Mume wangu amempa mimba mdogo wangu

Mume wangu amempa mimba mdogo wangu

Mnaoshauri aachane na mumewe kuna mambo mawili kama si matatu:

1. Mumewe being desperate atamuoa huyo mdogo mtu (in which im not sure kama bado hajafanya hivyo) kawafukuza kwake na hajui walipokwenda. Mdogo mtu hana kazi, lazima atamtegemea shemeji mtu. Mume mtu ni mfanyabiashara, vi shilingi vya hapa na pale havimpigi chenga. In her life, she (leah) will never get away with this itakuja kuonekana ni mke alishindwa kumzalia mtoto and mume ended up eloping with her sister. Itakuuma zaidi kuliko kuachana na mumeo

2. Mtoto atakayezaliwa bado atakuwa anakupa uchungu, unless kama utakuwa na control juu ya ukuaji wake na aku acknowledge kama "mama mkubwa" point ambayo ukiachana na huyu mumeo hii heshima haitakuwepo tuu. A second thing you will not get away with it.

3. Undugu una heshima, utakapomrudisha mumeo nyumbani, utaset clear boundaries na ndugu yako kwamba una maamuzi juu ya ndoa yako kama mke wa ndoa,nafasi ambayo yeye hatakuwa nayo.

So uchaguzi bado ni wako, ila kwa upumbavu wangu naona madhara yakuachana ni ya muda mrefu na kidonda chake kitakuuma zaidi kuliko hilo lililotokea.
Don Mangi emu niambie nikamtafute nimuombe msamaha?
Maana tangu afanye ujinga wake hajawahi tamka neno nisamehe zaid ya kusema yaishe basi.
Na Mimi Nina moyo Don Mangi nasikia maumivu pia.

Mimi ninathamani hata kama ni mwanamke sistahiri kuonewa kiasi hiki.

Liwalo acha liwe but I can't take any more step ahead with this man.
 
Asante heaven sent umeugusa moyo wangu mpaka nimejikuta nalia, to be honest siwezi endelea na hii ndoa, sioni future serious na huyu mtu.

Pole sana.

1. Uliolewa kwasababu ya mapenzi uliyonayo kwake mumeo. Kama bado UNAMPENDA na yeye ANAKUPENDA kwa dhati + hana mapenzi ya dhati kwa mdogo wako na unaweza kuthibitisha hilo basi endelea naye.

2. Kinyume na hapo anza maisha yako upya. Hii dunia ina wanaume wengi sana wanaokupenda(tunaokupenda) kuliko wewe unayodhani, tatizo lenu mabinti mnakariri sana mambo.

Fuata ushauri wa wanaume zaidi, kina dada chukua pole zao, katika issue kama hii kina dada wana panick sana, atleast wale wenye age za 50 watakupa ushauri constructive.
 
Nina miaka 4 kwenye ndoa, ninaomba kwanza nikushaurii, kwanza, ndoa inayo pendeza ni ile yenye watoto au mtto ndani ya nyumba ni si masstarz ndani ya nyumba, kitendo cha kusbubiri umalize shule ndo uzae ulikosea sana, nikujuze, mfano mimi nilipotaka kuoa, nje ya kuwa na hamu ya ndoa, nilikuwa na hamu sana ya kuitwa baba, kama mke wangu niliyemuuoa angeniambia mpaka amalize shule ndo azae, hakika ningezaa na mdogo wake, nje ya ndoa)

Pili, dada, hiyo dhambi ni ya mmeo, yeye kam amekuomba msamaha, msamehe, haraka sanaaa, maana ndani ya mafundisho ya ndoa kama kweli ulifunga ndoa yeneye mafundisho hilo si jambo la kuomba ndoa ivunjwe, sjui wewe ni dhehbu gani,ila kwa wakatoliki ili halipo kabsa, mmeo yeye anatakiwa kutubu mbere ya Mungu wake na hatasamehewe.

Tatu, umejiuliza kwa nini mmeo amegegeda mdogo wako,wakati naisi we bado mbiich kbsa hata mtt mmoja hujaazaaa? kuna kitu hapo, Masstz plus owning the house can be the source, sjui kama kweli yeye anafanya biashara na wewe unasoma mastaz sjui anakiwango gani cha elimu, ila naona famiily hisyo na amani na hasa km wewe ulifunga ndoa na mtu ambaye hana kiwango km chako cha elimu alafu unamletea habari zanimalize mastaz ndo tuzae.

Nne dada point hii naomba uisome kimnya kimnya, mbona nasikia hata moja ya watu maharufu nchini na kiongozi mkubwa tu, nae amezaa na mdogo wa mkewe, tena watto wawili sio mmoja wakati mkewe bado analipa?wewe sikiza muhite mmeo, kumbuka Mungu ikupa mme mmoja mkiwa hai, akifa yeye utampata mwingine wa lkuzeeka nae km Mungu atamchukua mapema, tena nikwambie hukutakiwa ili jambo kulireta umu ndani.

ushauri, ameni ilo eneo, mwambie mdogo wako arudi kijijini, akizaa alete mtt, na wewe huyo utamlea vizuri hivi pata picha wewe ukimaliza mastaz na huszae, wakati uo mmeo kazaaa na mdogo wako si utalea damu yako?tuliza mawazo, mrudie mmeo.
Ni rahisi kusema hivyo ukiwa nje ya uhusika.
 
Mungu gani anataka wanawake wapange ratiba za lini anatka kuzaa na lini hataki?? tatizo la wanawake wengi huku kusoma kwenu kunawapotosha sana, yaani wewe uolewe alafu hapohapo upange ratiba ya kuzaa, na sio wewe tu ni wengi wanagongewa wadogo zao au beki tatu na humu pia wamo ila hizo mimba hazijaingia ndio maana wako vifua mbele kukutetea.

Hilo umelitaka mwenyewe kwa kupanga ratiba za mechi na lini uzae, ndoa changa kabisa na makalenda kibaoooooooooooo. ulitakiwa ukae na ndoa yako kwanza kisha upate kamtoto kakumliwaza mzee ndio sasa ukasome hayo madudu yako. sasa masters ukae 2 years bila kuzaa, then PhD ukae 5 years bila kugegedwa we utakuwa unawazimu sio bure.

Mliobaki sasa hili ni somo kwenu, ukiolewa angalia ndoa kwanza kiasi cha 5 years, sio leo kesho unaanza minyodo ya masters. Ukija kuona jamaa ameparamia muhudumu wa tigo pesa anaweza kuoa kabisa na wewe ukabaki na makabrasha yako ya masters.
Me naona we ndo unawazimu..kwani elimu anayosoma ni kwa ajili ya nani kama sio familia yake...nini kashindwa kufanya katika ndoa yake......we mwanaume unaita elimu madudu leo unazaa watoto unawapeleaka international school for what? Ili wapate faida gani? Madudu unayosema au? why usiwaache waolewa na wazae tu sababu kwa akili yako ndo kazi ya mwanamke...
 
kuna jamaa pale tangibovu muhaya, kazaa na mtu na mdogo wake tena watoto wa kutosha tu na bado anaendelea nao wote wawili kama mke mkubwa na mdogo.
 
Na wewe beba mimba ya mdogo wa mumeo,kama mbwai na iwe mbwai tu,akimwaga mboga na wewe mwaga ugali
 
Mimi binafsi tatizo naliona ulivyokataa kuzaa mpaka umalize masters. Mume kavumilia two years
 
1. Wewe unamakosa elimu uliyokuwa nayo ya degree ilikuwa inatosha kuzaa na baadaye kuendelea kusoma hiyo masters kutokana na wewe kusoma ulishindwa kutimiza wajibu wako japo wewe umedai ulitimiza, kwangu mimi naona hukutimiza sababu kuzaa na penyewe ni wajibu.
2. Cha kufanya mdogo wako atoe hiyo mimba ili kukulindia heshima yenu na ukoo wenu.
3. Zaa haraka sana na mme wako mwaka huu usiishe bila kushika mimba...!!
4. Fikiria hata wewe kweli miaka minne wenye ndoa bila mtoto..???? naungana na wanaume wezangu wanaowalalamikia wanawake waliosoma...!!

ANGALIZO:- Elimu zinatudanganya sana na kusahau maisha yetu ya kawaida kabisa na kwenye maelezo yako umesema wakupishe kwenye nyumba kwa sababu ni yako. hilo nalo nitatizo pia inaonekana unalingia elimu na mali yako. badilika hilo ni tatizo pia...
Sijakataa kuzaa haya tulikubaliana wote.

Pili kama alitaka mtoto kwani alitaka kutoa mimba?
 
mdogo wako alipokuita na kukuambia ukweli kwa kukuomba msamaha ulipaswa kumuelewa na kulifanyia kazi pale ulipowaita wote wawili. Ila kwa kuwaitia wazazi pande zote 2 ni wazi uliamua kuwaaibisha na kuwa vua nguo waziwazi. Ulipaswa kumuelewa mdogo wako kwann aliamua kukuelezea ukweli huku akijuta

Inawezekana sababu ya mumeo kuchepuka ni vile unavyoishi nae coz una mahitaji yote na uwezo ndo maana unampotezea na hata wazo la kupata mtoto baadae ukimaliza masomo inaonekana umempangia ww. Hivyo basi ni dhahiri kuna mengi unampangia zaidi ya hili kwani hata kielimu na kimaisha hakufikii tena ukizingatia nyumba ni yako.

Kwa nafasi ya elimu yako ulikuwa na uwezo wa kulimaliza hili jambo ulipokuwa na watuhumiwa kabla hujalipeleka juu zaidi kwa wazazi. Jitahidi kuwa mvumilivu ndani ya ndoa na kumaliza changamoto na mume wako kabla ya kupeleka nje kwa usuluhishi kwa shida na raha, matatizo na furaha.

Ndoa zina changamoto sana, usiwabebeshe mzigo wazazi wakupe ushauri wa kuachana nae.

Niwapongeze Wazazi wamekusihi sana umsamehe na muendelee na maisha ya ndoa sema HUJISIKII kuendelea kuishi na mwanaume huyo.
Mapenzi ni hisia na kama hujisikii ni bora ukae pembeni utakuja kujuta zaidi ya hivi.

Pole sana
Shule yako umeitendea haki. Salute!
 
Nimeelewa kwa nini unajiita leah2, lakini mbona huyo wajina lako pamoja na ndugue waliolewa na mwanamme mmoja!!?

Kama amekiri msamehe mmeo maisha yasonge au tayari umeshapotoshwa na wanaume wa dar!! angalia usije kuwa unaruka majivu then ukaangukia motoni

Elewa kuwa hakuna aliemkamilifu na hilo nijaribu tu, yakupasa ulishinde. Ebu rejea kiapo chenu cha ndoa

Samehe 7 X 70
mkuu achana na hizo ngonjera za 7*70! inaruhusiwa ndoa kuvunjwa kwa 7bu ya UZINIFU, sembuse huyo muasherati kazini na mdogo mtu! heshima iko wapi hapo?
 
  • Thanks
Reactions: nao
Habari za asubuhi wanajamvi,

Nimekuwa kwenye wakati mgumu kwa muda sasa.

Nimeolewa na Nina miaka miwili kwenye ndoa lakn sikuwa tayari kuzaa kwakuwa tulikubaliana mpaka nimalizie masomo yangu ya masters ambayo natarajia kumaliza mwaka huu.

Tumekuwa tunaishi vizuri tu na mume wangu nikimtii na kuwajibika kwa majukumu yangu yote kama mke kwa mumewe pamoja kuwa Ninafanya kazi na kusoma pia.

Mimi ni muajiriwa lkn mume wangu wangu ni mfanyabiashara kariakoo.

Nina mdogo wangu ambaye aligraduate mwaka jana akaomba akae kwangu wakati anatafuta kazi, sikuona shida nikamkubalia.

Tangu aje tumekuwa tukiishi vizuri tena kwa amani.

Kama Dada nilijitahidi kumtengea mdogo wangu bajeti yake toka kwenye mshahara wangu kwa kila mwenzi iliaweze kumudu kufuatilia mambo yake kirahisi.

Baada yakuwa nae kwa miaezi mitano nikaanza kuona mabadiriko kadhaa.
Akawa karibu na mume wangu sana, sikujali nikajua ni ushemeji tu.

Siku moja nilirudi nyumbani mapema sikukuta mtu.

Nikaendelea na maandalizi ya chakula cha jioni, nikiwa jikoni nikasikia sauti ya mume wangu na mdogo wangu wanabishana.

Niliposogea dirishani nisikilize vizuri huku nikichungulia nje nikaona dogo analia na mume wangu anambembeleza huku akimfuta machozi.

Nikatulia nione nini kinaendelea, nikasikia mume wangu anamwambia itabidi tuitoe maana Dada yako akijua wote tutakuwa nawakati mgumu..

Nikachukua simu yangu nikawa nawarekodi, baada ya muda wakaingia ndani nami nikajifanya sijui chchte.

Sikuwauliza chchte nikijipa muda wa kufanya utafiti zaidi.

Baada ya wiki, mdogo wangu akaniambia kuwa ana shida na Mimi.

Nikamsikiliza akaniambia kuwa ana mimba..

Sikuhamaki wala kuonyesha kama najua chchte, nilimuulize nani muhusika akajibu hajui.

Nikamwambia kama hujui sina namna ya kukusaidia siku ukijua utaniambia nijue jinsi ya kukusaidia.

Akaanza kulia na kunipigia magoti huku akisema nisamehe Dada, nikamwambia wala hujanikosea.

Nikamwambia wewe ni mtu mzima umeamua kuzaa kunashida gani?

Baba wa mtoto naamini yupo kwahiyo sikuhukumu.

Akasema, kuna jambo nataka nikwambie..
Niikamwambie aniambie..
Akasema lakini naomba unisamehe, shemeji ndo amenipa mimba.

Kwakweli niliumia sana, nikamuuliza wana muda gani tangu waanze mahusiano akajibu ni miezi minne sikujibu neno, nikaendelea na shughuli zangu.

Mume wangu alikuwa matembezi, aliporudi nikawaita wote wawili, nikamwambie Dogo aseme alichoniambia mbele ya shemeji yake.

Akasema tena ana mimba ya shemeji yake..mume wangu kusikia vile akataka kuwa mkali..

Nikamwambia hana haja ya kufoka, nikanyamaza sikusema wala kulaumu chchte.

Nikaamua kuwaita wazazi wangu na wake pia bila wao kujua,

Walipo kuja nikawambie Mimi ndiye niliyewaita lkn mume wangu na mdogo wangu ndiyo wanachakuwaambia.

Walipoulizwa wanasemaje dogo akaeleza kuwa anamimba ya shemeji yake..

Mume wangu alipoulizwa kwa unyonge sana alikubali. Wazazi wakaniuliza Nina maamuzi gani?
Nikawajibu nimeamua kumuachia mume mdogo wangu.

Wazazi wakanisihi nimsamehe na tuendelea na maisha ya ndoa..na dogo arudi kwa wazazi.

Niliwakatalia nakuwambia kuwa nisingeweza kuvumilia ndoa ya aina Ile..nikamwambia wasijipotezee muda wao kuniambia cha kufanya niliwaita waje wasikie uchafu niliofanyiwa then baada ya hapo mimi ndo nitoe maamuzi
Nilisisitiza maamuzi yangu nikutoendelea na ndoa tena.

Waliniambia nisichukue uamuzi bila kutafakari wakanipa wiki tatu za kufikiria Leo hii ni siku ya nane tangu nipewe muda wa kutafakari..

Niliwaomba niwe mbali na watuhumiwa wangu kipindi cha kutafakari.

Nikawasihisi watuhumiwa wao ndo wanipishe nyumbani kwangu, maana tunapoishi ni kwangu.

Wameondoka na sijui walipo kwenda.

Binafsi sijisikii kuendelea kuishi na huyu mwanaume ingawa kweli tumeshafunga ndoa lkn siwezi kuwa na raha ya ndoa ktk mazingira kama haya.

Najiuliza heshima yangu iko wapi?

Jamii inanionaje?

Na mtoto atayezaliwa ntamuonaje?

Naona dhambi hii ni kubwa sana siwezi kuibeba.

Wadau naomba msaada maamuzi niliyochukua naweza kuwa sahihi? Nisaidie plz.

Naomba plz sihitaji matusi wala mizaha nahitaji ushauri na faraja.

Naamini ktk wingi wamashauri hapakosi hekima.
Pole sana dada Leah.... Hili jambo ni gumu kwa binadamu Yeyote pamoja Na uamuzi uliouchukua ambao kwangu naona ni sahihi nakusihi Endelea kumuomba Mungu akupe uvumilivu kwa wakati huu mgumu kwako .usijarbu kufanya chochote kitakachokudhuru
 
Dada Leah2 pole sana kwa mtihani mgumu. Pia nakupongeza kwa kuweza kuwa jasiri na kufuatilia mambo kwa upole. Nimejifunza jambo la maana sana kutoka kwako.

Kuhusu hii ndoa yako mi naona hauna haja ya kuwaza sana. Ni kweli jamaa hakuheshim na inawezekana alikubali kufunga ndoa nawe kwa sababu za kiuchumi. Kwa ninavyoona wewe unacareer nzuri na kipato cha uhakika na hivyo huyo shemeji mume aliamua kukuoa tu juu ya hilo ila hakupendi ki ukweli.

Fanya maamuzi ya haraka ya kuachana nae kabla mtoto hajazaliwa maana akishazaliwa stori inaweza ikabadilika. Hakikisha mnaachana kisheria kabisaaa ili asikusumbue baadae. Jipe muda kidogo baada ya hili tatizo kabla hujaanziasha uhusiano mwengine.

Halafu hao wanaosema eti ulikosea kwenda kusoma ni maselfish tu. Mimi nimezaa baada ya kupata masters na immediately nilipopata mtoto nimeanza PhD. Kwa mwanamke kusoma kunahitaji kujitoa sana hasa baada ya kuwa na watoto. Kuamua kumaliza masters yako sio kigezo cha mumeo kuzaa na mdogo wako.Tena usipoangalia anao watoto wengine huko nje sema Mungu ametaka kukuonyesha mapema kwamba huyo jamaa ni opportunistic tu na wala hana mapenzi kwako.
Asante sana my dear.
 
Leah ninakusihi,km mwanandoa, hayo mabo yote mwachie, Mungu, kuna leo na kesho, pia husdiriki, kumwambia mdogo wako atoe mimba eti kisa kulinda soni yako na mmeo, mnajua mtakaye mmua angekuwa nani?na ni kwambie mdgo wako akifa wakati anatoa mimba, utajikisiaje? je wewe huspo zaa? na mtt wa mdogo wako yupo itakuaje? hacheni hizo, Leha mrudie mmeo, nendenei kanisani kaomba kumuona padri, nina imani mtashauriwa vizuri, sjui kwa nini naiona ndoa yenu km yakikatoliki lakini nakusihi, mrudie mmeo, huyo ndochaguo lako, ebu rejea ushauri wangu hapo juu, km nilizo zitaja ni weekneszao, work on it mamy!
Amina.
 
Naomba nijue ndoa yako ni ya imani gani???sasa tujue ndoa yako ni ya imani gani,
lakini pia mpk umefunga bado unasema hapo ni kwako na sio kwa wewe na mmeo na wewe basi ulishaanza siku nyingi kujiweka superior hata kabla ya ndoa,kama ndoa yako inaweza kuvunjwa tafadhali ivunje na uanze maisha mapya bila kuuliza mdogo wako ataishije,kama ndoa yako ni ya kanisani,nenda Kanisani fikisha hilo na uombe radhi kuwa ndoa itakuwepo(haitavujika) lakini utashika hamsini zako!!!Na pete uivue kabisa ifungie kabatini,uanze maisha mapya ambayo yatakufanya usiolewe mpaka mmeo afe,na uwe unahusiano nje ya ndoa!!lakini kubwa lingine na mgawanyo wa mali,kama ndoa inavunjika mahakamani ask for divorce ili kila kitu kigawanywe equally,kama haivujiki ndoa tumia busara na ujasiri mgawane half ya kila kitu!!!as hauna mtoto kuanza maisha mapya ya kwako kwako ni rahisi kidogo!La mwisho mrudie Mungu maana from hapo hata masomo yako unaweza usifannye viziuri,iwe ni kusali saaana na Kusoma tuu!!!
POLE KWA UNAYOPITIA
 
Kifupi Leah2 huyo mme wako ni malaya...hata ungemzalia watoto 8 bado angefanya ufilauni wake..ukiona mtu anafanha ufuska nyumbani ujue kazini kashamaliza vibinti vyote vya field na wale wahudumu...Hapo bado wale anaokutana nao njiani...

Hao wanaosema Kisomo chako kimesababisha wanakupotosha..naamini yote uliofanya ni kwa ajili ya kuinua kipato cha familia..

We unangaika kutafuta maisha mwenzako anakusaliti nyumbani....Biblia inasema ndo haivunjiki isipokuwa kwa sababu ya uasherati...hapo ndoa katika ulimwengu wa roho haipo hata kama ungeilazimisha...lile agano mliloagana kanisani limeshavunjika

Endelea kusoma na kumsihi Muumba wako akuumbie wa kwako...akupe mme wako...huyo hakuwa wako..
Najisikia kufarijika kwa ushauri wako, thank you.
 
Cheating ya mumewe haihusiani na mke kwenda shule ni tabia. Na sio kwamba alitaka sana mtoto maana walikubaliana wasubiri na ndio maana akamuomba shemejiye atoe mimba. Mnaotetea sijui mnatetea nini. Mdada kusamehe ni muhimu kwako wewe tena nakushauri usamehe. Kurudiana naye, search your heart.
 
Dada angu, mm naona haya maisha watu watakushauri vingi lkn wewe ndio unamjua vzr mmeo, pia hatujui unampenda kiasi gani mmeo.
Pia kwa kuwaitia wazazi uliwapa adhabu kubwa sana, lkn pia baada ya hapo kama mngekubalia ingekuwa siri ya familia yenu
 
Back
Top Bottom