wa CCM Zanzibar na CUf Zanzibar wakutane baada ya kikao hiki cha bunge, yeye haoni kuwa kuna walakini katika hilo tangazo, linatoa image gani kwenye jamii, mbona tunamatatizo makubwa katika huu muungano, hasa sisi watanganyika. Mtu anaongoza bunge kwa vijembe na mipasho utadhania MC wa kitchen party.

Ukimuuliza kiongozi hasa wa kutoka huku Tanganyika kuhusu muungano atakimbilia hata kabla ya kutfakari, nimeapa kuulinda muungano, mungano gani huo usio hojiwa utadhania umetoka kwa MUNGU kama msahafu, tunataka na sisi watanganyika ifike mahali tusikie tangazo la wabunge kukutana CCM taganyika na wapinzani tanganyika.

Habari ndio hiyo wamenza wao na sisi tumalizie.
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom